Mbona kamanda Chacha Wangwe hakuzikwa kitaifa na chama wakati alikuwa makamu mwenyekiti wa chama. Mpaka leo hata familia yake mmeitelekeza bila msaada wowote. Acheni uhuni huu.
Rip,hakua na visasi na watu kweli?
Na naona wafuasi na viongozi wao wanafurahia haya matendo haramu kwa kudhani kwamba wao wako salama.Wamewageuza Watanzania kama Nyumbu ambao mwenzao anakamatwa na kuliwa na Simba halafu wengine wanaendelea na taratibu za maisha kana kwamba kilichotokea ni jambo la kawaida lisilo na athari za kimaisha.Wanashindwa katambua ya kwamba unapotajwa kuwa kiongozi wa Tanzania moja ya dhamana kubwa uliyo nayo ni kulinda uhai wa kila Mtu awe Mtanzania au yeyote aliyomo ndani ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Jamani hili ni jinamizi au nininii? Si juzi tu ITV wametuonyesha migambo wamechoma nyumba za watu geita bila kuuliza wala kumsikiliza mtu? Au hii ni Geita nyingine?
Ah where are going?
Mbona watu hao hao wa kanda ya ziwa walimuua Mabina na sisi CCM hatukunyooshea kidole kuwa ni CHADEMA ndio walihusika na mahuaji na badala yake tuliviacha vyombo vya dola vitoe taarifa? Ningeomba na nyinyi pia muwe na subira wakati vyombo vya dola vikiendelea kufanya upelelezi.
Unausianisha mambo yasiyokuwa na ufanano
Lazima kufuata sheria za nchi. Tukio la Geita lina utata. Mimi wasi wasi wangu mkulima wa kijijini hawezi piga picha nzuri kiasi hicho. Hili tukio halina tofauti na mtikila ndiyo maana inawezekana ni hao hao chadema. Ndiyo maana tusikurupuke tusubiri uchunguzi. Maana mke wa mtikila aliomba tume na sijui kama iliundwa.Ni hatari kweli huko tunakoenda. Haya yanatokea wakati tuna Masheikh wanaozea gerezani. Amani tutaiimba sana lakini kama haki haitotendeka basi tutarajie mgeuko. Wale masheikh walivyodhalilishwa wengi tulishangilia na hata kuona wale ni magaidi. Hawana haki ya kusikilizwa. Tukasahau tatizo kubwa la kimfumo ambalo wachache kwa kutumia pesa na mamlaka wana maamuzi juu ya uhai na haki za wengine. Isingedhaniwa siasa tena katika ngazi ya ubunge au udiwani ufikie watu Kutoana roho .Hizi roho ngumu za kuua zinatoka wapi ikiwa wauaji na waliouliwa sio Waislamu?. Sasa hapa najiuliza; Ni UPI UGAIDI NA NANI GAIDI? Yule aliyemuua Mawazo au yule aliyemtuma muuwaji? Haki itendeke kwa nani hasa??.
Mbona wafugaji na wakulima wanachinjana kwa mapanga na mishale? Hili huwa hamlioni? Report ya polisi inasemaje? Na wewe unasemaje kuhusu 'ushahidi' wako?barafuyamoto hao wote uliowataja hakuna hata mmoja kati yao aliyeuawa kwa kupigwa mapanga!! Maziwa na Tui la nazi vinafanana kwa rangi lakini ladha na uasili wake wala si kitu kimoja!!
Very Sad !! Jamani HAKI..HAKI... Haki...Haki ipo wapi?!!? (JUSTICE for all) Nimesikitika kusoma.....uzi huu!!
Tusikurupuke kushutumu chama. Mbona nyie chadema mlimuua chacha wangwe. Mbona nyie chadema mlimtishia kumuua Dr Slaa mpaka akakimbia nchi? Mbona nyie chadema inasemekana ndiyo mmehusika na kifo cha mtikila. Kwa nini marehemu apigwe picha style sawa na zile za mtikila? Kwa nini mpiga picha kapiga picha zenye ubora hivyo? Sidhani kama kuna hao vijana wa ccm wana kamera nzuri kiasi hicho zaidi yenu nyie chadema. Hivyo tuache kukurupuka tusubiri uchunguzi.CCM mnadhani nyie ndiyo wenye hatimiliki ya nchi hii.
Mtaweza kutuua wote mkatumaliza?
Bro hakika ilianza kupotea tangu kwa chacha wangwe sitasahau
Kadri siku zinavyoyoyoma ndivyo amani inavyotoweka ndani ya mioyo ya wapenda haki wengi wa nchi hii.
Hapa nchini Kila Mara Uchungu unawekwa kwenye akiba ya UCHUNGU MKUU!
Usipokuja asubuhi basi utegemea jioni.
Jana maadui wa Amani wameongeza tena UCHUNGU kwenye account ya mioyo ya wengi kwa Mauaji ya Alfonce Mawazo aliyekuwa Mwenyekiti wa Chadema mkoa Wa Geita.
NIMEKUWA NAJIULIZA SWALI HILI JADIDI,
Hivi kweli Dola hili kubwa limeridhika kabisa kuwa taifa la watekaji na wauaji?
Kama si hivyo naomba niambiwe,
Nani alimuua Daudi Mwangosi?
Nani walimuuwa Dr Mvungi
Nani walimteka na Kumpiga vile Dr Ulimboka
Vipi kuhusu Absalomu Kibanda; na wengine wengi walioteswa na kuuawa vilevile kama hawa!
Mpaka sasa ni hatua gani zilichukuliwa na vyombo husika ili haki itendeke, na ionekane wote kutendeka.
Hofu yangu hapa ambayo kwa kweli sijui kama wenzangu wanayo ni pale
Kikombe cha Uovu na Ubaya wa taifa kinapojaa na kumwagika sana!
Yaani ni kana kwamba foleni imesogea na zamu yetu imewadia!
Swali ni kuwa ili msambaratiko huu utimie je utapelekewa na mauaji ya nani, wapi, na lini?
Na je tokea sasa zimebaki hatua ngapi ili tuvuke mstali na kuvuna kile tulichokipanda wenyewe kwa gharama ya ujinga na ulevi wetu!
Napatata mashaka makubwa juu dhamira ya watesaji na wauaji hawa! Hivi kwani wao hawaoni kuwa wanalipeleka taifa hili kusiko?
Najua wakurupukaji watakuja na mengi lakini
Huu si Utabiri wa kiganga la!
Hii ni kanuni ya asili tu!
Mtu huzaliwa na baadaye hufa.
Taifa huundwa hatimae huparanganyika.
Mwisho kabisa,
Ukimwona mtu mzima juu ya mti, anaelekea kwenye tawi kavu; ukamwonya asikubali; akianguka chini, je ni wewe uliyemsababishia anguko lake? Hapana!
Ukivunja kanuni ya asili ni lazima upate stahili yako.