FRANC THE GREAT
JF-Expert Member
- May 27, 2016
- 5,500
- 8,060
- Thread starter
-
- #21
Watafiti hawa katika utafiti huu mpya walitumia mbinu tofauti kidogo za kitafiti tofauti na hiyo unayoisema ikiwemo miundo mipya ya kihisabati kuweza kubaini na kuhesabu muda wa matukio mbalimbali kuhusiana na umri wa Mwezi. Hawakusafiri kwenda Mwezini.Mkuu vipi Hawa watafiti waliiona ile bendera ya wamarekani huko Mwezini?
Hivi miezi kumi na mbili ya kwenye calendar inapatikana wapi hasa maana mi nauona mmoja tu?
Samahani kwa kuuliza maswali nje ya mada
Ahsante
Nalog off
Miaka mingi sana. Takribani bilioni moja!Ahsante kwa majibu mazuri boss. Ilichujua muda gani wa mfumo wa solar kukomaa na kuwa thabiti na vinatumika vigezo gani kujua keamba tayari imeishakomaa hakuna muda wa ziada unahitajika ku stabilize?
Hili tamko umelitumia kimakosa, sababu maelezo yako yanaashiria kilicho husika hapo, hakina ufahamu, hakina utashi, hakina lengo, hakina uwezo na hakina hekima.Maneno; kuumbwa ama kuumbika yametumika kuashiria process ama mchakato wa kufanyika kwa kitu fulani taratibu ama gradually. Huo ndio msingi hasa wa kitafiti juu ya nadharia hizo. Naweza pia kusema, kufanyika ama kufanywa na kadhalika, yote ni sawa hapa katika kuashiria processes za kukamilisha uwepo wa kitu fulani.
Kwanza unatuthibitishia vipi uwepo wa "Solar System" nani alishuhudia hili au habari hizi mtu wa kwanza kuzielezea alikuwa nani ?Kisayansi kupitia nadharia mbalimbali, miili hii katika Solar System ilifanyika kupitia mchakato wa taratibu (gradually) kwa miaka
Hizi kumbukumbu za kufikirika au uhalisia ? Kama hazithibitiki kwanini zinaenezwa na kufanywa zionekane kuwa ni habari za kweli, wakati hata kwa kutumia njia za Kisayansi habari hizi hazithibitishwi ?miaka kadhaa kupitia mabadiliko mbalimbali ndipo kufikia kuwa hivi ilivyo hivi leo lakini ukienda katika upande mwingine hasa wa kiimani, kuna utofauti mkubwa tu katika hilo suala la mchakato wa uumbwaji maana zipo imani zinazosimamia katika uumbwaji wa haraka ama papo hapo na kadhalika.
Miaka mingi sana. Takribani bilioni moja!
Kwa mujibu wa tafiti, Solar System imekuwa "stable" kwa miaka kati ya bilioni 3 mpaka 4 hivi sasa.
Solar System tuitambuayo hivi sasa kama "stable" ni katika viwango vya kibinadamu ukilinganisha na hapo awali wakati wa mlundikano wa protoplanets kipindi ambacho Dunia bado ilikuwa ikikamilika na isingeweza ku-sustain uhai kama sasa.
Lakini tukizungumzia mabadiliko mbalimbali katika mfumo huu yapo na yataendelea kuwepo kulingana na tafiti mbalimbali. Wanasayansi na watafiti wa masuala ya anga wamekuwa wakitafuta kujua wakati ama vipindi sahihi vya kufanyika kwa mabadiliko mbalimbali katika Solar System.
Chukulia mfano Mwezi; Tokea kipindi ambacho ulikuwa na uyeyuko na bahari ya magma mpaka kukauka na kuganda kwake ni approximately miaka karibu milioni 200. Hiyo ni katika Mwezi tu vipi kuhusu sayari nyinginezo kubwa kubwa ambazo nazo zilikuwa katika mchakato wa kufanyika kwake?
Kuhusu stability ya Solar System hapo baadaye ni fumbo kubwa.
