Mwezi una umri mdogo kuliko tulivyodhani! Je, unaamini?

Kuruhusu maji kufanya hivi ama vile ni jambo jingine. Mimi siko huko bali niko hapa; hilo bonde limetoka wapi? Nani kalileta hapo? Kwanini liitwe bonde?

Why "bonde"?
Haupo huko wakati maji yanafanya athari ?
Yameumbwa na Mola muumba mwenye hizo sifa zote hapo juu nilipo kutajia. Mwenye uwezo, mwenye kujua, mwenye malengo, mwenye hekima.
Swali langu liko pale pale na hulikwepo,nithibitishie tu ya kuwa hayo maumbo yamesababishwa na UPEPO usipate tabu. Hili ndiyo swali la msingi.
Unahitaji uthibitisho upi kuhusiana na kuumbika kwa maumbo hayo?
Kwamba UPEPO ndiyo umesababisha haya maumbile, au unasoma bila kuelewa nini mzee ? Halafu natumia lugha rahisi sana. Mfano, naomba unithibitishie ya kuwa Mlima Kilimanjaro umesababishwa na UPEPO ndiyo maana ukawepo.
Unafahamu uwepo wa maumbo ya kijiografia? Unafahamu maana ya 'umbo'?
Nafahamu kuhusu Jiografia ni kuwa wanajaribu kuelezea maumbo ambayo yapo na ilikuwaje yakawepo, kwa kutumia mawazo yao binafsi bila ushahidi wowote wa kielimu.

Nina fahamu vizuri sana maana ya umbo.
Ushahidi ni kupitia maumbo ya kijiografia ambayo yapo katika mazingira yetu hayahaya tunayoishi kila siku. Hayo maumbo yanatokea tu papo hapo, out of nowhere?
Hakuna aliyesema yanatokea out of nowhere" ila tunataka ututhibitishie ya kuwa haya unayo sema ni ya kweli au huwa mnasema ili kujifurahisha tu ?
Mtoa majina ya maumbo hayo si hoja bali hoja ni kile kilichosababisha kuwepo kwa maumbo hayo mbalimbali katika mazingira yetu.
Hii ni hoja tena hoja ya msingi sana, na huthibitisha ukweli wa muumbaji, vipi aumbe pasi na kujja alichokiumba ? Ndiyo maana nilikwambia uwezo siyo tu sifa pekee ya muumbaji, bali ufahamu na lengo hazikwepeki, ona sada hiki kidogo tu cha majina kina kushinda na kinaonyesha lazima muumbaji ajue hili.
 
Naomba niliweke hili sawa kwa faida ya wengi: KUUMBWA | MUUMBAJI | MUUMBA

Kabla ya yote, nilisema hapo awali kwamba sifa kuu ya muumbaji yeyote ni moja tu ambayo ni "uwezo wa kuumba". Hoja yako ya vigezo vyako vitano (5) unayoitumia hapa ni hoja dhaifu. Haina mashiko!

Hebu sasa niliweke hili sawa kwa faida ya wengi. Pay attention!

Kulingana na tafsiri ya neno "muumbaji" au "muumba" kutoka katika kamusi niliyonayo karibu hapa; Kiswahili-Kiingereza [TUKI]: Tazama mshale mwekundu pichani hapo:



MUUMBA:
Kuna tafsiri mbili hapo ambazo ni "creator" pamoja na "God". Nilikwisha sema hapo awali kwamba, neno "muumbaji" au pia "muumba" lina tafsiri zaidi ya moja. Kuna tafsiri ya kawaida ambayo ni "creator" pia kuna tafsiri nyingine ya kiimani ambayo ni "God".

Sasa,
Hiyo tafsiri ya kwanza kabisa "creator" yenye herufi "c" ndogo mwanzoni mwa neno hilo ndio ninayoitolea ufafanuzi hapa. Kwa utafutaji mwepesi kabisa kupitia mtandao pamoja na vyanzo mbalimbali vyenye kutoa maana za maneno [kamusi], haya ndio majibu:






CREATOR:
1) A person or thing that brings something into existence.
2) A person or thing that creates.
3) Something or someone which creates or makes something.

Uchambuzi:

A person katika tafsiri hizo ni binadamu yeyote yule ambaye kutokana na tafsiri ile ya kiswahili hapo awali, binadamu pia anaweza kuwa muumba ama pia muumbaji kwa maana ya kwamba, anaweza kuumba ama kufanya uumbaji.

