Mwenyekiti wa CHADEMA, Freeman Mbowe ajitokeza Magomeni, akamatwa na Polisi

Quinine

JF-Expert Member
Joined
Jul 26, 2010
Posts
22,227
Reaction score
49,628
Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe amekamatwa na Polisi baada ya kuwasili Magomeni Mapipa akiwa anazungumza na wanahabari kuhusu maandamano

Ikumbukwe kuwa Septemba 11, 2024, Mbowe alitangaza kufanyika maandamano ya kulaani matukio ya watu kutekwa na mauaji, akiwemo kada wake, Ali Kibao.

Hata hivyo, Jeshi la Polisi kupitia msemaji wake, David Misime lilitangaza kuyapiga marufuku.

Kwa mujibu wa Mbowe, wameamua kuweka mkazo kuhusu suala hilo, baada ya maombi ya mahitaji, ikiwemo kutaka kujiuzulu kwa Waziri wa Mambo ya Ndani, Hamad Masauni, viongozi waandamizi wa ulinzi na usalama kama sehemu ya uwajibikaji.

Amesema jambo lingine waliloliomba ni kurejeshewa kwa viongozi wa chama hicho, waliotekwa kwa nyakati tofauti wakiwa hai au hali ya umauti, akiwemo Deusdetith Soka, Dioniz Kipanya, Jacob Mlay na Mbwana Kombo.

Soma Pia: LIVE Yanayojiri kwenye Maandamano ya CHADEMA 23/9/2024

Your browser is not able to display this video.


Your browser is not able to display this video.
 
Huyu kweli kiongozi wa mfano......kafika sehemu ya tukio 😀
 
Alikacha maandamno yake haramu sio 🤣
 
Polisi acheni kunyanyasa vyama vya upinzani.
 
Kuna mtu kaingizwa kingi halafu kajaa mazima.

Yaan wameamua kutumia power yake mwenyewe kumuumiza, huu mchezo una wenyewe aisee.

Hivi kuna asiejua nani ana remote control ya mbowe?

britanicca
 
Alikua anatafuta picha za kupigia kampeni mwakani hana lolote😂😂😂
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…