Mwanza: Watu 6 wafariki kwa kugongwa na gari wakifanya mazoezi

Mwanza: Watu 6 wafariki kwa kugongwa na gari wakifanya mazoezi

Barabara inapojengwa msanifu huweka kitu kinaitwa Road shoulders

Kazi ya shoulders ni kufanya watembea Kwa miguu kupita pamoja na makundi ya wenye uhitaji maalumu

Sasa hivi shoulders zinatumika vibaya na viongozi wanaangalia tuu humo utakuta ndio sehemu ya Jogging, machinga kupanga vitu chini, pamoja na parking za magari Kwa baadhi ya sehemu mfano msimbazi road nk
Najiuliza swali je dereva akikosea hapo wa kulaumiwa ni serikali, au dereva?
Tuchukue hatua kabla ya kuanza kulalamika

R I P wote mliopoteza maisha Mungu awapokee salama muendako
 
Barabara inapojengwa msanifu huweka kitu kinaitwa Road shoulders

Kazi ya shoulders ni kufanya watembea Kwa miguu kupita pamoja na makundi ya wenye uhitaji maalumu

Sasa hivi shoulders zinatumika vibaya na viongozi wanaangalia tuu humo utakuta ndio sehemu ya Jogging, machinga kupanga vitu chini, pamoja na parking za magari Kwa baadhi ya sehemu mfano msimbazi road nk
Najiuliza swali je dereva akikosea hapo wa kulaumiwa ni serikali, au dereva?
Tuchukue hatua kabla ya kuanza kulalamika

R I P wote mliopoteza maisha Mungu awapokee salama muendako
Mfano ile barabara ya Morogoro kutoka komoa hadi Masika mzigo una sehemu ya magari watembea kwa mguu na waendesha baiskeli ila bado kuna mbwa zinapita na bodaboda huu upande wa watembea kwa miguu trafiki wakamate uso dog mara moja please
 
Watu 6 wamefariki dunia na wengine 14 kujeruhiwa katika ajali iliyohusisha gari binafsi, ambalo limewagonga wananchi waliokuwa wakifanya mazoezi kandokando ya barabara eneo la Sabasaba Ilemela Mwanza leo Julai 22, 2023 majira ya asubuhi.


=====
Taarifa za awali ni kwamba Watu 6 wamefariki dunia na wengine 14 kujeruhiwa katika ajali iliyohusisha gari binafsi, ambalo limewagonga wananchi waliokuwa wakifanya mazoezi kandokando ya barabara eneo la Sabasaba Ilemela, Jijini Mwanza.

Chanzo cha ajali ni mwendokasi na Dereva kutozungatia Sheria na alama za barabarani.

Miili ya Waliofariki na Majeruhi wa ajali wamepelewa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mwanza Sekou toure.

============

UPDATES...
Kaimu Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mwanza, Gideon Msuya “Imetokea katika Wilaya ya Ilemela, gari aina ya Toyota Hilux lenye namba za usajili T476 DZL ikitoka Sabasaba kuelekea Buswelu ilipoteza mwelekeo kutokana na mwendokasi na kusababisha ajali iliyoua watu 6, kujeruhi 14 waliokuwa wakifanya mazoezi ya kukimbia ambapo jumla yao walikuwa 27.

"Majeruhi wanne wapo Hospitali ya Bugando, wengine 10 wapo Hospitali ya Rufaa ya Mkoa ya Sekou Toure.

“Juhudi za kumtafuta Dereva zinaendelea kwa kuwa alikimbia mara baada ya tukio hilo.”

UPDATES
======

Mwanza. Watu sita wamefariki papo hapo na wengine 16 wakijeruhiwa baada ya kugongwa na gari aina ya Hilux double cabin eneo la Shule ya Msingi Lumala Wilaya ya Ilemela mkoani Mwanza.

Kaimu Kamanda wa Polisi mkoa wa Mwanza, Gideon Msuya amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo asubuhi ya leo Julai 22, 2023 wakati kikundi cha vijana kilichotambulika kwa jina la Adden hotel kikiwa kinafanya mazoezi ya kukimbia katika barabara ya sabasaba kuelekea Kiseke wilayani humo.

Msuya amesema msako wa dereva wa gari hiyo unaendelea baada ya kulitelekeza kwenye kituo cha mafuta kisha yeye kutokomea kusikojulika.

Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Sekouture, Dk Bahati Msaki amesema wamepokea miili ya watu watano huku mmoja akifariki akipatiwa matibabu hospitalini hapo na majeruhi 8 wanaendelea na matibabu huku 8 wakipatiwa rufaa kwenda Hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando kwa uangalizi maalum.

“Vijana hao walikuwa wanafanya mazoezi ya mwendo wa pole wakiwa na kundi lao Linalotambulika kwa jina la Adden hotel,”amesema Dk Msaki

Dk Msaki amesema miili ya marehemu ipo katika Hospitali ya Mkoa Sekou Toure huku taratibu za kuikabidhi kwa ndugu zinaendelea kuratibiwa na hospital ya Sekou Toure na Jeshi la polisi Mkoa wa Mwanza.

“Nitoe pole kwa familia waliopoteza wapendwa wao na tuendelee kuwaweka kwenye maombi majeruhi wote wapate uponyaji wa haraka na waruhusiwe warudi nyumbani kuendelea na majukukumu yao,”amesema Dk Masala
View attachment 2696406View attachment 2696408
...Inaelekea Njemba alikuwa Kasi Sana! Mpaka vyuma vya gari vimepinda hivyo Kwa kugonga TU Watu ??[emoji26]
RIP Marehemu na Poleni Sana Wafiwa..
 
Juzi kati nipo maeneo ya redstone-moshi (saa 12 asubuh) zile basi za mikoani zilichonifanya pamoja na lile roli dah kweli Mungu bado ananipenda. na kiherehere cha kukmbia ile rod kiliisha sku ile ile
 
hivi hawa walikuwa wanakimbia katikati ya bara bara au?? sema barabara za bongo zimebana mnooo yanii watembea kwa miguu hakuna nafasii kabisaa so jamaa itakuwa alikuwa mwendo wa ngirii alafu hawa jamaa wanatabia ya mmoja anatangulia mbele na kibendera chekundu sasa haitoshi aiseee... jogging za makundi bongo ni risk mnoo
 
ninatoa pole za dhati kwa wanamazoez wenzetu,Mungu afanyike faraja kwa familia [emoji120]

Ajali zingne hazina kinga,tuwe waangalifu tunapokua barabaran,maderava wengi sio watu makini,zile kaz znachosha na kuvuruga akili
 
Tuna maeneo mengi ya kukimbia na kufanyia mazeoezi mbali na barabara mkuu.
Basi na tuendelee kukimbia katikati ya barabara sasa
 
Back
Top Bottom