Mwanza: Wanafunzi Mapacha wa Chuo cha Mipango wafariki Dunia kwa kuzama Ziwa Victoria

Mwanza: Wanafunzi Mapacha wa Chuo cha Mipango wafariki Dunia kwa kuzama Ziwa Victoria

Wewe binafsi si unaamini kuna kiumbe cha kufikirika kinaitwa jini? It’s so sad jinsi udini ulivyofunika ufahamu wako . Isingekuwa udini una akili nzuri sana tu
[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Ndio maana baadhi yenu waafrika mnakuwa maskini wa vipato(am sorry to utter this)....kwa kutotaka kuwekeza katika maarifa.....nina boti yangu ya uvuvi hapo nyamisati kutwa inakaribia kuzama kwa mzigo wa samaki....wenzangu wananishangaa...SIRI SIRI SIRI....hafundishwi mpumbavu wa fikra.... hafundishwi "goyyim"....

Vingi havionekani na "wapumbavu"....ukiwa na telescope unaziona SAYARI kulingana na nguvu ya hiyo telecoscope....binafsi yangu nimeinunua "AMAZON" baada ya kudunduliza....haya mjinga wewe kataa kuwa sayari hazionekani....peleka visenti vyako "ubanda wa kangara" na kununua "mizoga yenye gono tu" [emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Sasa nini kiliwaua akati wanajua kuogelea???
...Ina maana mmoja alitaka kumuokpa mwenzie aliyekuwa anazama?? Ilikuwaje Mapacha Wawili wanaojua kuogelea Wakafa Wote Kwa Pamoja??
 
Kwahiyo yake mawimbi tunayoyaona ni majini? Kweli sijaona mwisho wa ujinga km nilivyodhani. Nchi hii kuna watu ni wajinga mpaka mnashangaza na kuacha rekodi.
Mkuu umeshawahi kuvua?!!!

Baharini yako mawimbi....huwa yanasababisha ajali....

Wako samaki wenye umeme....huwa wanasababisha ajali.....

Na pia yako mengine pia huwa yanasababisha ajali pia....ila ninyi "mbubu na wenye "mbango" mnaomlalamikia maisha yenu mh.Chifu Hangaya upumbavu huwa hauwatoki....karibu tunywe Al Kasus hapa nyamisati....nasubiri hesabu ya samaki.....[emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Ungeelewa Maana ya neno jinni kwa Kiswahili usingapata tabu kukijuwa.
Wenzake tunayatumia katika kupata pesa na maisha yanaendelea....aendelee kuatamia ufukara tu....[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
 
Japo pengine watu watakimbilia ushirikina lakini pengine hiki ndicho kilichotokea.

Kwa vile wote ni waogeleaji wazuri pengine walikuwa wameshaogelea kwa muda mrefu. Inawezekana mmoja alipata tatizo la misuli kukaza na akaanza kuzama. Mwenzake alipoona pacha wake anazama akaenda kumwokoa bila kuchukua tahadhari. Kwa sababu ya panic huyu aliyekuwa anazama akamrukia mwokoaji kwa namna ambayo hakuweza kuogelea tena na wote wakaishia kuzama.

Ni hatari sana kumwokoa mtu anayezama maana anakuwa tayari katika panic mode na anaweza akakung'ang'ania hata mikono ambayo ndiyo unaihitaji sana katika kuogelea. Mtu anayezama inabidi umshike kwa mbali tena kwa mkono mmoja tu halafu umvute huku wewe ukiogelea. Ukijichanganya tu ukamsogelea kuna hatari ya wote kufa. Hapo lazima kuna mmoja amekufa akijaribu kuokoa maisha ya mwenzake.

Na hili tatizo la misuli kukaza aisee linashangaza sana maana hata mimi lilishawahi nitokea. Mimi ni mwogeleaji mzuri tu mpaka wa maji yanayotembea. Nimechukua pia darasa la kuogelea kabisa ili kujifunza jinsi ya kubakia juu ya maji bila kutumia nguvu nyingi.

Sasa siku moja nilikuwa naogelea katika bwawa kubwa la hoteli moja iitwayo Omni Resorts kule Orlando, Florida. Nilikuwa nimeogelea kwa zaidi ya masaa mawili na kilichokuwa kimenibakiza pale ni kwamba kulikuwa na mishangazi ya uhakika kibao myeusi na mizungu ipo kwenye bikini tu inajibinua. Basi nikajikuta nimefurahia kutazama ile misambwanda ya kufa mtu huku nasukumizia na chicken wings za hapa na pale. Na mingine tukawa tumezoeana zoeana mpaka tunapiga na vistori vya hapa na pale.

