Mwigulu Nchemba, hata kama Magufuli hayupo hai ulipaswa kumheshimu

Mwigulu Nchemba, hata kama Magufuli hayupo hai ulipaswa kumheshimu

Endelea kujifanya umesikiliza sana ukasau umuhimu wa tafakuri baada ya kusikia. Ulimwengu huu unaendeshwa kwa tafakuri siyo kwa kusikia. The same person for more than five years hajawahi katika ukumbi wa Bunge kumsifia JK Wala kumtamka akihusianisha utawala wake na Magu....alikaa kimya kulinda ugali wake. Leo hii anataka kuendelea kuishi kwenye nafasi hiyo badala amwone Rais aliyepo na kumpongeza au kumsifia anamfanya Rais Kama mwanafunzi akilinganisha umahiri wake na walimu waliomkuza.

Unapofanya ulinganisho kwenye ngazi au taasisi kubwa Kama ya Urais lazima uangalie damage ya ulinganisho unaofanya. Mitandao inaandika daily kuhusu habari zisizo za kuaminika kwamba JK anaongoza nchi, wewe Kama Waziri badala yakumeza mate usimshtue mwizi unaamua kukoa makusudi ili mwizi akimbizwe kwa kelele za wanakijiji. Pls tujifunze siasa tukiongeza na taalum kidogo ya econimic diplomacy.

Bajeti ya nchi haisomwi kisiasa Wala kishabiki, inasomwa kiuchumi kufungua mjadala wa kiuchumi siyo mjadala wa kisiasa na madaraka.

Mwigulu umekosea kusema ukweli wakati rangi yako toka huko nyuma watu wanaijua....ulirudishiwa Uwaziri kwa siasa hizihizi ila Sasa hivi unapaswa kujiamini kwamba unaweza ukasimama bila JK Wala mama Samia. Usipende sana kujificha kwenye kivuli Cha waliokuzidi madaraka....jitengenezee jina lako
 
  • Thanks
Reactions: Ame
Mleta uzi kasimama upande aliopenda yeye
4. Mwigulu alikuwa straight kwénye kumsifia Kikwete, alikuwa akijenga hoja ya ubora wa mama. Akaonesha umahiri wa Kikwete
Mkuu usihangaike na #pushgang. Wakisikia jina JK wanaanza kuwashwawashwa kwenye makalio.
 
Mwigulu hana Hatia sababu Jiwe alidharau wateule wake hadi Wananchi na Mkewe pia... so Kama hatuoni faida ya Iddi Amin au Hittler na Jiwe pia ukatiri wake sikuupenda kamwe..
 
TIMU FULANI BADO TU WANAPATA TABU SANA,YAANI UTAFIKIRI MWENDA ZAKE ATAKUJA KURUDI,POLENI SANA.
KUBALINI YALIYOTOKEA TWENDENI NA MAM SAMIA,HICHO MLICHONACHO WAZARAMO WANAITA "GUBU", FUNGENI PAZIA TUSONGE MBELE.
 
Nilikua nasikiliza hotuba yake hapa bukoba.. alipo fika hilo eneo nikazima TV na kwenda kulala.


Anajipendekeza kwa JK ili ateuliwe 2025 kuwa Rais.
Nimemsikiliza Mhe. Mwigulu Nchemba akimwagia sifa za umairi Jakaya Mrisho Kikwete, nimeshangazwa sana na kitendo hiki kwa sababu zifuatazo;
Mwiguli alikuwa anawasilisha hotuba ya bajeti ambayo kimsingi haina hoja mahususi inayolazimisha kumtaja JK, Magu Wala Mkapa. Ni Nini kimemsukuma kuweka paragraph hii kwenye hotuba yake? Anamsuta Nani?
Hata Kama JK alikuwa kiongozi, Magufulu pia alikuwa kiongozi. Unapotoa sifa za kiongozi ambazo hazishabiani na kiongozi asiyekuwepo Duniani huku huko nyuma hukuwahi kutoa sifa Kama hizo kwake nikuutangazia umma kwamba huna na ujawahi kuwa na heshima kwake Bali ulikuwa unatafuta madaraka.
Lakini pia kumtaja JK kwa kumuunganisha na Mama Samia kunaleta picha kwamba bila JK uamini Kama Rais aliyepo anaweza kuongoza nchi. Naweza nisiwe sahihi lakini mitandao yote inaandika kwamba JK ndiye anayeongoza nchi kwa Sasa, Waziri wa fedha na timu yako kitendo chakuibgiza sifa za JK nikumdhalilisha Rais kwa kuonyesha umma kwamba wanayosema wanaharakati na watu wengine ni sahihi.
Lakini pia napata mashaka na uwezo binafsi wa mtu huyu katika nafasi hii nyeti, Wizara ya fedha ni nyeti. Aina ya bajeti aliyowasilisha inahitaji elimu kubwa kwa umma iweze kuonekana kwamba ina malengo chanya na kuepusha upotoshaji wakimantiki unaoweza kufanywa na watu wasio serikalini. Kuwasilisha bajeti Kama hii huku ukiweka sifa za JK kumeligawa Taifa na chama pia. Watu wengi wameondoka kuijadili bajeti wamejadili udhalimu na unafiki wakimfumo unaofanywa na wanasiasa kuwasaidia kuendelea kuteuliwa. Madhara yake ni kwamba upotoshaji utakuwa mwingi nakupunguza imani ya wananchi kwa serikali.

