Mwenye ushahidi au maelezo toshelezi jinsi Katiba ilivyomletea umasikini/utajiri

Mwenye ushahidi au maelezo toshelezi jinsi Katiba ilivyomletea umasikini/utajiri

Sidhani kama vichwapanzi wanaweza kukuelewa
Mimi hapa nimekuwa masikini wa kutupa kutoka katika maisha ya kawaida Kwa sababu ya katiba mbovu. Nilikua na Nyumba zangu mbili kimara zikavunjwa na sasa naishi uchochoroni Tandale uzuri, nimepanga chumba kimoja tu nalala chini sina chochote mali zangu zoote zilipotea hapa nilipo nimechoka na kupauka kama kipande cha muhogo mkavu

Nyumba zangu zilivunjwa kutokana na maamuzi ya Raisi kichaa aliyepewa madaraka makubwa na katiba iliyopo. Katiba ya sasa iliyompa nguvu ya kuamua anavyotaka yeye na hakuna wa kumfanya lolote Kwa sababu tayari anakua ana nguvu kuliko sheria au kuliko mfumo mzima uliomuwrka kwenye madaraka hayo

Nyumba zilivunjwa licha ya kesi kuwa ipo mahakamani kwenye zuio. Nilikua na biashara ya maduka katika Nyumba zote hizo iliyoniingizia kipato cha kuendesha maisha yangu na familia yangu kwa ustawi na muelekeo wa maendeleo kieleimu, kiuchumi na kijamii katika ngazi ya familia ambayo ilisimama katika misingi ya malezi bora na muelekeo chanya

Lakini bahati mbaya kutokana na katiba mbovu iliyo toa nafasi ya kuvunja haki ya utu wa mtu Kwa sababu ya ukubwa wa maamuzi ya kimadaraka aliyopewa Raisi. Baada ya kuvunjiwa nyumba Familia yangu yote ilisambaratika binti yangu kwa sasa anaishi kwa bwana na tayari ana watoto wawili akiwa na umri wa miaka 17 tu. Kijana wangu wa kiume sasahivi ni muokota chupa na siso huku akiwa nimtumiaji mzuri wa mihadarati

Watoto wangu wote walikatisha masomo wakiawa katika umri mdogo wa elimu ya msingi na kupoteza ndoto zote walizokuwa wakiziota kielimu, maisha yao yamepoteza dira wakiwa wanaishi kwa kubahatisha kama mimi baba yao huku nikiwa sina tena nguvu wala uwezo wa kuwasaidia Kwa sababu mimi mwenyewe sijielewi nimevurugwa kukucha nashinda hospitali kupambana na presha na sukari vilivyoanza baada ya kupoteza msingi wa maisha yangu

Haya yote ni matokeo ya kupoteza dira ya maisha baada ya kuvunjiwa Nyumba. Familia yangu ilisambaratika tukakosa sehemu ya kuishi mali zangu zote zilipotea ikiwemo vitu vya ndani watoto wangu walikwenda kuishi kwa rafiki wa Mama yao aliekuwa akiishi Tandale kwa mtogole huku Mama mtu akijaribu biashara ya Samaki feri iliyopelekea kupata bwana wa kumstiri na ndoa kuvunjika Kwa sababu mimi nilikua nimesha pagawa

Kwa kifupi ushahidi huo unakutosha kuanzia sasa jua kuwa KATIBA na MAISHA ni sawa na chumvi na mboga mpunbavu wewe
 
Mikopo tunayokopa Tanzania bara kwa maendeleo na wa zanzibar walikua wana 3% yao inapelekwa huko, na mlipaji wa mkopo ni Tanzania bara hiyo ni shida inayoletwa na katiba tena nasikia sahivi wanachukua 7% sio 3% tena
 
Sasa watu wachache kupiga pesa ndio Katiba.

Mbona Yuda alipiga pesa na hawakuwa hata na katiba. Upigaji ni Moja ya dhambi kongwe.


Sijaona katiba inapoingia hapo. Dadavua Kwa kina kidogo Bro
Ondoa upofu wa fikra
 
Mikopo tunayokopa Tanzania bara kwa maendeleo na wa zanzibar walikua wana 3% yao inapelekwa huko, na mlipaji wa mkopo ni Tanzania bara hiyo ni shida inayoletwa na katiba tena nasikia sahivi wanachukua 7% sio 3% tena
 
Wakati wa uanaharakati mazingira wa Pro. Wangari Maathai Kenya, kuna kiongozi mkubwa wa nchi alikuwa anshangaa mwanamama anayesema mvua inatokana na miti wakati inatoka mawinguni😂😂😂😂😂
 
[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787]
Wakati wa uanaharakati mazingira wa Pro. Wangari Maathai Kenya, kuna kiongozi mkubwa wa nchi alikuwa anshangaa mwanamama anayesema mvua inatokana na miti wakati inatoka mawinguni[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Kumbe tunabishana na mtoto mdogo hapa? Wewe ni muha wa Kigoma, sivyo? Unashindwaje kuelewa kwamba katiba imara inaleta uwajibikaji? Kiongozi akijua anaweza kuchukuliwa hatua muda wowote ule, anaweza kufanya UHALIFU wa wazi wazi?

