Mwanaume andaa future nzuri kwa wanao, ila usitegemee lolote kwa wanao

Mwanaume andaa future nzuri kwa wanao, ila usitegemee lolote kwa wanao

Kuna wazee wanaomba pesa Kwa watoto wakati alipokea mafao na hukuwapa hata Senti Moja watoto na mafao yote Kwisha. Watoto pia wanafamilia na wanamajukumu ya kipesa. Mzazi anakuwa anasumbua watoto wakati hakujiandaa na maisha ya uzeeni. Tengeneza maisha Yako bila kuja kutegemea watoto wakuletee chakula. Wengi hujisahau na kuona kuwa akipata pesa ya mafao ndiyo ataanza kuwekeza. Wekeza ukiwa Bado kwenye mzunguko wa pesa. Unakuta mtu anajenga nyumba ya kwenye kiwanja Cha 20 Kwa 20 na Hana hata uwezo wa kulima mchicha. Tafuta shamba kubwa nje ya mji au kijijini Anza kuwekeza kidogo kidogo mifugo na kilimo na siku ukistaafu unakwenda kuishi huku. Huwezi kutegemea kulishwa na watoto.
Haya ndio mawazo chanya yatayopelekea kuwa na Uzee mwema...ur smart
 
Mwanaume tafuta pesa kwa bidii, wape watoto elimu bora, wape mahitaji yao muhimu, jenga nyumba nzuri waishi vizuri, lakini ukizeeka usitegemee lolote kutoka kwa wanao.

Enjoy maisha ya uzee kwa pesa zako mwenyewe ulizochuma ujanani.
Ndugu yako pekee wa uzeeni ni hadhina uliyojiwekea ujanani
 
Mwanaume tafuta pesa kwa bidii, wape watoto elimu bora, wape mahitaji yao muhimu, jenga nyumba nzuri waishi vizuri, lakini ukizeeka usitegemee lolote kutoka kwa wanao.

Enjoy maisha ya uzee kwa pesa zako mwenyewe ulizochuma ujanani.
Wakati mwingine sisi MADINGI tunazingua sana.

Mtoto akikwambia hana pesa basi unakasirika..
 
Na huo ndio ukweli sasa ninyi endeleeni kukataa ndoa na kujaza single mothers mitaani mkifikiri mnawakomoa wanawake, fainali uzeeni mwisho wa siku mama atabaki na watoto wake watamlea wakati baba atabaki na malaya wake aliokuwa anawanunua, mnaacha kutulia na familia zenu na kuwapa muda wake zenu na watoto wenu mnajikuta miamba kuzini na malaya na kulewa na washkaji kila siku
Huu ni ukweli mchungu.

Tafiti zinaonyesha watoto wengi wazee wao wanapokuwa wazee huwa wanamsahau baba. wengi ni sababu ya kukosa bond ya baba tangu wakiwa wadogo.

Fainali uzeeni wataelewa nini maana ya ndoa.
 
Mwanaume tafuta pesa kwa bidii, wape watoto elimu bora, wape mahitaji yao muhimu, jenga nyumba nzuri waishi vizuri, lakini ukizeeka usitegemee lolote kutoka kwa wanao.

Enjoy maisha ya uzee kwa pesa zako mwenyewe ulizochuma ujanani.
Fact
 
Wewe ni utakuwa baba msumbufu uzeeni... huwezi sema unaivest Kwa mtoto, mtoto ni jukumu lako la lazima,maana ulimleta Kwa Raha zako...
Unakunywa kinywaji gani,? Kaa agiza njoo DM nilipie.

Mtoto ni zao la wazazi, na ni jukumu lao mpaka siku yule mtoto ajitegemee na hata akishindwa inabidi wazazi wamlee bila kipingamizi.

Nakupa dole gumba, Mtoto sio majukumu yake kumsaidia mzazi, na hata asipofanya hivyo hana hatia, kibinadamu, kibiblia na kama kuna moto huko mbinguni, hatochomwa.
 
