Mwanao anaongoza darasani au alikua anaongoza, nini ulifanya kufanikisha hilo?

Mwanao anaongoza darasani au alikua anaongoza, nini ulifanya kufanikisha hilo?

Sikuwa napenda kusoma kwa kuumiza kichwa au kukariri..nilikuwa nasoma nielewe hivyo sikuwahi kuwa na alama za juu sana lakini sikuwahi kufeli..hiyo ndio kanuni yangu ya Maisha hadi leo.
Wanangu kwa alama zozote wanazopata nawapongeza na kimsingi naangalia wastani wao na upeo wao wa kuelewa mambo kwa ujumla wake na sio wako nafasi ya ngapi.
 
Kufika elimu ya juu siyo kwamba ndiyo ulikuwa na akili sana hapana
Umesoma shule gani?
mzazi wako alikuwa anatambua umuhimu wa elimu kiasi gani?


Sent from my TECNO KC8 using JamiiForums mobile app
Kama huna akili hata usome cambridge hufiki kokote ,mzazi kutambua umuhimu wa elimu hakumsaidii mtoto kilaza,akili ni vipaji vya kurithi genetically inherited
 
Kama ni kilaza focus na kipaji chake usimpotezee mtoto muda maana elimu yetu haina maana sana sikuhizi! Kazi hamna mtoto unamkalisha darasani miaka 17 ni upuuzi tu
Leo itakuwa hujalala aiseee!!! Wewe umesoma mpaka elimu imekuwezesha kujiunga JF halafu unawazuia wengine wasiipate elimu!??? Au ndiyo yale ya mtumwa mfiche kitabu asikisome!???
 
Mkuu, badala ya kufikiria nafasi ya kwanza mpaka ya tatu hebu jaribu kumfundisha mwanao namna ya kusoma mwenyewe na kuelewa......

Hujaainisha mwanao ni level gani ya elimu ila kuanzia secondary inabidi umfundishe mwanao kujitegemea kujisomea na kuelewa mambo kisha akuelezee alichoelewa( kama naww huelewi ni kipengele kingine). Kwa upande wangu niliweza kujisomea isipokuwa mathematics na physics hayo nilifundshwa.

Mfundishe asome vitu kabla hawajasoma darasani na avielewe vizuri kwa sababu akianza kufundshwa ataelewa zaidi ya alichosoma akiwa mwenyewe.

Kingine waacheni watoto wajifunze mambo mengi kama kusoma vitabu mbali na shule, kutembea sehemu tofauti tofauti, kukaa na wengine kupiga story japo kwa muda mchache lakini pia kuangalia tv vipindi tofautitofauti hii itawapa uwezo wa kufahamu mambo mengi. Kwenye kujisomea kuna kitu cha kufananisha taarifa mpya na ambayo umewahi kuiskia awali hivyo inaongeza kumbukumbu kwa mtoto.

Mimi, sikuwahi toka top ten ya darasani na hata mitihani yangu yote ya taifa kidato cha 4 na 6 nilifaulu vizuri kwa baadhi ya njia nilizoainisha hapo juu.
 
hahaha sijui umewaza nini ila upo sahihi, inawezekana nafasi ya juu kwenye wanafunzi 20 au 40
Suala siyo idadi ya wanafunzi, bali kiwango cha ufaulu. Unaweza kuwa wa mwisho kati ya wanafunzi 200, lakini yule wa kwanza amekuzidi alama ^tar-know^ au ^sea-tar^ au ^sir-bar^!!! Anyways, namba moja ni namba moja tu.
 
Kama huna akili hata usome cambridge hufiki kokote ,mzazi kutambua umuhimu wa elimu hakumsaidii mtoto kilaza,akili ni vipaji vya kurithi genetically inherited
Na mazingira yana mchango mkubwa katika kuinoa akili ya mtoto. Mfano, inaweza kuwa mbegu bora, ikapandwa kwenye udongo usiyo na rutuba matokea yake ni kuzaa mazao hafifu (kukosekana palizi=malezi bora).
 
Mimi nilikua naongoza kuanzia vidudu hadi olevel lakini high school nikawa nakua wa mwisho unaniweka kundi gani?

Chuo nikawa nikaongoza darasa zima mwaka wa kwanza halafu miaka 2 iliyofuata nikawa naambulia C nakua kundi gani?

Kwenye interview za ajira zote zilizofanya kubwa kubwa nikawa nakua wa kwanza halafu choka mbaya taasisi inapumulia mashine nikawa nakua wa mwisho nakua kundi gani?
Unaweza ukawa wa mwisho kwenye darasa lenye watanfunzi wenye akili sana au ukawa wa kwanza kwenye darasa la wajinga.
 
