Pre GE2025 Mwenyekiti CCM Arusha (Baba yake Sabaya): Ukichagua upinzani serikali haitakuletea maji

Pre GE2025 Mwenyekiti CCM Arusha (Baba yake Sabaya): Ukichagua upinzani serikali haitakuletea maji

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Huu uwe mwanzo wa kuwachukulia hatua za kisheria viongozi kama hawa vinginevyo Wananchi wanaweza kuzichukulia kauli kama hizi kuwa wametumwa na kiongozi mkuu wa nchi, hivyo kumchonganisha na umma ambao umekuwa na malalamiko mengi hasa kipindi hiki
 
Kwani wapinzani siyo walipa kodi? wapinzani siyo watanzania?

Hivi watu wenye hizi mentality wanapataje uongozi? Huwa sielewi kabisa.

-Kaveli-
 
Kwani wapinzani siyo walipa kodi? wapinzani siyo watanzania?

Hivi watu wenye hizi mentality wanapataje uongozi? Huwa sielewi kabisa.

-Kaveli-
Wachunge midomo yao hata kama wanalipa kodi
 
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Arusha, Thomas Ole Sabaya akizungumza na Wanachama wa chama chake amenukuliwa akidai kuwa Katiba Mpya haiwezi kuwa na faida ya kuwaletea huduma ya maji.

Kupitia video iliyotolewa na Mtandao wa Siasa za Bongo, amenukuliwa amesema “Katiba Mpya italeta maji hapa? Mnakuja kuleta uchafu tu, na sisi tutakaa hivihivi, tutaendana na wale wa chama chetu, wale mtakaoenda pembeni tuone Mkuu wa Mkoa aje akulete maji, (anageuka kumtazama Mkuu wa Mkoa wa Arusha, John Mongella) unajipenda Mkuu? Rais Samia atakukubali tena?”

Chanzo: Siasa za Bongo
 
Mwenyekiti wa CCM Mkoa wa Arusha, Thomas Ole Sabaya akizungumza na Wanachama wa chama chake amenukuliwa akidai kuwa Katiba Mpya haiwezi kuwa na faida ya kuwaletea huduma ya maji...
Yaani hiki kizazi kina laana.

Huyu mzee ndie baba yake Lengai Ole Sabaya

Limao halija wahi zaa papai.

Sijui Ccm huwa wana tokana wapi na hizi hewa za chooni
 
Kitendo cha CCM na wajumbe wake kumpitisha huyu Mzee kugombea nafasi yake, na kumpa ushindi kwa kupata kura nyingi, hili taifa lazima tuwe serious kujikomboa haya mambo tusiyachukulie kama utani.

CCM kuna DNA ya ushetani ambao lazima uondolewe kwa namna yoyote ile kwa kutumia nguvu ya umma, na wala sio masanduku ya kura.

Sent from my SM-G900H using JamiiForums mobile app
 
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Arusha Thomas Ole Sabaya amewaonya wakazi wa Longido kutokuchagua wapinzani kwenye uchaguzi ujao wa serikali za mitaa, kwani serikali haitopeleka huduma muhimu kwenye maeneo yatakayokaliwa na viongozi wasiotokana na CCM.

Sabaya aliyekuwa akizungumza kwenye kikao cha Halmashauri kuu ya CCM wilaya ya Longido ametoa kauli hiyo muda mfupi, baada ya kufanyika kwa maandamano ya CHADEMA mkoani Arusha.
View attachment 2922327
Amesema yeyote atakayechaguliwa nje ya CCM atawajibika yeye na wananchi wake kujitafutia huduma muhimu na Mkuu wa mkoa hatokanyaga katika maeneo yenye kuongozwa na wapinzani.

Kauli ya Ole Sabaya imekuwa na hisia mseto mitandaoni,watumiaji wengi wa mtandao wa X (zamani twitter), wakisema kuwa rais Samia Suluhu Hassan hajaeleweka vyema na wasaidizi wake serikalini na ndani ya chama chake kutokana na kutoishi kwenye falsafa yake ya maridhiano.
Wengine pia akiwemo mwanasiasa John Heche anasema kauli kama hizo zinasababisha chuki zisizo na msingi kwenye jamii kwa kuaminisha watu kuwa watanzania walio nje ya CCM hawana haki kama walizonazo wanachama wa chama hicho tawala.

Rais Samia alitambulisha falsafa yake ya Maridhiano na upatanishi katika kujenga upya Tanzania tuitakayo, suala ambalo ndani yake linahimiza ushirikiano,ustahimilivu na kufanya kazi kwa pamoja na vyama pinzani katika kujitafutia maendeleo.

Kwani tatizo la nchi kuwa gizani uongozi ni chama gani?

Je wanaoathirika ni chama gani?
 
Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Arusha Thomas Ole Sabaya amewaonya wakazi wa Longido kutokuchagua wapinzani kwenye uchaguzi ujao wa serikali za mitaa, kwani serikali haitopeleka huduma muhimu kwenye maeneo yatakayokaliwa na viongozi wasiotokana na CCM.

Sabaya aliyekuwa akizungumza kwenye kikao cha Halmashauri kuu ya CCM wilaya ya Longido ametoa kauli hiyo muda mfupi, baada ya kufanyika kwa maandamano ya CHADEMA mkoani Arusha.
View attachment 2922327
Amesema yeyote atakayechaguliwa nje ya CCM atawajibika yeye na wananchi wake kujitafutia huduma muhimu na Mkuu wa mkoa hatokanyaga katika maeneo yenye kuongozwa na wapinzani.

Kauli ya Ole Sabaya imekuwa na hisia mseto mitandaoni,watumiaji wengi wa mtandao wa X (zamani twitter), wakisema kuwa rais Samia Suluhu Hassan hajaeleweka vyema na wasaidizi wake serikalini na ndani ya chama chake kutokana na kutoishi kwenye falsafa yake ya maridhiano.
Wengine pia akiwemo mwanasiasa John Heche anasema kauli kama hizo zinasababisha chuki zisizo na msingi kwenye jamii kwa kuaminisha watu kuwa watanzania walio nje ya CCM hawana haki kama walizonazo wanachama wa chama hicho tawala.

Rais Samia alitambulisha falsafa yake ya Maridhiano na upatanishi katika kujenga upya Tanzania tuitakayo, suala ambalo ndani yake linahimiza ushirikiano,ustahimilivu na kufanya kazi kwa pamoja na vyama pinzani katika kujitafutia maendeleo.
Yule Mwenyekiti wa CCM mkoa waTabora anazikwa lini?
 
Amchukulie hatua huyo mzee anayeiga tabia za Magufuli kwenye zama hizi.
Kuchukua hatua kupo Kwa namna nyingi ,Kuna namna nyingine zinabaki siri lakini Kuna nyingine sio siri.
Namna ya kwanza, kuonywa. Hii inaweza kuwa siri ama likawa onyo la hadharani
Namna ya pili, kuwajibika. Hapa mhusika anapima upepo na akiona upepo ni mkali anaamua kuwajibika. Kuwajibika pia kupo Kwa namna mbili, kuomba radhi ama kujiuzulu.
Namna ya tatu , kuwajibishwa. Ikibainika kitendo hiko kina athari za Moja Kwa Moja basi Kwa maslahi mapana anawajibishwa.

Sasa nije kwako, unataka hatua ya namna gani ichukuliwe?

Jibu lako tayari ninalo ila nataka nisikie kutoka kwako
 
Sijafurahishwa na kauli hiyo na hasa Kwa kuwa inatoa hukumu ya jumla badala ya hukumu Kwa mtu mmoja mmoja.

Falsafa za viongozi kuanzia wa alamu ya kwanza mpaka sasa ni kuhakikisha maendeleo ya watu yanapatikana bila kujalisha din zao, kabila zao au vyama vyama ila Leo umetumika ubaguzi wa uchama ambao ni hatari Kwa afya ya demokrasia na siasa safi.

Maamuzi ya wazazi yasiwe sababu ya watoto kuumia au kuumizwa. Kwa sababu Kwa Sheria za nchi yetu mtu aliye chini ya miaka 18 anatambuliwa kama mtoto hivyo Sheria ya uchaguzi pia imemkataza mtoto kutopiga kura.

Kwa mantiki hiyo, kauli ya Mwenyekiti sabaya inaweza kuwa ni chanzo Cha watoto kutopewa haki zao za msingi kama elimu Kwa sababu ya maamuzi ya upigaji kura ya wazazi wao. Tumeanza kuwabagua watu Kwa vyama vyao, tutakuja kuwabagua Kwa kabila zao na mwishowe Kwa dini zao. Hilo likemewe Kwa nguvu zote, Rais ameonesha dhamira ya dhati kabisa kuunganisha watu wote
👍🤝🔊
 
Kuchukua hatua kupo Kwa namna nyingi ,Kuna namna nyingine zinabaki siri lakini Kuna nyingine sio siri.
Namna ya kwanza, kuonywa. Hii inaweza kuwa siri ama likawa onyo la hadharani
Namna ya pili, kuwajibika. Hapa mhusika anapima upepo na akiona upepo ni mkali anaamua kuwajibika. Kuwajibika pia kupo Kwa namna mbili, kuomba radhi ama kujiuzulu.
Namna ya tatu , kuwajibishwa. Ikibainika kitendo hiko kina athari za Moja Kwa Moja basi Kwa maslahi mapana anawajibishwa.

Sasa nije kwako, unataka hatua ya namna gani ichukuliwe?

Jibu lako tayari ninalo ila nataka nisikie kutoka kwako
Piga chini ili iwe fundisho kwa wapuuzi wengine wa aina hiyo.
 
Back
Top Bottom