Issue hapa napingana na mtoa mada anaposema
==Mwanaume tafuta pesa kwa bidii, wape watoto elimu bora, wape mahitaji yao muhimu, jenga nyumba nzuri waishi vizuri, == mpaka hapa ni sawa! Huo ndiyo uanaume.

Nampinga kwa nguvu zote kuanzia hapa lakini ukizeeka usitegemee lolote kutoka kwa wanao. Hasa neno USITEGEMEE. Investment ni risk inajulikana na ndiyo maana unazaa watoto wengi ili angalau upate wa kukufaa.
Mtoto si investment.

Ukimlea mtoto kama investment unafanya biashara ya utumwa iliyochangamka tu.

Ukimlea mtoto ili aje kukufaa unafanya biashara ya nipe nikupe, ila wewe unageuza tu kufanya "nakupa ili unipe".

Kulea mtoto na kumpa mazuri si biashara, ni wajibu wa kizazi katika familia.

Ndiyo maana unatakiwa kumlea mtoto vizuri hata kama ana matatizo ya akili na hawezi kukusaidia lolote.

Ndiyo maana unatakiwa kumlea mtoto vizuri hata kama ana ugonjwa utakaomfanya afe miaka mingi kabla yako.

Msilinganishe kulea mtoto na inbestment au biashara, mnatukanisha wajibu wa kizazi na kifamikia wa kulea mtoto ambao umepita bishara na investment.
 
Kwa Nini umtegemee mtoto acheni zenu bwana nyie ndio mnakuwa wazee wasumbufu mkiendekeza hayo mawazo,andaa vitega uchumi vyako mtoto umtegemee akupe msaada wa Hali sio mali...Hivi hamuoni wenzetu kina Mo Dewji wanavyoenjoy kisa kuwa na Babu wenye akili ,,, acheni mawazo ya kizembe eti nizae watoto wengi Ili nipate wa kunisaidia uzeeni!hayo ni mawazo duni sana
Waafrika wengi bado wanafanya biashata ya utumwa.

Wanawauza watoto wao wa kike ili kupata mahari.

Hata wakiwalea watoto wao, wanawalea kibiashara, kimkakati, wakifikiri "namlea huyu aje kunisaidia baadaye".

Ni muendelezo wa biashara ya utumwa tu.
 
Waafrika wengi bado wanafanya biashata ya utumwa.

Wanawauza watoto wao wa kike ili kupata mahari.

Hata wakiwalea watoto wao, wanawalea kibiashara, kimkakati, wakifikiri "namlea huyu aje kunisaidia baadaye".

Ni muendelezo wa biashara ya utumwa tu.
Kuna Mmoja amekazana eti zaa watoto wengi ni investment....Kweli huu ni utumwa mamboleo
 
Kuna Mmoja amekazana eti zaa watoto wengi ni investment....Kweli huu ni utumwa mamboleo
Waafrika wengine huwa eti na sisi tunashangaa kwa nini hatuendelei ? 🤣🤣🤣

Kwa mawazo kama haya mpaka leo?

Yani hatujaweza kitu cha msingi cha kuheshimu utu wa mtu, hata mtoto wako mwenyewe.

Yani unamnyima mtoto haki yake ya kuishi anavyotaka, unamvika mzigo wa kukutumikia wewe, kwa sababu tu umemzaa na kumlea?

Halafu, hata ukiondoa habari za maadili. Biashara ya kumlea mtoto ili aje kukutunza ni ujinga. Kwa sababu hakuna guarantee mtoto ataishi kukupita wewe. Unaweza kumzika yeye. Then what?

Ni mawazo fulani ya kijima na kijinga sana.
 
Waafrika wengine huwa eti na sisi tunashangaa kwa nini hatuendelei ? 🤣🤣🤣

Kwa mawazo kama haya mpaka leo?

