Mwenye jengo akamatwe, eneo liuzwe, mali zake zifilisiwe, halafu hela zote wapewe majeruhi na waliofiwa

Mwenye jengo akamatwe, eneo liuzwe, mali zake zifilisiwe, halafu hela zote wapewe majeruhi na waliofiwa

Halafu wewe ndio unakuja kupewa uongozi au hata ukuu wa mkoa nahisi utachinja sana watu,uongozi ni hekima na busara
Hekima na busara nyingi nchini kwetu ndio zimesababisha mianya ya rushwa, wizi, uzembe, ufisadi nk.

China iliyokuwa inashindwa uchumi hata na Zimbabwe miaka ya 70, leo hii ndio nchi ya pili kwa uchumi duniani, hii yote imewezekana baada ya kuweka mambo ya busara na hekima pembeni. Sasa sisi tutakalia kuzubazwa na mambo ya hekima na busara huku hao wanaotufubaza na mambo hayo ya heshima na busara wakiendelea kutuibia na kujitajirisha wao na familia zao.
 
Niaje waungwana

Kwa kile kilichotokea jana hapo K'koo, mimi nashauri kwanza mwenye ghorofa lililoanguka akamatwe, mali zake zifilisiwe, na kiwanja kilichokuwa na jengo kiuzwe ili hela zitakazopatikana zitumike kuwasaidia wale wote waliojeruhiwa na waliofiwa na baba zao, wame zao, wake zao, watoto wao nk.

Ni ukweli ulio wazi kwamba baada ya msiba huu wa taifa kuisha na kila mtu kuendelea na maisha yake, kuna ndugu zetu ambapo watabakia na ulemavu wa kudumu, kuna watu ambao watabakia mayatima baada ya kupoteza baba au mama katika janga hilo. Sasa watu wa aina huyo ni nani atakaewasaidia kuwasomesha, kuwalea, kuwahudumia nk.

Najua kwa upande wa serikali ni vigumu sana wahanga kupata msaada hapo baadae. Maana janga likishaisha kila mtu ataelekea ya kwake, hivyo waliofiwa na wazazi wao hawatopata msaada tena. Kwa nchi za wenzetu ile bajeti inayotengwa kila mwaka kwa ajili ya majanga ingetumika kuwasaidia waliokumbana na majanga hayo japo kwa kuwapa mitaji waathirika.

Lakini kwa nchini kwetu ndo hivyo tena, fedha za majanga zinaishia kutumiwa na viongozi fulani kwa kununua viwanja na kujenga majengo makubwa makubwa huko Mbweni, Salasala, Bunju nk.

Halafu yanapotokea majanga ya ghafla kama haya unakuta wanakuja na majembe pamoja na kuleo kuchimbia kifusi kizito cha tani zaidi ya 50. Kuna watu wameachwa yatima wengine wamepoteza viungo vyao kizembe kwa sababu ya tamaa ya mtu mmoja.

Hivyo huyo mtu aadhibiwe kwa kunyang'anywa kiwanja ili kuizwe na hela kupelekwa kwa wahusika, hii ikiwa pamoja na kutaifisha mali zake zote alizochuma iwe kihalali au kiharamu ili kufidia hasara aliyowapa wenzake hapa duniani na pia iwe fundisho kwa wapumbavu wengine wenye mawazo finyu kama yake.

Soma Pia: Ghorofa limeporomoka Kariakoo asubuhi ya leo Novemba 16

Ushauri mzuri kwa mamlaka na wahusika mbali mbali.

RIP kwa watanzania wenzetu wote waliokufa katika ajali hiyo. Na wale waliopata majeraha Mungu muweza wa yote awaponye.

Asanteni
Acha upumbavu, Maskini mna tabu sana , kwani hilo ni jengo la kwanza kuanguka duniani hii
 
Huyo tajiri uchwara na tamaa za kijinga
Kuna vijana wangapi hawana ajira na wamesoma wangeweza hata kusimamia ila ameoana awape kibarua cha elfu 50 kina maiko
Waarabu huwa wana msemo wa kuwa Bahili huwa wanapata hasara x2
Zile NONDO ukiziangalia wewe hata km sio fundi unashtuka kidogo huyu fundi maiko aliwaza nini kupachika NONDO hizi kwenye jengo linalobeba tani kwa tani za mizigo
 
Niaje waungwana

Kwa kile kilichotokea jana hapo K'koo, mimi nashauri kwanza mwenye ghorofa lililoanguka akamatwe, mali zake zifilisiwe, na kiwanja kilichokuwa na jengo kiuzwe ili hela zitakazopatikana zitumike kuwasaidia wale wote waliojeruhiwa na waliofiwa na baba zao, wame zao, wake zao, watoto wao nk.

Ni ukweli ulio wazi kwamba baada ya msiba huu wa taifa kuisha na kila mtu kuendelea na maisha yake, kuna ndugu zetu ambapo watabakia na ulemavu wa kudumu, kuna watu ambao watabakia mayatima baada ya kupoteza baba au mama katika janga hilo. Sasa watu wa aina huyo ni nani atakaewasaidia kuwasomesha, kuwalea, kuwahudumia nk.

