Mwanaume una njia zote za kufupisha ahadi ya mpenzi wako, kama utaamua

Mwanaume una njia zote za kufupisha ahadi ya mpenzi wako, kama utaamua

Equation x

JF-Expert Member
Joined
Sep 3, 2017
Posts
33,679
Reaction score
49,841
Wikiend iliyopita, nilikuwa nimejichokea kiaina; nikaona bora niende zangu 'club' moja ya karibu angalau nipate kinywaji kidogo, huku nikiburudika na mziki pamoja na kuosha macho kwa watoto wazuri.

Baada ya kuingia club, mhudumu akaniongoza mpaka kwenye meza moja ambayo haikuwa na mtu; nikamwagiza kinywaji changu, na kumsisitiza anihudumie mpaka mwisho nitakapoondoka pale ukumbini.

Ilikuwa mida ya saa nne usiku, watu wanazidi kuingia na mambo ya ukumbini yanazidi kufana vizuri. Watoto waliopiga pamba kali, viuno vya nyugwi n.k wakazidi kupendezesha ukumbi.

Kwa wastani tu; warembo walikuwa wengi sana, na walikuwa wazuri. Ni wewe tu, na makali ya meno yako.

Imefika saa sita usiku pombe ikawa imeniingia vizuri kichwani, hakuna kuona aibu. Nilishangaa nimegeuka nyuma yangu, nikaona bonge la kifaa 'my type', nikajikuta nimepata ujasiri wa kumshika mkono na kumvuta karibu na meza niliyokuwepo.

Nikashika kiganja cha mkono wake na kukiweka kifuani kwangu, na kuanza kumpa sifa za hapa na pale. Baadaye nika-kiss kiganja chake, nikamwita aliyekuwa ananihudumia alete kiti kingine, na aongeze vinywaji.

Tukaanza kufahamiana, yeye ni mke wa mtu na ameajiriwa wizara R na kwa sasa yupo masomoni, hapa mkoani. Nikamwambia hakuna matata, tutakuwa tunapeana kampani pale inapobidi.

Ghafla DJ akapiga mziki wa msanii K-Ci & jojo, nikajikuta namwinua mtoto tukaanza kucheza 'zero distance' huku akikizungusha kiuno taratibu bila kuchezesha kifua. Dah... wakubwa wanafaidi sana wakuu.

Sijakaa sawa, midomo ikawa inawasiliana kwa nguvu ya sumaku; muhudumu naye analeta tu vinywaji huku naye akiwa anajihudumia.

Kuja kucheki kwenye 'wallet' pesa imekata, na kuondoka ukumbini nikalale siwezi; ikabidi nimwambie mrembo nisindikize 'home' nikaongeze mpunga.

Ikabidi niwaage mabaunsa pale mlangoni, ninarudi; ili wasinichaji gharama zingine za kiingilio.

Baada ya kufika 'home' nikamuacha mrembo sebuleni, nakwenda chumbani kwangu na kuchukua salio kidogo.

Sikupenda kuwa na papara ya kumtaka kimapenzi hapo 'home', nilitaka ajue hivyo vitu sio vigeni kwangu.

Tukarudi 'club'; baada ya kufika tukaendelea na vinywaji mpaka kwenye saa kumi usiku; baada ya hapo tukaagana na akaniahidi, atanitunuku wiki ijayo tukishafahamiana zaidi.

Nikajibu, ok hakuna tatizo.

Nilipofika nyumbani, nikajitafakari; nikaona wiki ijayo mbali, ikabidi nijifanye ninaumwa.

Palipokucha, majira ya saa nne asubuhi, nampigia simu, kumjulisha hali yangu si nzuri kutokana na uchovu wa mkesha. Namuomba aje anijulie hali nyumbani; naye akanijibu, atakuja mida ya jioni.

Kufika mida ya saa moja usiku, mtoto huyu hapa anagonga mlango. Nikamkaribisha, nikampa 'wine' kidogo huku akiwa amekaa kwenye sofa.

Tukawa tunapiga stori huku tukiendelea kupata kinywaji chetu, pamoja na kusikiliza mziki wa taratibu.

Baada ya muda, nikamsogelea kwenye sofa alilokuwa amekaa, na mambo mengine yakaanza kuendelea.

Kuja kushtuka tupo chumbani; Yale mambo ya wiki ijayo yakawa yametimizwa ndani ya siku moja.

Kwa sasa tunaitana 'honey'
 
Ktk wale watakofika mbinguni wakiwa wamechoka mkuu wewe huchomoki lazima utakuwa mmoja wao.

Unaenda kuongeza salio la kutumia bar na hali hii ya petrol 3k+?
😂😂😂 Mungu ametupa viumbe vyote tuvifurahie
 
Ktk wale watakofika mbinguni wakiwa wamechoka mkuu wewe huchomoki lazima utakuwa mmoja wao.

Unaenda kuongeza salio la kutumia bar na hali hii ya petrol 3k+?
Mkuu ,siku ya jumanne ,ambayo ilikuwa siku ya idd nilitoka zangu kwenda kwenye kibaa fulani maarufu mtaani kwetu

Mfukoni Nina laki na ishirini,lengo tukapige chupa mbili tatu Mimi na mshikaji wangu mmoja tu.

