Mwarabu mlokole
JF-Expert Member
- Jul 8, 2023
- 231
- 386
Mkuu mbona huyo mwenyekiti "mnyamagana" kaongea ukweli mtupu?Kweli kabisa Katibu wa Itikadi taifa aweza kutema pumba za aina hii?
Au Mwenyekiti wa chama wilaya kama Nyamagana iliyo katikati ya jiji kama Mwanza kuwa na upeo kama huu halafu mnamtuma kutetea mkataba Tata kama Bandari?
Mnavyofanya ni labda kuwadharau wananchi wenu kuwa ni mbumbumbu au CCM yenyewe haina uwezo wa kujitambua na hapo ndio mwisho wa uwezo wake.View attachment 2694945
duuu! ujinga ni mzigo sana. hivi kweli umeaminiwa kwenye nafasi kama hii unaweza kuongea upuuzi kama huo. yaani uhuru na maslahi ya nchi yeye kipa umbele na dhumni lake ni kuchanganya damu na waarabu. Nyerere na wenzake wangelijua wanapigania uhuru kukomboa watanzania wenye akili kama hizi basi wasingefanya kazi hiyo.Kweli kabisa Katibu wa Itikadi taifa aweza kutema pumba za aina hii?
Au Mwenyekiti wa chama wilaya kama Nyamagana iliyo katikati ya jiji kama Mwanza kuwa na upeo kama huu halafu mnamtuma kutetea mkataba Tata kama Bandari?
Mnavyofanya ni labda kuwadharau wananchi wenu kuwa ni mbumbumbu au CCM yenyewe haina uwezo wa kujitambua na hapo ndio mwisho wa uwezo wake.
View attachment 2694945
Mwenyekiti wa chama tawala wilaya unamwita MC? unajuwa mamlaka aliyo nayo ndani ya wilaya na athari zake akiropoka?Kazi ya MC hata ikiwa msibani yeye jukumu lake ni kuleta hamasa tu, hayo mengine mtajua wenyewe
Wewe ulitaka ajibu hoja gani kuhusu mkataba wa DP?Mwenyekiti wa chama tawala wilaya unamwita MC? unajuwa mamlaka aliyo nayo ndani ya wilaya na athari zake akiropoka?
Bado nitaendelea kusimamia hoja yangu kuwa ni wakati sasa Serikali kuwekeza kwenye kuwawezesha Wazawa kuendeleza nchi yao na Wageni watumike tu kama wabia. Historia ya uwekezaji nchini kupitia wageni, hasa kwenye rasimali za Taifa, anayenufaika ni huyo mwekezaji, km makampuni ya uchimbaji madini. Kuendelea kutegemea wageni kwa maendeleo ni moja ya njia kuu ya kudumisha ukoloni-mamboleo.Uwekezaji twautaa, tena kwa sana tu.
Tatizo ni pale utaambiwa nipishe ili nikuwekeze!!!!
Chama kinapowatuma makada wake, wawapime na uwezo wao akii.
Sophia Mjema nina uhakika hajui tofauti ya mwalo na bandari!
Na huyo mwingine sijui zuzu la wapi, aachoongea anakijua mwenyewe.
View attachment 2695026
mwenyekiti wa chama tawala hana mamlaka yoyote. wala katiba ya nchi haimtambui,badala yake ni chama husika tu ndiyo kinatambua nafasi yake na majukumu yake. kama tutaendelea kuamini kwamba mwenyekiti wa chama ana mamlaka basi tutajifedhehesha mbele ya haki zetu na ni ujinga mkubwa. pili tutawakweza wasiokwezeka. mwenyekiti wa chama ni chamani tu na si umma. mwajiri wake ni chama na anatekeleza ilani ya chama. hapaswi kuingilia wala kuamulisha vyombo vya dola, na wasaidizi wa serikali ngazi zote za mkoa na wilaya. ujinga wetu ndiyo unawapa nguvu hiyo.Mwenyekiti wa chama tawala wilaya unamwita MC? unajuwa mamlaka aliyo nayo ndani ya wilaya na athari zake akiropoka?
Ushamba wa maendeleo kwa viongozi wengine ni mzigo kwa wananchi.Bado nitaendelea kusimamia hoja yangu kuwa ni wakati sasa Serikali kuwekeza kwenye kuwawezesha Wazawa kuendeleza nchi yao na Wageni watumike tu kama wabia. Historia ya uwekezaji nchini kupitia wageni, hasa kwenye rasimali za Taifa, anayenufaika ni huyo mwekezaji, km makampuni ya uchimbaji madini. Kuendelea kutegemea wageni kwa maendeleo ni moja ya njia kuu ya kudumisha ukoloni-mamboleo.
Hivyo basi, nawasihi Viongozi wa vyama vya Siasa na Serikali kuwa na maono yenye kuondokana na UTEGEMEZI kifikra na vitendo.
Kwa pigo hizi 👇👇 unategemea nn!
"Tutakapolimaliza ya bandari ya Dar es Salaam hata Mwanza hapa tuna bandari, tunawataka Waarabu hapa, waje Waarabu DP world sijui na nani, waje hapa watuendelezee bandari ya Mwanza.
"Tukitoka hapa tunahamia Ukerewe, tukitoka hapo ni visiwa vyote vya ukala, wape Waarabu. Waarabu oyeee.
"Tunataka hata watoto wa Kiarabu wajae Mwanza hapa jamani, kuchanganya rangi raha. Waarabu safii, DP World oyeee!
"Kazi yetu sisi ni hamasa, na hamasa mnaiona. Asanteni sana kwa kunisikiliza, Mungu Baba wa Mbinguni awabariki. Chama Cha Mapinduzi kipo madarakani, kitaendelea kuwa madarakani mpaka utukufu wa Yesu Kristo utakapokuja mara ya pili. Hapo vipi?"
Wahamasishaji kazini, kazi kwelikweli!