Aprinary Jr
New Member
- Nov 27, 2018
- 2
- 1
Wapumzike kwa amani
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
MmhWamefikia kumi nsaivi nasikia
Mfano ile barabara ya Morogoro kutoka komoa hadi Masika mzigo una sehemu ya magari watembea kwa mguu na waendesha baiskeli ila bado kuna mbwa zinapita na bodaboda huu upande wa watembea kwa miguu trafiki wakamate uso dog mara moja pleaseBarabara inapojengwa msanifu huweka kitu kinaitwa Road shoulders
Kazi ya shoulders ni kufanya watembea Kwa miguu kupita pamoja na makundi ya wenye uhitaji maalumu
Sasa hivi shoulders zinatumika vibaya na viongozi wanaangalia tuu humo utakuta ndio sehemu ya Jogging, machinga kupanga vitu chini, pamoja na parking za magari Kwa baadhi ya sehemu mfano msimbazi road nk
Najiuliza swali je dereva akikosea hapo wa kulaumiwa ni serikali, au dereva?
Tuchukue hatua kabla ya kuanza kulalamika
R I P wote mliopoteza maisha Mungu awapokee salama muendako
...Inaelekea Njemba alikuwa Kasi Sana! Mpaka vyuma vya gari vimepinda hivyo Kwa kugonga TU Watu ??[emoji26]Watu 6 wamefariki dunia na wengine 14 kujeruhiwa katika ajali iliyohusisha gari binafsi, ambalo limewagonga wananchi waliokuwa wakifanya mazoezi kandokando ya barabara eneo la Sabasaba Ilemela Mwanza leo Julai 22, 2023 majira ya asubuhi.
=====
Taarifa za awali ni kwamba Watu 6 wamefariki dunia na wengine 14 kujeruhiwa katika ajali iliyohusisha gari binafsi, ambalo limewagonga wananchi waliokuwa wakifanya mazoezi kandokando ya barabara eneo la Sabasaba Ilemela, Jijini Mwanza.
Chanzo cha ajali ni mwendokasi na Dereva kutozungatia Sheria na alama za barabarani.
Miili ya Waliofariki na Majeruhi wa ajali wamepelewa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Sekou toure.
============
UPDATES...
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Gideon Msuya “Imetokea katika Wilaya ya Ilemela, gari aina ya Toyota Hilux lenye namba za usajili T476 DZL ikitoka Sabasaba kuelekea Buswelu ilipoteza mwelekeo kutokana na mwendokasi na kusababisha ajali iliyoua watu 6, kujeruhi 14 waliokuwa wakifanya mazoezi ya kukimbia ambapo jumla yao walikuwa 27.
"Majeruhi wanne wapo Hospitali ya Bugando, wengine 10 wapo Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Sekou Toure.
“Juhudi za kumtafuta Dereva zinaendelea kwa kuwa alikimbia mara baada ya tukio hilo.”
UPDATES
======
Mwanza. Watu sita wamefariki papo hapo na wengine 16 wakijeruhiwa baada ya kugongwa na gari aina ya Hilux double cabin eneo la Shule ya Msingi Lumala Wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza.
Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza, Gideon Msuya amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo asubuhi ya leo Julai 22, 2023 wakati kikundi cha vijana kilichotambulika kwa jina la Adden hotel kikiwa kinafanya mazoezi ya kukimbia katika barabara ya sabasaba kuelekea Kiseke wilayani humo.
Msuya amesema msako wa dereva wa gari hiyo unaendelea baada ya kulitelekeza kwenye kituo cha mafuta kisha yeye kutokomea kusikojulika.
Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Sekouture, Dk Bahati Msaki amesema wamepokea miili ya watu watano huku mmoja akifariki akipatiwa matibabu hospitalini hapo na majeruhi 8 wanaendelea na matibabu huku 8 wakipatiwa rufaa kwenda Hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando kwa uangalizi maalum.
“Vijana hao walikuwa wanafanya mazoezi ya mwendo wa pole wakiwa na kundi lao Linalotambulika kwa jina la Adden hotel,”amesema Dk Msaki
Dk Msaki amesema miili ya marehemu ipo katika Hospitali ya Mkoa Sekou Toure huku taratibu za kuikabidhi kwa ndugu zinaendelea kuratibiwa na hospital ya Sekou Toure na Jeshi la polisi Mkoa wa Mwanza.
“Nitoe pole kwa familia waliopoteza wapendwa wao na tuendelee kuwaweka kwenye maombi majeruhi wote wapate uponyaji wa haraka na waruhusiwe warudi nyumbani kuendelea na majukukumu yao,”amesema Dk Masala
View attachment 2696406View attachment 2696408
Matumbi wapi tabata au🤣Leo nimebutulia na bodaboda tairi la nyuma nilikuwa na baskeli matumbi pale maboda boda bora wanavyokufa na ajali kwakweli washenzi sana.
🤓🤓🤓🤓 Wee jamaa kuwa seriously basiArusha kuna jamaa huwa anakimbia kinyumenyume kwenye barabara kuu,ujinga
Kuna watu wanatembea na earphone na earpods hao kujeruhiwa ni nuktaMiundombinu yetu ni hovyo.
Ni kweli usemavyo. Hapa kwetu si kukimbia tu hata kutembea kando ya barabara ni hatari tupu ukijumlisha na ujinga wa watu wetu ni balaa juu ya balaa.
Mkuu mbona una makasiriko🤣🤣🤣🤣Hili ndio tatizo
Kujionyesha bila aibu
Ndio laana hizo na wataparamiwa sana kwa kukosa akili
Jitu zima linafanya jogging kwenye barabara kote kujionyesha
Mi ni mfanya mazoez ila hz joging club huwa zinaniboa mno ni watu wapenda sifa sana kujionyesha kutwa kupiga makelele mbona wengine tunafanya mazoez kimya kimya wao sijui huwa wanajikuta nani?Alafu asubuhi asubuhi wanatupigia kelele...
Piga tizi, jenga afya yako kimya kimya,,,
Sio hasira bali wanakera kwa kutokujitambuaMkuu mbona una makasiriko[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
watu 6 kwa pamojaa sio mchezooo...Tuna maeneo mengi ya kukimbia na kufanyia mazeoezi mbali na barabara mkuu.
Basi na tuendelee kukimbia katikati ya barabara sasa
Hii ndio tz🤣🤣🤣🤣Fanyia mazoezi kwako, uwanjani au open space.hii ni Tz barabara ni ndogo driver akibanwa anakuletea, ukikimbia mitaani akiitiwa mwizi umekwisha.
Chaguo ni lako!