Lakini kuna kitu cha pili hapo baada ya neno "person", nacho ni "thing". Kwa utafutaji mwepesi pia katika vyanzo mbalimbali vyenye kutoa maana za maneno, "thing" ni kitu chochote kile isitoshe, hata kisicho na uhai.




Maana yake ni kuwa, kwa kutumia tafsiri yetu pale awali [muumba], kitu chochote kile chenye uhai ama kisicho na uhai kinaweza pia kuwa muumba ama kufanya uumbaji. Mfano; maji, upepo n.k. kama jinsi ilivyo katika maumbo mbalimbali ya kijiografia.

Swali: Kitu kisicho na uhai kina hivyo vitu vyote vitano ulivyovitaja hapo awali? Je, kina ufahamu? Je, kina utashi? Je, kina lengo? Je, kina uwezo? (pengine). Je, kina hekima?

HAPANA!

Kwa maana hiyo, ni sahihi kabisa kulitumia neno hilo katika mifano ya vitu visivyokidhi zile sababu zako ama vigezo vyako vitano (5) kuhusu "muumba" ama "muumbaji". Maana yake ni kwamba, vile vigezo vyako vitano havina sababu yeyote ile ya kuwepo wala maana yeyote ile ya kumzuia mtu yeyote kulitumia neno hilo katika vitu visivyokidhi hivyo vigezo vyote.

Asante!
 
Safi kabisa, kwanza kabisa nasikitika ya kuwa hata kusoma Kamusi pia hujui. Hapo hakuna maana mbili, bali maana ni moja kisha ikamuweka wazi anae kusudiwa, ndiyo maana ukaambiwa muumba kisha ikafata creator, kisha mkato kwa maana ya God, yaani hayo ni majina na ufafanuzi wake. Kwamba muumba ni "God". Ndiyo maana huwezi kukuta katika Kiswahili tamko hili limetumika kwa kitu nje ya Mola. Kwa maana hiyo unae tumia tamko hili unakuwa upo kwenye makosa, na hiyo kamusi yako hakuna sehemu inayosema ya kuwa Muumba ni kitu nje ya Mola au kitu kisicho kuwa na ufahamu na maarifa.

Pili, kuna neno na maana ya neno, wewe tu niambie ni kwa lugha gani unayo ijua watu wake huwa wanatumia tamko "Creator" nje ya "God" ?

Naendelea ....
 
Karibu!

Ni kweli kwamba Giant Impact Hypothesis ndio nadharia inayotumika zaidi kwa sasa lakini ni kweli pia kwamba hilo halitoi majibu ya asilimia 100 kuhusiana na chimbuko la mwezi. Lakini hilo pia halituzuii kuchimbua kwa undani zaidi kujua ni nini kilitokea.

Kuhusu kuviweka hivyo vitu hapa ni moja ya jambo ambalo nimekuwa nikiliandaa kama nilivyosema hapo awali wakati nilipokuwa nikihitimisha bandiko langu. Mchanganuo mzima wa kufanyika kwa utafiti huu nitauweka hapa muda si mrefu na pia kupitia "link" ambayo maelezo yote yamechapishwa humo.

Mfanano wa composition kati ya Mwezi na Dunia unahitaji more detailed explanation kutokana na published results na si kila kitu nitakiweka hapa kama kilivyo na isitoshe najaribu kuvielezea katika lugha nyepesi zaidi ila kila moja wetu angalau aweze kupata kitu fulani.

Haya,

Kulingana na tafiti, composition ya Mwezi ni sawa na ya sayari yetu ya Dunia huku pia kukiwa na mfanano wa miamba iliyopo hapa Duniani pamoja na ile iliyopo huko Mwezini.

Kivipi?

Isotopic compositions zinazofanana:

In 2001, a team at the Carnegie Institution of Washington reported that the rocks from the Apollo program carried an isotopic signature that was identical with rocks from Earth, and were different from almost all other bodies in the Solar System.

Ripoti ilichapishwa katika link hii ya Astrophysics Data System:
Oxygen Isotopes and the Moon-Forming Giant Impact

Oxygen isotopic compositions kati ya sampuli ya sayari yetu pamoja na ile ya Mwezi inaonesha kuwepo kwa uwiano wa karibu kati ya hizo isotopes za oxygen katika Mwezi na katika sayari yetu hii.

Indirect evidence for the giant impact scenario comes from rocks collected during the Apollo Moon landings, which show oxygen isotope ratios nearly identical to those of Earth.

