Elections 2015 Mwigulu Nchemba: Huu Unyama Una baraka zote za Dr. Slaa na genge lake

Elections 2015 Mwigulu Nchemba: Huu Unyama Una baraka zote za Dr. Slaa na genge lake

Kwa kweli mwigulu nchemba ameongea kweli hawa chadema wanataka tuwe kama wasomalia kila siku vita,tunashukuru watanzania wanaelewa umuhimu wa aman yetu na hawapo tayari kuiingiza nchi kwenye dimbwi la damu.Tunatamani upinzani ila sio chagadema.
 
ukibishana na mjinga na wewe pia utakuwa mjinga na kukosa hekima na busara, poor mwigulu ni kama dekio au fagio la chooni, unajua wakati mwingne kwel ccm inatia huruma sana na hasira sana bac sisi werevu tupotezee huu ujinga wa hao watu nina imani kubwa na watanzania watawapuuza hao vicha wenye uchu na madaraka
 
Wewe dogo Mwigulu, unapata wapi ujasili wa kufanya ushetani huo, utaacha lini tabia ya kuwadhalilisha waremavu, hivi ungekuwa wewe ni mlemavu, halafu wenzio wanakutumia kama mtaji wa kisiasa, kwa kukupandisha majukwani ukidhalilishwa kwa ulemavu wako, ungejisikiaje, huyo Tesha ulimpeleka Mbeya kata ya Iyela ukampandisha majukwani, ccm ikaambulia patupu, muache kijana wa watu apumnzike, na nyie haki za binadamu mko wapi, hamyaoni haya, ni nani asiyejua kuwa wewe unafanya kazi ya kuwatengenezea kesi za ugaidi viongozi wa Chadema, ni nani asiyejua wewe ndiye uliyehusika na bomu kule Arusha, ni na nani asiyejua unahusika na kifo cha Dr sengondo Mvungi, una laana wewe, damu za watu wasio na hatia zinakulilia.
 
Hivi hajui kuwa anaingilia kesi iliyokomaa mahakamani kule Igunga ya Tindikali? Mbona ana dharau mahakama?
 
Siasa puuzi namna hii si za watanzania. Hao wanaotembea na mwigulu hawajisikii kuzalilisha hutu wao? Nini vyombo vya dola vinaweza kufanya juu ya mwigulu kuhamasisha chuki ndani ya nchi? Inamaana hawa jamaa hawakutendewa haki na mahakama?

Kama cdm itatumia picha za mauaji Arusha na matukio mengine ya kinyama yaliyofanywa na polissm na greenguard nini serikali itafanya?

Mwigulu stop foolishness! Watanzania hacheni kutamaza na kusikiliza upuuzi huo! mkanda wa rwanda 1994 ulipochuja kutishia watanzania wasichague upinzani sasa mmebadirisha mbinu kwa kuumiza watu wenu ndani alafu mnawatumia kama vikalagosi? Shame on you!
 
Watanzania hawana haki ya kulia maisha magumu kwani wameipenda ccm kwa dhiki bila raha. Huwezi kuwa na maendeleo kwa kudumisha chama/kikundi kimoja madarakani. Hata watumishi wa umma hawakai kituo kimoja cha kazi milele, basi notion hiyo itumike pia kwenye siasa.
 
Kwa kweli mwigulu nchemba ameongea kweli hawa chadema wanataka tuwe kama wasomalia kila siku vita,tunashukuru watanzania wanaelewa umuhimu wa aman yetu na hawapo tayari kuiingiza nchi kwenye dimbwi la damu.Tunatamani upinzani ila sio chagadema.

ukiacha tabia za ushabiki na kufuata mkumbo kama watoto wa kondoo, simama kama wewe, ningejua jinsia yako ningekuelewa
 
mkuu kwanini hawachukuliwi hatua kama ni wao wamefanya unyama huo?
 
Hawa jamaa wanaotembezwa na ulemavu wao namna hiyo sijui hata wanajisikiaje mioyoni mwao! Unawezaje kumruhusu mwanasiasa kutumia ulemavu wa kiwango hicho kama mtaji wake kisiasa wakati huo huo ukiwa unaonyeshwa kama picha mbele za watu? Au kwa wenzetu hawa kwao hii ni ajira kwa maana kwamba wanajiingizia kipato kwa kuonyeshwa hadharani namna hiyo?

Mkuu wanalipwa. Take this one; pale maeneo ya mwananyamala kwa mama zakari upande wa kulia kuna mtaa una gereji bubu... Mtaa ule kuna makada-wa CCM ni almost siku ya nne leo wanapita nyumba hadi nyumba kwa malengo yafuatayo: mosi ni kujua wanachama wa ccm ni wangapi na pili wanashawishi kama si mwanachama uchukue kadi ya ccm. Kazi hii hufanywa na mjumbe na kijana toka ofisi za ccm m/nyamala ujiji pale. Wanaongozana na mwanamke ambaye anajitambulisha ni mhanga wa siasa chafu za chadema kwa lile Bomu la Arusha. Hama mkono mmoja na upande wa uso kama ameungua. Yeye hujieleza kwanza na ndipo mjumbe hukuomba ujiunge ccm. Sijui kama ni mkakati wa uchaguzi wa serikali za mtaa au lah! That lady anakunja fedha pale ofisi za ccm ujiji.
 
mkuu kwanini hawachukuliwi hatua kama ni wao wamefanya unyama huo?
Mungu atawapiga kofi na wananchi wanaendelea kuwakataa kwenye sanduku la kura, ona juzi kati apa, 23 kwa 3
 
1622176_673540786041329_124503048_n.jpg
1780655_673540839374657_1516800168_n.jpg
1902026_673540866041321_296530695_n.jpg

Naibu Katibu Mkuu CCM Bara Mh:Mwigulu Nchemba akizungumza na Wananchi wa kata ya Ifakara wakati wa Mkutano wa Kufungua Kampeni uliofanyika Jana Tar.27/02/2014.Hapa akiwa na Wahanga wa siasa chafu zinazodaiwa Kufanywa na Chadema kupitia Vijana wake wa Redbrigade.Mwenye T-shirt ya Njano ni Mzee Alphonce John ambaye alitopolewa Macho kwa dispisi wakati wa Uchaguzi wa Udiwani huko Kahama Mwezi uliopita.