Utavuna ulichopanda, na naamini au natabiri hii itakuwa bajeti yako ya mwisho Kama Waziri wa fedha. Soon utajionea labda kama hawataona damage yako kwa macho ya Tanzania mpya
 
Hata Kama JK alikuwa kiongozi, Magufulu pia alikuwa kiongozi. Unapotoa sifa za kiongozi ambazo hazishabiani na kiongozi asiyekuwepo Duniani huku huko nyuma hukuwahi kutoa sifa Kama hizo kwake nikuutangazia umma kwamba huna na ujawahi kuwa na heshima kwake Bali ulikuwa unatafuta madaraka
Mkuu 'Beatrice', ninakubaliana nawe katika mada yako hii.

Lakini ninakuomba sana, katika hawa viongozi wa leo, ni kiongozi gani; labda Lukuvi? Sijamsikia hata siku moja, sijui.

Huyo Mwigulu, kama Kigwangala, kama akina Kabuti Kalamaganda..., hebu niambie, yupo kiongozi leo hii katika viongozi waliopo anayesimama kwa kichwa chake? Huyo aliyekuwa Makamu; angalau yeye mara nyingi alijinyamazia ilipobidi anyamaze, lakini hata yeye ni kundi hilo hilo.

Mwigulu anajuwa ni nani sasa ambaye ni 'King maker' wa viongozi wajao wa taifa hili. Anajipigia paramanda aonekane kwa mhusika ili wakati ukiwadia, achaguliwe yeye.

Mwigulu hana sifa yoyote ya uongozi, lakini kama ilivyozoeleka sasa ndani ya taifa hili, viongozi hatuwapati kwa kuwa na sifa za uongozi. Anayejuwa kulamba viatu ndiye mwenye nafasi kubwa ya kuongoza nchi.

Hivi kweli utaniambia Ndugai yupo alipo kwa kuwa na uwezo wa mahali hapo? Yupo hapo kwa sababu alijuwa wapi pa kujiegemeza ili asimame.

Vile vile tambua kwamba, kwa Mwigulu kumumwagia sifa Kikwete, moja kwa moja sifa hizo zinamsuza Samia, kwa vile Kikwete ndiye godfather. Kwa kufanya hivyo, Mwigulu analinda maslahi yake.
 
Mkuu usihangaike na #pushgang. Wakisikia jina JK wanaanza kuwashwawashwa kwenye makalio.
Watu nyie mlimchonganisha JK na kanda ya kaskazini enzi hizo, sasa mnatafuta kuchonganisha na kanda ya magharibi mki tumia Mh. Rais na kumwonyesha kama vile yeye pekee hawezi; kesho mtakuja na nyingine, dhambi ya ubaguzi haikuwahi kuwaacha wabaguzi salama...ni watu msiojiamini wala hamnaga aibu za uso...Poleni, njia ya mwongo ni fupi, hii marathoni hamuiwezi ukitimia mwaka tu mtakimbiana hapa pale mambo yote yatakapo wageuka na kuwatazama usoni...Uovu haukuwahi kushinda, wala giza halijawahi tamalaki mbele ya mwanga...Njia yenu imejaa mashimo na utelezi...Be warned!
 
mh, ila yanayomkuta JK kikwete nina hakika hata Nyerere hakuwahi kuyakabili......jamaa anaandamwa sana aisee;

wakati wa utawala wake chadema walihakikisha hafanikiwi kwa lolote, kiubishi ubishi sana akapenya!