The proto-Earth as a significant source of lunar material:

A giant impact between the proto-Earth and a Mars-sized impactor named Theia is the favoured scenario for the formation of the Moon. Oxygen isotopic compositions have been found to be identical between terrestrial and lunar samples, which is inconsistent with numerical models estimating that more than 40% of the Moon-forming disk material was derived from Theia:

The proto-Earth as a significant source of lunar material

Mfanano wa composition pekee kati ya Mwezi na Dunia hautoshi kuibeba hypothesis. Kuna changamoto mbalimbali ambapo kuna masuala mengine zaidi ambayo kupitia kwayo tunaweza kusema ndio msingi wa hypothesis:

Kuna vitu kama, bahari ya magma tunaita Lunar Magma Ocean, mfanano wa muelekeo wa Earth's spinning na Moon orbit, migongano mingineyo inayopelekea debris discs na kadhalika.

Kiini cha Dunia ni kikubwa kuliko ambavyo ingetegemewa kuwa katika mwili wa ukubwa ama size kama yake. Hiyo ndio statement niliyoisema.
Hilo ni kutokana na kitu kinachoitwa core merging; muunganiko kati ya core ya Dunia na ile ya Theia. Hili limeelezwa katika nadharia ya Giant Impact.

The giant impact hypothesis states that an impact between a theoretical Mars-sized planet Theia and the early Earth formed the modern Earth and Moon. During this impact the majority of the iron from Theia and the Earth became incorporated into the Earth's core.

In addition to explaining Earth's large moon, the Theia hypothesis can also explain why Earth's core is larger than would be expected for a body its size; Theia's core and mantle mixed with Earth's.


Kupitia mbinu kama vile seismology, planetary dynamics n.k. tunaweza kupata kufahamu masuala mbalimbali yahusuyo planetary cores. Pia, katika suala la cores, kuna utofauti mkubwa kati ya cores za sayari mbalimbali. Mfano; Core ya Dunia inatajwa kuwa asilimia zipatazo 55 ya nusu kipenyo chake (radius). Kubwa kiasi! At most 50% pengine ingetosha kutokana na umbile lake...Hahaha!

Ukiitazama sayari ya Venus pamoja na sayari yetu almost zinafanana kwa size lakini ukitizama katika size za cores zake, ni tofauti. Size ya core ya Dunia ni kubwa zaidi kuliko core ya Venus. Hizi sayari mbili huitwa "sister planets" kutokana pia na uwiano wa maumbile yake lakini ukitizama cores zake ndipo tunarudi palepale katika "kutokutegemewa" kwa ukubwa wa core ya Dunia ukilinganisha na size ya umbile lake.

Lakini, sayari ya Mercury inatajwa pia kuwa na kiini kikubwa ukilinganisha na sayari nyingine zote katika Solar System kwa asilimia 75-85 ya nusu kipenyo chake. Inaaminika kuwa ni kutokana na kupoteza materials nyingi sana katika umbile lake la nje wakati wa mapema zaidi wa kufanyika kwa Solar System.

Asante!
 
Baada ya mugangano huo SAYARI ndogo ya THEIA ilielekea upande upi?
Haikuelekea upande wowote bali iliungana na Dunia wakati ambapo Dunia ilikuwa 'changa'.

The giant impact hypothesis states that an impact between a theoretical Mars-sized planet Theia and the early Earth formed the modern Earth and Moon. During this impact the majority of the iron from Theia and the Earth became incorporated into the Earth's core.
 
Katika kipindi hicho duniani kulikuwa hakuna uhai wa viumbe?

Je theia inaweza kuwa chanzo cha kuleta maji ya bahari na mito duniani.?
 
Katika kipindi hicho duniani kulikuwa hakuna uhai wa viumbe?

Je theia inaweza kuwa chanzo cha kuleta maji ya bahari na mito duniani.?
Ndio, kulingana na studies mbalimbali. Uhai imetajwa kuwepo atleast miaka bilioni 3.7 iliyopita kutokana na tafiti mbalimbali.

Kuhusu swali la pili;
Ndio! Sayari ndogo hiyo inatajwa kuweza kuwa chanzo cha uwepo wa maji Duniani baada ya ule mgongano.
 
Ndio, kulingana na studies mbalimbali. Uhai imetajwa kuwepo atleast miaka bilioni 3.7 iliyopita kutokana na tafiti mbalimbali.

Kuhusu swali la pili;
Ndio! Sayari ndogo hiyo inatajwa kuweza kuwa chanzo cha uwepo wa maji Duniani baada ya ule mgongano.
Unafahaku Fuvu la binadamu wa kale lina umri gani?
Mijusi wa kubwa wa kale (dinosorous) Wana umri gani? Maana huenda ndio jamii wenye umri mkubwa
Dunia yetu ina umri gani?
 
