Mwezi una umri mdogo kuliko tulivyodhani! Je, unaamini?

Mwezi una umri mdogo kuliko tulivyodhani! Je, unaamini?

FRANC THE GREAT

JF-Expert Member
Joined
May 27, 2016
Posts
5,500
Reaction score
8,060
Habari!

Mara nyingi tumekuwa tukijiuliza maswali mengi kuhusiana na masuala mbalimbali yahusuyo Mwezi. Sio ule wa kwenye kalenda bali huu tuuonao angani karibu kila iitwapo leo hasa nyakati za usiku. Yeah, huohuo kama duara fulani linalong'aa.

Kwa muda mrefu sasa tafiti mbalimbali zimekuwa zikifanyika ili kuweza kubaini mambo mbalimbali kuhusiana na Mwezi na tafiti zimekuwa zikileta majibu tofauti tofauti. Utafiti mpya uliofanyika hivi karibuni umebaini kuwa, Mwezi una umri mdogo sana kuliko tulivyofikiria ama tulivyokuwa tukifahamu hapo awali, pungufu ya miaka takribani milioni 85 hivi. Je, unaamini hilo?

Subiri hapohapo!

1350px-Artist's_concept_of_collision_at_HD_172555.jpg


Kulingana na nadharia inayokubalika na watafiti mbalimbali, Mwezi uliumbwa kutoka katika vipande vipande vilivyotokana na mgongano kati ya Dunia na sayari ndogo inayoitwa Theia, nadharia inayofahamika kama The Giant Impact Hypothesis pia ikijulikana kama Big Splash. (Tazama mfano katika mchoro uliopita).

Vipande hivyo vilivyo katika myeyuko hatimaye viliungana na kuwa mwili mmoja ambao ulianza kuzunguka dunia, ndio huo Mwezi unaouona angani karibu kila siku ndugu msomaji wa bandiko hili.

Maana yake ni kwamba, sehemu ya mwamba ambao ulifanikisha kufanyika ama kuumbwa kwa Mwezi ulitokea duniani, na unaweza kutumika hadi leo kuweza kubaini umri wake. Utafiti unaonesha kuwa Mwezi uliumbwa wakati ambao Dunia ilikuwa ikikaribia kuumbwa kikamilifu. Tazama mchoro ufuatao jinsi ambavyo mchakato huo wa kufanyika kwa Mwezi unavyoaminika kutokea kama inavyoonekana katika matukio hayo manne.

Researchers have long believed the Moon formed as a result of a cosmic collision between an Earth that was still forming and another planetoid, commonly known as Theia.

Simple_model.png


Utafiti huu mpya kuhusu umri wa Mwezi umefanyika nchini Ujerumani kupitia shirika la anga za juu la nchi hiyo Deutsches Zentrum für Luft- und Raumfahrt ama kwa kifupi DLR.

Kabla sijaendelea mbele zaidi,
Nikupe pole ndugu msomaji uliyekumbana na changamoto pale ulipojaribu kulitamka hilo jina la hilo shirika la Ujerumani ila kwa lugha nyingine unaweza kuliita, German Aerospace Center.

Kulingana sasa na huu utafiti 'wetu' mpya, Mwezi una umri wa miaka takribani bilioni 4.425, miaka ambayo ni milioni 85 pungufu kutoka umri uliokuwa ukidhaniwa ama kufahamika hapo awali wa miaka bilioni 4.51. Are you there?!

Watafiti 'wetu' pia walibaini kuwa Mwezi ulikuwa na bahari ya magma wakati mchakato wa kuumbwa kwake ukiendelea.

BAHARI YA MAGMA

Hili ni tabaka la mwamba myeyuko linaoaminika kuwepo katika umbo la dunia na sayari nyinginezo wakati uumbwaji wa sayari hizo unapokuwa ukikamilishwa.

Magma oceans exist during periods of Earth's or any planet's accretion when the planet is completely or partly molten. A magma ocean also occurred on the Moon during and following its formation. [Wikipedia]

1594840622742.png

PICHA: Mfano wa mwezi ukiwa na bahari ya magma.

Katika harakati za kulibaini hilo pengo la miaka milioni 85, watafiti walitumia miundo ya kimahesabu kuweza kuubaini muundo wa Mwezi katika kipindi chote cha uwepo wake, wakitumia bahari ya magma niliyoielezea hapo awali kama msingi katika utafiti wao.

