intelligent man
JF-Expert Member
- Aug 13, 2015
- 705
- 1,123
Nyamhongolo ni stand kubwa mnoo
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Naunga mkono baadhi ya hoja .ila Kwa uzoefu wangu pia maeneo ambayo umeyarefer ni Peri urban Yani nje kidogo ya mji ...ndio utapata hizo disturbance . eneo pekee ambalo Lina majaruba na liko mjini ni kati nyegezi kuja mkuyuni pembeni mwa reli pale ..na Yale ni maeneo ya viwanda..na hifadhi za reli ...eneo lingine maybe nyamhongolo ambapo ni eneo la viwanda na uwekezaji maaalumuNimefika Mwanza na kuzurula kwa wiki 2 Kuna madhaifu makubwa sana kadhaa nimeyaona.
1- Kwanza Kuna uhaba mkubwa sana wa mtandao wa Rami wa barabara za mitaa. Hii kitu imesababisha Jiji limekuwa disorganized mnooo.
Na ardhi ya Mwanza ilivyo, ni kichanga, bila Rami mvua inanyesha inachota mchanga na kuacha barabara ni mashimo matupu.
Yaani usafiri tegemezi maeneo ya karibu tu ndani ya Jiji yamebaki ni Bajaj na Bodaboda. Mtu nayekaa Kisesa ana afadhali kiusafiri kuliko mtu wa Kishiri, Mahina, Nyanguruguru, nk.
2- Mwanza Jiji Kuna lundo kubwa la kiwanja/maeneo yaliyoachwa tu ambayo hayajulikani ni ya Nani.
- Hali hii imepelekea kukua na kukomaa kwa genge zito untouchable la matapeli tena wazee kabisa.
- Kwasababu hiyo kwa uwoga watu wameamua kukacha maeneo ya karibu na kwenda kujazana mbali kabisa ya mji Kama Usagara, Isangijo, Kitumba Kisesa, Mwahuli, Fela, Nyanshishi nk.
Imagine, katikati ya mji kabisa unakuta Kuna watu wanachunga ng'ombe tena wengi kabisa!!!
3- Ubovu wa routes za daladala. Nadhani hili linatokana na pia na Ubovu wa barabra za mitaa. Yaani daldala Ina route ya Magu-Nyanshishi kweli????!!
Mwanza mji unapanuka zaidi kuliko barabara na route za magari, baadaye daladala zinawekwa kwa kulazimisha tu lakini Hali ni mbaya na Tete sana.
4- Majaruba ya kutengeneza kila Kona. Hayo maeneo ni Bora yangepandwa miti kuboresha mji.
Miradi mikubwa iliyopo bado ni hiyo hiyo, soko la makoroboi, stand ya Nyegezi, Daraja busisi.
Kuna upembuzi tu wa barabara za Busenga, Veta- Nyanguruguru, Kuna nyingine Inapita Isela kwenda Kisesa Ila mpaka Sasa bado ni stori tu.
Huu ni mtazamo wangu kwa uzoefu wangu.
Changamoto kubwa kwa Mwanza niliyoiona suala la usafiri siyo stressful Kama Dar.Stendi ya nyamhongolo.. haiwezi kujaa kiurahisi hivyo .na kama inajaa waondoe tata zote ziishie kisesa..yabaki magari makubwa ...
Stendi ya kisesa isiwe ya hiace za vijijini tu Bali pia hizo tata ziondolew nyamhongolo.zipelekwe huko
Hii concept yako imekaa kwenye ruti za mjini.....ila mim Nazungumzia ruti za vijijini huko ..Changamoto kubwa kwa Mwanza niliyoiona suala la usafiri siyo stressful Kama Dar.
Mwanza bado abiria wanaringa kupanda daladala. Ukiwa na hiace lako limechoka utapiga yowe masaa 6 abiria hawapandi.
Abiria wanataka daladala jipya au lenye TV wanasubiria Hilo Hilo.
Hivyo, wengi wanahisi wakiweka coaster kubwa hasa milango 2 Kama za Dar hawapata idadi ya abiria kujazana gari.
Hata kwasasa coaster nyingi kubwa ni zile zinazoenda sehemu Kama Buswelu au Buhongwa ambako Kuna abiria wengi.
Labda niulize kidogo, ukitoka National, ukashuka chini Kama unaenda Mahina, Nyanguruguru, mpaka huko mbele naambiwa ukienda unafika Buzuruga kwa short cut huo ni siyo katikati ya mji???Naunga mkono baadhi ya hoja .ila Kwa uzoefu wangu pia maeneo ambayo umeyarefer ni Peri urban Yani nje kidogo ya mji ...ndio utapata hizo disturbance . eneo pekee ambalo Lina majaruba na liko mjini ni kati nyegezi kuja mkuyuni pembeni mwa reli pale ..na Yale ni maeneo ya viwanda..na hifadhi za reli ...eneo lingine maybe nyamhongolo ambapo ni eneo la viwanda na uwekezaji maaalumu
Yeah ....hayo maeneo yote uliyataja sio katikati ya mji ni pembeni.....ni maeneo ambayo ni Peri urban na ndio hayo yenye changamoto kubwa kihudumaLabda niulize kidogo, ukitoka National, ukashuka chini Kama unaenda Mahina, Nyanguruguru, mpaka huko mbele naambiwa ukienda unafika Buzuruga kwa short cut huo ni siyo katikati ya mji???
