Mwenye ushahidi au maelezo toshelezi jinsi Katiba ilivyomletea umasikini/utajiri

Mwenye ushahidi au maelezo toshelezi jinsi Katiba ilivyomletea umasikini/utajiri

Ngoja kidogo nijaribu kufafanua kwa kadri ya mtazamo wangu.....

Katiba ni sheria mama katika kuongoza na kuendesha nchi.

Katiba nzuri huzalisha utawala bora unaozingatia haki na usawa kwa wananchi wake pasi na kuangalia hadhi na nafasi ya mtu.

Katiba bora inayozingatia haki na usawa huleta uwajibikaji na uwajibishwaji kwa wote na wale wanaokiuka.........

Katiba bora ambayo huzaa utawala bora na uwajibikaji huzalisha sera nzuri na mipango ya kimaendeleo kwenye jamii husika....sera hizo na mipango mizuri ikiingia katika uwajibikaji humgusa mwananchi moja kwa moja.

Kwa mfano katiba inasema kila mtu ana haki ya kuishi kwa amani na usalama.....jeshi la polisi kupitia wizara ya mambo ya ndani au jeshi la ulinzi kupitia wizara ya ulinzi vitalazimika kutunga sera na mipango ya kumhakikishia huyu mtu usalama na amani itakayomfanya kuweza kufanya shughuli zake za kujiletea maendeleo pasi na hofu yoyote.

Mfano katiba inasema kuwa kila mtu ana haki ya kuishi....serikali kupitia wizara ya afya watatunga sera na mipango ya kuboresha huduma za afya ili watu waishi maisha mazuri yenye siha njema......na sheria kali na adhabu vitatungwa kwa yoyote atakayejaribu kudhurumu haki hiyo.

Hiyo ni mifano ya mambo machache yanayoonyesha namna ambavyo katiba inakugusa moja kwa moja au sio moja kwa moja kupitia sera na mipango katika utekelezaji wa matakwa ya kikatiba.

NB;
Huo ni mtazamo wangu tu kwa jinsi nilivyoona.....
 
Kwanza tungekuwa na katiba imara muda huu kama sio kufa John Joseph Pombe Magufuli angekuwa jela maana kauli zake zilikuwa zinachochea fujo. Imagine kauli kama ile ya nikulipe mshahara halafu umtangaze mpinzani ile kauli inachochea fujo vurugu na visasi sasa hayo maendeleo na huo ugali mezani vitakujaje kama nchi ina machafuko?
 
Halafu pia katiba inaleta utabirikaji wa viongozi predictability leo mnaona katiba sio muhimu kwakuwa ccm iko madarakani na ina wafavor nyinyi! Siku game likigeuka na ccm ikawa wapinzani ndio mtajua umuhimu wa katiba.
 
Huoni manufaa ya media zenye nguvu na zilizo huru zinazoweza kuibua ufisadi bila woga na watu wakawajibika? huoni kuna kasoro kama mtu mmoja anaweza kuzima internet nchi nzima? unaona sawa mwanasiasa kama mkuu wa wilaya kukuweka ndani bila mashtaka?
Ndugu bado waTanzania wengi wapo gizani tena la Totoro kabisa ambalo haoni hata mbele ya mkono wake.....

Imagine swali linaulizwa na mtu ambaye ana access na vitoa taarifa na maarifa kiganjani je mwananchi wa huko mashambani atakuwa na hali gani.

Ndio maana serikali ya CCM kwa makusudi kabisa wanaharibu mifumo ya kielimu ili watu waendelee kubakia ujingani.....maana huo ndio mtaji kwao.

Sasa kama mtu hajui namna sheria mama inavyomgusa moja kwa moja utamueleza nini kuhusu utawala bora na uwajibikaji?

Kwa kweli tuna safari ndefu.
 
Ulaya na Marekani baada ya kuuwana sana na mavita kibao wakaona watengeneze sheria kali na wazilinde ili kutoruhusu tena umwagaji damu ulaya.

Rejea napoleon wars unification wars civil wars spanish wars nk huku afrika mnasubiri mpaka tuchinjane kwanza ndio mlete katiba mpya. Rejea kenya
 
Ndugu bado waTanzania wengi wapo gizani tena la Totoro kabisa ambalo haoni hata mbele ya mkono wake.....

Imagine swali linaulizwa na mtu ambaye ana access na vitoa taarifa na maarifa kiganjani je mwananchi wa huko mashambani atakuwa na hali gani...
Aisee ni Hatari mno...hadi naona kama hii ni kejeli labda!

Huwa naumia sana Kiongozi msomi anapowapotosha watu kuwa Katiba Si mkate!
 
Aisee ni Hatari mno...hadi naona kama hii ni kejeli labda!
Huwa naumia sana Kiongozi msomi anapowapotosha watu kuwa Katiba Si mkate!
Hicho unachokiona sio kejeli bali ni uhalisia wa huku mitaani.....watu wana uelewa mdogo sana juu ya mambo yanayowazunguka.

Watu wengi wanauimba wimbo wa katiba mpya kwa sababu unaimbwa na wanasiasa lakini wengi wao hata hawajui maana ya katiba Nini?

Ukitazama sera zetu na mipango ya elimu ndio utajua kwanini CCM wanaendelea kubakia madarakani.....
 
Katiba bora inaweka Msingi Imara wa UUwajibikaji na Uwazi..Leo hii Kuna miradi inabiniwana mtu mmoja na Bunge oinaipitishakwa woga, Leo tuwekeza kwenye Gesi ,kesho Umeme wa jua ..hakuna mwongizo na huko kote Fedha zinateketea, Kila mwaka ÇAG anaanika madudu lakini hakuna kinachofanyika ..Bunge haina meno!