Kulingana na wazo hilo kwamba Mwezi ulikuwa na bahari kubwa ya magma, watafiti walihesabu jinsi madini yaliyofanyika kutokana na kupoa na kuganda kwa magma yalivyokuwa yakibadilika kuendana na muda. Kwa kufuata mbadiliko wa bahari ya magma, wanasayansi waliweza kuufuatisha na kubaini muda na wakati wa uumbwaji wa Mwezi.

Nisiwachoshe ila haya ni kati ya yale yaliyojiri katika utafiti huu mpya pia ni machache tu katika yale yaliyokusanywa katika tafiti zingine kadha wa kadha zilizowahi kufanyika katika miaka ya nyuma zinazohusiana na umri sahihi wa Mwezi. Zaidi yaliyojiri katika tafiti tutapata kuyajua hapo baadaye. Asante na karibu kwa maoni yako kuhusiana na hili!



FRANC THE GREAT,
Semper magnas.
 
View attachment 1508451
PICHA: Moja ya mwamba wa kale zaidi wa Mwezi. [NASA/JSC/AACO]

Kwa kuwa huu mwamba umehifadhiwa kitambo, haukuwahi kuweza kuwasaidia watafiti kubaini umri wa mwezi?

Pili, kati ya hiyo dunia na theia, ni kipi kilikua kina asili ya mwanga kinachosababisha mwezi ung'ae ?

Hapo kwenye sehem au eneo husika ambapo dunia iligongwa na theia, kumeweza kutambulika ni eneo lipi kwa sasa duniani?
Kuna madhara yoyote yanayoonekana hadi leo kimazingira kuthibitisha hilo ndio eneo uso wa dunia umeathirika na hiyo ajali?

Mwisho kabisa kwa sasa, hakuna vipande vyovyote vilidondoka baada ya hiyo ajali? Inamaana vyote vilitumika kuunda mwezi?
 
Kwa kuwa huu mwamba umehifadhiwa kitambo, haukuwahi kuweza kuwasaidia watafiti kubaini umri wa mwezi?

Pili, kati ya hiyo dunia na theia, ni kipi kilikua kina asili ya mwanga kinachosababisha mwezi ungae ?

Hapo kwenye sehem au eneo husika ambapo dunia iligongwa na theia, kumeweza kutambulika ni eneo lipi kwa sasa duniani?
Kuna madhara yoyote yanayoonekana hadi leo kimazingira kuthibitisha hilo ndio eneo uso wa dunia umeathirika na hiyo ajali?

Mwisho kabisa kwa sasa, hakuna vipande vyovyote vilidondoka baada ya hiyo ajali? Inamaana vyote vilitumika kuunda mwezi?
Tafiti mbalimbali kupitia mwamba huo zimekwisha wahi kufanyika hapo kabla kuhusiana na umri wa Mwezi na uumbwaji wake kwa ujumla na umri uliokuwa ukitambulika hapo awali kabla ya huu utafiti mpya ni miaka ipatayo bilioni nne nukta tano moja (4.51).

Kuhusiana na kung'aa kwa Mwezi ni kutokana na kuakisi mwanga wa Jua katika Solar System. Tunaweza kuuona Mwezi uking'aa hasa nyakati za usiku kutokana na umbo lake lenye kuakisi (reflect) mwanga. Mwezi hauzalishi mwanga bali unaakisi mwanga wa Jua kama vile Dunia pia haizalishi mwanga bali inapokea mwanga kutoka katika Jua hilohilo.

Tukielekea katika mgongano,
Dunia iligongana ama iligongwa na sayari ndogo ya Theia kipindi ambacho bado ilikuwa katika process ama mchakato wa kuumbwa kwake na haikuwa kama Dunia hii iliyopo hivi sasa. Ilikuwa ni Dunia 'changa'.

Wakati wa mgongano huo, vipande vya mwamba myeyuko vilipasuka kutoka sehemu ya koti (mantle) ya Dunia 'changa' iliyokuwa ikimalizikia kuumbwa, vipande ambavyo ndivyo viliungana pamoja na mabaki ya Theia kupelekea kufanyika kwa Mwezi ambao ulikuwa katika hali ya myeyuko (molten) kwa kipindi kirefu sana kabla ya kuganda kabisa.

