TANZIA Mwanasheria Mkuu wa Kwanza Mzalendo na Jaji Mstaafu Mark Bomani afariki dunia

TANZIA Mwanasheria Mkuu wa Kwanza Mzalendo na Jaji Mstaafu Mark Bomani afariki dunia

Umemaliza mwendo babu Judge Mark Bomani RIP, Poleni familia ya mwendazake pamoja na marafiki zake wote wa karibu kama Judge Joseph S. Warioba, Amb. Juma V. Mwapachu & co.

Makubwa aliyoshiriki ktk nchi yetu ni mengi ikiwa pamoja na hili rasimu ya serikali tatu ya shirikisho yafafanuliwa serikali ya Muungano, serikali ya Tanganyika na serikali ya Zanzibar na sababu ya iwe Tanganyika na siyo Tanzania Bara jjaji mstaafu Mark Bomani anafunguka: Published on 15 Jun 2013 The United Republic of Tanganyika and Zanzibar The United Republic of Tanganyika and Zanzibar is renamed United Republic of Tanzania | South African History Online :
RASIMU YA KATIBA MPYA TANZANIA--SERIKALI TATU --NA MARK BOMANI


  1. Magawanyo wa serikali 3
  2. Mabunge matatu
  3. Mipaka na majukumu ya hizi serikali
  4. Mkokoteni mbele ya farasi na itegemewe farasi auvute mkokoteni huu
  5. Kitendawili cha mkokoteni mbele ya farasi kwanza kipatiwe ufumbuzi na kura za maoni za wananchi na siyo kufanyiwa uamuzi na viongozi
  6. Na kama wananchi wataweza wanautaka basi waseme kwa uhuru kabisa pia kinyume chake kama hauwataki wauseme kwa uhuru kabisa
  7. Viongozi kusema mfano Wazanzibari hawautaki huu Muungano, lini waliulizwa hivyo?
  8. Uraia wa jumla au wa sehemu yaani uTanganyika au uZanzibari ndani ya Muungano
  9. Cold War : Uhusiano wa kimataifa 1964 : Dar es Salaam waliegemea Magharibi wakati Zanzibar waliegemea Mashariki
  10. Gharama za serikali 3 ni mzigo au la ? Ni kujipanga zaidi au vipi? Mfano wenzetu Kenya wana serikali 47 za county pamoja na mabunge 47 ya county lakini mambo yanaendelea vipi kuhusu huku kwetu serikali 3?
 
Miaka 50.jpg
nimevutiwa na background
 
Mark bomani na paul bomani wanaundugu au ni majina tuh kufanana??
 

Habari zilizotufikia ni kwamba Mwanasheria Mkuu wa Tanzania, Jaji Mark Bomani amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Septemba 11, 2020, katika Hospitali ya Taifa Muhimbili.

Mtoto wake amethibitisha kifo hiki. Shughuli za msiba zipo nyumbani kwa Marehemu Mikocheni jijini Dar es Salaam.
View attachment 1565939
Jaji Mstaafu Mark Bomani enzi za uhai wake akiwa na mkewe wakikata keki katika hafla ndogo ya kusherehekea miaka 50 ya ndoa yao mwaka 2017

WASIFU WAKE KWA UFUPI

Mzaliwa wa Pemba, Zanzibar. Mwanasheria Mkuu wa 2 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na mzawa wa kwanza kushika wadhifa huo. Kwa miaka 11 alisimama kidete kuitetea serikali ya Mwl. Nyerere. Jana, Septemba 10, 2020 amemaliza kazi aliyotumwa duniani.

Alizaliwa mwaka 1943 huko wilayani Wete kisiwani Pemba, Zanzibar. Elimu ya msingi alipatia huko huko kabla ya kujiunga na shule ya sekondari ya wavulana ya Tabora, Tanganyika. Baadae alienda nchini Uganda na kujiunga na elimu ya juu katika Chuo Kikuu cha Makerere.

