Gazeti la mwananchi lilianzisha kura za mtandaoni ama poll ya kuuliza wadau ni sera za kiongozi yupi wa Tanzania kati ya Mkapa, Kikwete, Magufuli na Samia wanazozikubali.
Matokeo ya kura yakaonesha Kikwete kupata 17% sawa na Samia, Mkapa kupata 7% na Magufuli kupata 57%.
Baada ya matokeo hayo kutoka, Mwananchi wameamua kuomba radhi kwamba uchaguzi ama vigezo vilivyotumika havikuwa sahihi wanaomba radhi😂.
View attachment 2973698View attachment 2973699
Sera za Uchumi za MaRais? Yaani kila Rais wa Tanzania ana sera zake za uchumi?
Mwananchi waliuliza swali ambalo halina maana kabisa. Tanzania imetawaliwa na chama kimoja tu cha siasa tangu tupate uhuru: TANU/CCM. Tangu 1995 tuna mfumo wa vyama vingi vya siasa. Sera za Uchumi huandaliwa na serikali ya chama tawala na kupitishwa na bunge ambalo siku zote limekuwa na wabunge wengi wa hicho chama tawala: CCM.
Sasa kama Mwananchi wanaona kuwa kila Rais wa Tanzania ana sera zake za uchumi na Watanzania wanaamini hivyo basi kiwango cha ujinga nchini (literacy level) kimeshakuwa kikubwa sana. Itakuwa inamaanisha kwamba hatujui kabisa maana ya
sera za uchumi (
economic policies). LABDA kama kinachotafutwa ni UTENDAJI wa Rais lakini sio "sera zake".
Kubwa zaidi, kwanza hilo ni swali gumu sana kwa watanzania wengi ambao huelewa "
itikadi" ni chama cha siasa, "
sera" ni miradi ya ujenzi wa miundombinu na ununuzi wa mitambo, vifaa na vitendea kazi mbalimbali! Pili, hawana uwezo wa kuelewa serikali inavyoweza kucheza na "
microeconomic tools" kupunguza mfumuko wa bei, kuongeza ajira, uwekezaji, kuboresha upatikanaji wa huduma za jamii, kuboresha utendaji wa sekta ya umma kwa ujumla, kuimarisha thamani ya sarafu, na mambo kama hayo. Hata mambo muhimu kama "
value for money" kwenye miradi/manunuzi hawayajui wala kuyajali. Mbaya zaidi wametawaliwa na ushabiki uliokithiri wa viongozi na vyama vya siasa. Kila kitu wanaona kiko katika rangi "
nyeusi" au "
nyeupe" tu. Hawana uwezo wa kuelewa "kijivu" zenye mikolezo mbalimbali.
Hii
poll haikuwa na maana yoyote kwa umma wa Watanzania labda kama Mwananchi walikuwa wanataka kujua Rais wa Tanzania mwenye washabiki wengi hivi sasa - jambo ambalo halina afya njema kwao. Labda ndio maana wamelazimika kuiondoa na kuomba radhi.