Yani hatujaweza kitu cha msingi cha kuheshimu utu wa mtu, hata mtoto wako mwenyewe.

Yani unamnyima mtoto haki yake ya kuishi anavyotaka, unamvika mzigo wa kukutumikia wewe, kwa sababu tu umemzaa na kumlea?

Ni mawazo fulani ya kijima sana.
Binafsi,siafiki kabisa huo ujinga,wanangu wanasoma shule nzuri Kwa kadri ya uwezo alionijalia Mungu,nawatunza ila sifikirii any return from them.Natamani siku nimezeeka waendeleze miradi yangu,siku nimekufa waendeleze nilichokianzisha ila sifikirii eti wao ndio waanze kunihangaikia Matunzo,Natamani wanisaidie ki Hali tu sio mali...
 
Wenzio wanawezaje?pambana.
Wewe je? Umeweza
Mtoto si investment.

Ukimlea mtoto kama investment unafanya biashara ya utumwa iliyochangamka tu.

Ukimlea mtoto ili aje kukufaa unafanya biashara ya nipe nikupe, ila wewe unageuza tu kufanya "nakupa ili unipe".

Kulea mtoto na kumpa mazuri si biashara, ni wajibu wa kizazi katika familia.

Ndiyo maana unatakiwa kumlea mtoto vizuri hata kama ana matatizo ya akili na hawezi kukusaidia lolote.

Ndiyo maana unatakiwa kumlea mtoto vizuri hata kama ana ugonjwa utakaomfanya afe miaka mingi kabla yako.

Msilinganishe kulea mtoto na inbestment au biashara, mnatukanisha wajibu wa kizazi na kifamikia wa kulea mtoto ambao umepita bishara na investment.
Hili si la leo. Enzi hizo kabla ya Uhuru, Mwanaume alikuwa akioa wake wengi ili apate watoto wengi. Alitegemea hao watoto na wanawake wawe ndiyo Wafanyakazi katika mashamba yake, watunze Mifugo yake etc. Maana halisi ya kuwa na wake wengi ilikuwa kupata watoto wengi ili apate cheap labour.

Hii ilisababisha ongezeko la watu. Njia ya kupunguza ongezeko la watu (population); serikali ikaanzisha pamoja na mikakati mingine, njia ya kupunguza vizazi ikiwa ni pamoja na ulazima wa kumpeleka mtoto shule. Hii si kwamba serikali ilitaka watu wasome! La hasha lengo la serikali lilikuwa ni kumfanya mzazi aone burden ya kuwa na watoto wengi ambao hawana faida kiuchumi. Kwani unazaa mtoto na anapokuwa anahitajika kwenda shule na si kuingia shambani akalima mashamba yako.

Hili Lilifanya wazazi kupunguza idadi ya watoto maana ukizaa wengi unakuwa mtumwa wao.

Kwa sasa wimbi la vijana wa JF waliobadili kibao kwa wazazi, ati wahakikishe wanamtunza mtoto hadi wazazi wafe, hii itasababisha kataa ndoa wawe washindi kwani ukioa, utazaa mtoto na huyo Mtoto atakuwa liability kwako hadi uingie kaburini. Sasa kwanini uingie katika mdomo wa mamba ukiwa na akili zako. Wakati machangu wa kuondoa uhanga wapo kibao mitaani. Na hapo utabakisha chenji ya kuweka akiba ya uzeeni.

Hivi vitu ni muhimu kwa nyie ma Azaboys kuyajua pia.
 
Wewe je? Umeweza

Hili si la leo. Enzi hizo kabla ya Uhuru, Mwanaume alikuwa akioa wake wengi ili apate watoto wengi. Alitegemea hao watoto na wanawake wawe ndiyo Wafanyakazi katika mashamba yake, watunze Mifugo yake etc. Maana halisi ya kuwa na wake wengi ilikuwa kupata watoto wengi ili apate cheap labour.

