Mwanangu wa kiume miaka 4 lakini haongei ni kupiga makelele tu

Nahitaji msaada mtoto aongee
Pole sana ndugu yangu. Ushauri wangu ni kuwa kamwe usikubali kukaa na kuomboleza kuwa umepata mzigo au una bahati mbaya. Kuna watu wenye changamoto nyingi sana kwenye hii dunia. 1. Onyesha upendo kwake, na usitumia fimbo au ukali kujaribu kumrekebisha. 2. Kwa asilimia kubwa, maelezo yako yanaonyesha mtoto wako ana ugonjwa wa usonji (autism) na hii ni condition ya maisha na haina tiba japo kuna dawa za kutuliza baadhi ya dalili (hili unatakiwa kutafuta dr bingwa wa watoto kwa uhakika zaidi. Ukipata specialist wa mambo ya usonji itakuwa vizuri) 3. Inawezekana kuwa amerithi kutoka kizazi chenu au ni mazingira alipitia tangu akiwa tumboni kwa mama yake au baada ya kuzaliwa. 3. Achana kabisa na watu wanaokumbia kuwa ni majini au amelogwa. Utamaliza fedha zako bure na mtoto hatapona. 4. Dr akihakikisha ni usonji, basi kubaliana na hali ila kuwa karibu na muumba kwa sababu ndiye muweza wa yote. Soma na jifunze namna ya kumhudumia mtoto mwenye usonji ili upunguze changamoto zake. Msisitizo: ni muhimu sana dr a-confirm ni ugonjwa gani au condition gani, na ikiwezekana waone ma-dr zaidi ya wawili.
 
Huyo ana autism
TIba yake pekee ni therapy,atakaekwambia umpe hiyo 5m akusaidie atakuibia tu!
Nakuekea namba hapa mpigie huyo uwahi kumpeleka mwanao, hapo wana occupational and speech therapist.
Ukimuwahi na hizo therapy ataongea tu
Uwe na subra,ninakwambia haya out of experience,+255656050300
 
Huyo Mtoto ana Usonji (Autism) mpeleke hospitali Watakupa Jinsi gani ya kumlea
 
Mtoto inabidi aanze kukaa na kusimama akiwa na miezi mingapi maana wangu ana miezi mitatu ila hapendi kulala lala ana taka kusimama simama
Muache afanye anavyoona yeye usimlazimishe kukaa (baada ya Miezi 6 anaweza kukaa) hua anakaa mwenyewe Ila kutembea unamfundisha kusimama kwanza akizoea anaanza kutembea kidogo kidogo hadi anatembea mwenyewe bila shida yoyote unaanza kumtuma akuletee spana
 
Umekosea sana hapo ulipoweka ahadi ya 5m kwa atakayekusaidia.
Huwezi kupata msaada kwa Mungu maana Mungu halipwi.
Hakuna mwanadamu anaweza kuponya, wanadamu wanatibu Mungu anaponya.
Tubu kwa Mungu akusamehe dhambi zako ili amponye mwanao.
Muahidi Mungu utamtumikia maisha yako yote siyo kumuahidi 5m.
Kama umewaahidi wanadamu hiyo 5m, Mungu anasema amelaaniwa yule amtumainie mwanadamu huku moyoni mwake amwmwacha Mungu.
 
Nimeleta mada hapa nipate msaada,Mungu kaweka maarifa Kwa wanadamu,na kila mtu yupo na shida zake na kazi zake Sasa mtu ataacha kazi zake akusaidie wewe na hakujui,Mimi ndiye mwenye shida na mwenye hasara,Mungu anisaidie tu Kwa kweli
 
Pole mkuu, duniani kuna mapito mengi
 
Pole sana mkuu I can feel u.
 
Hiki kitu kitoe akilini mwako chief.

Ampeleke kwa specialist wa watoto wamsaidie mtoto mengine itakuwa ni kuendelea kupoteza muda.
Safi sana..
Nimependa Jibu watu hupoteza Ndugu na watoto kwa mawazo finyu wanayowaza..
Ila jibu lako limenifurahisha sana
 
Nimeleta mada hapa nipate msaada,Mungu kaweka maarifa Kwa wanadamu,na kila mtu yupo na shida zake na kazi zake Sasa mtu ataacha kazi zake akusaidie wewe na hakujui,Mimi ndiye mwenye shida na mwenye hasara,Mungu anisaidie tu Kwa kweli
Umeona namba nimekutumia za therapist?anaitwa george
Mpigie alafu uende hapo kituoni ukaone kwamba haupo peke yako wapo wengi wenye autism
 
Exactly yaan n kama unaongelesha jiwe, mtoto anakuangalia tu
Ndio hivyo hapo ni kumkubari tu hali yake na kushukuru Mungu km anatembea wengine kutembea hawatembei wanabebwa tu mpaka wanakua wakubwa wa kujitegemea wanabebwa tu wazazi hawachoki kuishi nao,
 
Acheni ujinga aisee. Yan eti anapenda hicho kitu cha kuning’iniza nguo ya mama ake ya ndani anakuja nayo sebuleni? 😂😂😂

Mkuu uko serious? Kwamba huyo mke hajui kutunza vitu? Kyupi mnawekaje sehemu zinapoonekana na mtoto?
Unaanzaje kuweka emoji ya kucheka kwenye habar kama hii? Ina maana ww umeona chupi ya mwanamke tu kuliko ujumbe uliopo?
 
Hiyo ni ASD bhna Autism..
Msimpotoshe bhasi
 
Pole sana kwa mitihani unayopitia. kujaribu tu, kuna maalim yupo Mkulanga kwa mwarabu (kituo kwa Mwarabu) wanamwita Malamba. Kabla kwenda na mtoto nenda mwenyewe Kwanza ukajue siku hizi utaratibu wake ukoje. huduma zake ni bure kabisa labda siku hizi iwe tofauti
 
Daaah pole sana hata Mimi Kuna wakati anasaga meno na anachelewa kulala sana anaweza kulala saa tisa na Kuna wakati anacheka pekeake
Muwahishe hospital kama bado hajaanza matibabu,nakumbuka hii ni moja wapo wa dalili za mwanzo kabisa nilizokuwa naziona kwa mwanangu.

Hiyo ni degedege na wataalamu wanasema ndiyo huzidi kuuvuruga ubongo wa mtoto muwahishe kuna dawa atapewa zitamsaidia though umechelewa kidogo,kijana wangu nilimuanzishia matibabu pale MNH akiwa na miaka 2 yalimsaidia sana kwa kumuangalia mtu hawezi kumjua mpaka amuulize kitu ndiyo atagundua.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…