Aliporudi masomoni, Mark Boman alijiunga na chama cha TANU na mwaka 1965, Mwalimu Nyerere alimteua kuwa Mwanasheria mkuu wa Serikali ya Tanzania. Alikuwa Mtanzania mzawa wa kwanza kushika nafasi hiyo aliyohudumu mpaka mwaka 1976

Baada ya kazi ya Serikali, Mark aliteuliwa na kuwa mshauri mkuu wa maswala ya kisheria wa umoja wa mataifa nafasi aliyohudumu kwa takribani miaka 14 (1976 - 1990), akishiriki vyema katika michakato iliyopelekea kupatikana kwa uhuru wa nchi za Namibia na Afrika Kusini.

Moja kati ya huduma kubwa za kimataifa alizowahi kuzifanya ni kushiriki katika majadiliano ya amani baina ya pande mbili wakati wa vita ya kwanza ya wenyewe kwa wenyewe nchini Burundi. Mark, alikuwa Katibu mkuu wa Mwl. Nyerere na Mzee Mandela wakati wote wa zoezi hilo.


Baadhi ya mada kuhusu Jaji Bomani
> Jaji Mark Bomani: Serekali 2 au 3 zisijadiliwe kwenye Bunge la Katiba!
> Jaji mstaafu Mark Bomani naye atoa mpya..
> Jaji Mstaafu Mark Bomani akataa Tanzania kuitwa Tanzania Bara, ataka iitwe Tanganyika
> Jaji Mark Bomani: Ni vizuri kukawepo kura ya maoni kuhusu Muungano (Referendum)
> Jaji Mstaafu Mark Bomani aunga mkono Serekali 3 asema wasemao ni harama hawana mashiko
> Muungano lazima ujadiliwe kwa Ukweli na Uwazi! - Jaji Mark Bomani
> Jaji Bomani: Wageni wanaimaliza nchi kupitia sekta ya madini
> Jaji Bomani apigilia msumari Katiba Mpya
> Jaji Bomani: ZEC imejipunguzia imani
> Jaji Bomani awachafua wazanzibari
> Bomani: Gamba litapasua CCM
Pumzika kwa Amani Mzee wetu
 
Hali si hali watu, watanzania baadhi kama siyo wote wamechoka, kufuatia kifo cha Jaji mstaafu Mark Bomani, hii ni tweet ya rais wa Tanzania;

"Nawapa pole familia na wote walioguswa na kifo cha Jaji Mstaafu Mark Bomani. Nitamkumbuka kwa mchango wake mkubwa Serikalini katika masuala ya sheria na katika chama akiwa Mjumbe wa Baraza la Wadhamini wa CCM. Mwenyezi Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi, Amina."

Baada ya tweet hiyo hapa chini ni baadhi ya comments za wananchi wake wakimpa pole
😂...
Screenshot_20200911_204427.jpg



Moderator au Mhariri huu uzi haukutakiwa kuunganisha hapa, mnakosea sana sana 😡, hii mafa hai ingiliani na hii mlipoiweka.

Muwe fair na mnachosha kiukweli, please muiondoe kwenye bandiko hili na mnajua ila mnajifanya hamjui.

Mmeondoa nilichokusudia ili muiunganishe hapa ili content zifanane how come mh?
 
Hali si hali watu, watanzania baadhi kama siyo wote wamechoka, kufuatia kifo cha Jaji mstaafu Mark Bomani, hii ni tweet ya rais wa Tanzania;

"Nawapa pole familia na wote walioguswa na kifo cha Jaji Mstaafu Mark Bomani. Nitamkumbuka kwa mchango wake mkubwa Serikalini katika masuala ya sheria na katika chama akiwa Mjumbe wa Baraza la Wadhamini wa CCM. Mwenyezi Mungu aiweke roho yake mahali pema peponi, Amina."

Baada ya tweet hiyo hapa chini ni baadhi ya comments za wananchi wake wakimpa pole 😂...

View attachment 1566754
CCM IMECHOKWA
 
Mwenyewe nilizipitia hizo comments nikajiuliza Magu sijui kitu gani kinamfanya afikiri anapendwa, raia wamemsiliba haswa!
Kwani duniani wavuta bangi wanakosa?
Pamoja na yesu kuponya na kufufua watu lakini wachawi wakataka afe, sasa wewe unashangaa nini?
 
Back
Top Bottom