Inaaminika kwamba katika miaka bilioni 5 ijayo na kuendelea Jua litafikia stage ya uwepo wake inayofahamika kama 'red giant' kabla ya kifo chake na litatanuka katika kiwango cha kuzimeza baadhi ya sayari za karibu na haifahamiki kwamba sayari yetu itakuwa katika hali gani. Maana yake ni kwamba, Solar System nayo ina 'expiry date' ama 'life span' yake.
Kisayansi, matokeo ya jambo husika hayawezi kupatikana hivihivi kabla ya kufahamika kwa jambo lenyewe. Hata elimu yenyewe imetokana pia na misingi hiyohiyo ambayo iliwekwa hapo zamani.Usipate shida, wewe kama unaweza thibitisha, ila najua huwezi mzee,hata kwanini. Sababu nadharua unabaki kuwa mtazamo wa mtu ambao hauna ushahidi, hii ndiyo maana ta nadharua, kwahiyo unapo taka nadharia ithibitishwe hiyo inakuwa tena siyi nadharia.
Hivi hujawahi kuona shida hapa au katika hii misingi ya Sayansi ? Unaanzaje kuweka msingu kabla ya kupata matokeo ya jambo husika ? Huoni hapo hufabyika juhud ili ule uongi ulazimishwe uonekand kuwa ni Ukweli ?
Mimi tangu nakuwa mpaka leo hii, na baada ya kusoma ile misingi kumi ya kila Elimu, ukweli ni kuwa watu huisoma kwanza Elimu kisha ndani yake hutengeneza misingi kulingana na Elimu husika yaani Ukweli ulivyo. Sasa nyinyi mnaenda kinyume nyume sana, ndiyo maana tunaona mambo mengi ya uongo katika Sayansi.
Naendelea....
Safi kabisa, naomba ytupe uthibitisho wa nadharia hii, uliyo ielezea katika uzi wako. Kama huna uthibitisho wa hilo, je ni sawa haya maelezo ulivyo ya weka bila uthibitisho ?Nadharia ya kisayansi inapovumbuliwa na kuwekwa wazi, ni ili iweze kujaribiwa (tested) na yeyote yule na kwa wakati wote (all time). Nadharia inaweza kupatiwa uthibitisho mara kadhaa na bado ikabaki kuwa nadharia ili kupanua wigo wa nadharia hiyo kujaribiwa zaidi na zaidi kwa hoja na tafiti mpya.
Vizuri, je kuna jaribio lolote lililo fanywa juu ya nadharia hii uliyo tuelezea ? Yaani jaribio la Kisayansi, kama lipo naomba utufajid ni jaribio gani ?Katika kila majaribio kuendana na wakati, wanasayansi wanaweza kujiridhisha pia wanaweza kuachana ama kuacha kuzifanyia kazi nadharia ambazo zitashindwa kutoa majibu ya masuala mbalimbali kutokana na tafiti zilizokwisha kufanyika hali inayoweza kupelekea kuvumbuliwa kwa nadharia nyingine (mpya).
Kilichopo hapo hakina shida yeyote kinadharia. Linapokuja suala la kuyathibitisha mambo mbalimbali yanayotokana na nadharia hizo ndipo tunapoingia sasa katika hizi tafiti mbalimbali zinazofanyika hivi sasa.Sasa mathalani haya maelezo hasa ta hapo juu uliyi yaweka kwako wewe unadhani yalipaswa yaje hivi hivi pasi na uthibitisho wowote kuonyesha Ukweli wake au hivyo hivyo yalivyo kuja bila ithibati ni sawa tu ?
Embu tuwe wakweli japo kidogo mzee.
Tuendelee....
Safi kabisa, mintarafu jambo hilo, kisayansi nitakuwa sahihi kabisa kusema hili si jambo la Kisayansi sababu hili jambo halielezeki Kisayansi zaidi ya maelezo tu.Kisayansi, matokeo ya jambo husika hayawezi kupatikana hivihivi kabla ya kufahamika kwa jambo lenyewe. Hata elimu yenyewe imetokana pia na misingi hiyohiyo ambayo iliwekwa hapo zamani.
