Mwanaume anaetumia TikTok na Instagram huwa napata mashaka na jinsia yake

😀😀😀tuambie kwanza wewe unachotumia hapo ndiyo kikao kitaanzia
 
Yaani niache kuona vidada vikikata viuno tiktok nikusikilize wewe..

Acha hizo mara moja aisee..

Tusipangiane maisha.
 
Yaani babu upo sahihi kabisa kabisa kabisa ningekupa like hata milion nane kama inawezekana mwanaume uliotimia huwez kua tiktok au insta wengi wao wana matatizo kiafya kiakili na hata kimwili ukikosa yote hayo ujue anapend umbea yupo kama demu au mshamba
 
Mimi nipo tiktok, mbona sijaona umbeya kule, upo sehemu gani? Kule kuna clip za vichekesho na mziki. Ni kweli unaijua tiktok au umesimuliwa tu?
 
Kuna kitu mnatakiwa kujifunza.

Ule ni mtandao, kuna kila aina ya vitu, umachagua unachotaka, ukitaka Mpira upo, ukitaka biashara zipo, ukitaka misosi ipo, UNACHAGUA.

Mimi nipo tiktok ila sijui kama Mange naye yupo kule sababu sina interest naye!
 
Kuna jamaa flan wa interior design na wale wafuga samaki wapo Insta huko..hahaha moja nime apply pahala fundi kakimbia...[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]mbele watu wanajenga Nyumba aiseee....
Sana mkuu
Kuna mambo ya kila aina na mafunzo na hobbies za kila aina ni wewe tu

Miaka ya nyuma yaani zamani sana nilikuwa mdau wa racing cars
Sasa huwa nakumbushia kujiangalia kwenye Arab drifting hapo ndio utaona ukichaa wangu Enzi hizo yaani kukimbia 160mph ni kawaida sana [emoji1] [emoji1787]
 
Saafi sana Mkuu....
Kuna kazi nakueleza mafundi wamezikimbia...hii yote ni kuona vya wenzetu na kujifunza.
Huku Tiktok ndio usiseme kabisa..unafuata watu wako kadhaa then unaangalia pa kuchekea maisha yanaenda.
 
Yani wewe Ni obviazi kabisa😁😁 vijana wa ovyo nchini Ni wengi

Kwa hio team cruiser wawepo twitter mbona hizo mitandao Ni tofauti kabisa ...haya mafunga sound kwenye magari nao wawepo twitter Yani bidhaa zao wa tweet huko hivi una elimu wewe kiazi? Nauliza Tena..je Elon musk nao wanaona hao kina mange kila waking au page za udaku?je kwann wewe unaona😁 Yani wewe elimu huna
 
Kuna kitu watu hawajui social media huwa zinakuletea vitu kutokana na vile unavopenda. Mfano unapenda umbea unafungua kila saa.
Kweli kabisa yaani unachoweka na kuwaza ndio utaangalia
Ila kuna vijana wanafikiri Insta ni kuangalia makalio tu

Hawajui kuwa wanaweza kuwa wajuzi wa mambo mengi sana
Namjua mdada mmoja ame trend kwa kutengeneza cake zinazofanana na bidhaa nyingi sana na ameanza akiwa nyumbani
Yaani geti kali haswa ila kwa sasa anaingiza hela balaa anitwa Ahlam al najdi
Kuna wengi mafundi wanaingiza hela sana
Kila kitu ukitaka unapata
 
Saafi sana Mkuu....
Kuna kazi nakueleza mafundi wamezikimbia...hii yote ni kuona vya wenzetu na kujifunza.
Huku Tiktok ndio usiseme kabisa..unafuata watu wako kadhaa then unaangalia pa kuchekea maisha yanaenda.
[emoji38] [emoji23] [emoji38]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…