MwanaHalisi ladai Ben Saanane huonekana kwa jamaa zake

MwanaHalisi ladai Ben Saanane huonekana kwa jamaa zake

Huu uzi ni mwiba kwa manyumbu!
Maana Ben ni wao, Mwanahalisi na Kubenea ni wao basi tabu tupu... Wanakanyagana tu hapa.
 
Tanzania yani si upinzani wala walioko madarakani wote ni wachumia tumbo tu.
 
Bora Uwe mwizi km Lowassa kuliko kuwa mhalifu
Kweli lowassa bado anawatesa sana kiakili na hamtakuja mkae mkasamsahau lowassa.
Yani ccm hamjawahi kuwa na ajenda nyingine kwa upinzani zaidi lowassa.
 
Hivi katika pita pita zangu ikatokea nimeonana na Ben, alafu nikimwambia mtu nimemwona Ben sehem flani ni tatizo?
 
CHADEMA INAMSALITI BEN SAA NANE: TAHADHALI KWA VIJANA WENGINE

Toka kutoweka kwa Ben Saanane kuripotiwe sikuwahi kuandika chochote zaidi ya maoni machache kwenye maandiko ya watu wengine katika mtandao wa “facebook”, na zaidi kusoma kupitia JF, na mitandao kadha wa kadha. Sikufanya hivyo kwa sababu, mosi suala la uhai wa mtu ni suala nyeti sana, na kulifanyia siasa ni ishara ya ukosefu wa ustaarabu, maana ni jambo linaloiumiza familia sana na wote walio na mahusiano ya karibu na Ben.



KUTOWEKA KUTUMIWA KISIASA

Kwa mara ya kwanza nimesikia kikundi kinachoitwa UTG, ambacho kimemtambulisha Malisa kama Mwenyekiti wake na Ben Saanane kama Katibu wa hicho kikundi, na viongozi wengine wa hicho kikundi ni wanachadema kindakindaki. Lakini wakasema hawafungamani na chama chochote (naona wana mioyo miwili, wa kufungamana na chama na ule usiofungamana na chama).

Katika kurasa za vijana hao za facebook walikuwa wakihusisha kupotea kwa Ben na ukosoaji wake wa PHD ya Mh. Rais, Dr. John Pombe Magufuli. Wakisema mtu mwenye IQ kubwa hadi ya kuhoji PHD ya Rais awezaje kupotea? Katika maoni yangu niliwaambiwa wafikiri kabla ya kuandika, kwanza kukosoa jambo lolote hakuhitaji IQ, hivyo nikawashauri ni kheri kuwa na akiba ya maneno na subira kuliko kukurupuka, lakini yote waliyoendelea nayo hadi mradi wa kuuza tsheti kupitia kutoweka kwa Ben twakujua. Na katika tamko lao wakatoa siku tatu ili serikali na Chadema watoe taarifa ya alipo Ben.

Siku ya tatu ya tamko la UTG, Mh. Tundu akaongea na waandishi wa habari, naye akalifanya suala hilo kisiasa na kuonyesha serikali inajua au imehusika kumteka na maneno yake hayakutofautiana sana nay a vijana wa UTG, kuwa kumkosoa Rais na serikali yake ndio kumesababisha Ndugu Saanane kupotea. Akazungumza mengi na yote twayafahamu.

NAFASI YA MWAJIRI WA BEN SAANANE NA KUTOWEKA KWAKE

Nimekuwa mtumishi wa Makao Makuu ya CHADEMA, kama Msaidizi wa Mwenyekiti wa Tiafa. Watumishi wote wako chini ya ofisi ya Katibu Mkuu, chini ya Kurugenzi ya Fedha na Utawala, ambaye Mkurugenzi wake, ni Mh. Anthony Komu (MB). Kila asubuhi lazima mtumishi afike ofisni kabla au saa mbili kamili asubuhi na anasaini kitabu cha wafanyakazi getini kwa mlinzi kabla ya kuingia ndani. Hivyo ikitokea mtumishi hajaonekana kazini, siku hiyo hiyo ofisi ya Katibu Mkuu inachukua hatua ya kujua kwa nini hujaonekana.