Hypothesis ndio hiyo nadharia iliyopo hapo (Giant Impact). Nadharia hiyo imevumbuliwa kisayansi ili iweze kujaribiwa kwa muda wote. Pia nadharia hiyo mpaka sasa ndio yenye nguvu kuliko baadhi zilizokuwepo hapo awali kisha kuwekwa 'kapuni' kwa kushindwa kutoa majibu ya maswali kadha wa kadha yenye utata kuhusiana na kufanyika kwa Mwezi.Safu kabisa, mfano katika mada yako hii, ni wapi huu msingi wa "Hypothesis" umetumika, maana naona wameelezea jambo kama vile huyi anaye elezea hilo jambo alikuweoi kitu ambacho ni Uongo wa wazi kabisa.
Tena kwa maelezo yako ya awali yana onyesha wazi kabisa ni nadharia,hypothesis yake iko wapi ?
Hapa ndipo huwa tunaona ugonjwa wa akili wa Wanasayansi, yaani jambo ambalo halina asili, mnaanzaje vipi kulifanyia utafiti huoni, haya ni matumizi mabaya ya akili na kupoteza muda ?Kilichopo hapo hakina shida yeyote kinadharia. Linapokuja suala la kuyathibitisha mambo mbalimbali yanayotokana na nadharia hizo ndipo tunapoingia sasa katika hizi tafiti mbalimbali zinazofanyika hivi sasa.
Kaka najaribu kukuelewa haya unayo yaandika lakini, yanapingana na uhalisia, hili ndiyo tatizo kubwa.Tafiti zinaweza kuipa nguvu nadharia ama pia zinaweza kuipa changamoto nadharia. Uwezo wa nadharia kuweza kutoa majibu ya maswali tata kuhusiana na masuala yahusuyo mambo mbalimbali ndio unaoipa nadharia nguvu ya kukubalika zaidi kisayansi.
Kadri nadharia inapojitetea pale ijaribiwapo ndipo inapokuwa na nguvu zaidi.
Kaka unaweza kuniambia ni Sayansi gani iliyo tumika hapo kuvumbua hiko kitu, kitu ambacho msingi wake ni dhana na hakina ushahidi ? Kwa maana huyo mtu alijuaje kwamba umri wa Mwzi ni mdogo kuliko Dunia kwa kuchukua udongo,udongo ambao hawajatupa ushahidi kwamba ni kweli umetoka huko au kutuonyesha habari hizo wamezitoa wapi ?Hypothesis ndio hiyo nadharia iliyopo hapo (Giant Impact). Nadharia hiyo imevumbuliwa kisayansi ili iweze kujaribiwa kwa muda wote. Pia nadharia hiyo mpaka sasa ndio yenye nguvu kuliko baadhi zilizokuwepo hapo awali kisha kuwekwa 'kapuni' kwa kushindwa kutoa majibu ya maswali kadha wa kadha yenye utata kuhusiana na kufanyika kwa Mwezi.
Neno hilo linafaa kabisa kuwa hapo kama kiashirio cha mchakato wa kufanyika kwa kitu fulani. Kwa lugha nyingine naweza kusema "formed". Ukizipitia hizo nadharia mbalimbali utapata kufahamu jinsi neno hilo lilivyotumika.Hili tamko umelitumia kimakosa, sababu maelezo yako yanaashiria kilicho husika hapo, hakina ufahamu, hakina utashi, hakina lengo, hakina uwezo na hakina hekima.
Nini, nakusudia hapo, ni kuwa ili kitu kiumbwe lazima awepo muumbaji na muumbaji awe na sifa hizo tano nilizo zitaja hapo juu. Namaanisha ya kuwa tafuta neno muafaks uliweke hapo ila tamko "kuumbwa" halikai hapo kwa vyovyote vile.
Naendelea....
Uthibitisho katika masuala ya kisayansi ni kupitia kitu kinachoitwa 'evidence'.Kwanza unatuthibitishia vipi uwepo wa "Solar System" nani alishuhudia hili au habari hizi mtu wa kwanza kuzielezea alikuwa nani ?