Siku ya mwisho nataka kuondoka, nilipanda daladala Kijereshi nikaenda mpaka Kishiri ( hapa barabara ni ya vumbi na mabonde ), nilipofika Kishiri nikagundua ni sehemu ambayo wananchi wameichangamsha sana lakini haina mkono wa serikali kabisa.
Nilipofika hapo Kishiri center, tukapelekwa Kuna sehemu panaitwa Bukaga ni mbele ya Kishiri center barabara ni vumbi Ila watu wamejenga kweli. Hiyo barabara inaenda mpaka inakutana na Rami ya Kisesa Usagara eneo la Sumve. Kumbuka hii Kishiri yote ni Nyamagana.
Kuna siku ndio nilichoka, nilipelekwa Luchelele Malimbe huko karibu na ziwa, kutoka kituo Cha daladala nauli ya Bajaj elfu 4!!
Hapo ndio nikagundua kwanini watu wanajaa Kisesa kuliko baadhi ya maeneo ya Nyamagana na Ilemela.
Ingawa rami ya sabasaba imesaidia kuifungua Buswelu, na maeneo yake ya pembeni.
Kwahiyo kwa Mwanza tukizungumza Urban tunazungumzia wapi?Yeah ....hayo maeneo yote uliyataja sio katikati ya mji ni pembeni.....ni maeneo ambayo ni Peri urban na ndio hayo yenye changamoto kubwa kihuduma
Hizi tata ndio zinachangia stendi kuwa ndogo, au wangeweka stendi ndogo nje.Stendi Ina capacity ya mabas 120 ,,,kinachowavuruga ni hizo tata za kwenda simiyu ,mugumu,bunda ,kisorya,nyambiti,musoma na kiabakari ...wazipeleke kwenye stendi ya kisesa...ni njia nyepesi isiyo na gharama
Anzia mkolani Hadi town then town Hadi ilemela ,town Hadi nyakato ...Kwahiyo kwa Mwanza tukizungumza Urban tunazungumzia wapi?
Au kublock kabisa... Maana mi sioni haja ya mtu kutukana matusi ya ajabu ajabu...Naomba Tujitahidi kucontrol hisia zetu, kuna baadhi ya comment sio nzuri kuzisoma zinaudhi.
Tutumie maneno ya staha bila kutukana na kumuudhi mwingine.
JF wangeweka kipengele cha kumwezesha aliyeanzisha uzi kufuta au kuedit baadhi ya comment ingekuwa vizuri zaidi.
Ni kubwa kama utahusisha n parking ya malory mkuu.Hii stendi ni kubwa mno kwa vyovyote vile haiwezi kujazwa na mabasi labda kama daladala zinaingia mpaka ndani ya stendi. Kusema Buzuruga na Nyamhongolo zinafanana ukubwa sio kweli, nyamhongolo ni kubwa karibia mara 2 ya Buzuruga. Kama Buruga ilikuwa haijazi mabasi iweje nyamhongolo ijae?
Hizi taarifa za nyamhongolo kujaa zimetoka wapi au kuna mtu mmoja kaamua kuzusha?
Halafu kusema basi likae zaidi ya nusu saa lipigwe faini sio sawa. Hii stendi sio kwamba mabasi yanapita yanakuja kuishia hapo na kuanzia safari hapo.
Kwa mfano gari litoke msoma lishushe ndani ya nusu saa linapata wapi abiria wa kujaza halafu ukumbuke halipo moja tu kuna mabasi mengi ya ruti hiyo
Ilemela wametisha asee👍👍👍👍👍Hawa ilemela.ndani ya robo Moja wameingiza bilioni 5 .kama wakienda hvi robo zote watakuwa na bilioni 20 .
Lakini hii ni Mwanza ya mwaka 2010 huko. Sasa hivi ni miaka 10 baadaye lazima fikra ziendane na ukubwa wa mji.Anzia mkolani Hadi town then town Hadi ilemela ,town Hadi nyakato ...
Nyegezi
Butimba
Mkuyuni
Igogo
Town
Kirumba
Isamilo
Pasiansi
Kitangiri
Nyamoro
Nyakato
Mabatini
Mbugani
Pamba
Hizi ndio kata za mjini
Hii stendi ata ukiwa ndani utaona tu udogo wake siku ukija Mwanza utaenda kujioneaStendi Ina capacity ya mabas 120 ,,,kinachowavuruga ni hizo tata za kwenda simiyu ,mugumu,bunda ,kisorya,nyambiti,musoma na kiabakari ...wazipeleke kwenye stendi ya kisesa...ni njia nyepesi isiyo na gharama
Nje ya stand pale ndio daladala zinashusha. Kwahiyo ukitaka hizo bus ndogo zipakie tena hapo nje, inakuwa changanyikeni.Hizi tata ndio zinachangia stendi kuwa ndogo, au wangeweka stendi ndogo nje.
Zipelekwe stendi ya kisesaNje ya stand pale ndio daladala zinashusha. Kwahiyo ukitaka hizo bus ndogo zipakie tena hapo nje, inakuwa changanyikeni.
Pale nje waparekebishe kuna eneo kubwa sana, watenge sehemu ya daladala na sehemu ya kupark tata.Nje ya stand pale ndio daladala zinashusha. Kwahiyo ukitaka hizo bus ndogo zipakie tena hapo nje, inakuwa changanyikeni.
Kumbuka Kuna mpango pia wa kukenga Njia nne, Mjini mpaka Nyanguge??!!!Pale nje waparekebishe kuna eneo kubwa sana, watenge sehemu ya daladala na sehemu ya kupark tata.