Haya wahi kuchukue elfu saba yako sasa
 
Kumbe tunabishana na mtoto mdogo hapa? Wewe ni muha wa Kigoma, sivyo? Unashindwaje kuelewa kwamba katiba imara inaleta uwajibikaji? Kiongozi akijua anaweza kuchukuliwa hatua muda wowote ule, anaweza kufanya UHALIFU wa wazi wazi?

Haya wahi kuchukue elfu saba yako sasa
Braza taratibu basi tukuelewe wote kwa faida ya wengi. Kama unapanic sana!!
 
Mtoa mada ni mtoto. Maendeleo ya nchi 80% huletwa na serikali ambao ni wanasiasa. Na nchi ili iendelee Inahitaji uongozi Bora ambao hutokana na katiba Bora. Huwezi kua na viongozi Bora wanaotokana na katiba mbovu never ever.

Leo hii Kodi zetu ziko juu sana kutokana na maamuzi ya viongozi wanaotokana na katiba. Mbovu tuliyonayo. Viongozi hawawajibiki. Nape anakujubu anavyotaka. Makamba anhujumu tanesco kutokana na katiba mbovu.

Mwigulu anaweka na kuongeza Kodi kila sehemu bila kuulizwa. Hii inapelekea Biashara kufa na kuongeza umaskn.

Bashe naye Hana msaada kwa wakulima. Wakulima wamebaki huko wanatapatapa kama watoto yatima. Serikali hii inayotokana na katiba mbovu ndo inaongeza umaskn kila siku kwa watu
 
Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kwamba ili nchi ipate maendeleo inahitaji Mambo manne.
Nayo ni (1) Watu (1) Ardhi (3) Uongozi (4) Siasa safi ambayo itatokana na katiba bora.
 
Kenya walipata katiba mpya miaka kadhaa iliyopta, je katiba hiyo imemaliza njaa na umasikini kwenye taifa lao? Je gap kati ya matajiri na masikini limeisha? Je ajira zimeongezeka?

Mimi ninachoona Taifa ili lisonge mbele pamoja na ustawi wa maisha ya watu tunahitaji viongozi bora wenye kuumizwa na shida za wananchi. Leo hii hata tukipata katiba mpya sidhani kama itabadilisha maisha ya raia kama viongozi watakuwa sio wazalendo.

Kwa sasa naona katiba inadaiwa na wanasia sana kuliko raia wa kawaida tafsiri yake ni kwamba raia wanatambua kuwa shida haipo kwenye katiba.

Ni hatari sana kuwa na katiba ambayo wanasiasa na vyama vyao wanataka kuingiza maslahi yao. Katiba tuliyonayo ni bora sana kama vyama vitatuletea wagombea bora, na katiba bora zaidi itapatikana ikiwa itaundwa na wananchi wenyewe na sio kwa msukumo wa wanasiasa na vyama vyao.
Hao viongozi waziri unaowasema watapatikanaje Sasa bila katiba Bora yenye kuweka Msingi wa kwenda mahakamani kura zikiibiwa. Katiba ikiwa mbovu kama hii tuliyonayo rais akiamka anaweza kusema chochote na kikawa Sheria na wewe kikakuathiri moja kwa moja na huna pa kwenda mana mahakama zote zinapewa marlekezo kwamba funga nani acha nani. Mfano mzuri ni dictator jpm
 
Mm nilivyoanza kuskia mambo ya katiba mpya nikajua italeta chakula mezani, kumbe bado unatakiwa kupambana vile vile ili upate chakula hata kama katiba imechakaa

Kwani hii katiba iliyopo sasa ilileta chakula mezani ndio ikawekwa? Kwanini tusiondoe kabisa hata katiba hii iliyopo ili chakula kiwe kingi mezani?
 
Kama katiba mpya ndiyo muarobaini wa umasikini wa mtu mmoja mmoja,

Je matajiri wa sasa wao wanatumia katiba ipi?

NB:Kuna watu wamefanikiwa kimaisha bila hata kufungamana na CCM.
Hata gerezani kuna wenye afya njema lkn wote wanakula chakula cha aina moja na huu ni mwaka 10 wako wote, ila una mawazo ya kitoto sana.
 
Bila Katiba mpya, hatutaweza kutoboa kamwe. Yaani zaidi ya asilimia 90 MATUMIZI BINASI, zinazobaki ndio zitaleta maendeleo kweli? MAISHA MAGUMU = KATIBA MBOVU

Bajeti.PNG
 
Kwani hii katiba iliyopo sasa ilileta chakula mezani ndio ikawekwa? Kwanini tusiondoe kabisa hata katiba hii iliyopo ili chakula kiwe kingi mezani?
Wap nimeandika katiba inaleta chakula.?
 
Back
Top Bottom