Angalia jinsi miktaba ya Madini ilivyo Siri na kule tunaibiwa ..hakuna Uwazi!Mlipokuwa mnashangilia JPM akizungumzia Miktaba mibovu ya Madini mlifilkir suluhisho ni kuwa mkali na kuleta propaganda!? Alifikianwapi..suluhisho hapo ni kuwa na Uwazi ...Katiba!

Kama akili za mtu anayeweza kuingia JF zipo hivi, vipi za Mchunga mbuzi kule Maniambia!
Swali kwenye uzi hujalijibu mkuu. Hayo uliyajibu yanamafuaa kwa wanasiasa vipi kuhusu kuodoa njaa na unasikini?
 
Kama katiba mpya ndiyo muarobaini wa umasikini wa mtu mmoja mmoja,

Je matajiri wa sasa wao wanatumia katiba ipi?

NB:Kuna watu wamefanikiwa kimaisha bila hata kufungamana na CCM.
 
Kama katiba mpya ndiyo muarobaini wa umasikini wa mtu mmoja mmoja,

Je matajiri wa sasa wao wanatumia katiba ipi?

NB:Kuna watu wamefanikiwa kimaisha bila hata kufungamana na CCM.
Akili ya division 0
 
Kupitia katiba hii hii tumeshudia mafisadi wakipelekwa mahakamani, tumeshudia wazembe wakitumuliwa kazini, tumeshuhudia mali hasili zikilindwa na kulinufaisha taifa sasa hapo tatizo ni katiba au ni wale wanaosimamia katiba.

..tatizo la wanaosimamia katiba linatokana na matobo na mianya iliyoko ktk katiba yenyewe.

..Tanzania tuna KATIBA WEZESHI kwa wahujumu, mafisadi, na majizi ya rasilimali.

..Wanaopelekwa mahakamani ni wale wasiopendwa au waliokosana na genge lililoko madarakani.

..Chukulia suala la Sabaya. Kwanza jiulize aliweza vipi kufanya uhuni wote alioufanya. Pili jiulize kwanini ni yeye peke yake amebuzwa mahakamani.

..Au kama ulifuatilia kesi ya Mbowe. Hivi mpelelezi mkuu wa kesi ile anastahili kupandishwa cheo?

..Zaidi, fuatilia madudu yaliyotokea huko nyuma kama kashfa ya Escrow. Uhuni huo uliwezekana kwasababu Katiba na Sheria zetu haziwezi kuzuia wizi wenye baraka za IKULU.
 
Lengo la katiba mpya ni kumpunguzia madsraka rais, kushughulikia kero za muungano.na kutafuta tume huru ya uchaguzi. Mengine mbwembwe tu za kina lisu.

Hii imelenga kuiondoa ccm madarakani kupitia ballot box.

Katiba mpya haina cha kuongeza ama kupunguza ukali wa maisha ya mtanzania ila imelenga kurahisiha safari ya wanaodai katiba mpya kuingia ikulu and nothing more.

Niwape methali
Zimwi likujualo jalikuli likaakwisha
Heri nusu shari kuliko shari kamili
Majuto ni mjukuu

Mimi nilienda ccm kumfuata magu nikitokea cdm ambako nlimfuata dr. Slaa. Kwa sasa nina kadi za hivi vyama 2 ila kiukweli kati ya hivi vyama hakuna kiongozi ninayemkubali kwa sasa.

Kwa ccm labda waziri mkubwa na kwa cdm kwa mbali sana mzee wa konyagi. Ila toto tundu aka mzee wa marisasi 30 huyo mdomo wake umejaa matusi, kejeli na uhuni tu akili hana, anawaza kupeleka washeli ubeliji.

Ubeliji ukifuatilia sana historia imehusika kufanya mauaji ya viongozi wengi africa akiwemo P lumumba, imehusika kutengeneza migogoro mingi africa na dam za ndugu zetu wengi zikamwagika. Nina wasiwasi mno pengine kile kifo kilixhoshangiliwa sana na toto tundu wamehusika pia.
 
Wakenya wape muda kidogo, Kenya ule upuuzi wa Raisi kuzima internet nchi nzima kama alivyowafanyia Magu au watu kama Makonda na Sabaya kuweka watu ndani bila mashtaka wamesahau sasa and it will never come back, pesa wanakusanya inatumika ilipokusanywa kwa utaratibu mzuri sio chama cha siasa kinaamua, kuna mengi watafanikiwa kutokana na check and balance waliyoiweka kwenye katiba, na media sasa zina nguvu kuongea bila woga kitu ambacho ni muhimu sana kwa ustawi wa nchi inayofuata haki
Kenya inakatiba mpya miaka mingapi nyuma?

Hao waliokuwa wakizima internet hawakuwa ndani ya katiba mpya?
 
Katiba bora inaweka Msingi Imara wa UUwajibikaji na Uwazi..Leo hii Kuna miradi inabiniwana mtu mmoja na Bunge oinaipitishakwa woga..,Leo tuwekeza kwenye Gesi ,kesho Umeme wa jua ...
Mayo tena wajina wa babu yangu unaniangusha sana kusema JPM hakufanikiwa kwenye madini. Hivi kodi alikuwa anakusanya kwenye madini ambazo ndizo zilizofanya maendeleo mbalimbali huku akiacha kuwasumbua wananchi na vikodi vidogo vidogo leo hii umesahau?
 
Back
Top Bottom