Baada ya Theia kuigonga Dunia (Big Splash), pia kukafanyika muunganiko kati ya Theia na Dunia 'changa' huku kiini chake kikiungamanishwa na kiini cha sayari ndogo ya Theia katika tukio linalofahamika kama Formation of the Core ambapo katika utafiti wa hivi karibuni, umri wa Mwezi umeweza kuhusishwa na tukio hilo la kuhitimisha kuumbwa kwa Dunia.

Matokeo yake:
Watafiti kupitia nadharia hii ya Big Splash wameeleza sababu ya Dunia kuweza kuwa na Core ama kiini kikubwa kuliko ambavyo ingetegemewa kuwa katika mwili wa ukubwa ama size kama yake. Hiyo ni kwa sababu kiini na koti ya sayari ndogo ya Theia viliungana na kiini na koti ya Dunia katika kipindi hicho cha Formation of the Core.

Mabaki ya sayari ndogo ya Theia yaliyotokana na tukio la kugongana kwake na sayari ya Dunia yapo na yamepatikana katika sehemu zote mbili, yaani Duniani na katika Mwezi kupitia tafiti zilizokwisha kufanyika hapo awali. Pia sampuli ya mwamba wa Mwezi iliyopatikana imeweza kubaini mfanano wa kimuundo ama composition na miamba ya Dunia.

Asante!
 
Tafiti mbalimbali kupitia mwamba huo zimekwisha wahi kufanyika hapo kabla kuhusiana na umri wa Mwezi na uumbwaji wake kwa ujumla na umri uliokuwa ukitambulika hapo awali kabla ya huu utafiti mpya ni miaka ipatayo bilioni nne nukta tano moja (4.51).

Kuhusiana na kung'aa kwa Mwezi ni kutokana na kuakisi mwanga wa Jua katika Solar System. Tunaweza kuuona Mwezi uking'aa hasa nyakati za usiku kutokana na umbo lake lenye kuakisi (reflect) mwanga. Mwezi hauzalishi mwanga bali unaakisi mwanga wa Jua kama vile Dunia pia haizalishi mwanga bali inapokea mwanga kutoka katika Jua hilohilo.

Tukielekea katika mgongano,
Dunia iligongana ama iligongwa na sayari ndogo ya Theia kipindi ambacho bado ilikuwa katika process ama mchakato wa kuumbwa kwake na haikuwa kama Dunia hii iliyopo hivi sasa. Ilikuwa ni Dunia 'changa'.

Wakati wa mgongano huo, vipande vya mwamba myeyuko vilipasuka kutoka sehemu ya koti (mantle) ya Dunia 'changa' iliyokuwa ikimalizikia kuumbwa, vipande ambavyo ndivyo viliungana pamoja na mabaki ya Theia kupelekea kufanyika kwa Mwezi ambao ulikuwa katika hali ya myeyuko (molten) kwa kipindi kirefu sana kabla ya kuganda kabisa.

Baada ya Theia kuigonga Dunia (Big Splash), pia kukafanyika muunganiko kati ya Theia na Dunia 'changa' huku kiini chake kikiungamanishwa na kiini cha sayari ndogo ya Theia katika tukio linalofahamika kama Formation of the Core ambapo katika utafiti wa hivi karibuni, umri wa Mwezi umeweza kuhusishwa na tukio hilo la kuhitimisha kuumbwa kwa Dunia.

Matokeo yake:
Watafiti kupitia nadharia hii ya Big Splash wameeleza sababu ya Dunia kuweza kuwa na Core ama kiini kikubwa kuliko ambavyo ingetegemewa kuwa katika mwili wa ukubwa ama size kama yake. Hiyo ni kwa sababu kiini na koti ya sayari ndogo ya Theia viliungana na kiini na koti ya Dunia katika kipindi hicho cha Formation of the Core.

Mabaki ya sayari ndogo ya Theia yaliyotokana na tukio la kugongana kwake na sayari ya Dunia yapo na yamepatikana katika sehemu zote mbili, yaani Duniani na katika Mwezi kupitia tafiti zilizokwisha kufanyika hapo awali. Pia sampuli ya mwamba wa Mwezi iliyopatikana imeweza kubaini mfanano wa kimuundo ama composition na miamba ya Dunia.