Najua kwa upande wa serikali ni vigumu sana wahanga kupata msaada hapo baadae. Maana janga likishaisha kila mtu ataelekea ya kwake, hivyo waliofiwa na wazazi wao hawatopata msaada tena. Kwa nchi za wenzetu ile bajeti inayotengwa kila mwaka kwa ajili ya majanga ingetumika kuwasaidia waliokumbana na majanga hayo japo kwa kuwapa mitaji waathirika.

Lakini kwa nchini kwetu ndo hivyo tena, fedha za majanga zinaishia kutumiwa na viongozi fulani kwa kununua viwanja na kujenga majengo makubwa makubwa huko Mbweni, Salasala, Bunju nk.

Halafu yanapotokea majanga ya ghafla kama haya unakuta wanakuja na majembe pamoja na kuleo kuchimbia kifusi kizito cha tani zaidi ya 50. Kuna watu wameachwa yatima wengine wamepoteza viungo vyao kizembe kwa sababu ya tamaa ya mtu mmoja.

Hivyo huyo mtu aadhibiwe kwa kunyang'anywa kiwanja ili kuizwe na hela kupelekwa kwa wahusika, hii ikiwa pamoja na kutaifisha mali zake zote alizochuma iwe kihalali au kiharamu ili kufidia hasara aliyowapa wenzake hapa duniani na pia iwe fundisho kwa wapumbavu wengine wenye mawazo finyu kama yake.

Soma Pia: Ghorofa limeporomoka Kariakoo asubuhi ya leo Novemba 16

Ushauri mzuri kwa mamlaka na wahusika mbali mbali.

RIP kwa watanzania wenzetu wote waliokufa katika ajali hiyo. Na wale waliopata majeraha Mungu muweza wa yote awaponye.

Asanteni
Mbona Mabasi yanaua Kila siku sijawahi sikia mwenye basi akikamatwa na Mali zake kuuzwa kugawiwa waliopata ajali?
 
Hilo linawezekana kabisa lakini sio kwa awamu hii

Kwanza huyo mmiliki hatawalipa chochote hao wahanga na badala yake yeye ndio atalipwa na kampuni ya bima na mwaka mmoja baadae anaruhusiwa kujenga upya Hilo gorofa lake na ataendelea kufanya biashara kama kawaida.

Nchi ikishakuwa corrupted kwenye Kila sekta tegemea kuona mambo mazito yakichukuliwa kwa wepesi sana.
 
Serikali yako imemkalia kimya sababu inamjua ni mtata na hayupo mwenyewe ana genge lake behind ndio maana husikii hata mmoja anaemnyooshea kidole
Sidhani kama serikali imemkalia kimya sababu ya utata. Hakuna mwenye nguvu mbele ya serikali. Ila naweza kukubaliana na wewe kama utasema kuwa jamaa ana kadi na ni mwanachana kindaki ndaki wa kijani, hapo nitakuelewa.

Ukitaka kujua kama serikali inaweza kumhenyesha jamaa, athubutu kuunga mkono au kufadhili chama cha upinzani wazi wazi ndo utapojua kwamba serikali ni dude la namna gani. Jamaa anaweza kupewa kesi ya uhujumu uchumi au ya uhaini kwamba alitaka kumuua kiongozi mkubwa wa nchi, kupindua serikali nk.
 
Mtanganyika mmoja wapo ni wewe wahi mahakamani ukamfungulie kesi mwenye Jengo uone anavyoinunua mahakama mpaka wewe mwenyewe
Ipo siku Mimi wewe na yule tutabadili fikra na kuamini tunaweza kubadili nchi yetu. Tusi wape nguvu watesi wetu waone akili zetu zimefika mwisho. Ipo siku mahakama zitatenda haki. Ya Mungu ni mengi!
 
Sidhani kama serikali imemkalia kimya sababu ya utata. Hakuna mwenye nguvu mbele ya serikali. Ila naweza kukubaliana na wewe kama utasema kuwa jamaa ana kadi na ni mwanachana kindaki ndaki wa kijani, hapo nitakuelewa.

Ukitaka kujua kama serikali inaweza kumhenyesha jamaa, athubutu kuunga mkono au kufadhili chama cha upinzani ndo utapojua kwamba serikali ni dude la namna gani. Jamaa anaweza kupewa kesi ya uhujumu uchumi au ya uhaini kwamba alitaka kumuua kiongozi mkubwa wa nchi, kupindua serikali nk.
Babu Serikali hata kumzungumzia haijathubutu ndio ujue yeye ni dude kubwa kiasi gani
 
Zile NONDO ukiziangalia wewe hata km sio fundi unashtuka kidogo huyu fundi maiko aliwaza nini kupachika NONDO hizi kwenye jengo linalobeba tani kwa tani za mizigo
Majumba mengi hayana ubora ni mda tu tutaona mengi
Hawa waliopewa kazi ya kubomoa ukuta ni wengine maana walianza majuzi tu kubomoa ukuta wa gorofa
Sasa hawa wameambiwa watoe miguu utasimama na nini?
Hao walioweka nondo ni makanjanja wengine
 
Ipo siku Mimi wewe na yule tutabadili fikra na kuamini tunaweza kubadili nchi yetu. Tusi wape nguvu watesi wetu waone akili zetu zimefika mwisho. Ipo siku mahakama zitatenda haki. Ya Mungu ni mengi!
Hio siku ni lini ambayo mahakama itatenda haki? Na hapo unataka kusemaje kwamba mahakama ikamkamate mwenye Jengo na kumfungulia kesi?
 
Back
Top Bottom