Mwanafunzi wa UDSM akamatwa kwa kusambaza taarifa na Takwimu za uongo za Covid-19 WhatsApp

Mwanafunzi wa UDSM akamatwa kwa kusambaza taarifa na Takwimu za uongo za Covid-19 WhatsApp

Tangazo Hilo Kazi msijesema hamkuambiwa

Ova
IMG-20200411-WA0003.jpg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndo maana wamemkamata ili athibitishe hao wagonjwa 200 wapo wapi?.
huyo ni mtuhumiwa tu akiwaonesha hao wagonjwa walipo ataachwa HURU.
Taarifa sahihi ni ipi? Askari wamejuaje kuwa hio taarifa sio sahihi? Je, ilileta madhara gani kwa jamii?

"baba unahonga hawara elfu kumi,
watoto wanakufa na njaa nyumbani"
 
Taarifa sahihi ni zile zinazotolewa na serikali kupitia kwa Waziri wa Afya Ummy Mwalimu na si vinginevyo.

Sent using Jamii Forums mobile app
Hakuna nchi inayoitwa "mpk ss Tanzania" tuna jamhuri ya muungano wa Tanzania au kwa kifupi JMT, inawezekana huyo binti alikuwa anaongelea mtaa mmoja huko china
 
Taarifa sahihi ni zile zinazotolewa na serikali kupitia kwa Waziri wa Afya Ummy Mwalimu na si vinginevyo.

Sent using Jamii Forums mobile app

Mathalani wewe Yonga imetokea umekufa nami nikaandika mtandaoni kuwa "Yonga amekufa" hii itakuwa ni taarifa isiyo sahihi na ni kosa? wakati serikali ikisema hiyo itakuwa sio kosa? ukweli sheria ile very soon itahitaji marekebisho kwani inaleta mgongano kwenye uhuru wa kuongea
 
Tbc nao walitoa taarifa zisizo sahihi
Vp wao hawakamatwi?
 
Mathalani wewe Yonga imetokea umekufa nami nikaandika mtandaoni kuwa "Yonga amekufa" hii itakuwa ni taarifa isiyo sahihi na ni kosa? wakati serikali ikisema hiyo itakuwa sio kosa? ukweli sheria ile very soon itahitaji marekebisho kwani inaleta mgongano kwenye uhuru wa kuongea
Inaweza kua inahitaji marekebisho sawa sikatai lakini kwa sasa tuifuate sheria iliyopo kabla ya hayo marekebisho unayo yataka.

Halafu kumbuka kauli ya waziri mkuu alisema kwamba anayepaswa kutoa taarifa za ugonjwa huu ni waziri wa afya tu na ikishindikana atatoa yeye au makamu au rais mwenyewe

Kuna aina za taarifa mkuu sio kila taarifa hairuhusiwi kutolewa kuna taarifa zingine lazima zitolewa na mamlaka husika kwa maslahi mapana ya taifa na wamefanya maksudi ili kuondoa taharuki hivi kila mtu akianza kutoa taarifa zake kuhusu corona we unaona itakua sahihi kwa jamii yetu?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ukweli siku zote una tabia ya kuuumbua
Maswali ya kitoto hayo. Taarifa sahihi ni zile zinazotolewa na waziri mhusika. Askari wamejua kuwa taarifa za mtuhumiwa sio sahihi kwa kuwa ni tofauti na taarifa ya Waziri ambaye anaarifiwa kutoka pembe zote za nchi na baada ya kujumlisha takwimu hizo ndipo anatangaza.

Huyu mtu binafsi amepata wapi takwimu zake? Swali la mwisho kwamba taarifa ya mtuhumiwa imeleta madhara gani ni la kipuuzi mno na halihitaji hata kujibiwa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga linamshikilia Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Mwaka wa Tatu Kitivo cha Kiswahili Mariam Jumanne Sanane (23) kwa kosa la Kuchapisha na kusambaza taarifa na takwimu za uongo kuhusu Corona kwenye mitandao ya kijamii ikiwemo Whatsapp.

Akitoa taarifa kwa Vyombo vya Habari leo Jumamosi Aprili 11,2020,Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba mtuhumiwa alikamatwa Aprili 9,2020 majira ya saa mbili na dakika saba(2:07) usiku eneo la Mwadui, mtaa wa Tabora, kwenye machimbo ya almasi wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga kwa kosa la kuchapisha na kusambaza taarifa za uongo kwenye mitandao ya kijamii.

“Tarehe 26/03/2020 Askari wa kikosi kazi cha mtandao kilifanikiwa kuona ujumbe kwenye whatsapp uliotumwa na mtuhumiwa unaosema ‘mpk ss Tanzania ina wagonjwa wapatao takribani 230 wa Covid 19 na waliofariki ni 04”,ameeleza Kamanda Magiligimba.

Amesema mtuhumiwa amepekuliwa na kukutwa na simu iliyotumika kutuma ujumbe huo na ameshahojiwa na atafikishwa mahakamani kwa makosa ya kuchapisha na kusambaza taarifa za uongo mtandaoni pamoja na kutoa takwimu za uongo.

Kamanda Magiligimba ametoa wito kwa wananchi kuwa makini na matumizi ya mitandao ya kijamii na kuacha kupotosha watu kwani kufanya hivyo ni kosa la jinai na hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.

Usikute nasikia Mtaani, yeye sio chombo cha Habari wala msemaji was chochote
 
Taarifa sahihi ni ipi? Askari wamejuaje kuwa hio taarifa sio sahihi? Je, ilileta madhara gani kwa jamii?
angetoa ushahidi wa hao watu 230 waliogua na 4 waliokufa kama alivyosema angekuwa sahihi Kama hauna ushahidi huo huyo dada ajiandae na kuingia kwenye mikono ya sheria.
 
Ng'wanamalundi,
Ni kweli,,kwa hizo nchi lazima suala liwe critical na liwe na athari zinaonekana,lakini sio kea kufuatilia magroup ya watu wanapiga soga wasapu,ujue Kuna kupiga soga Ama kuchat na Kuna kutoa taarifa rasmi.

Mfano,online TV Kama kwanza ingetoa hizo takwimu Kama sehemu ya taarifa zake,amo blog tuseme ya Mr mchuzi ingeweka article za takwimu hizo,Hapo sawa.

Lakini watu wanachat,kuchat Ni sawa na mko kijiweni tu mnapiga story,hizo SI taarifa rasmi na hazina athari inayoweza ku influence situation
Kwani taarifa zinawezaje kuenea si zinaenea kwa style hizi hizi
 
Back
Top Bottom