Na pia kwa nafasi yake kama Katibu Myeka wa Mwenyekiti, maana yake ni kwamba kila siku lazima uwasiliane na mkuu wako wa kazi, akupangie majukumu au umpe taarifa ya majukumu uliyotekeleza na kadhalika, kutoweka kwa mtu wa namna hiyo hadi wiki tatu hujatoa taarifa, si polisi tu bali hata kwa wazazi kunazua shaka ya uhusika wako katika sakata hilo.

Kwa mujibu wa gazeti moja la siku, siku ya tatu ya Ben kutoonekana nyumbani, mmiliki wa nyumba anayoishi alienda makao makuu ya CHADEMA na kuulizia kama wanajua alipo maana hajamuona siku tatu na simu zake hazipatikani, wao wakamjibu hawajui na inavyodhihirika hawakuchukua hatua yoyote.

Kwa msingi wa mazingira haya kuna ishara kubwa sana kuwa kutoweka kwa Ben Saanane ni kazi ya ndani ya chama na haswa hao viongozi wakuu na walitaka kulitumia hilo tukio kwa manufaa yao ya kisiasa.

KWA NINI NAWAZA CHADEMA SASA INAMSALITI BEN?

Jana, Mwanahalisionline.com wamesema Ben yupo, anaonekana kwenye vijiwe vya kahawa na kwa marafiki zake na haendi ofisini wala nyumbani. Huku likisema limemnukuu mjumbe wa Kamati Kuu (CC) ya CHADEMA, ambaye hawakumtaja akisema huo ni mkakati binafsi wa Ben wa kujitafutia umaarufu ili kupata nafasi za uongozi.

Sikumbuki kuwahi kuona gazeti lolote likitoa dokezo la habari watakayoitoa wiki inayofuata. Pia gazeti hili tunafahamu linamilikiwa na Mkurugenzi wa fedha na Utawala wa Chadema, na pia Mbunge wa Ubungo, Mh. Said Kubenea. Na ma ra zote limetumika kama propaganda mashine ya CHADEMA, na limetumika kuwachafua na kuwasafisha watu kadhaa kisiasa kwa manufaa ya wamiliki na chama chao.

Ukisoma katikati ya mistari utagundua kwamba, viongozi hao wakuu wa CHADEMA walikubaliana na Ben kuwa ajifiche na wafanyie tukio hilo siasa, kumbuka walienda ziara Ulaya na malalamiko yao yalikuwa ya kukandamizwa na kutekwa. Kuna kila dalili sasa jambo hilo limewageuka, maana watu wengine pia wanaweza tumia akili zao na kufikiri nje ya sanduku.

Sasa kwa kuogopa tukio hilo kugeuka, sasa wameanza kuwaandaa watu kuwa Ben kajificha mwenyewe kwa manufaa ya kisiasa, kwa wiki nzima watu wakisubiri gazeti la Mwanahalisi hiyo jumatatu litoe taarifa kamili. Tayari wameshaanza kuonyesha kaijificha kwa sababu ana tamaa ya vyeo na yuko tayari kufanya lolote kupanda cheo. Pamoja na kusingle out ili msalaba uwe juu yake, huo pia utaendana na mkakati wa kusitisha ajira na career yake ndani ya CHADEMA ili hata akiamua kusema ukweli basi wajue ni kwa sababu kaondolewa nafasi yake na sasa anaongea kama mkosaji.

Kwa hiyo habari hiyo ya Mwanahalisi ni mkakati wa wao kujisafisha na kumuangushia Ben jumba bovu, ili kama ni kushitakiwa na ashitakiwe yeye kwa ulaghai alioufanya.

Na sipati picha habari hiyo ingeandikwa na gazeti la uhuru, hadi leo mitandao ya kijamii ingejaza server kwa makombora kutoka kwa mashabiki wasiofikiria ambao wamebatizwa jina la nyumbu kwa uwezo wa kuona, kutafakari na kutenda mambo.


ONYO KWA VIJANA

Vijana wengi sana wanatumika vibaya kisiasa na mwisho wanakuwa desperate na kutelekezwa, lazima kuwa makini na viongozi wengi wa vyama hasa vya upinzani. Tumewaona wengi wakibeba mikoba na hadi wengine wakisahau kuandaa maisha yao ya kesho, wakitumika kama ngazi za wao kupanda huku wakipanda wanawaacha chini. Matukio haya yatupe fikra na namna za kuwafanya hawa viongozi pia wawajibike, tofauti na hapo utatumika na mwisho wa siku analoenda kufanyiwa Ben nawe utafanyiwa. Mwenye sikio na asikie, mwenye jicho na atazame.



