Mwanasheria Mkuu: Wabunge wa CHADEMA wa Viti Maalumu waliapishwa kwa mujibu wa Sheria na Katiba, CHADEMA isiwaguse

Hawa jamaa wako desperate na hela za mabeberu mpaka wanafanya upuuzi uliopitiliza!
 
AG ajibu hoja za Katibu Mkuu Mnyika kama alivyoweka wazi kwenye press conference. Nyaraka zile zilizopo NEC zenye majina, sahihi na mihuri nani kagushi? Kamati kuu ya chama imekaa lini kuteua majina?
Siyo anatoa jibu la jumla kama anawajibu watu sokoni.
 
Nasema kesho sitakosa bando, haya maisha yako kasi mno.
 
Hahahahaha mbn unasikitika Sana? au umeanza kuona dalili kuwa CDM iko thabiti
Mwaka jana kulivuja sauti ya wabunge wa Chadema Said Kubenea na Anthony Komu wakipanga njama za kumuuwa Boniface Jacob ili hatimae wafanikishe adhima yao ya kumng'oa Freeman Mbowe kwenye uenyekiti wa chama.....
 
Inavyoelekea chama tawala kinafanya kila namna ili CHADEMA iwafukuze wakina Halima. Wanafanya hivi kwa sababu wakishafukuzwa, watabaki bungeni kwa ridhaa ya chama tawala na hivyo hawatakuwa na uhuru wa kusema au kufanya wanachotaka maana chama tawala kikiamua kuwa hawana tija hawatakuwa na pa kukimbilia.

Kama CHADEMA hakitawafukuza, Chama tawala kitakuwa hakina leverage juu yao na hivyo wataweza kuendelea kujinasibu kama wapinzani. Lakini kwa namna ambavyo wameonekana kukubali kukumbatiwa na Chama Tawala baada ya kuapishwa, kama watakataa kuachia ubunge wao, hata kama Mbowe atakuwa anawaonea huruma , chama chao kitakuwa hakina jinsi ila kuwafukuza.

Watafukuzwa lakini watabaki bungeni kwa ridhaa ya Tume na Spika ila kila mtu atajua wao ni sehemu ya Chama Tawala na hivyo watakosa legitimacy hata wakijitahidi kuisimamia na kuikosoa serikali maana itajulikana kuwa ni maigizo tu maana mwisho wa siku kura zao hazina uzito.

Aidha, itawabidi wakubali kutumiwa kukichafua chama chao cha awali, kitu ambacho kitazidi kuwaharibia. Wakati huo huo wafia chama wa CCM hawatakuwa na imani nao maana watajua kuwa mwaka 2025 watawanyang'anya nafasi zao. Hii miaka mitano watavuna, wote watakuwa mawaziri vivuli, kiongozi wao atakuwa KUB lakini baada ya hapo watakuwa na wakati mgumu sana.

Ukweli mwingine ni kuwa kuna wanawake wengi wenye uwezo walikuwa wanatamani nafasi zao ndani ya chama chao lakini walishindwa kutoboa kwa jinsi walivyokuwa wamejijenga kwa jamii na uongozi wa chama. Hii ndio nafasi yao ya kuchukua nafasi hizo na hawata jivunga.

Amandla...
 
AG anazidi kuwachoresha CCM.
Wataguswa kwa barua ya kutimukiwa ili akae nao hapo bungeni kama wabunge wa mataga.
 
Hao ni wabunge halali lazima AG awalinde
 
The thing is katika taasi ya CHADEMA kuna watu wakubwa kuliko taasisi yenyewe , hiki kitu siyo rahisi kukikuta katika taasisi zinazo jielewa

Hapo kifuatacho ni kalipio kali basi (msitegemee kusikia akina halima wamefukuzwa , )

[emoji1787][emoji1787]
 
Yupo katikati ya sheria!
AG aendelee kufuata maelekezo ya pombe na Chadema waachwe wafate katiba ya nchi pamoja na katiba yao kuwashughulikia wanachama wao afu wakutane na huyo Ag katikati ya sheria....Covid 19 itokomezwe Chadema....hakuna namna.
 
Hakuna MTU mkubwa kuliko taasisi...
 
Mwaka jana kulivuja sauti ya wabunge wa Chadema Said Kubenea na Anthony Komu wakipanga njama za kumuuwa Boniface Jacob ili hatimae wafanikishe adhima yao ya kumng'oa Freeman Mbowe kwenye uenyekiti wa chama....
Hushangai kwamba serikali haijakanusha tuhuma nzito za CHADEMA ? Hiyo ndiyo habari kuu
 
Kwani Chadema iko juu ya sheria?

Kwani AG anawashwa washwa nini si taratibu zote za kisheria zilifuatwa namely:

1. Kamati kuu ya CDM iliwapitisha.
2. Forms zao zina baraka zote za CDM.
3. Katibu mkuu CDM aliwasilisha majina yao kwa mkurugenzi wa tume Dr. Mahera.
4. Supika akapata majina tokea tume.
5. Supika akawaapisha.
6. Nao wakaishukuru CDM na Mbowe.

Wanaitwa kuhojiwa kuhusu hayo yeye AG anawashwa washwa?

Asubirie sindano imwingie.

Itapendeza zaidi Lissu akihudhuria kikao cha kesho hata kwa voice link achilia mbali video.

Aluta continua!
 
Wacha uongo mbona walitoa tamko tangu juzi tenalimo humu JF.
 
Wabunge wanachapa kazi. Kongole halima mdee
Your browser is not able to display this video.
 

Wale walikubali makosa na kuomba msamaha kuwa hawatarudia tena na hao kama wanakunali makosa na kujibua ubunge watasamehewa maana chama kitakuwa hakijawa sehemu ya wizi wa kura
 

Mfumo dume Kwani hao akina Mdee walikuwa wanaume walipo kuwa CHADEMA na sasa ndo wamekuwa wanawake. Kama kuna mfumo dume mbona wote walipewa majimbo ya kugombea. Wanaacha kuhangaika na adui wa nchi hii sasa wanahwanyika wao. Fukuza wote kesho hakuna kitu kitatokea na huyo AG hili halimuhusu anayetakiwa kusemea ni Mahela siyo yeye
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…