Mwigine mwenye Shati la Kijana ni Kijana Musa Tesha ambaye alimwagiwa Tindikali na Vijana wanaodaiwa Kuwa wa Chadema huko Igunga wakati wa Uchaguzi Mdogo wa Jimbo hilo.Mh:Mwigulu Nchemba jana amesisitiza Wananchi wa Kalenga kuwa makini na siasa Chafu za Chadema zinazofanywa sehemu mbalimbali hasa kwenye nyakati kama hizi za Uchaguzi.Amesisitiza kuwa kwenye Chaguzi zozote Vyama vya siasa vinashindanisha Sera na hoja kuhusu Maendeleo ya Wananchi wa eleo hilo,Mkataba wa CCM na Wananchi ni Maendeleo katika Taifa hili,Umoja na Mshikamano ndio ngao ya MwanaCCM yeyote.

Mwigulu Nchemba amesema dhambi ya Mauaji na Unyama unaoendelea kwenye mikutano ya siasa na maeneo mbalimbali haitamwacha Dr.slaa Salama kutokana na yeye kuwa kiongozi anayebariki Siasa chafu hizo.

Chanzo:Kalenga

KAMA NI KWELI "KWANINI HAJAKAMATWA HUYU DR SLAA MPAKA LEO? AU TUNA DANGANYWA MAANA DR SLAA Hana JESHI LA POLIS, Hana JESHI LA WANANCHI, Hana KITENGO MAALUM CHA UJASUSI". Ila ninachojua POLISI Hutumika na ccm KATIKA MATUKIO YA KUTESA NA KUNYANYASA WATU ndiyo maana wanashindwa kukamata wahalifu ina baki KUDANGANYA WANANCHI KUWA DR SLAA NDIO KAFANYA HAYA. NASEMA KAMA NI KWELI KWANINI ASIKAMATWE AFUNGULIWE MASHITAKA?
 
Hivi huyo Tesha analipwa sh ngapi? mbona anakubali kudhalilishwa hivyo?

siku ubongo wake utakapomaliza likizo ndiyo atajua nani mmbaya wake.
 
Kaka mwigu muogope Mungu kama umeenda Scoan ukatubu.Please acha kumshuhudia jirani yako uwongo(Dr Silaa)wambie wananchi serekali itawafanyia mini wananchi na sio siasa za chuki Mungu hapendi
 
Chadema ni chama cha wanyama na wauaji hakipaswi kuwepo hapa tanzania.
 
1622176_673540786041329_124503048_n.jpg
1780655_673540839374657_1516800168_n.jpg
1902026_673540866041321_296530695_n.jpg

Naibu Katibu Mkuu CCM Bara Mh:Mwigulu Nchemba akizungumza na Wananchi wa kata ya Ifakara wakati wa Mkutano wa Kufungua Kampeni uliofanyika Jana Tar.27/02/2014.Hapa akiwa na Wahanga wa siasa chafu zinazodaiwa Kufanywa na Chadema kupitia Vijana wake wa Redbrigade.Mwenye T-shirt ya Njano ni Mzee Alphonce John ambaye alitopolewa Macho kwa dispisi wakati wa Uchaguzi wa Udiwani huko Kahama Mwezi uliopita.

Mwigine mwenye Shati la Kijana ni Kijana Musa Tesha ambaye alimwagiwa Tindikali na Vijana wanaodaiwa Kuwa wa Chadema huko Igunga wakati wa Uchaguzi Mdogo wa Jimbo hilo.Mh:Mwigulu Nchemba jana amesisitiza Wananchi wa Kalenga kuwa makini na siasa Chafu za Chadema zinazofanywa sehemu mbalimbali hasa kwenye nyakati kama hizi za Uchaguzi.Amesisitiza kuwa kwenye Chaguzi zozote Vyama vya siasa vinashindanisha Sera na hoja kuhusu Maendeleo ya Wananchi wa eleo hilo,Mkataba wa CCM na Wananchi ni Maendeleo katika Taifa hili,Umoja na Mshikamano ndio ngao ya MwanaCCM yeyote.

Mwigulu Nchemba amesema dhambi ya Mauaji na Unyama unaoendelea kwenye mikutano ya siasa na maeneo mbalimbali haitamwacha Dr.slaa Salama kutokana na yeye kuwa kiongozi anayebariki Siasa chafu hizo.

Chanzo:Kalenga

Ha ha ha ha ha CCM walichelewa kuzindua kampeni zao kumbe walikuwa hawajakamilisha maandalizi ya kuwaandaa misukule yao ya kuzunguka nayo kwenye kampeni.Wakawachukue na wale mabinti wa kingereza waliomwagiwa tindikali Zanzibar pamoja na mapadri wote na mashekhe waliomwagiwa tindikali wazunguke nao kwenye kampeni waendelee kusema kuwa walimwagiwa tindikali na CHADEMA.
 
Back
Top Bottom