Asante!

Kwa kuwa vitu vyoote hivi vimejengwa kwenye nadharia ( Big splash), ina maana kuna uwezekano utafiti mwingine siku za mbeleni ukaonyesha taarifa zingine au tofauti na hizi zilizotolewa hivi karibuni kuhusu umri wa mwezi.

Kuhusu ung'avu wa mwezi, naelewa unaakisi mwanga wa jua, swali ilikua kati ya Theia na Dunia, ni kipi kilikuwa na hiyo tabia ya kuakisi mwanga? Au hiyo ni tabia mpya iliyojitokeza kwa mtoto mchanga aliyejulikana kama mwezi?

Ni kitu gani kilipelekea solar system ikapoteza uelekeo hadi sayari zikagongana? Ni kitu kinaweza kutokea tena?

Shukrani
 
Kulingana na nadharia inayokubalika na watafiti mbalimbali, Mwezi uliumbwa kutoka katika vipande vipande vilivyotokana na mgongano kati ya Dunia na sayari ndogo inayoitwa Theia, nadharia inayofahamika kama The Giant Impact Hypothesis pia ikijulikana kama Big Splash. (Tazama mfano katika mchoro uliopita).
Naomba kuuliza swali hapa, hivi inakuwaje huwa mnatumia nadharia kuelezea jambo au kulijengea hoja jambo fulani, mathalani hii nadharia, sababu inaonekana wazi kabisa hakuna anae weza kuthibitisha ukweli wa nadharia hii, wala hakuna nadharia yoyote inayoweza kuifanya nadharia nyingine kuwa ya kweli. Hili mnalichukuliaje upande wenu ?
Vipande hivyo vilivyo katika myeyuko hatimaye viliungana na kuwa mwili mmoja ambao ulianza kuzunguka dunia, ndio huo Mwezi unaouona angani karibu kila siku ndugu msomaji wa bandiko hili.
Kuna yeyote aliye shuhudia hili ?
Maana yake ni kwamba, sehemu ya mwamba ambao ulifanikisha kufanyika ama kuumbwa kwa Mwezi ulitokea duniani, na unaweza kutumika hadi leo kuweza kubaini umri wake. Utafiti unaonesha kuwa Mwezi uliumbwa wakati ambao Dunia ilikuwa ikikaribia kuumbwa kikamilifu. Tazama mchoro ufuatao jinsi ambavyo mchakato huo wa kufanyika kwa Mwezi unavyoaminika kutokea kama inavyoonekana katika matukio hayo manne.
Ushahidi wa maneno haya tunaupata wapi au walijuaje hili ?


Naendelea .....
 
Watafiti 'wetu' pia walibaini kuwa Mwezi ulikuwa na bahari ya magma wakati mchakato wa kuumbwa kwake ukiendelea.
Sifa ya tamko "kuumba au kuumbwa" linahitaji nini na nini ? Kwanini useme mwezi kuumbwa, hali ya kuwa vijenzi vyake havina ufahamu na kwanini asiwepo mjenzi mwenye maarifa na kujua lengo la kuumba huo mwezi ?

Hili walilijuaje au walitumia nini kulijua hali ya kuwa suala hili linaelezewa katika msingi wa nadharia, yaani kubahatisha na makisio ?
Hili ni tabaka la mwamba myeyuko linaoaminika kuwepo katika umbo la dunia na sayari nyinginezo wakati uumbwaji wa sayari hizo unapokuwa ukikamilishwa.
Uumbwaji wa sayari hizo umeumbwa na nani ? Nauliza hivi kutokana na mtiririko wako wa maelezo ya kuwa "....na sayari nyinginezo wakati wa uumbwaji.... "
 
Mkuu vipi Hawa watafiti waliiona ile bendera ya wamarekani huko Mwezini?

Hivi miezi kumi na mbili ya kwenye calendar inapatikana wapi hasa maana mi nauona mmoja tu?
Samahani kwa kuuliza maswali nje ya mada
Ahsante
Nalog off
 
Tungejua umri wa Dunia ili turejee tivabu vya historia huenda akina Adamu na Hawa waliishi bila uwepo wa mwezi.
Umri wa Dunia unakadiriwa kuwa miaka bilioni 4.543. Baada ya miaka takribani milioni 118 ndipo Dunia ilipogongana na sayari ya Theia na kupelekea kuzaliwa kwa Mwezi.

