TANZIA Mwandishi nguli wa Fasihi nchini, Edwin Semzaba afariki dunia

TANZIA Mwandishi nguli wa Fasihi nchini, Edwin Semzaba afariki dunia

Rest in eternal peace. He was a good person
 
Ukitaja majina ya Waandishi 10 mahiri wa vitabu nchini basi jina la Edwin Semzaba halikosekani.
1453057090155.jpg

Huyu alikuwa Mwanamasumbwi, Muigizaji Mwandishi na Mhadhili wa Chuo kikuu cha UDSM.
Moja ya kazi zake zilizompatia umaarufu ndani na nje ya Tanzania ni kitabu cha "Ngoswe penzi kitovu cha Uzembe"
1453057232905.jpg

Kikiwa ni kitabu kilichodumu kwa muda wa miaka 20 kikitumika kama kitabu cha kiada kwa shule za Sekondari.."Kitabu cha Ngoswe nilikiandika nikiwa kidato cha pili wakati huo nikiwa na miaka 16 tu tena ilikuwa sababu ya kukimbia somo la Hesabu hivyo wakati najificha nilitumia muda huo kuandika na hii ilikuwa mwaka 1967 wakati wa sensa ya kwanza kabisa ya watu na makazi kufanyika nchini. Enzi hizo mwanafunzi wa Livingstone College na sasa Kigoma sekondari"..Anasema Edwin Semzaba.
Vitabu vingine alivyowshi kuviandika ni pamoja na;
Tendehogo 1982
Sofia wa Gongo la mboto 1985
Mkokoteni 1988
Tausi wa Alfajiri 1996
Funke buge buge 1999
Tamaa ya boimanda 2002
Marimba ya Majaliwa 2008
Rest in piece Edwin Semzaba Daima tutakukumbuka hasa kwa kazi zako.
 
Edwin Semzaba
 

Attachments

  • 1453058147330.jpg
    1453058147330.jpg
    16.7 KB · Views: 53
R.I.P Edwin semzaba wa ngoswe.
 

Attachments

  • 1453058136934.jpg
    1453058136934.jpg
    8.6 KB · Views: 72
R.I.P Mzee Semzaba. Ngoswe Penzi kitovu cha uzembe, Kwa sasa yanatendeka makazini na hata mambo yanaharibika.
 

Attachments

  • Semzaba-Ngoswe.jpg
    Semzaba-Ngoswe.jpg
    15 KB · Views: 83
Back
Top Bottom