Mwanza: Walimu 250 waandamana kudai malipo ya kazi ya anwani za makazi

Mwanza: Walimu 250 waandamana kudai malipo ya kazi ya anwani za makazi

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
2,780
Reaction score
6,607
Walimu 250 kutoka Wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza wameandamana hadi ofisi za Halmashauri ya Jiji la Mwanza kudai posho zao za kazi ya kuweka alama za anwani za makazi waliyoifanya kwa siku tano.

Watumishi hao waliandamana jioni ya Aprili 8, 2022 ambapo malipo hayo ni Sh 100,000 kwa siku tano ambapo kila siku malipo yalikuwa ni Sh 20,000 kwa mtu mmoja.

Akizungumzia hali hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Robert Gabriel alisema atawasiliana na viongozi wa mradi huo na viongozi wa kata kisha atatoa taarifa kwa walimu hao kuhusu malipo yao.

“Wanatufokea, wanatutukana, sisi ni watumishi wa umma, sasa hivi wanaanza kutuzungusha kuwa tutalipwa kwa kaya kitu ambacho ni tofauti na makubaliano yetu,” alisema mmoja wa waandamanaji hao.

Chanzo: Nipashe
 
Walimu wa nchii kama wana laana vile..yani laki 1 ndio ya kumfanya mtu aandamane. ?

Ndio mana nilikataa na siku zote sitaruhusu ndugu ama rafiki awe mwalimu..bora atafute kazi nyingine ya kufanya.

Ualimu ni umasikini wa kujitakia.

#MaendeleoHayanaChama
Mkuu kwao nyingi mshahara wao wenyewe haba halafu makato mengi.
Ni haki yao walipwe maana walifanya kazi.
 
Walimu 250 kutoka Wilaya ya Nyamagana mkoani Mwanza wameandamana hadi ofisi za Halmashauri ya Jiji la Mwanza kudai posho zao za kazi ya kuweka alama za anwani za makazi waliyoifanya kwa siku tano.

Watumishi hao waliandamana jioni ya Aprili 8, 2022 ambapo malipo hayo ni Sh 100,000 kwa siku tano ambapo kila siku malipo yalikuwa ni Sh 20,000 kwa mtu mmoja.

Akizungumzia hali hiyo, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mhandisi Robert Gabriel alisema atawasiliana na viongozi wa mradi huo na viongozi wa kata kisha atatoa taarifa kwa walimu hao kuhusu malipo yao.

“Wanatufokea, wanatutukana, sisi ni watumishi wa umma, sasa hivi wanaanza kutuzungusha kuwa tutalipwa kwa kaya kitu ambacho ni tofauti na makubaliano yetu,” alisema mmoja wa waandamanaji hao.

Chanzo: Nipashe
Yaani waliwatelekeza wanafunzi madarasani wao wakaenda kufanya kazi isiyo na tija kwa wanafunzi!
 
Walimu wa nchii kama wana laana vile..yani laki 1 ndio ya kumfanya mtu aandamane. ?

Ndio mana nilikataa na siku zote sitaruhusu ndugu ama rafiki awe mwalimu..bora atafute kazi nyingine ya kufanya.

Ualimu ni umasikini wa kujitakia.

#MaendeleoHayanaChama
Hao walimu unaowadharau ndiyo wanaokufundishia watoto wako.

Tuwape heshima basi kwa kujitolea kwao. Ni haki yao kudai kilicho chao, wewe unaona laki moja ndogo, bila ya kuifanyia kazi nani atakupa hiyo laki bure bure tu?
 
na kuhonga kote ili "wafikiliwe zaidi" bado wamekopwa, pumbavu Sana!

Hii nchi ngumu, Nina class mate wangu ambaye form four aliambulia four ya mwisho, ni katibu muhtasi taasisi moja nyeti nchini (TRA, BOT, ...) ana kazi za nje ya kituo mikoani huko..hadi mwenyewe anachagua aende au asiende maana ni za kumwaga, kwa wiki anakunja milioni 2 hadi 3....

Nesi wa hapa N'gwashilalage ambaye yeye ndio daktari, mfamasia, laboratory technician (kazi zote anafanya yeye) serikali haina habari naye hata kumpa kifuta jasho cha IST tu ya mtumba!...

Namalizia na wimbo; Mbinguni kuna makao mazuri, Mbinguni kuna furahaaaa X3
 
na kuhonga kote ili "wafikiliwe zaidi" bado wamekopwa, pumbavu Sana!

Hii nchi ngumu, Nina class mate wangu ambaye form four aliambulia four ya mwisho, ni katibu muhtasi taasisi moja nyeti nchini (TRA, BOT, ...) ana kazi za nje ya kituo mikoani huko..hadi mwenyewe anachagua aende au asiende maana ni za kumwaga, kwa wiki anakunja milioni 2 hadi 3....

Nesi wa hapa N'gwashilalage ambaye yeye ndio daktari, mfamasia, laboratory technician (kazi zote anafanya yeye) serikali haina habari naye hata kumpa kifuta jasho cha IST tu ya mtumba!...

Namalizia na wimbo; Mbinguni kuna makao mazuri, Mbinguni kuna furahaaaa X3
Wape wapeee vitu mbolegwa😁😁
 
Back
Top Bottom