Hizi kumbukumbu za kufikirika au uhalisia ? Kama hazithibitiki kwanini zinaenezwa na kufanywa zionekane kuwa ni habari za kweli, wakati hata kwa kutumia njia za Kisayansi habari hizi hazithibitishwi ?
Ninacho kiona mimi katika maelezo yaki ni kuwa Wanasayansi wabapenda sana "Short Cut" yaani ile nitazamo yao na mawazo yao ndiyo wanataita "Facts au Evidence", ushauri wangu ni kuwa tunatakiwa kuanza kufikiria upya juu ya Sayansi,hasa sayansu ya umbile ya ulimwengu.
Hili tatizo lingine naona unalazimisha mambo kwa lipi huko kuitwe kuumba ? Kinacho umba lazima kiwe na hizo sifa. Kwa mfano maji huwa tuna sema mathalani "Bonde hili ni matokeo ya mvua kubwa iliyo nyesha wiki iliyo pita" na hakuna lugha inayo kubali ya kuwa Mvua imeumba. Unatakiwa unatazame upya suala la matumizi maneno.Pia neno "kuumbwa" si lazima lihusishwe na mtu ama kitu chenye hivyo vitu ulivyovitaja hapo bali linaweza pia kutumika kwa namna nyingine. Mfano; maji yana uwezo wa kuumba vitu mbalimbali katika mazingira yetu tunayoishi kila siku. Kwenye Geography huko kuna vitu kama vile gullies pia kuna masuala ya water erosion na matokeo yake ya kufanyika kwa landforms mbalimbali.
Upepo hauwezi kufanya hilo, bali unakuwa ni sehemu ya matikeo ya hicho unacho kidai,ila kuhusu uumbaji lazima kihusike kabla ya kuwepo na kuja kuwepo kitu hicho. Lakini tukiingia ndani zaidi kuhusu matumizi ya hili tamko, tutaona wazi kabisa ya kuwa halituwi ila na mmoja peke yake.Upepo pia unaweza kufanya vivyo hivyo. Kuna vitu kama vile mushroom rocks, sand dunes na kadhalika.
Safi kabisa, onyesha wepesi wa hoja hii.ufahamu, utashi, lengo, uwezo pamoja na hekima kama sifa za muumbaji ni hoja nyepesi ambayo kwa kawaida inaweza kuwa challenged kirahisi sana.
Hili halipo na halijawahi kuwa. Tamko kuumba linamili katika hizo nukta tano, sababu hata lugha inakataa hilo, yaani ni sawa sawa na wewe utuambie ya kuwa moto umeumba joto, au shoka limeumba kipande cha mti, na kusahahu nani aliyesababisha uwepo wa upepo huo au mvua hiyo ?Katika mfano niliyoutoa hapo kuhusiana na masuala ya kijiografia, sidhani kama maji pamoja na upepo vimekithi vigezo vyote hivyo ulivyovitaja lakini vitu hivyo viwili vinaweza kuumba maumbo mbalimbali ya kimazingira. Je, upepo au maji yana ufahamu? Je, yana utashi? Je, yana lengo? Uwezo je? (pengine). Hekima je?
Ambayo kiuhalisia ni mawazo yao binafsi wakayapa jina hilo la "Evidence/Facts" ukweli ambao siyo sahihi.Uthibitisho katika masuala ya kisayansi ni kupitia kitu kinachoitwa 'evidence'.
Sahihi kabisa, ila jambo hilo lazima kuwepo watu wa mwanzo walio shuhudia jambo hilo kisha urithi ukafata mpaka kutufikia sisi. Sasa habari inapokuja bila uthibitisho hata wa mtu wa mwanzo, tena habari ambayo ilitakiwa awepo aliye shuhudia huku ni kuihujumu Elimu na kufungua mlango wa kila mtu kujitungia anacho kitaka.Evidence sio lazima kwenda kulishuhudia jambo kwa macho likitendeka...la hasha! Bali ni ushahidi uliopo unaoweza kuthibitisha kuwa jambo fulani lilifanyika ama lilitokea ama lilitendeka hapo zamani.