Basi bana baada ya kukaa kwenye kijua kwa muda kwenye hivi viti vya kulaza hivi nikajitosa kule kwenye kina kirefu (futi 12). Eeee bana eeeh!

Najaribu kuogelea hivi hakuna kinachojongea. Misuli imekaza mikono na miguu haisogei. Kengele ya tahadhari ikalia kuwa haki ya nani kuna hatari ya ngosha kufia kwenye pool leo. Na mijimama yote hii dah! Aibu iliyoje!

Nikajaribu tena lakini nikakuta hakuna kinachojongea na hapo tayari nshapiga vikombe kadhaa vikubwa tu. Bahati nzuri sana karibu yangu kidogo kulikuwa na familia ya kizungu inaogelea na mtoto mmoja tineja aliniona akamwambia babake "I think he is drowning". Yule baba alimwita mhudumu mmoja aliyekuwa karibu hapo wana haya mafimbo marefu mwisho yana kama kikofia nchani huwa wanayatumia kuondolea uchafu unaoelea kwenye pool akaninyoshea nikadaka lile lifimbo macho yamenitoka hatari nahema balaa. Wakanivuta nikatoka nje.

Kwa vile nilikuwa nimeogelea pale kwa muda mrefu yule mfanyakazi akawa ananiuliza "What happened?" Nikamwambia I just can't move my hands and legs...Oooh muscle issues. It happens sometimes. Mpaka leo huwa nawaza ningekuwa peke yangu siku ile sijui ingekuwaje [emoji15]

Tangu hapo nikisikia mwogeleaji mzuri amezama wala huwa sishangai. Na baadaye niliambiwa kuwa tatizo hilo linaweza kusababishwa na upungufu wa madini ya Magnesium mwilini na au sehemu fulani ya misuli kukosa hewa ya Oksijeni kwa ghafla. Inapaswa kuwa hydrated pia maana ukiwa dehydrated misuli inaweza kukugomea wakati wo wote. Ulaji wa chungwa moja au mawili pamoja na ndizi pia unasaidia kuzuia tatizo hilo. Wacheza soka na michezo mingine pia wanalijua tatizo hili na sijui huwa wanatumia mbinu gani kulizuia.

[emoji3591][emoji3591][emoji3591] Vijana wadogo tu masikini maisha yao yamekatizwa. Wapumzike salama [emoji1545]
[emoji106]
Ngosha wa Orlando Florida huyoooo.....

Yashilagga guukuuu [emoji1787]
 
Dah,huzuni,yaani unatafuta kujua hata nini kilitokea unakosa majibu kabisa,ili mradi tu ilikuwa wafe...
 
Sishangai sababu iliyotolewa na hilo jeshi la uokoaji , jumapili moja nikiwa maeneo ya kigamboni kule darajani nanyosha miguu , chini walionekana watu wakiogelea kipindi hicho hawajaanza kukataza watu kuogelea pale , kwa mbali kulikuwa na vijana wawili ( baadae ilifahamika kuwa ni wanachuo toka DUCE ) waliokuwa wakipiga kasia wakiwa kwenye ile mitubwi midgo ainayopark pembezoni mwa bahari ,.

huku na kule wakawa pale katikati ya daraja , sijui ikawaje mtubwi ukapinduka juu chini , eeehh !! Katika wote wawili hamna hata mmoja ajuaye kuogelea bahati nzuri mmoja alikuwa karibu na mtubwi ule akaushika ili asizame , huyu mwingine alikuwa mbali kidogo ukizingatia kuogelea hajui basi huwezi amini kijana alizama. Watu tukiwa tunamuona hivi hivi . Ilikuwa yapata saa kumi na mbili na nusu jioni huwezi amini askari wa pale walipewa taarifa mapema tu juu ya lile tukio lakini pindi walipo fika huwezi amini waliishia kutufukuza wotee tuliokuwepo pale na kututaka turudi kesho asubuhi kwa ajilii ya kuuchukua mwili eti kwasababu bahari haijawahi kukaa na uchavu katika tika .
 
Kuna samaki anaitwa mkunga kwa kiingereza electric eel.

Huyu samaki ana uwezo wa kukupiga shoti.

Inaaminiwa wengi wanaopotea baharini na kwenye maziwa yawezekana walipigwa shoti na mkunga wakapatwa na stroke au cardiac arrest na kuzama.
Exquisite [emoji7]
 
Back
Top Bottom