Kipindi hicho chote, Dunia ilikuwa bado haijamalizikia kufanyika, kulingana na nadharia ya Giant Impact.
 
Umri wa Dunia unakadiriwa kuwa miaka bilioni 4.543. Baada ya miaka takribani milioni 118 ndipo Dunia ilipogongana na sayari ya Theia na kupelekea kuzaliwa kwa Mwezi.

Kipindi hicho chote, Dunia ilikuwa bado haijamalizikia kufanyika, kulingana na nadharia ya Giant Impact.
achana nae na nadharia yake.
 
Kwa kuwa vitu vyoote hivi vimejengwa kwenye nadharia ( Big splash), ina maana kuna uwezekano utafiti mwingine siku za mbeleni ukaonyesha taarifa zingine au tofauti na hizi zilizotolewa hivi karibuni kuhusu umri wa mwezi.

Kuhusu ung'avu wa mwezi, naelewa unaakisi mwanga wa jua, swali ilikua kati ya Theia na Dunia, ni kipi kilikuwa na hiyo tabia ya kuakisi mwanga? Au hiyo ni tabia mpya iliyojitokeza kwa mtoto mchanga aliyejulikana kama mwezi?

Ni kitu gani kilipelekea solar system ikapoteza uelekeo hadi sayari zikagongana? Ni kitu kinaweza kutokea tena?

Shukrani
Tafiti mbalimbali zimekuwa na matokeo tofauti tofauti lakini kumekuwa na base ama msingi katika tafiti hizi kuhusiana na umri wa Mwezi. Kuwepo kwa tafiti zingine hapo baadaye zitakazoleta majibu mengine au zaidi ya haya inawezekana kabisa na hata sasa zipo lakini hizi nadharia huwa zinasimama kama msingi katika tafiti hizo mbalimbali.

Nadharia zinazohusu chimbuko la Mwezi pia ziko nyingi.

Kabla ya hii nadharia ya Giant Impact kulikuwepo na nadharia nyingine tatu (3) maarufu kuhusiana na jinsi Mwezi ulivyoweza kufanyika;

1) Nadharia mojawapo ilipendekeza, Mwezi pamoja na Dunia vilikuwa mwili mmoja lakini mapema katika historia yake, mwili huo uligawanyika katika miili miwili yaani Mwezi pamoja na Dunia kutokana na kujizungusha kwa kasi sana na kupelekea kupoteza utulivu katika mhimili wake.

2) Nadharia nyingine ilipendekeza kuwa, Mwezi na Dunia vilifanyika kwa pamoja kutokana na nyenzo moja lakini kwa kujitegemea yaani kila kimoja kivyake.

3) Pia kulikuwepo na nadharia nyingine iliyopendekeza kufanyika kwa Mwezi mahali pengine kabisa nje ya Solar System lakini ulinaswa na Dunia ulipokuwa ukipita karibu yake kutokana na gravitational force ya Dunia.

Hizo nadharia tatu hapo zilikuwepo kipindi kirefu na zilikuwa na mapungufu mengi tu mpaka kufikia kuanzishwa sasa kwa nadharia nyingine ya nne maarufu kama Giant Impact Hypothesis ambayo kwa sasa pia hufahamika kama Giant Impact Theory niliyokwisha kuielezea hapo awali ambayo imekuwa ni msingi mkubwa wa kufanyika kwa tafiti mbalimbali.

Tabia ya Mwezi kuakisi mwanga:
Tabia hii ya kuakisi mwanga wa Jua ipo katika sayari zote katika Solar System ikiwemo Dunia, kulingana na tafiti mbalimbali zilizokwisha kufanyika kwa muda mrefu sana. Kwa maana hiyo, hata tabia ya Mwezi pia kuakisi mwanga imetokana na tabia ya 'wazazi wake' kuakisi mwanga.

Sayari kugongana:
Kupoteza uelekeo huko unakokusema ni kutokana na mchakato wa Solar System kujijenga, kulingana na nadharia pamoja na tafiti mbalimbali. Inaaminika, kulikuwepo na idadi kubwa sana ya sayari 'changa' hapo awali kabisa wakati Solar System ilipokuwa ikijijenga. Hizi sayari 'changa' zinafahamika kama Protoplanets ambazo zilikuwa hazijamalizikia bado kuumbika ama kuwa sayari kamili ikiwemo pia Dunia.