Hatukatai juu ya uwepo wa tafiti mbali mabli, swali linakuja tafiti hizo zimejengeka katika msingi gani na je ni tafiti za kweli na kwanini zifanyike na je zinaweza kufanyika ?Kwa lugha nyingine tunasema, "available facts or information". Ndio maana ya uwepo wa tafiti mbalimbali, kusudi ama lengo kuu ni kukusanya ushahidi kuhusiana na masuala mbalimbali ya kisayansi.
Nilikuuliza huko awali lakini hukunijibu swali hili, je maelezo haya kwa mtazamo wako unahisi ni sawa yalivyokuja bila ushahidi na bila kuambiwa mtu huyo alijuaje au alizipataje hizi habari ? Au mnaridhika tu sababu zimekuja kwa jina la kuvutia la "Sayansi" ?Kinachopo hasa katika nadharia ya kisayansi kuhusiana na "kuumbwa" kwa Mwezi ni mchakato wa kufanyika kwa Mwezi katika hali ya utaratibu au kwa lugha nyingine 'gradually' kama nilivyosema hapo awali kupitia mabadiliko mbalimbali katika vipindi tofauti tofauti mpaka kufikia kukamilika kwake.
Nakushukuru nawe pia mkuu kwa mchango wako kupitia maswali.Nashukuru sana mkuu, niseme wazi uko izuri kwa muktadha wa namna ulivyojibu maswali yangu tena kwa lugha adhim ya kiswahili, hongera sana.
Niseme tu kwa vile mie sio mtaalam, bado hizi zote zinabaki kuwa nadharia kutokana na vile wanavyogundua watafiti. Usitaajabu kuambiwa chochote kupingana na taarifa tulizonazo kwa sasa. Habari tunazozishikilia na kuzitambua kwa sasa ni zile smbazo watafiti wetu wanatupasha kwa kadri ya uwezo walionao kwa sasa.
Narudia tena, uko vizuri kwenye eneo lako.
Nikutakie mafanikio na ufanisi uzidi kuwa msaada na mchango wako ulete tija na kugusa jamii.
Kisayansi, hiyo ni scientific hypothesis, inaelezeka kisayansi kwa kujibu hoja mbalimbali kuhusiana na masuala hayo. Na kwa sababu ni scientific hypothesis ni lazima tuijaribu. Nadharia yeyote isiyojaribiwa kisayansi hiyo si nadharia ya kisayansi, au tunaweza kusema kuwa nadharia hiyo sio "scientific".Safi kabisa, mintarafu jambo hilo, kisayansi nitakuwa sahihi kabisa kusema hili si jambo la Kisayansi sababu hili jambo halielezeki Kisayansi zaidi ya maelezo tu.
Maana hili jambo unalo tueleza hakuna anae jua hali yake ya hakika, isipokuwa dhana tu na utunzi wa kupendeza, sababu mueleza jambo hili kwanza halulishuhudia wala hakuchukua toka kwa wale walio lishuhudia bali hata hao walio shuhudia hawakuwahi kuwepo. Kwa minajili hiyo hili tukio halina tofauti na hadithi za ESOPO.
Jambo lipi hilo ambalo halina asili?Hapa ndipo huwa tunaona ugonjwa wa akili wa Wanasayansi, yaani jambo ambalo halina asili, mnaanzaje vipi kulifanyia utafiti huoni, haya ni matumizi mabaya ya akili na kupoteza muda ?
Hivi mathalani, kwa jambo hili katika mada yako, vipi wana sayansi waanze kufanya utafiti juu ya jambo ambalo kwanza halina asili, pili haliezeki kisayansi, tatu linajulikana kabisa haliwezi kuthibitishwa ?
Kaka najaribu kukuelewa haya unayo yaandika lakini, yanapingana na uhalisia, hili ndiyo tatizo kubwa.
Mathalani unaweza kunipa mfano wa nadharia yoyote inayo jitetea na mwisho wa siku nadharia hiyi ikasimama imara ?