Hii ilisababisha ongezeko la watu. Njia ya kupunguza ongezeko la watu (population); serikali ikaanzisha pamoja na mikakati mingine, njia ya kupunguza vizazi ikiwa ni pamoja na ulazima wa kumpeleka mtoto shule. Hii si kwamba serikali ilitaka watu wasome! La hasha lengo la serikali lilikuwa ni kumfanya mzazi aone burden ya kuwa na watoto wengi ambao hawana faida kiuchumi. Kwani unazaa mtoto na anapokuwa anahitajika kwenda shule na si kuingia shambani akalima mashamba yako.

Hili Lilifanya wazazi kupunguza idadi ya watoto maana ukizaa wengi unakuwa mtumwa wao.

Kwa sasa wimbi la vijana wa JF waliobadili kibao kwa wazazi, ati wahakikishe wanamtunza mtoto hadi wazazi wafe, hii itasababisha kataa ndoa wawe washindi kwani ukioa, utazaa mtoto na huyo Mtoto atakuwa liability kwako hadi uingie kaburini. Sasa kwanini uingie katika mdomo wa mamba ukiwa na akili zako. Wakati machangu wa kuondoa uhanga wapo kibao mitaani. Na hapo utabakisha chenji ya kuweka akiba ya uzeeni.

Hivi vitu ni muhimu kwa nyie ma Azaboys kuyajua pia.
Badili hiyo mentality,,Andaa maisha ukizeeka usisumbue watoto,ukifa ufe Kwa amani umeacha Legacy hata kama ni kiwanda Cha matofali
 
Wewe je? Umeweza

Hili si la leo. Enzi hizo kabla ya Uhuru, Mwanaume alikuwa akioa wake wengi ili apate watoto wengi. Alitegemea hao watoto na wanawake wawe ndiyo Wafanyakazi katika mashamba yake, watunze Mifugo yake etc. Maana halisi ya kuwa na wake wengi ilikuwa kupata watoto wengi ili apate cheap labour.

Hii ilisababisha ongezeko la watu. Njia ya kupunguza ongezeko la watu (population); serikali ikaanzisha pamoja na mikakati mingine, njia ya kupunguza vizazi ikiwa ni pamoja na ulazima wa kumpeleka mtoto shule. Hii si kwamba serikali ilitaka watu wasome! La hasha lengo la serikali lilikuwa ni kumfanya mzazi aone burden ya kuwa na watoto wengi ambao hawana faida kiuchumi. Kwani unazaa mtoto na anapokuwa anahitajika kwenda shule na si kuingia shambani akalima mashamba yako.

Hili Lilifanya wazazi kupunguza idadi ya watoto maana ukizaa wengi unakuwa mtumwa wao.

Kwa sasa wimbi la vijana wa JF waliobadili kibao kwa wazazi, ati wahakikishe wanamtunza mtoto hadi wazazi wafe, hii itasababisha kataa ndoa wawe washindi kwani ukioa, utazaa mtoto na huyo Mtoto atakuwa liability kwako hadi uingie kaburini. Sasa kwanini uingie katika mdomo wa mamba ukiwa na akili zako. Wakati machangu wa kuondoa uhanga wapo kibao mitaani. Na hapo utabakisha chenji ya kuweka akiba ya uzeeni.

Hivi vitu ni muhimu kwa nyie ma Azaboys kuyajua pia.
Hii logical fallacy inaitwa "argument from tradition".

Unajua argument from tradition ni nini?

Better yet, unajua logical fallacy ni nini?
 
Mwanaume tafuta pesa kwa bidii, wape watoto elimu bora, wape mahitaji yao muhimu, jenga nyumba nzuri waishi vizuri, lakini ukizeeka usitegemee lolote kutoka kwa wanao.

Enjoy maisha ya uzee kwa pesa zako mwenyewe ulizochuma ujanani.
Uko sawa kabisa...
Tunayashuhudia na tumeyashuhudia
👏👏👏👏
 
Back
Top Bottom