Idadi kubwa ya hizi sayari 'changa' zilikuwa zikigongana na kuungana zenyewe kwa zenyewe na kuumba miili mingine mipya yaani sayari katika ukamilifu wake. Kulingana na tafiti mbalimbali, hilo linauwezekano mdogo sana kutokea tena ukizingatia kwamba Solar System yetu imekwisha mature. Hilo halipo tu katika sayari kugongana bali hata katika sayari kutemwa au kuondolewa katika mfumo ama kwa lugha ya kisasa tunasema "kukatwa".

Stability katika Solar System ni suala nyeti sana katika masuala mazima ya Astronomy na limekwisha fanyiwa kazi na wanasayasi wengi sana katika historia hata kabla ya uwepo wa mbinu za kisasa zaidi za kitafiti. Wanasayansi kwa kutumia mbinu hizi za kisasa hasa miundo ya tarakilishi, wameweza ku-predict mwenendo wa Solar System katika wakati ujao na kutafiti uwezekano wa migongano ya sayari hapo baadaye.

Mfano:
Watafiti wameweza kubaini uwezekano mdogo sana wa sayari ya Mercury kugongana na sayari ya Venus au Dunia katika miaka zaidi ya bilioni moja ijayo. Hivyo, uwezekano wa kutokea kwa migongano hiyo ni mdogo sana ambapo kwa sasa tunaweza kusema kuwa Solar System yetu ni tulivu.
 
Naomba kuuliza swali hapa, hivi inakuwaje huwa mnatumia nadharia kuelezea jambo au kulijengea hoja jambo fulani, mathalani hii nadharia, sababu inaonekana wazi kabisa hakuna anae weza kuthibitisha ukweli wa nadharia hii, wala hakuna nadharia yoyote inayoweza kuifanya nadharia nyingine kuwa ya kweli. Hili mnalichukuliaje upande wenu ?

Kuna yeyote aliye shuhudia hili ?

Ushahidi wa maneno haya tunaupata wapi au walijuaje hili ?


Naendelea .....
Hahaha! Kwanini unasema hakuna anayeweza kuthibitisha nadharia hiyo?

Kisayansi, nadharia ndio msingi katika kuweza kujifunza na kufahamu masuala mbalimbali yaliyokuwepo, yaliyopo na yatakayokuwepo hapo baadaye. Nadharia ndio starting point kabla ya kuelekea katika utafiti ama uchunguzi wa kubaini ukweli na kupata hitimisho la jambo lolote kisayansi.

Tafiti mbalimbali zinazofanyika ili kuweza kubaini masuala mbalimbali husimamia katika hizo nadharia kadha wa kadha ambazo wanasayansi wamekuwa wakizisoma na kujifunza kwazo kwa kipindi kirefu huku tafiti mbalimbali zikiendelea kufanyika siku hadi siku kuzithibitisha.

Pia katika nadharia kuna vitu viwili:

1) Hypothesis
2) Theory

Hypothesis ni nadharia inayotokana na mapendekezo ya kisayansi ambayo yatahitajika kufanyiwa utafiti wa kina na kujaribiwa kisayansi ili kupata uthibitisho juu ya nadharia hiyo lakini kwa upande wa Theory ni nadharia inayotokana na kanuni mbalimbali zinazotoa ufafanuzi wa mambo ya kisayansi kupitia ushahidi wa kitafiti uliopo ama uliokwisha kufanyika ama/pia majaribio ya kisayansi yenye kuthibitisha masuala mbalimbali yanayoihusu nadharia hiyo.
 
Sifa ya tamko "kuumba au kuumbwa" linahitaji nini na nini ? Kwanini useme mwezi kuumbwa, hali ya kuwa vijenzi vyake havina ufahamu na kwanini asiwepo mjenzi mwenye maarifa na kujua lengo la kuumba huo mwezi ?

Hili walilijuaje au walitumia nini kulijua hali ya kuwa suala hili linaelezewa katika msingi wa nadharia, yaani kubahatisha na makisio ?

