Mwanajeshi awatesa vijana na mmoja kufariki akiwatuhumu kumwibia tv yake. Je, hii ni haki?

Mwanajeshi awatesa vijana na mmoja kufariki akiwatuhumu kumwibia tv yake. Je, hii ni haki?

Chagu wa Malunde

JF-Expert Member
Joined
Jul 11, 2015
Posts
8,734
Reaction score
5,750
Waziri mwenye dhamana wa mambo ya ndani. Wewe una dhamana juu ya usalama wa raia na mali zao. Hakuna raia anayependa kutetea watu wanaojihusisha na uhalifu. Ila nchi yetu inatawaliwa na kuongoza kwa misingi ya sheria na haki.

Tarehe 26/10/2019 watuhumiwa wapatao watano walikamatwa na Migambo ambao walitumwa na mtendaji wa Kata ya kahama Wilaya ya Ilemela mkoani mwanza kwa tuhuma ya wizi wa Milango. Kuna Mwanajeshi ambae anadai kuwa alikuwa ameibiwa Tv flat screen alianza kuwapiga watuhiwa na kuwatesa akidai hawa ndio wezi wa Tv yake. Mmoja wa watuhumiwa hao maarufu Omela alipigwa sana na alifariki. Mmoja wa watuhumiwa alipigwa na kug'olewa jino. Raia mwema mmoja alijaribu kusaidia ili watuhumiwa wapelekwe polisi nae alipigwa.

Ndugu za marehemu wanaogopa hata kufuatilia kesi hii. Polisi Kirumba wamedanganya kuwa walipigwa na wananchi wenye hasira kali. Katiba ya jamhuri ibara ya 13(6)(b) ipo wazi juu ya watu kutojichukulia sheria mikononi.

Tukio hili la watuhumiwa kupigwa na kuteswa mpaka mmoja akafa limefanyika ndani ya ofisi ya mtendaji wa kata ya kahama wilaya ya Ilemela na mtendaji na mwenyekiti walikuwepo. Sasa kwa nini wapotoshe kuwa walipigwa na wananchi wenye hasira kali!
 
hiyo ndio kazi yake rasmi...kutatua kero za wananchi

LA ajabu ana deal na petty issues kama za akina kigogo2014 au yule mama aliyemtimua polisi kwenye pagala lake
Tumuombe Mungu ashughulikie hili suala haki ipatikane
 
Wezi wa milango!
😡😡😡😡😡😡
Nimekumbuka nilivyoibiwa milango yangu tisa (9) ya mninga, tena nilikuwa nimefunga na vitasa, waling'oa bila kujali, sikuamini nilivyokuta frame peke yake, top zimebebwa.
 
Mwanajeshi ambae anadai aliibiwa Tv anawapiga watuhumiwa na kuwatesa akishirikiana na Migambo wa Kata.

Anawapiga na kuwatesa watuhumiwa hadi mmoja amafariki. Lakini polisi Kirumba Wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza hawachukui hatua.

Je, nchi hii inatawaliwa na sheria? Mtuhumiwa anatakiwa atendewe haki kama katiba inavyosema. Ibara ya 13(6)(c) mmoja wa watuhiwa alifariki.

Waliteswa ndani ya ofisi ya kata. Je, Mkuu wa Wilaya au Mkurugenzi anajifanya hajui? Na kwanini Mwanajeshi achukue sheria mkononi?

Tukio hili limetokea tarehe 26/10/2019 mbele ya Mtendaji wa kata na Mwenyekiti.

Na mtendaji wa Kata anayo mamlaka ya kushughulikia kesi za jinai? Mpaka watu wateswe na mmoja kuuawa?
 
Rais Magufuli saidia familia ya huyu Mama ambae mume wake alipigwa na kuteswa na mwanajeshi akishirikiana na migambo huko Mwanza, Wilaya ya Ilemela kata ya Kahama tarehe 26/10/2019 majira ya mchana mpaka jioni.

Aliteswa yeye na watuhumiwa wanne kwa kosa la kuiba milango. Kuna mwanajeshi aliwahisi hawa ndio wezi wa Tv yake. Hivyo aliwatesa ili waseme. Mmoja wa watuhumiwa maarufu kama Omela alifariki.

Wengine waliumizwa na mmoja aling'olewa jino. Tukio hili lilitokea ndani ya ofisi ya mtendaji wa kata hiyo.

Waziri wa mambo ya ndani amepewa taarifa. RCO anafahamu na RPC pia. Mtuhumiwa mmoja alishikiliwa kwa siku saba na akapewa kesi ya unyang'anyi wa kutumia silaha.

Aliachiwa kwa mazingira yanayoashiria rushwa. Mpaka sasa Mwanajeshi huyu na migambo waliowatesa watuhumiwa hawa hawajachukuliwa hatua zozote.

Tukio limetokea mbele ya walinzi wa amani. Mtendaji na Mwenyekiti.Polisi Kirumba wanapotosha ukweli wa tukio hili.
 
Huyu jiwe mnampa promo sana. Yaani hata masuala ya mahakamani mnataka akayaamue yeye? Yeye ndiye muweza wa yote Tanzania (mungu wa Tanzania)??

Tunazidi kumjengea udikteta zaidi
 
Back
Top Bottom