- Earth's radius ni 6371km, na core ina 3471km which is slightly higher than 50% .. Venus ina radius ya 6052km, na core yake ina radius ya 3200km which is also slightly higher than 50% , Hizi hesabu hazilingani kabisa na maelezo yako hapo.

Mercury pekee ndio inaonyesha silicate- metal ratio ya utofauti na paka leo bado wanasayansi wanatafuta sababu ya hilo. Hypothesis zipo ndio kama uliyoisema hapo lakini haimaanishi ndicho kilicho tokea.

- Pia unaposema ocean of magma, can u account for the sources of heat in the moon that would've caused the ocean of magma 85 million years after the solar system was formed?

Source ya heat pekee inayoweza kutengeneza hiyo ocean of magma ni heat from when the planets were formed, ambayo kulingana na hypothesis mwezi hauwezi kua nayo maana haukuwepo.

Kutokuwepo kwa evidence ya volcanic activities mwezini na uwepo wa volcanic rocks (basalt) zenye umri wa zaidi ya miaka billioni 4 mwezini kunatoa evidence kwamba the moon was formed at the same time with other bodies kwenye solar system.
 
Katika kipindi hicho duniani kulikuwa hakuna uhai wa viumbe?

Je theia inaweza kuwa chanzo cha kuleta maji ya bahari na mito duniani.?
- Dunia ya mwanzo ilikua ujiuji na homogenious, ilianza kupoa taratibu na wakati huohuo vitu vizito kama Iron na Nikel vilizama katikati kwa sababu ya uzito wake( vikatengeneza core),

- Vitu ambavyo ni vizito kidogo kama magnesium na silicate vilizama pia juu ya core (kutengeneza mantle ambayo ni ujiuji). Na juu kabisa baada ya kupoa zaidi ilitengeneza crust ambalo ni ganda gumu.

- Wakati dunia inapoa ilitoa gases mbalimbali kama Sulphur, Carbondioxide nk kwa process inayoitwa degasing na inasemekana pia kwamba components zinazounda maji pia zilitoka pamoja na hizo gases wakati dunia ikiendelea kupoa.

- Gase ni nyepesi zaidi hivyo ilikaa juu zaidi na ikatengeneza primitive atmosphere. Atmosphere ambayo haikuweza kufaa kwa maisha yeyote.

- Kiumbe wa kwanza wanaosemekana kuwepo duniani na Autotoph (Cyano bacteria).. hawa waliishi miaka bilioni 2 iliyopita na inasemekana ndio waliohusika kuzalisha oxygen katika atmosphere na kufungua milango kwa viumbe wengine wanaotumia oxygen.
 
Asante kwa maelezo yaliyo shiba
 
Unafahaku Fuvu la binadamu wa kale lina umri gani?
Mijusi wa kubwa wa kale (dinosorous) Wana umri gani? Maana huenda ndio jamii wenye umri mkubwa
Dunia yetu ina umri gani?
Hao wanyama unaowaita mjusi wakubwa waliishi miaka takriban milioni 200 iliyopita. Katika Period ya Jurassic na Era ya Mesozoic. Hao sio viumbe wenye umri mkubwa, dunia ina miaka bilioni 4.5.

- Fuvu la kale linamiaka millioni 2 tu.
 
Usiuchoshe ubongo wako kwa vitu ambavyo haviwezi kukusaidia maishani.
 
Unafahaku Fuvu la binadamu wa kale lina umri gani?
Mijusi wa kubwa wa kale (dinosorous) Wana umri gani? Maana huenda ndio jamii wenye umri mkubwa
Dunia yetu ina umri gani?
Nafikiri umekwisha pata jibu la swali lako.
 
Tunahitaji watu vichwa kama nyie, hizi ndo nyuzi za kusoma aisee, Full maarifa.
 
Usiuchoshe ubongo wako kwa vitu ambavyo haviwezi kukusaidia maishani.
Mwanzo wa ungumbaru na upumbavu wa mtu mweusi ndo huwa huu. Mzee mafanikio kwenye maisha si chakula tu na kuzaliana tu!, ila unatakiwa ujijue upo wapi, upo na nini na unafanya nini. Lengo la maisha halikuwa kuja kufanya kazi na kula, ila kuja kujifunza yote yaliyo mbele yetu.
 
Una akili timamu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…