anaandamwa kuwa eti alimsaliti lowassa.....yet, hakuna mwenye kuujua undani hadi sasa.

wakati wa utawala wa mwendazake, aliandamwa mno kwa kukosolewa kuwa hakufanya chochote wakati wa utawala wake na hata kunyamazishwa 'kibabe' mbele ya kamera pale aliojaribu kutoa maoni, hilo lilifanywa na mwendazake mwenyewe na 'washikadau' wake.

sasa hivi (wakati huu wa awamu hii ya sita), anaandamwa kwa kila hatua anayoichukua mama.....kwamba eti ndiye anayeongoza nchi sasa. kama hilo halitoshi, anaambiwa kuwa anahusika na kuondoka kwa mwendazake. kivipi? hakuna mwenye jibu.

Mungu ni mkubwa, na mapito haya pia yatapita......pole sana JK Kikwete, tunapokuona na tabasamu lako pamoja na yote haya, hakika wewe ni jasiri sana!🙏🙏🙏🙏🙏 Kama unataka kusoma kuhusu uvumilivu basi shule ni JK
 
mh, ila yanayomkuta JK kikwete nina hakika hata Nyerere hakuwahi kuyakabili......jamaa anaandamwa sana aisee;

wakati wa utawala wake chadema walihakikisha hafanikiwi kwa lolote, kiubishi ubishi sana akapenya!

anaandamwa kuwa eti alimsaliti lowassa.....yet, hakuna mwenye kuujua undani hadi sasa.

wakati wa utawala wa mwendazake, aliandamwa mno kwa kukosolewa kuwa hakufanya chochote wakati wa utawala wake na hata kunyamazishwa 'kibabe' mbele ya kamera pale aliojaribu kutoa maoni, hilo lilifanywa na mwendazake mwenyewe na 'washikadau' wake.

sasa hivi (wakati huu wa awamu hii ya sita), anaandamwa kwa kila hatua anayoichukua mama.....kwamba eti ndiye anayeongoza nchi sasa. kama hilo halitoshi, anaambiwa kuwa anahusika na kuondoka kwa mwendazake. kivipi? hakuna mwenye jibu.

Mungu ni mkubwa, na mapito haya pia yatapita......pole sana JK Kikwete, tunapokuona na tabasamu lako pamoja na yote haya, hakika wewe ni jasiri sana!!
Wapambe nuksi wanamsababishia matatizo baba wa watu...Kwakweli shule ya uvumilivu inapaswa kusomwa kwake...And always smiling!

He has to draw a line na baadhi ya anaowafikiria ni watu wake...Ile kuwa diplomatic wanaitumia kwa advantage yao huku gharama akibeba yeye binafsi...
 
Imeandikwa kwa damu takatifu so bad...Haitofutika kirahisi...Pole sana! Najua unaumia ila nifanyeje, Mungu kaamua kumvindicate na kumpa heshima ya milele
mungu yupi?Mungu wa mbingu na dunia hawezi kumpa heshima mtu anayetesa wengine, mporaji na mtukanaji
 
mh, ila yanayomkuta JK kikwete nina hakika hata Nyerere hakuwahi kuyakabili......jamaa anaandamwa sana aisee;

wakati wa utawala wake chadema walihakikisha hafanikiwi kwa lolote, kiubishi ubishi sana akapenya!

anaandamwa kuwa eti alimsaliti lowassa.....yet, hakuna mwenye kuujua undani hadi sasa.

wakati wa utawala wa mwendazake, aliandamwa mno kwa kukosolewa kuwa hakufanya chochote wakati wa utawala wake na hata kunyamazishwa 'kibabe' mbele ya kamera pale aliojaribu kutoa maoni, hilo lilifanywa na mwendazake mwenyewe na 'washikadau' wake.

sasa hivi (wakati huu wa awamu hii ya sita), anaandamwa kwa kila hatua anayoichukua mama.....kwamba eti ndiye anayeongoza nchi sasa. kama hilo halitoshi, anaambiwa kuwa anahusika na kuondoka kwa mwendazake. kivipi? hakuna mwenye jibu.

Mungu ni mkubwa, na mapito haya pia yatapita......pole sana JK Kikwete, tunapokuona na tabasamu lako pamoja na yote haya, hakika wewe ni jasiri sana!!
... kwani kuna vita? .................. JK
😅
1623357776361.png
 
Back
Top Bottom