Mwanamke kutojua kupika inaweza kuwa sababu ya kupewa talaka?

Mwanamke kutojua kupika inaweza kuwa sababu ya kupewa talaka?

Cha usiku kitamu
Muhimu kujua

Alafu sio kama sijui kupika chakula kabisa ila nahisi sipo qualified enough
Madarasa yapo mengi na ni vizur kulifanyia kazi mapema maana ushajua udhaifu wako
 
Tena chukua tahadhari mapema maana kuna mzee mwenyew miaka 67 aliwahi kufanya hivyo kwa mke wake, na akadai kuwa ameshindwa kumvumilia habadiliki.
Yani tahadhari nimeshaanza kuchukua
 
Katika 'pita pita' zangu zote sijawahi kukutana na mwanamke wa kiswahili hajui kupika, natamni nikutane nae nione anafananaje.
Wapo wengi sana huku
 
Kwanini asijue kupika?
Kutokujua kupika kwa mwanamme au mwanamke ni dalili za uzembe,uvivu,ugoigoi nk.
Alikuwa busy sana na shule
Kasoma boarding schools. . .kamaliza chuo ndoa ikafuata ,hakuwa na muda wa kujifunza kazi za nyumbani
 
Mwanamke ndani ya nyumba mbali na yote basi ufanikiwe kuwa nayo haya matatu makubwa.... Ulimi unaotoa maneno matam kwa mmeo, ujue kumpikia mumeo chakula kizur kuijenga afya yake, na tatu chakula cha chumbani(kitandani) nacho ujue kukipika na kupakua vema. Nimekumegea tu ayo kwa uzoefu wangu wa miaka kadhaa ndani ya ndoa.
Nashukuru sana kwa haya ya msingi
 
Sa usipojua kupika mumeo atakula wapi?
Japo sio sababu ya kuachwa ila ni vizuri ujue kupika
Kweli ni muhimu kujua kupika ila nahisi kuna mengine pia yalimfanya aachwe
 
What's up wakuu
Mko bwax?
Basi sawa(in chief engineer's voice)

Kwenu wakuu mliofanikiwa kuoa ama kuolewa ama wenye experience na hizi issues

Hivi ni muhimu kiasi hiko kwa mwanamke kufahamu namna ya kupika chakula?Leo katika stories za hapa na pale na my babes tukajikuta katika hii mada ya upishi

Kuna best yangu(kanizidi kama miaka minne hivi) aliolewa mwaka jana na ana miezi mitano tu katika ndoa yake . .nimepata ubuyu kuwa sasa hivi yupo kwao na talaka juu eti kisa tu alikuwa hajui kupika

Binafsi sijawahi kuona umuhimu wa kujua kupika

Asa wakuu hivi suala la kutojua kupika tu linaweza kufanya mtu akapewa talaka?
Naombeni kufahamishwa maana nishaanza kuogopa huku
usijali olewa na mimi tutakua tunakula hotelini hata watoto wakizaliwa tutakua tunakula nao hotelini
 
Alikuwa busy sana na shule
Kasoma boarding schools. . .kamaliza chuo ndoa ikafuata ,hakuwa na muda wa kujifunza kazi za nyumbani
Sio kisingizio!!! Wengine tumesoma boarding kuanzia primary hadi chuo na bado tulipata mda wa kujifunza kupika! Mzazi wake nae alimuendekeza... Yaani mie mama ilikua nikirudi likizo nanyoosha miguu siku ya kwanza tu, siku inayofuata nakabidhiwa jiko... Awepo mdada msaidizi au asiwepo kazi kwenda mbele.
 
Back
Top Bottom