Uumbwaji wa sayari hizo umeumbwa na nani ? Nauliza hivi kutokana na mtiririko wako wa maelezo ya kuwa "....na sayari nyinginezo wakati wa uumbwaji.... "
Maneno; kuumbwa ama kuumbika yametumika kuashiria process ama mchakato wa kufanyika kwa kitu fulani taratibu ama gradually. Huo ndio msingi hasa wa kitafiti juu ya nadharia hizo. Naweza pia kusema, kufanyika ama kufanywa na kadhalika, yote ni sawa hapa katika kuashiria processes za kukamilisha uwepo wa kitu fulani.

Kisayansi kupitia nadharia mbalimbali, miili hii katika Solar System ilifanyika kupitia mchakato wa taratibu (gradually) kwa miaka kadhaa kupitia mabadiliko mbalimbali ndipo kufikia kuwa hivi ilivyo hivi leo lakini ukienda katika upande mwingine hasa wa kiimani, kuna utofauti mkubwa tu katika hilo suala la mchakato wa uumbwaji maana zipo imani zinazosimamia katika uumbwaji wa haraka ama papo hapo na kadhalika.
 
Tafiti mbalimbali zimekuwa na matokeo tofauti tofauti lakini kumekuwa na base ama msingi katika tafiti hizi kuhusiana na umri wa Mwezi. Kuwepo kwa tafiti zingine hapo baadaye zitakazoleta majibu mengine au zaidi ya haya inawezekana kabisa na hata sasa zipo lakini hizi nadharia huwa zinasimama kama msingi katika tafiti hizo mbalimbali.

Nadharia zinazohusu chimbuko la Mwezi pia ziko nyingi.

Kabla ya hii nadharia ya Giant Impact kulikuwepo na nadharia nyingine tatu (3) maarufu kuhusiana na jinsi Mwezi ulivyoweza kufanyika;

1) Nadharia mojawapo ilipendekeza, Mwezi pamoja na Dunia vilikuwa mwili mmoja lakini mapema katika historia yake, mwili huo uligawanyika katika miili miwili yaani Mwezi pamoja na Dunia kutokana na kujizungusha kwa kasi sana na kupelekea kupoteza utulivu katika mhimili wake.

2) Nadharia nyingine ilipendekeza kuwa, Mwezi na Dunia vilifanyika kwa pamoja kutokana na nyenzo moja lakini kwa kujitegemea yaani kila kimoja kivyake.

3) Pia kulikuwepo na nadharia nyingine iliyopendekeza kufanyika kwa Mwezi mahali pengine kabisa nje ya Solar System lakini ulinaswa na Dunia ulipokuwa ukipita karibu yake kutokana na gravitational force ya Dunia.

Hizo nadharia tatu hapo zilikuwepo kipindi kirefu na zilikuwa na mapungufu mengi tu mpaka kufikia kuanzishwa sasa kwa nadharia nyingine ya nne maarufu kama Giant Impact Hypothesis ambayo kwa sasa pia hufahamika kama Giant Impact Theory niliyokwisha kuielezea hapo awali ambayo imekuwa ni msingi mkubwa wa kufanyika kwa tafiti mbalimbali.

Tabia ya Mwezi kuakisi mwanga:
Tabia hii ya kuakisi mwanga wa Jua ipo katika sayari zote katika Solar System ikiwemo Dunia, kulingana na tafiti mbalimbali zilizokwisha kufanyika kwa muda mrefu sana. Kwa maana hiyo, hata tabia ya Mwezi pia kuakisi mwanga imetokana na tabia ya 'wazazi wake' kuakisi mwanga.

Sayari kugongana:
Kupoteza uelekeo huko unakokusema ni kutokana na mchakato wa Solar System kujijenga, kulingana na nadharia pamoja na tafiti mbalimbali. Inaaminika, kulikuwepo na idadi kubwa sana ya sayari 'changa' hapo awali kabisa wakati Solar System ilipokuwa ikijijenga. Hizi sayari 'changa' zinafahamika kama Protoplanets ambazo zilikuwa hazijamalizikia bado kuumbika ama kuwa sayari kamili ikiwemo pia Dunia.