Basi, kuanzia saa kumi na moja to kumi na mbili vyombo vikaanza kukolea

Mara huyo nikaanza kucheza wimbo wa msanii Rema uitwao calm down

Baa nzima wakaanza kunipigia makofi

Na Mimi udhaifu wangu nikisifiwa tu basi Hilo wengi wanaonifahamu Hawapati taabu

Wanajua muda si mrefu Nini kitatokea hasa ukizingatia mtaani kwangu Mimi nipo kwenye kumi bora

Nikaona Sina Cha kuwalipa zaidi ya kuwapiga maji ,kwa sauti nikawaambia wahudumu walete vinywaji kwa kila mtu.

Nikatoka nje nikatoa kilo tano kwenye simu,kitendo cha kurudi nakuta watu wengi kumbe wanapigiana simu dah!!!!!!

Hadi natoka usiku wa saa sita usiku nikawa nadaiwa 40k yaani

120,000+500,000=620,000+40,000=

660,000/=

Na kesi na mke wangu imeisha jioni hii kwa kunilaumu kutumia pesa vibaya ilhali maisha yetu ni ya kipato Cha chini

Lakini kesi nimeshinda kwa kumpoza na 300k na Ahadi kibao

Tatizo mnamiliki magari kabla ya muda wenu,au kwa sifa uonekane una gari
 
Mimi niliwai danganywa hivyo hivyo, kumbe ni njia yako ya mkato kuuza uchi. Ukiwajulia hawa viumbe ata hawakutesi
 
Mkuu ,siku ya jumanne ,ambayo ilikuwa siku ya idd nilitoka zangu kwenda kwenye kibaa fulani maarufu mtaani kwetu

Mfukoni Nina laki na ishirini,lengo tukapige chupa mbili tatu Mimi na mshikaji wangu mmoja tu.

Basi, kuanzia saa kumi na moja to kumi na mbili vyombo vikaanza kukolea

Mara huyo nikaanza kucheza wimbo wa msanii Rema uitwao calm down

Baa nzima wakaanza kunipigia makofi

Na Mimi udhaifu wangu nikisifiwa tu basi Hilo wengi wanaonifahamu Hawapati taabu

Wanajua muda si mrefu Nini kitatokea hasa ukizingatia mtaani kwangu Mimi nipo kwenye kumi bora

Nikaona Sina Cha kuwalipa zaidi ya kuwapiga maji ,kwa sauti nikawaambia wahudumu walete vinywaji kwa kila mtu.

Nikatoka nje nikatoa kilo tano kwenye simu,kitendo cha kurudi nakuta watu wengi kumbe wanapigiana simu dah!!!!!!

Hadi natoka usiku wa saa sita usiku nikawa nadaiwa 40k yaani

120,000+500,000=620,000+40,000=

660,000/=

Na kesi na mke wangu imeisha jioni hii kwa kunilaumu kutumia pesa vibaya ilhali maisha yetu ni ya kipato Cha chini

Lakini kesi nimeshinda kwa kumpoza na 300k na Ahadi kibao

Tatizo mnamiliki magari kabla ya muda wenu,au kwa sifa uonekane una gari
Uliitendea haki siku hiyo
 
Mkuu ,siku ya jumanne ,ambayo ilikuwa siku ya idd nilitoka zangu kwenda kwenye kibaa fulani maarufu mtaani kwetu

Mfukoni Nina laki na ishirini,lengo tukapige chupa mbili tatu Mimi na mshikaji wangu mmoja tu.

Basi, kuanzia saa kumi na moja to kumi na mbili vyombo vikaanza kukolea

Mara huyo nikaanza kucheza wimbo wa msanii Rema uitwao calm down

Baa nzima wakaanza kunipigia makofi

Na Mimi udhaifu wangu nikisifiwa tu basi Hilo wengi wanaonifahamu Hawapati taabu

Wanajua muda si mrefu Nini kitatokea hasa ukizingatia mtaani kwangu Mimi nipo kwenye kumi bora

Nikaona Sina Cha kuwalipa zaidi ya kuwapiga maji ,kwa sauti nikawaambia wahudumu walete vinywaji kwa kila mtu.

Nikatoka nje nikatoa kilo tano kwenye simu,kitendo cha kurudi nakuta watu wengi kumbe wanapigiana simu dah!!!!!!

Hadi natoka usiku wa saa sita usiku nikawa nadaiwa 40k yaani

120,000+500,000=620,000+40,000=

660,000/=

Na kesi na mke wangu imeisha jioni hii kwa kunilaumu kutumia pesa vibaya ilhali maisha yetu ni ya kipato Cha chini

Lakini kesi nimeshinda kwa kumpoza na 300k na Ahadi kibao

Tatizo mnamiliki magari kabla ya muda wenu,au kwa sifa uonekane una gari
Hahaha 😂😂😂
 
Back
Top Bottom