Mwanaume unaanzaje kuoa binti ambae uchumbani hajawai ama ni mvivu kukufulia, kukupikia, kufanya usafi wa chumba / nyumba, n.k.

Mwanaume unaanzaje kuoa binti ambae uchumbani hajawai ama ni mvivu kukufulia, kukupikia, kufanya usafi wa chumba / nyumba, n.k.

kwanza mambo ya uchumbani kupikiana yanahusu nini? Hao siyo Waislam na kama ni Waislam basi hawafati Uislam wao.
 
Mie nnapajuwaje Kizimkazi. Mimi kwetu mkuranga, shungubweni beach. tena kwetu kuni ni za mikoko. Ukipikia hizo kila mtu atauliza chakula umepikaje hiki? hajuwi siri ni moashi wa mikoko.

Khaa, ulitaka tupikie nini?
Duh yani miharufu ya moshi tena kwenye chakula? Mtakuwa mnakula vyakula vya hovyo sana huko shungubweni.
 
Naandika uzi huu kwasababu nazidi kujionea baadhi ya ndoa hizi za kizazi kipya zimekuwa za ajabu sana, hata ile tafsiri ya kuvuta jiko imeanza kupotea.

Na tuache masikhara, ndoa zetu za kiafrika mwanamke ana majukumu yake na mwanaume ana majukumu yake na kuna majukumu ya wote kwa pamoja, Mwanamke upo nae kwenye uchumba yupo lege lege hatimizi majukumu yake huyo unamuoaje ?


Mwanamke upo nae uchumbani kila siku yeye kuagiza vyakula ilhali stoo imejaa vyakula vya kupika na gesi ni kama yote, mwanaume unajitahidi kwa mafumbo kupika kama ulivyokuwa bachela lakini yeye dish bado halikamati anakusifia "oh unajua kupika" yani hajiongezi, yani akipika ni mpaka kwa kujivuta ama iwe kwajili ya kujiposti status ama instagram ili asifiwe.

Nguo zako nazo ni mvivu kukufulia.

Usafi wa chumba ama nyumba bado unaufanya wewe wakati yeye yupo..

Muda wote huo wewe unatimiza majukumu yako ya kumpa pesa ya matumizi unayoihangaikia asubuhi mpaka jioni na pengine hadi usiku.

Unaoaje sample hii ??

Ewe kijana, unapokuwa na mchumba ukimleta hapo chumbani ama nyumbani kwako, hapo ndio eneo la la kumsahishia mtihani wa mahitaji muhimu ya ndoa, akibaki kukushangaa, akijivuta vuta, yupo bize na simu, huyo tayari ana F sio wa kufunga nae ndoa, fanya nae mambo mengine ila sio wa ndoa.
Kwani uchumba ni ndoa?
 
Siku hizi ndoa zimekuwa kama biashara.

Wanawake wenye maokoto ama mambo safi ndio wanaolewa sana.

Wanaume wamekuwa wavivu sana. Hawajali hayo mambo ya kupikiwa. Wanatazama maokoto ya mke tu.

Hata kama hajui kufua wala kupika anaolewa tu akiwa na maokoto
Ahsante kwa kusema hili mkuu..!
Nina mfano hai kabisa ila nashindwa kuuweka hapa..!!
Hivi Depal unakumbuka hii issue..?
 
Usioe au kuolewa kwa tamaa za ngono...

Ndoa ni zaidi ya ngono..
 
Ahsante kwa kusema hili mkuu..!
Nina mfano hai kabisa ila nashindwa kuuweka hapa..!!
Hivi Depal unakumbuka hii issue..?
Katika threads zako? Nitajikumbushia
Bora tusaidike sisi ambao hatujui kitu oote 😂😂
 
Uislam unafatwa 100% ambae haufati huyo ni mtu binafsi na ni mjinga mjinga kama wewe, Uislam upo na habadiliki.

Wewe umeshaingia kuufata Uislam?
Labda kama ni kuswali ila mambo mengine wewe ni kilaza wa uislam.

Si unaona mwenyewe jinsi watu wengi wanavyokujia juu hapa jukwaani??
Una majibu mabovu, ya hovyo, unapenda ligi huku ukijibu watu kwa kuwakejeli.
Wakati uislam hauko hivyo, uislam ni unyenyekevu sio shari.

Wewe unamjibu mtu ili umkere na sio kumuelimisha, binafsi napenda kuelimishwa na sio kukerwa. Na mara nyingi siulizi ili unikejeli bali kutaka kujua tu lakini majibu yako yananyong'onyesha ari ya kuujua uislam

Unahubiri uislam kwa kutweza imani za wengine. Huo kwangu ni UJINGA.
 
Kwanza kwetu hatutaki mchezo, mke anakaa kwao au awe kishajengewa ndiyo wanahamia kwake na mumewe. Hukuti hata siku moja kwetu tunaishi kwa mume. Kisa cha kunyanyaswa?

Mwanamke mwenye maadili hakai kwa mume, tumeshayaon awengi yanawakuta.

Kwanza mwanamme kabla hajakuoa hata paja halioni wacha chupi. Saa ngapi akuletee ujinga.
Samahani. Nchi gani hii unaizungumzia nikatembee?
 
Back
Top Bottom