Mwigulu Nchemba awaambia Watanzania wahamie Burundi wasipoweza kulipa tozo za miamala

Mwigulu Nchemba awaambia Watanzania wahamie Burundi wasipoweza kulipa tozo za miamala

Wananchi tunahitaji kujua kama Kauli ya Waziri wa fedha Bwn. Mwigulu kwa wananchi wanaolalamikia makali ya tozo kuwa kama wanahisi wanaonewa wahamie Burundi ni ya serikali au ya kwake binafsi.

Tunataka kufahamu hivyo ili tuweke rekodi zetu sawa.

Kwakua Waziri ni sehemu ya Serikali na anaingia kwenye vikao vya baraza la mawaziri.

Kama baraza zima lilibariki tozo basi pia limebariki na kauli hii ya kuhamia Burundi.

Maana kama hukubaliani na tozo basi unapaswa kuhamia Burundi na wananchi wengi tu hawakubaliani nazo.

Serikali itufafanulie kuhusiana na hili jambo ili ukweli ufahamike maana kauli ya serikali ni amri kwa wananchi.
Ni ya serikali. Hivi Rais Samia huu mzigo anawezaje kukaa nao??? Yaani inakera, kwanza ni kashfa kubwa sana kuwaambia watanzania wenzako eti wahamie Burundi???? Yaani disgusting 🤮
 
Ulijipiga kifua na kufurahi huku ukikenua meno. Ukatuambia tuhamie Burundi. Sasa mnashughulikia nini.?
Screenshot_20220912-184510.jpg
 
Tulikuona kwa macho yetu uso mkavu na ukiwa serious kuwa kama hatutaki kulipa tozo tuhamie Burundi.

Sasan mtu aliyekosoea bahati mbaya atatamka maneno kama haya?

Leo hii unadai wewe ni binadamu na ulikosea!

Hao binadamu uliosema wahamie burundi ni wanyama?
 
Back
Top Bottom