Kama huna akili hata usome cambridge hufiki kokote ,mzazi kutambua umuhimu wa elimu hakumsaidii mtoto kilaza,akili ni vipaji vya kurithi genetically inherited
Yaani mtu aende mpaka Cambridge kusoma ama akutane na walimu wa Cambridge, halafu unasema hajafika kokote!??? Remember kuna watu miaka yao ^see-tea-knee^ ama ^sir-bee-knee^ duniani, lakini hawajawahi hata kufika mtaa wa saba pale maeneo.
 
Na mazingira yana mchango mkubwa katika kuinoa akili ya mtoto. Mfano, inaweza kuwa mbegu bora, ikapandwa kwenye udongo usiyo na rutuba matokea yake ni kuzaa mazao hafifu (kukosekana palizi=malezi bora).
Ni kweli sasa huyu mtoa post inaonekana kila kitu kipo sawa ila mtoto kilaza,hapo ajitathmini yeye na mama watoto wake kichwani zilikwemo?ni sawa wewe unataka mwanao awe footballer bila kuwa na kipaji,atachemsha tu
 
, mdogo wangu alikua anashika nafas ya kwanza kwanzia darasa la 1 had la 3 kati ya wanafunzi 80 darasani ila alivyo hamishwa shule akaanza kuwa wa 13+ kat ya watoto 40 hajawahi kuwa ndan ya top 10
Lakn uwezo huo huo alio nao akirudishw kule alipotoka atawaburuza tena inategemeana anaoshindana nao wana uwezo kiasi gani
 
wa mwisho kwenye majiniazi au wa mwisho kwenye vilaza?
Inategemea na walimu wanaofundisha na kusahihisha mitihani yao; kuna watoto ni so smart kiasi kwamba walimu wao wanashindwa kuhendo material yao, wanadhani wako OP. Haishangazi TO Elias Kihombo alifelishwa pale mahali mara kadhaa 🙂
 
Mie hata simfatilii na sinaga huo muda kabisa ila ndo hivo wa kwanza au wapili akishika watatu atarudi nyumban na kilio halaf m namshangaa sa unalia nini?

inaonekana hiyo tabia ya kufaulu kwa kiasi hicho hajairithi kwako kabisaaa kwa hiyo jitahidi tu kumuelewa
 
Unaweza ukawa wa mwisho kwenye darasa lenye watanfunzi wenye akili sana au ukawa wa kwanza kwenye darasa la wajinga.
Nilichokuja kugundua baadae elimu ya high school na kuendelea inataka mtu wa kukariri sana, msuli mkubwa hadi unatoboa usiku. Hicho kitu kilinishinda.

Nashukuru kwamba C zangu nilikua nazifidia na vitu vingine nje ya shule ambavyo ndio vimenisaidia sana.

Mfumo wetu wa elimu ni wa hovyo sana, unatujenga kukariri tuuu na kufaulu mitihani badala ya kutupatia skills za kupambana na maisha.

Huku mtaani ama hata kazini As hazihitajiki kabisa, watu wanachotaka ni wewe kua na uwezo na skills za kufanya kazi inayohitajika kwa viwango vinavyohitajika.

Nakumbuka nimewahi kufanya kazi moja na watu waliosoma Malaysia, Uk, France, Netherlands na Kenya, nikafanya poa sana hadi wasimamizi wakaniuliza kama nimesoma nje ya nchi, nikawaambia hapana. Hawakuamini na wala hawakutegemea kama ningeweza kufanya vile. Sasa hizo skills na capabilities nimezijenga mwenyewe, sikuzipata chuoni wala high school.

Vijana wanamaliza vyuo vikuu reasoning hakuna, analytical skills hakuna ila wana As nyingi.

Tubadili mfumo wa Elimu.
 
Leo itakuwa hujalala aiseee!!! Wewe umesoma mpaka elimu imekuwezesha kujiunga JF halafu unawazuia wengine wasiipate elimu!??? Au ndiyo yale ya mtumwa mfiche kitabu asikisome!???
Elimu ya kufungua jf sio zaidi ya form 4
 
Sasa mbona hizo nafasi za kwanza mie sijawahi kuzipata

Ama familia yako umemanisha wewe na mke wako?mie umenitoa 😢
Oooh babe usihuzunike. Unajua vile ww ni mimi na mm ni ww. Nikishinda mimi inatosha na ww umeshinda.😉😉
 
Back
Top Bottom