TANZIA Mwanasheria Mkuu wa Kwanza Mzalendo na Jaji Mstaafu Mark Bomani afariki dunia

TANZIA Mwanasheria Mkuu wa Kwanza Mzalendo na Jaji Mstaafu Mark Bomani afariki dunia

R.I.P Kwake, poleni sana Familia nzima ya Mzee Bomani tupo pamoja. Kuna Mtu wangu Mmoja wa muhimu 'Maishani' mwangu yawezekana huu mwaka ukawa ni mgumu sana Kwake kwani karibia 'Marafiki' zake wote wa karibu na aliowahi kufanya nao Kazi Serikalini na ' Urafiki' wao ulikuwa unakaribia wa 'Kindugu' akina Rais Mstaafu Mkapa na leo hii Mzee Bomani wamefariki dunia. Nendeni Wazee wangu ( Wetu ) Bomani na Mkapa.
Uzandiki wa kishamba usio na tija.
 
Kazaliwa 1943.

Jaji mkuu 1965.

Akiwa na miaka 22.
 
Unajua BAKWATA ilianzishwajee wewe sukule?
Hivi mmeokotwa wapi nyie takataka?
Mamuijui historia ya nchi yenu na wala hamsomi maandiko mbalimbali ili kupanua ufahamu wenu!
Viumbe wa ajabu sana wana mbogamboga.
Kwa hiyo umekuja na mitusi?
 
Pumzika kwa amani Jaji Mark Bomani. Hakika ulikuwa muungwana na uliishi maisha ya kistaarabu sana.
 
Mwanao kama unampenda kuna kazi usimuruhusu kusomea ikiwemo u_Polisi na u_Hakimu ...

kuna machozi ya watu mengi sana nyuma ya hizi kazi ambayo mwisho wake inakua ni laana ...
 
Jaji mstaafu Mack Bomani aliye kuwa mwana sheria mkuu wa serikali wa kwanza wa seriya tanzania amefariki dunia.

Amefia ktk hospital ya taifa ya Muhimbili.

Mungu alitoa Mungu ametwaa jina lake lihimidiwe

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Pigo kubwa sana , nakumbuka kaka yake aliyeitwa Paulo alishirikiana na Mwl Nyerere kuanzisha BAKWATA
Mkuu upo deep sana!!! Mwl alikuwa na hekima kubwa kutumia watu brain kufanikisha mambo. Juzi Sengerema msafara JPM Shehe wa wilaya ( Bakwata) sala yake ilikuwa kama vile kuapishwa kwa Rais mteule na kukandamizia na ombi la msikiti wa Kisasa wa Wilaya.
 

Habari zilizotufikia ni kwamba Mwanasheria Mkuu wa Tanzania, Jaji Mark Bomani amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Septemba 11, 2020, katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Mtoto wake amethibitisha kifo hiki. Shughuli za msiba zipo nyumbani kwa Marehemu Mikocheni jijini Dar es Salaam.
View attachment 1565939
Jaji Mstaafu Mark Bomani enzi za uhai wake akiwa na mkewe wakikata keki katika hafla ndogo ya kusherehekea miaka 50 ya ndoa yao mwaka 2017

WASIFU WAKE KWA UFUPI

Mzaliwa wa Pemba, Zanzibar. Mwanasheria Mkuu wa 2 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mzawa wa kwanza kushika wadhifa huo. Kwa miaka 11 alisimama kidete kuitetea serikali ya Mwl. Nyerere. Jana, Septemba 10, 2020 amemaliza kazi aliyotumwa duniani.

Alizaliwa mwaka 1943 huko wilayani Wete kisiwani Pemba, Zanzibar. Elimu ya msingi alipatia huko huko kabla ya kujiunga na shule ya sekondari ya wavulana ya Tabora, Tanganyika. Baadae alienda nchini Uganda na kujiunga na elimu ya juu katika Chuo Kikuu cha Makerere.

Aliporudi masomoni, Mark Boman alijiunga na chama cha TANU na mwaka 1965, Mwalimu Nyerere alimteua kuwa Mwanasheria mkuu wa Serikali ya Tanzania. Alikuwa Mtanzania mzawa wa kwanza kushika nafasi hiyo aliyohudumu mpaka mwaka 1976

Baada ya kazi ya Serikali, Mark aliteuliwa na kuwa mshauri mkuu wa maswala ya kisheria wa umoja wa mataifa nafasi aliyohudumu kwa takribani miaka 14 (1976 - 1990), akishiriki vyema katika michakato iliyopelekea kupatikana kwa uhuru wa nchi za Namibia na Afrika Kusini.

Moja kati ya huduma kubwa za kimataifa alizowahi kuzifanya ni kushiriki katika majadiliano ya amani baina ya pande mbili wakati wa vita ya kwanza ya wenyewe kwa wenyewe nchini Burundi. Mark, alikuwa Katibu mkuu wa Mwl. Nyerere na Mzee Mandela wakati wote wa zoezi hilo.


Baadhi ya mada kuhusu Jaji Bomani
> Jaji Mark Bomani: Serekali 2 au 3 zisijadiliwe kwenye Bunge la Katiba!
> Jaji mstaafu Mark Bomani naye atoa mpya..
> Jaji Mstaafu Mark Bomani akataa Tanzania kuitwa Tanzania Bara, ataka iitwe Tanganyika
> Jaji Mark Bomani: Ni vizuri kukawepo kura ya maoni kuhusu Muungano (Referendum)
> Jaji Mstaafu Mark Bomani aunga mkono Serekali 3 asema wasemao ni harama hawana mashiko
> Muungano lazima ujadiliwe kwa Ukweli na Uwazi! - Jaji Mark Bomani
> Jaji Bomani: Wageni wanaimaliza nchi kupitia sekta ya madini
> Jaji Bomani apigilia msumari Katiba Mpya
> Jaji Bomani: ZEC imejipunguzia imani
> Jaji Bomani awachafua wazanzibari
> Bomani: Gamba litapasua CCM

RIP Judge Mark Boman.
 
Back
Top Bottom