Mwanaume mbembeleze mwanamke baada ya ugomvi, mtatuua kwa stress

Mwanaume mbembeleze mwanamke baada ya ugomvi, mtatuua kwa stress

Hahah inategemea na kosa na kiwango cha thamani yako kwangu kilichobakia moyoni. Maana kero huwa zinashusha thamani ya upendo hasa zikiwa mara kwa mara.

Pia kuna wasichana ambao yeye anapenda attention sana ila hana mbinu za kiintelijensia za kuipata toka kwa mpenziwe, anachoona rahisi ni kuanzisha ligi ili mbishane tu mwishowe unamchoka sasa. Hii ni kwa wenye vile vi age vya 21-25! Kuna mmoja kala Red Card kwa sababu hio, mie sipendagi kelele af nashikwaga na hasira sana ila analazimisha msuguano ili tu asikie naongea tu hata kwa ubishani usio na maana...Really turns me off na sitakaa nikubembeleze kwa vitu vya namna hio.

Kanuni niliojiwekea, tukigombana nikachukia nikilala nikaamka nakuwa fresh kama kitu kibaya hakijatokea last night. Huwa si hold ugomvi au hasira, new day i'm refreshed na nashukuru mungu bibie amesha adopt hilo.

Hayo mambo ya kununiana week nzima au miezi naona ni utoto tu.
Umekuwa sasa
 
Ugomvi mara nyingi huanza polepole..
Wadada hua mnajisahau sana, wanaume atupendi viburi na majibizano,

Lamsingi ukiona noma ishaanza kuota mabawa, tumieni mbinu zenu ambazo ni built_in za kumtuliza mumeo/mwanaume wako kwa maneno ya upole,

Mkishindana mtaumia nyinyi sisi tunasahau mapema sana
 
Nakupenda Kigori
Kwenye mahusiano na maisha ya kawaida neno NAOMBA UNISAMEHE huwa lina maana sana. Hata ukilitamka kwa kumaanisha unahisi kabisa thamani yake.

Kwenye mahusiano pakiwa na tofauti lazima mmoja ajishushe ndo maisha yanaenda kwa furaha. Umekosea basi tambua nafasi yako katika mahusiano omba msamaha wala haitogharimu chochote!
 
Kuna rafiki yangu mmoja anawaambiaga wanaume wenzie ukiona mmegombana na mkeo akakununia wewe nenda kakaze mifuniko yote ya ndoo ndani kwenu yaani hakikisha umekaza kwa nguvu hadi anashindwa kufungua

Au mfichie vitu vyake vya muhimu na hakikisha umeficha sehemu ambayo hawezi kuviona yaani kwa namna yoyote ile akikosa msaada lazima atakuja tu kukuongelesha kukuomba umsaidie

Sasa alivyosema hivyo angalau nikaona kuwa huyo ni mwanaume kweli hata kama hawezi kukufuata kukubembeleza basi atatafuta tu namna ya wewe kuja kumuongelesha yaani angalau ataonyesha jitihada za kutaka msuluhishe na mwanamke ukiona hivyo unajiongeza

Kuliko yule mwanaume ambaye mkigombana unakuwa ndo umempata nafasi ya kwenda kulala nje ya nyumba yenu miezi na mchepuko na usipomsemesha ndo nitolee hiyo yaani hata yeye haonyeshi jitihada yoyote ya kutaka umuongeleshe aise kuna midume ina gubu halafu mtoto wa kiume kususa au kununa haipendezi jamani looh
Kuna wanawake wenye gubu kari hatakusemesha hadi mwezi uishe hata ufichi chupi yake......hasa wanawake wa mikoani wanamisimamo mikali sanaa hawana smile au jokes akiamuwa ameamuwa tu
 
Kwenye mahusiano na maisha ya kawaida neno NAOMBA UNISAMEHE huwa lina maana sana. Hata ukilitamka kwa kumaanisha unahisi kabisa thamani yake.

Kwenye mahusiano pakiwa na tofauti lazima mmoja ajishushe ndo maisha yanaenda kwa furaha. Umekosea basi tambua nafasi yako katika mahusiano omba msamaha wala haitogharimu chochote!

Usemalo nilakweli kabisaaa..
Tatizo nyinyi wadada wa dot.com hamjui/kujifunza namna yakuzima ugomvii mnataka kujifananisha na mwanaume, hapo ndipo kisanga huanzia..

Mwanaume hafananishwi na kitu chochote kile sawa na mwanamke vilevile..
Jueni nafasi zenu si kushindana..
 
Kwenye mahusiano na maisha ya kawaida neno NAOMBA UNISAMEHE huwa lina maana sana. Hata ukilitamka kwa kumaanisha unahisi kabisa thamani yake.

Kwenye mahusiano pakiwa na tofauti lazima mmoja ajishushe ndo maisha yanaenda kwa furaha. Umekosea basi tambua nafasi yako katika mahusiano omba msamaha wala haitogharimu chochote!
My dear siku hizi watu wameyafanya mapenzi yamekuwa kitu cha ajabu, hayana thamani tena. Full kuviziana, sijui tuendako.
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Kama umeniona vile. Naweza Nuna hata mwezi. Niliachana na mrembo mmoja hivi hivi. Ana kakiburi fulani hivi. Nikakausha na yeye akakusha. Mara wiki mara mwezi.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Ulikutana na kisiki mwenzio.
Ila mwanaume unanunaje?
 
Kwenye mahusiano na maisha ya kawaida neno NAOMBA UNISAMEHE huwa lina maana sana. Hata ukilitamka kwa kumaanisha unahisi kabisa thamani yake.

Kwenye mahusiano pakiwa na tofauti lazima mmoja ajishushe ndo maisha yanaenda kwa furaha. Umekosea basi tambua nafasi yako katika mahusiano omba msamaha wala haitogharimu chochote!
Mwanaume rijali kabisa hasemi NAOMBA UNISAMEHE! Kwa mwanamke wa jamii yetu unaleta udhaifu ndani ya nyumba.
 
Kuviziana huko vipi lakini dear...
Kama mtu una malengo naye mnaviziana nini eti, mie siwezii kukaa masaa kadhaa menuna nitalia tuu nitanyamaza namtafuta tuongee
Mama si afadhali wewe unaongelea hata ulie na malengo nae, wenzio ni wanandoa kabisaaaa na wananuniana na wanajisifia kununa(tena wanaume[emoji134])

Wengine anakosea yeye halafu anataka uombe msamaha wewe.
 
Back
Top Bottom