NAWATAKIA KHERI YA MWAKA MPYA NA UKOMAVU WA FIKRA 2017



Deo Meck.
 
Hamna lolote. chadema walitaka kuonyesha kwa mabwana wao huko nje kuwa serikali inaua watu. Ila kuna steps walijichanganya.

Chadema sumu sana kwa taifa hili. Tutaona zaidi.
Ishu ya Ben Saanane inaweza kuwa ni Self imposed exile baada ya kuona hatari fulani ya kukamatwa kwa uchochezi mitandaoni
 
Tunawaambia kila siku
Usishangae hata JF ipo kimya kuhusu member wake !!
Ajabu huyu jamaa inawezekana yupo humu humu akitumia Id nyingine
Ndio maana tunasema Mbowe anajua
Hizi ni kick zakipumbavu kweli!!!
Mjadala wa Huyu mtu ungefungwa tu
Maana hakuna lolote zaidi ya kucheza mchezo mchafu
Afu ebu tupazeeni sauti zetu juu ya JF maana kuna nyuzi zingne humu nzurui sana zinaelezea connection ya CHADEMA NA UPOTEVU WA BEN lakini zinaondolewa kweli kwa kasi ya ajabu.....
 
ivi kabla ya mbowe mwenyekt wachadema alikuwa nani namakao makuu ya chadema yapo wapo nakatbu waitkad nauwenez nnani?
 
Acha umburula wewe!!! Siko na info ulizoona za Kubenea! Niko na system inayojipendekeza kw mfalme alieambiwa PhD yake fake ato hadharani aseme na ajibu hapa tuhuma dhidi yake............andiko lake linamilikiwa na mtu mwingine ambae ndio wanadai lake sio yeye!!!(kutoa kutu kwa kutumia maganda ya korosho).....sio andiko lake.......hilo ndio limemfanya wamempoteza tunaju amefichwa sehemu tu ambapo haoni jua wala usiku.....ni taaa tuu wana toture kisaikolojia! Tunajua!!!!! Acha umburula
ben anaonekana na marafiki zake akina Godlisten Malisa wanarandaranda mitaani na kwenye vijiwe vya wahuni
 
Taarifa za Mhe.Kubenea kwamba Ben yupo mtaani anarandaranda na kujificha kwa rafiki zake, ni taarifa zinazopaswa kufanyiwa kazi na Jeshi la Polisi na uongozi wa Chadema. Takribani mwezi mmoja sasa polisi na Uongozi wa Chadema umetoa taarifa rasmi za kumtafuta Ben. Leo Kubenea anasema Ben yupo mtaani, anaonekana kwenye vijiwe vya kahawa.

Ni vizuri Polisi wakamkamata Kubenea aeleze ni mitaa ipi Ben alionekana, na ni vijiwe vipi vya kahawa alivyokutwa. Je alikua na nani? ni siku gani? aliyemuona ni nani? na kwanini alipomuona hakutoa taarifa polisi? Na kwa kuwa Kubenea anajua polisi wanamtafuta kwanini alipojua Ben yupo mtaani hakwenda kuripoti polisi ili awasaidie ktk kufanya uchunguzi? Kwanini Kubenea anawaacha Polisi watumie rasilimali kubwa kumtafuta Ben wakati anajua Ben amejificha ili kujipatia umaarufu wa kisiasa?

Kubenea anasema Ben anatafuta umaarufu, je ni umaarufu gani wa kujipoteza? Ili iweje? Kwa faida ya nani? Kwamba Ben akijipoteza ndo anakua maarufu? Halafu huo umaarufu unamsaidiaje? Kugombea nafasi ya uongozi kwenye chama? Ni nafasi gani ambayo mtu huchaguliwa kwa kujipoteza? Na ni akina nani watakua wajinga wa kumpa mtu kura kwa sababu tu alijipoteza? Hivi kujipoteza kwa Ben kunamuongezea kura au kunampunguzia?

