Pre GE2025 Mwenyekiti CCM Arusha (Baba yake Sabaya): Ukichagua upinzani serikali haitakuletea maji

Pre GE2025 Mwenyekiti CCM Arusha (Baba yake Sabaya): Ukichagua upinzani serikali haitakuletea maji

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
CCM kauli za kijinga kama hizi kwao ndio sifa , yaani ujinga ni kigezo kikuu cha uongozi huko ccm
 
Huu ujinga sijui hatakama unavumilika,unasema nikichagua mpinzani huleti maendeleo ilhali KODI ya kufanyia maendeleo inakusanywa kutoka kwa wafuasi wa vyama vya upinzani na wafuasi wa chama tawala,huo si ujinga?
Mzee na baadhi ya wanachama wa CCM,watanabaishe kua MKICHAGUA viongozi wa vyama vya upinzani,muwalipe kodi hao viongozi,wawaletee maendeleo,uone kama kutakua kelele.
Haiwezekani wakusanye pesa kwa kina la KODI,halafu hizo pesa ukafanyie maendeleo kwingine,huo ni uporaji.
Wabadilike.Sisi tusiokua na vyama,ikitokea mpinzani akapita maeneo yetu,tukose huduma muhimu kisa wapinzani wamechaguliwa halafu kodi tulipe,ni haki kweli?
 
Sijafurahishwa na kauli hiyo na hasa Kwa kuwa inatoa hukumu ya jumla badala ya hukumu Kwa mtu mmoja mmoja.

Falsafa za viongozi kuanzia wa alamu ya kwanza mpaka sasa ni kuhakikisha maendeleo ya watu yanapatikana bila kujalisha din zao, kabila zao au vyama vyama ila Leo umetumika ubaguzi wa uchama ambao ni hatari Kwa afya ya demokrasia na siasa safi.

Maamuzi ya wazazi yasiwe sababu ya watoto kuumia au kuumizwa. Kwa sababu Kwa Sheria za nchi yetu mtu aliye chini ya miaka 18 anatambuliwa kama mtoto hivyo Sheria ya uchaguzi pia imemkataza mtoto kutopiga kura.

Kwa mantiki hiyo, kauli ya Mwenyekiti sabaya inaweza kuwa ni chanzo Cha watoto kutopewa haki zao za msingi kama elimu Kwa sababu ya maamuzi ya upigaji kura ya wazazi wao. Tumeanza kuwabagua watu Kwa vyama vyao, tutakuja kuwabagua Kwa kabila zao na mwishowe Kwa dini zao. Hilo likemewe Kwa nguvu zote, Rais ameonesha dhamira ya dhati kabisa kuunganisha watu wote
Ameshaonesha upande wa CCM inaouficha usionekane.

Kama angelikuwa ameikera CCM, angeshaitwa Kamati ya Nidhamu Dodoma
 
Halafu kuna mpumbavu anasema Sabaya ateuliwe kuwa RC Dar. Majitu kama haya huwa yanafanya CCM wote tuonekane wajinga. Huyu mzee kwa historia yake alikuwa katili kuliko mwanae Sabaya.
 
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Arusha Thomas Ole Sabaya amewaonya wakazi wa Longido kutokuchagua wapinzani kwenye uchaguzi ujao wa serikali za mitaa, kwani serikali haitopeleka huduma muhimu kwenye maeneo yatakayokaliwa na viongozi wasiotokana na CCM.

Sabaya aliyekuwa akizungumza kwenye kikao cha Halmashauri kuu ya CCM wilaya ya Longido ametoa kauli hiyo muda mfupi, baada ya kufanyika kwa maandamano ya CHADEMA mkoani Arusha.
View attachment 2922327
Amesema yeyote atakayechaguliwa nje ya CCM atawajibika yeye na wananchi wake kujitafutia huduma muhimu na Mkuu wa mkoa hatokanyaga katika maeneo yenye kuongozwa na wapinzani.

Kauli ya Ole Sabaya imekuwa na hisia mseto mitandaoni,watumiaji wengi wa mtandao wa X (zamani twitter), wakisema kuwa rais Samia Suluhu Hassan hajaeleweka vyema na wasaidizi wake serikalini na ndani ya chama chake kutokana na kutoishi kwenye falsafa yake ya maridhiano.
Wengine pia akiwemo mwanasiasa John Heche anasema kauli kama hizo zinasababisha chuki zisizo na msingi kwenye jamii kwa kuaminisha watu kuwa watanzania walio nje ya CCM hawana haki kama walizonazo wanachama wa chama hicho tawala.

Rais Samia alitambulisha falsafa yake ya Maridhiano na upatanishi katika kujenga upya Tanzania tuitakayo, suala ambalo ndani yake linahimiza ushirikiano,ustahimilivu na kufanya kazi kwa pamoja na vyama pinzani katika kujitafutia maendeleo.


hii kauli huwa ni ya kijinga sana.maendeleo hayaletwi na serikali bali na wananchi wenye kwa kufanya kazi kwa bidii na kwa kulipa kodi ,na kwa kuchagua viongozi sahihi ambao siyo mafisadi bali wacha MUNGU
 
Simply
CCM haikujiandaa na mageuzi ya vyama vingi
 
Kwa kauli kama hizi.binafsi nazichukulia kama za ubaguzi
Viongozi wanaotoa kauli kama hizi wanapaswa kufunguliwa mashitaka mahakamani ili kuwa funzo.
Haiwezekani kiongozi mmoja anatoka huko anakotoka na kutumia lugha ambazo bila shaka ni ubaguzi na uchonganishi
 
Like father like son, yes ndiyo unaweza kuwaita hawa watu.

Msikilizeni Baba yake sabaya aliyekuwa DC jinsi anavyo mwaga ugoro bila aibu.

Eti ukiwachagua wapinzani serikali haitakuketea maji kijijini kwenu,huu ni wendawazimu wa kiwango cha SGR View attachment 2922294
Aibu hii kwa kiongozi wa karne ya 21 Tanzania hii
 
Back
Top Bottom