Idadi kubwa ya hizi sayari 'changa' zilikuwa zikigongana na kuungana zenyewe kwa zenyewe na kuumba miili mingine mipya yaani sayari katika ukamilifu wake. Kulingana na tafiti mbalimbali, hilo linauwezekano mdogo sana kutokea tena ukizingatia kwamba Solar System yetu imekwisha mature. Hilo halipo tu katika sayari kugongana bali hata katika sayari kutemwa au kuondolewa katika mfumo ama kwa lugha ya kisasa tunasema "kukatwa".

Stability katika Solar System ni suala nyeti sana katika masuala mazima ya Astronomy na limekwisha fanyiwa kazi na wanasayasi wengi sana katika historia hata kabla ya uwepo wa mbinu za kisasa zaidi za kitafiti. Wanasayansi kwa kutumia mbinu hizi za kisasa hasa miundo ya tarakilishi, wameweza ku-predict mwenendo wa Solar System katika wakati ujao na kutafiti uwezekano wa migongano ya sayari hapo baadaye.

Mfano:
Watafiti wameweza kubaini uwezekano mdogo sana wa sayari ya Mercury kugongana na sayari ya Venus au Dunia katika miaka zaidi ya bilioni moja ijayo. Hivyo, uwezekano wa kutokea kwa migongano hiyo ni mdogo sana ambapo kwa sasa tunaweza kusema kuwa Solar System yetu ni tulivu.


Ahsante kwa majibu mazuri boss. Ilichujua muda gani wa mfumo wa solar kukomaa na kuwa thabiti na vinatumika vigezo gani kujua keamba tayari imeishakomaa hakuna muda wa ziada unahitajika ku stabilize?
 
Hahaha! Kwanini unasema hakuna anayeweza kuthibitisha nadharia hiyo?
Usipate shida, wewe kama unaweza thibitisha, ila najua huwezi mzee,hata kwanini. Sababu nadharua unabaki kuwa mtazamo wa mtu ambao hauna ushahidi, hii ndiyo maana ta nadharua, kwahiyo unapo taka nadharia ithibitishwe hiyo inakuwa tena siyi nadharia.
Kisayansi, nadharia ndio msingi katika kuweza kujifunza na kufahamu masuala mbalimbali yaliyokuwepo, yaliyopo na yatakayokuwepo hapo baadaye. Nadharia ndio starting point kabla ya kuelekea katika utafiti ama uchunguzi wa kubaini ukweli na kupata hitimisho la jambo lolote kisayansi.
Hivi hujawahi kuona shida hapa au katika hii misingi ya Sayansi ? Unaanzaje kuweka msingu kabla ya kupata matokeo ya jambo husika ? Huoni hapo hufabyika juhud ili ule uongi ulazimishwe uonekand kuwa ni Ukweli ?

Mimi tangu nakuwa mpaka leo hii, na baada ya kusoma ile misingi kumi ya kila Elimu, ukweli ni kuwa watu huisoma kwanza Elimu kisha ndani yake hutengeneza misingi kulingana na Elimu husika yaani Ukweli ulivyo. Sasa nyinyi mnaenda kinyume nyume sana, ndiyo maana tunaona mambo mengi ya uongo katika Sayansi.

Naendelea....
 
Tafiti mbalimbali zinazofanyika ili kuweza kubaini masuala mbalimbali husimamia katika hizo nadharia kadha wa kadha ambazo wanasayansi wamekuwa wakizisoma na kujifunza kwazo kwa kipindi kirefu huku tafiti mbalimbali zikiendelea kufanyika siku hadi siku kuzithibitisha.
Sasa mathalani haya maelezo hasa ta hapo juu uliyi yaweka kwako wewe unadhani yalipaswa yaje hivi hivi pasi na uthibitisho wowote kuonyesha Ukweli wake au hivyo hivyo yalivyo kuja bila ithibati ni sawa tu ?

Embu tuwe wakweli japo kidogo mzee.

Tuendelee....
 
Pia katika nadharia kuna vitu viwili:

1) Hypothesis
Safu kabisa, mfano katika mada yako hii, ni wapi huu msingi wa "Hypothesis" umetumika, maana naona wameelezea jambo kama vile huyi anaye elezea hilo jambo alikuweoi kitu ambacho ni Uongo wa wazi kabisa.

Tena kwa maelezo yako ya awali yana onyesha wazi kabisa ni nadharia,hypothesis yake iko wapi ?
 
Back
Top Bottom