Mwanangu wa darasa la pili hili swali kakosaje? Au mwalimu ndiye hajielewi?

Mwanangu wa darasa la pili hili swali kakosaje? Au mwalimu ndiye hajielewi?

Shule za msingi zinafungwa Leo, Niko hapa napitia mitihani na ripoti za wanangu!
Kuna swali hili; Mwamuzi wa mchezo wa mpira wa miguu anaitwa nani?....mwanangu kajibu MWAMUZI kakosa...Eti mwalimu kawaambia jibu sahihi ni REFARII

Je; jibu sahihi ni lipi hapo? Kosa ni la mtoto Au mwalimu ndo hajielewi?
View attachment 1807698
View attachment 1807699
Kakosa hilo.

Mwambie mwanao kuwa refa pia ni neno la kiswahili hutumika
 
Mkuu mwanao mjanja mjanja sana. Katelezea kwenye swali mule mule, mwamuzi wa mpira anaitwa ...........nae karudia mwamuzi!

Hivi mkuu nikikuuliza fundi wa ujenzi wa nyumba anaitwa nani utasema fundi au muashi
Tukiuliza askari wa usalama barabarani anaitwa nani utasema askari au trafiki
Tukiuliza muendesha ndege anaitwa nani utasema mwendesha ndege au rubani

Mwamuzi wa mpira anaitwa Nani?
 
Labda Mwamuzi anaitwa Piereluigi Collina👇🤸‍♂️🤣
images (60).jpeg
 
Mtoto hafundishwi kama mtu mzima,mtoto anafundishwa kitotototo kuendana na mazingira yanayomzunguka huko mbele sasa ndo ataanza kujishepu mwenyewe kadri anavyopanda darsa..mfano,sisi tulipokuwa darsa la pili tulifundishwa (2-3=haiwezekani),na tukaamini hivyo hadi tulivyopanda darsa tukajua (2-3=-1) ..mtoto hufundishwa kwa staili ya kipekee sana
 
Waamuzi wa mpira wapo zaidi ya mmoja uwanjani,kwa ligi yetu wapo 4,,kwa ligi kubwa za ulaya baadhi ya mechi wapo 5.


Mwamuzi anayezungumziwa hapa ni mwamuzi wa kati,yaani REFARII. Hivyo swali lilipaswa kuwa:
Mwamuzi wa kati wa mpira wa miguu huitwa.............
Watoto wa sasa wanaweza wakasema VAR...maana nayo pia hutoa maamuzi[emoji848][emoji848]
 
Shule za msingi zinafungwa Leo, Niko hapa napitia mitihani na ripoti za wanangu!

Kuna swali hili; Mwamuzi wa mchezo wa mpira wa miguu anaitwa nani? Mwanangu kajibu MWAMUZI kakosa, eti mwalimu kawaambia jibu sahihi ni REFARII.

Je, jibu sahihi ni lipi hapo? Kosa ni la mtoto au mwalimu ndo hajielewi?

View attachment 1807716
View attachment 1807714
Huu muandiko mbona kama wa mtu wa sekondari?!!
 
Unajua mfundishaji wa watoto shuleni ni mfundishaji ndio lakini jina specific analoitwa ni mwalimu. Sasa ukijibu mfundishaji haujakosea Sana ila sio sahihi kwa 100%.

Ni sawa na ukamuita mtu mlimaji badala ya mkulima, au muendeshaji badala ya dereva.

Huyu mtoto hajakosa hilo swali kapata 100% swali limeulizwa kwa kiswahili lijibiwe kwa kiswahili hakuna namna
 
Mkuu mwanao mjanja mjanja sana. Katelezea kwenye swali mule mule, mwamuzi wa mpira anaitwa, nae karudia mwamuzi!

Hivi mkuu nikikuuliza fundi wa ujenzi wa nyumba anaitwa nani utasema fundi au muashi

Tukiuliza askari wa usalama barabarani anaitwa nani utasema askari au trafiki

Tukiuliza muendesha ndege anaitwa nani utasema mwendesha ndege au rubani

Mtoto ana akili sana mzee swali la kiswahili lijibiwe kwa kiswahili, referee sio kiswahili sijui umeelewa angeandika referee angekosea pakubwa kwanini ajibu swali la kiswahili kwa kingereza ?
 
Nafikiria dogo kwelie janja mingi ila ili jibu liwe refarii, hapa watu wa kiswahili inabidi waconfirm kama hilo neno limetoholewa rasm kwenye lugha yetu, vinginevyo tafsiri ya referee ni mwamuzi, dogo kapatia.
 
Refarii ndiyo jibu sahihi kwa mujibu wa kingozi cha mwalimu (marking scheme).

Mwamzi ni jina jumuishi sana mfano mwamzi mahakamani anaitwa Hakimu/Jaji.
Refarii ni kiswahili?
 
Back
Top Bottom