Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Mlimkamata kiharamia Abdul Nondo, mumemuua akwilina na Sasa mnamgeuzia kibao Merry Saanane, mjue Hawa Wana wazazi madogo zao marafiki effect yake Ni exponential, endeleeniWatoto wa shule gani?
Kama huyo binti ni wa chuo kikuu utasema ni mtoto huyo?
Sent using Jamii Forums mobile app
Na ndio kilichotokea na hakuna sifa watakayopata, wabunge wa shy nao hovyo tu yamenyamaza kimya, hivi Salome yule mbunge wa vitimaalumu yupo kweli? Hapa ndio namkumbuka Rachel mashishangaMaskini,, pengine alikusudia kuandika wagonjwa 23 ila akakosea 0 ikajiongeza bila yeye kukusudia.
Ndio imeshakua hivyo watamkazia ili wapatiepo sifa,, kwahiyo fine itamuhusu tu,,
Mkuu, tofautisha maoni na takwimu. Huyo binti hakutoa maoni ilà alitoa takwimu za walioathirika na waliokufa. Kazipata wapi? That's another question!!Maoni SI lazima mtu akitaka kutoa yapelekwe kwanza shirika la viwango,yakathibitishwe,maoni mtu hutoa tu,tofautisha kutoa maoni na kutoa taarifa rasmi
Ni issue ndogo mno hata kutumia kuipa muda wa kuifuatilia.Hajalazimisha kwamba takwimu alozotoa kipindi anachati wasapu nduo za kweli.
Takwimu rasmi SI zinafahamika,,kwanini upoteze human resource kusneak kwenye magroup watu wanapiga soga kutafuta mtu wa kukamata?
bado upoteze resource kumsaka na kumkamata na bado resource za kumweka ndani na kumpeleka mahakamani kwa kupiga soga?
😎😏😎😏😎
Huyo rpc nae bumuda tu kama sura lake,ukimuona utafikiria fundi majenezaJeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga linamshikilia Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), Mwaka wa Tatu Kitivo cha Kiswahili Mariam Jumanne Sanane (23) kwa kosa la Kuchapisha na kusambaza taarifa na takwimu za uongo kuhusu Corona kwenye mitandao ya kijamii ikiwemo Whatsapp.
Akitoa taarifa kwa Vyombo vya Habari leo Jumamosi Aprili 11,2020,Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga ACP Debora Magiligimba mtuhumiwa alikamatwa Aprili 9,2020 majira ya saa mbili na dakika saba(2:07) usiku eneo la Mwadui, mtaa wa Tabora, kwenye machimbo ya almasi wilaya ya Kishapu mkoani Shinyanga kwa kosa la kuchapisha na kusambaza taarifa za uongo kwenye mitandao ya kijamii.
“Tarehe 26/03/2020 Askari wa kikosi kazi cha mtandao kilifanikiwa kuona ujumbe kwenye whatsapp uliotumwa na mtuhumiwa unaosema ‘mpk ss Tanzania ina wagonjwa wapatao takribani 230 wa Covid 19 na waliofariki ni 04”,ameeleza Kamanda Magiligimba.
Amesema mtuhumiwa amepekuliwa na kukutwa na simu iliyotumika kutuma ujumbe huo na ameshahojiwa na atafikishwa mahakamani kwa makosa ya kuchapisha na kusambaza taarifa za uongo mtandaoni pamoja na kutoa takwimu za uongo.
Kamanda Magiligimba ametoa wito kwa wananchi kuwa makini na matumizi ya mitandao ya kijamii na kuacha kupotosha watu kwani kufanya hivyo ni kosa la jinai na hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Acha ujinga weewe. Wizara ya Afya pekee ndiyo inayo mamlaka ya kutoa taarifa zozote za magonjwa. Acheni utoto nyie bavichaWamsamehe tu, hii sheria huko mbeleni inabidi wake waifute, Uhuru wa kutoa maoni Hapa unakiukwa, kila mtu anajua takwimu rasmi ni zipi na kila mtu anafuatilia taarifa rasmi kwa umakini Sana,
Inayotolewa na Wizara ya AfyaTaarifa sahihi ni ipi?
Jr[emoji769]
Sasa anapewa nafasi ya kuthibitisha akiwa mahakamaniKwa kuwa wao serikali hawana takwimu kwa sasa, hizo za msomi (wanayemtumu) ni kweli.
Kamanda kuwa mpole. Binti amepewa nafasi ya kuthibitisha taarifa zake akiwa mahakamaniMathalani wewe Yonga imetokea umekufa nami nikaandika mtandaoni kuwa "Yonga amekufa" hii itakuwa ni taarifa isiyo sahihi na ni kosa? wakati serikali ikisema hiyo itakuwa sio kosa? ukweli sheria ile very soon itahitaji marekebisho kwani inaleta mgongano kwenye uhuru wa kuongea
Tii sheria bila shuruti.Mlimkamata kiharamia Abdul Nondo, mumemuua akwilina na Sasa mnamgeuzia kibao Merry Saanane, mjue Hawa Wana wazazi madogo zao marafiki effect yake Ni exponential, endeleeni