Mwanamke ajeruhiwa kwa risasi za polisi maeneo ya Sinza Dar es salaam

Mwanamke ajeruhiwa kwa risasi za polisi maeneo ya Sinza Dar es salaam

Mwanamke aitwaye Mariam mkazi wa Sinza Lion Dar es Salaam, amejeruhiwa kwa kupigwa risasi maeneo ya begani katika harakati za Polisi kuwatuliza raia wenye hasira kali waliokuwa wanataka kumpiga mwizi aliyekwapua simu kwenye bodaboda majira ya saa 12:00 asubuhi ya leo Mei 20, 2022

Kwa maelezo ya mashuhuda wa tukio hilo, wanadai baada mwizi huyo kukwapua simu alikimbilia nyumba iliyokuwa jirani na baadaye kidogo walitokea maaskari waliomwokoa mwizi lakini katika harakati za kuwatuliza raia, inadaiwa walifyatua risasi iliyomjeruhi raia huyo ambaye amekimbizwa hospitali

Chanzo: EATV

SOMA PIA:

Muliro azungumzia raia aliyejeruhiwa kwa risasi​

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro, amethibitisha tukio la mwanamke kujeruhiwa kwa risasi leo maeneo ya Sinza Lion, na kusema imempata kwa bahati mbaya baada ya Askari kufyatua risasi juu kwa lengo la kuwatawanya wananchi waliokuwa wanampiga mwizi wa simu.

Kauli hiyo ameitoa hii leo Mei 20, 2022, wakati akizungumza na East Africa TV & EA Radio Digital, ili kutoa ufafanuzi wa madai yaliyotolewa na mashuhuda wa tukio hilo kwa kusema kwamba mwanamke huyo aitwaye Mariam amejeruhiwa na polisi.

"Ni kweli tukio hilo limetokea na jeshi linaendelea kulifuatilia, lakini ni kwamba askari walifyatua risasi juu katika juhudi za kumuokoa mtuhumiwa na kwa bahati mbaya kuna mwanamke amejeruhiwa ingawa anaendelea vizuri," amesema Kamanda Muliro.

Aidha Kamanda Muliro akimzungumzia mwizi huyo amesema, "Huyo mtuhumiwa hatujamtambua kwa sababu hajaweza kuongea, alikuwa tayari amepigwa, hawezi kuongea, hivyo tunalichunguza tukio hilo".
Loh
Polisi polisi polisi.

Mbona wanyama hivi?
 
Mwanamke aitwaye Mariam mkazi wa Sinza Lion Dar es Salaam, amejeruhiwa kwa kupigwa risasi maeneo ya begani katika harakati za Polisi kuwatuliza raia wenye hasira kali waliokuwa wanataka kumpiga mwizi aliyekwapua simu kwenye bodaboda majira ya saa 12:00 asubuhi ya leo Mei 20, 2022

Kwa maelezo ya mashuhuda wa tukio hilo, wanadai baada mwizi huyo kukwapua simu alikimbilia nyumba iliyokuwa jirani na baadaye kidogo walitokea maaskari waliomwokoa mwizi lakini katika harakati za kuwatuliza raia, inadaiwa walifyatua risasi iliyomjeruhi raia huyo ambaye amekimbizwa hospitali

Chanzo: EATV

SOMA PIA:

Muliro azungumzia raia aliyejeruhiwa kwa risasi​

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, Jumanne Muliro, amethibitisha tukio la mwanamke kujeruhiwa kwa risasi leo maeneo ya Sinza Lion, na kusema imempata kwa bahati mbaya baada ya Askari kufyatua risasi juu kwa lengo la kuwatawanya wananchi waliokuwa wanampiga mwizi wa simu.

Kauli hiyo ameitoa hii leo Mei 20, 2022, wakati akizungumza na East Africa TV & EA Radio Digital, ili kutoa ufafanuzi wa madai yaliyotolewa na mashuhuda wa tukio hilo kwa kusema kwamba mwanamke huyo aitwaye Mariam amejeruhiwa na polisi.

"Ni kweli tukio hilo limetokea na jeshi linaendelea kulifuatilia, lakini ni kwamba askari walifyatua risasi juu katika juhudi za kumuokoa mtuhumiwa na kwa bahati mbaya kuna mwanamke amejeruhiwa ingawa anaendelea vizuri," amesema Kamanda Muliro.

Aidha Kamanda Muliro akimzungumzia mwizi huyo amesema, "Huyo mtuhumiwa hatujamtambua kwa sababu hajaweza kuongea, alikuwa tayari amepigwa, hawezi kuongea, hivyo tunalichunguza tukio hilo".
Pole dada yangu jamani.
 
Negligence

Halafu utakuta huyo askari alofanya hivyo anaachwa tu na ishu kupotezewa.


RIP Akwilina
 
Ya marehemu AKWILINA yanataka kujirudia tena risasi imepigwa juu lakn imempata mtu begani

Muliro jumanne maelezo yako hayatoshelezi

Sent from my TECNO F1 using JamiiForums mobile app
 
Inakuwaje polisi wanatumia risasi za moto katika tukio dogo kama hilo? mitaala inayotumika ktk mafunzo ya upolisi ipitiwe tena maana jeshi limejaaa mananga watu
 
uzembe kwa maana ipi???

kapigwa sehemi isiyo sahihi au alitakiwa auwawe kabisa dada mariamu??
Hivi sayansi ya fizikia ndio isemavyo? Kwamba risasi inapigwa juu halafu inampata mtu begani.
Ni ujinga uliopitiliza badala ya mkuu wao kusema askari amefanya kosa la kutumia silaha . Unatafuta kivuli.
Hivi huyo askari anasifa za kuwa kweli askari? Hawa ndio wanaotegemewa kuzua uhalifu. Kweli?
 
Hujayasikia ya marehemu Akwilina wewe?
Askari polisi wakiona kundi la watu ni aidha wanachanganyikiwa au wanatafuta sifa.Na pengine wanakuwa wanaongozwa na akili za ukevi tu.Ni hali imeshindikana vipi hadi urushe risasi?Huwa wanafikiria madhila yanayoweza kutokea kwa wananchi au hata wao wenyewe?Full kutetemeka ndiyo wanafanya mahovyohovyo.
 
uzembe kwa maana ipi???

kapigwa sehemi isiyo sahihi au alitakiwa auwawe kabisa dada mariamu??
Uzembe ni jambo lolote kulitenda kinyume na utaratibu.

Huo ni uzembe wa hali ya juu kuweza kumfikisha mhusika kwenye mahakama za kinidhamu!

Hauwezi hata siku moja ukamjeruhi mtu, eti ukadai ni bahati mbaya wakati askari mhusika alishapata mafunzo "bora" namna ya ushikaji na utumiaji sahihi wa silaha.

Kwenda kinyume na hapo ni uzembe wa kiwango cha lami.

Nimemshangaa Rpc kuanza kukinga kifua kwa askari mzembe!

Jeshini hakuna bahati mbaya kwa kufanya kosa lolote lile.

Yakiishia kwenye meza za media bila mhusika kufunguliwa mashitaka na kufikishwa mahakamani, hata huyo mama mjeruhiwa, kupata stahiki zake za fidia itakuwa ni vigumu!
 
Back
Top Bottom