NetMaster
JF-Expert Member
- Sep 12, 2022
- 1,454
- 4,925
Walengwa:
1. baba alietengana na mzazi mwenzake ila anaendelea kutuma pesa ya matumizi ya mtoto
2. Baba ambae anaishi nyumba moja na familia yake lakini anampa mke wake pesa ya chakula cha familia , mavazi, elimu, n.k bila watoto kujua.
aliotengana na ambao wanakuwa nje ya nyumba kikazi kwa muda mrefu
Unapowahudumia watoto kwa kumpa mama yao hela ya matumizi, hakikisha sometimes watoto wanajua kuwa wewe ndio unahudumia! wamama wengi huficha hii taarifa muhimu kwa watoto na inakuwa rahisi kuwajaza sumu kuwa wao ndio malkia wa nguvu wnawapambania kila kitu, hata wasipowaambia ni rahisi mtoto kujenga hi picha na kumuona baba yake hana umuhimu, watoto wanaweza hata kuanza kumuona baba yao ni kama mgeni asie na msaada wowote na hata kumpandisha zaidi cheo mama yao
hakikisha unapokua na watoto out bila mama yao geuza hio hali iwe uwanja wako wa kunyakua points, watoto wanapenda sana utoto na huo ndio udhaifu inabidi wao uutumie ili wakuone wa maana, wamezoea kula ugali wewe wanunulie sambusa, wamezoea kucheza game za simu ya mama gao wewe wapeleke zile center zenye magame makubwa, wamezoea kunywa maji wewe wapeleke vibanda vya juice, wavulana wanunulie vifaa vya michezo,