Kama kweli Ben yupo mtaani, je Kubenea haoni kuweka taarifa gazetini ni kumfanya azidi kujificha? Kwanini asingewaarifu polisi kwanza wamkamate then ndo aweke gazetini? Na hao marafiki zake Ben waliomficha huko mtaani ni mahiri wa ujasusi kiasi gani? Je wamewazidi akili polisi, usalama wa taifa na intelijensia ya Chadema? Je Kubenea kuandika habari bila kujibu maswali muhimu (5Ws +H) haoni kunaifanya habari hiyo kukosa uhalali wa kuaminika mbele ya jamii?

Na kwa kuwa Mwenyekiti wa Chadema Mhe.Freeman Mbowe alitamka hadharani kuwa kuna uwezekano Ben ametekwa, je Kubenea kusema Ben kajificha haoni anamfanya Mbowe kuonekana ameshiriki kumficha Ben? Kwa kuwa Kubenea ameshindwa kutaja vyanzo vyake vya habari haoni habari hiyo inaweza kuonekana ni ya kutunga maana haina credible source? Je ikija kubainika kuwa Ben ametekwa au amekufa, je Kubenea haoni kwamba atakua amewakosea sana watanzania, kuikosea familia ya Ben, na hata nafsi yake mwenyewe?

Sisemi kuwa Ben hawezi jificha, as a human being anaweza kufanya hivyo na ikibainika kajificha nashauri achukuliwe hatua kali za kisheria. Lakini ukweli ni kuwa habari ya Kubenea imeacha maswali mengi kuliko majibu.

Nahofia Kubenea asije kuwa ameandika habari hiyo kwa chuki binafsi dhidi ya Ben halafu baadae akaja kujuta. Nafahamu ugomvi binafsi kati ya Ben na Kubenea uliosababishwa na tofauti za kisiasa. Kuna mengi yalitokea ambayo siwezi kuyasema yote hapa lakini Ben na Kubenea wamewahi kunyukana kwa nyakati tofauti kwa sababu mbalimbali (ushahidi wa maandishi yao wakinyukana upo).

Sasa isije kuwa Kubenea anaendeleza mnyukano kati yake na Ben akasahau suala la uhai wa mtu ni muhimu kuliko tofauti zao za kisiasa. Ikibainika Ben amejificha Kubenea atakua shujaa kwenye hili, lakini ikija kubainika kuwa Ben amekufa, kuuawa au kutekwa, dhamiri ya Kubenea itamhukumu maisha yake yote. Ni vizuri kuwa na akiba ya maneno.!
 
UPDATE: Inaelekea wanaharakati wa Chadema huko Facebook nao "wana taarifa kuwa Ben hajapotea" kwa sababu ghafla wameitosa kampeni yao ya [HASHTAG]#BringBackBenAlive[/HASHTAG], in similar manner kama Mbowe alivyozi-abandon "Operesheni UKUTA Toleo la Kwanza" "Operesheni UKUTA Toleo la Pili" na hii ya majuzi "Operesheni KATA FUNUA." Usiamini maneno yangu, nenda Facebook, angalia posts za "vinara" wa [HASHTAG]#BringBackBenAlive[/HASHTAG] utamaizi ninachoeleza


Dhumuni la haya yote ni nini?
Kuna makundi yenye mkono kwenye harakati hii ya kupotea/kujificha etc kwa Ben.

Was Ben Double agent-na hivyo kila upande ukiziba mdodmo wake ?. Nawaza tu!.
 
1483909565488.jpg

Magoiga SN-Mwanza

Serikali ilipolifungia hili Gazeti baada ya kuandika kuhusu Kupotea kwa Dr Ulimboka waliandamana mitandaoni, na kusema linafungiwa kwasababu linaiandika vibaya CCM na serikali yake. Lakini leo wako mstari wa mbele kulitia MOTO na hata kushinikiza polisi wavamie ofisi zake kisa limeandika kuhusu kujificha kwa Ben. Hapo ndipo unapojua kuwa kuna shida ktk hiki kizazi. Sijawahi kuwa shabiki wa hili Gazeti na haitatokea,

ILA UKIONA WACHAWI WAMEGOMBANA yakupasa kufurahia maana muda siyo mrefu watatajana na utamjua hata mchawi wako aliyekuwa akikusumbua.

Katika maisha yako jitahidi sana usiwe mfuata msafara kwa rimoti ya aliyetangulia

Magoiga SN-Mwanza
 
Back
Top Bottom