Mwl. Mwakasege: Nilienda Mbinguni nikaongea na Yesu na Musa


Getee getteee (in kisukuma)
 
Hivi hakuna Shekhe ama hawa wazee wa dahaaaawa walioenda kuongea na Mungu ama mtume.
 

Unaamini watu wanaokutanaga na majini au mizimu?
 
Unaamini watu wanaokutanaga na majini au mizimu?
Kimsingi hakuna platform ya hovyo humu duniani kama JF, ni mtandao ambao umejaa wachawi na mawakala wa shetami na ndio maana kikiandikwa kitu chochote kimuhusucho Mungu, yatatokea mashambulizi na kashfa nzito sana za kila namna ila kwa umri na muda niliomtumikia Mungu nafahamu Mungu anajifunua kwa watu wengi yeyr binafsi na pia kuwafunulia kuhusu mbingu. Binafsi, nashuhudia kumuona mwenye haki Yesu Kristo si chini ya mara 4 toka nikiwa mdogo. Pia nashuhudia, Mungu kunifunulia na kuiona mbingu.

Kuhusumbingu, nakumbuka ilikuwa 2016. Siku hiyo niliamka kama kawaida saa 9 alfajiri na kusali. Ilipofika saa 11:45 nikasema nilale ili nikiamka niende kazini. Nilipolala kama saa 12 alfajiri niksona Malaika ananiambia nimetumwa nikufuate. Akanishika mkono, nikaoba natoka kwenye mwili upande wenye moyo. Nikapita kwenye bati la nyumba bila kizuizi. Safari ya kupanda juu ikaanza kwa speed ya ajabu. Nikaangalia chini na kuona mwili wangu, mke na mtoto wangu wamelala kitandani. Unaona nyumba na miti ya duniani, unaona kadunia kalivyo kadogo then unafika katika nchi ile ambayo "watu" wanaimba na kuabudu na tuliimba "Bwana Mungu nashangaa kabisa"

Sijui nielezeje muonekano wake nchi ile ila ni nzuri na ya meta meta. Hali ya hewa na mazingira ni tofauti na huku duniani. Nchi ile ni kweli na mji ule ni kweli. Jitahidi usikose kuingia mji ule.

Baadaye nikaambiwa turudi na kwa speed ya ajabu, najikuta naingia mwilini mwangu upande wa kushoto kwenye moyo, mwili ukawa kama umepigwa "shot" nikashtuka.
 
Endeleeni kupinga tu Mzee baba anakuja harafu mseme ujio wake ni wakushitukiza😁😁😁😁😁
 

Kama kweli, basi kwisha habari, litakuwa liongo kama Zumaridi tu.
 
Ninamheshimu sana Mlw. Mwakasege kama ni kweli kayasema hayo basi tena amenisikitisha sana kwa kweli..
 
Huwezi kupelekwa mbinguni ukiwa hai bhana!

Hata Yesu Kristo alipokua hai, aliwahi kwenda mlimani kusali na wafuasi kadhaa....ndipo mitume wakatoka mbinguni na kumfuata alipo ....mmoja wa wawafuasi akasema tujenge vibanda vitatu...
Kama wewe mkiristo acha uvuvu soma maandiko utaona watu kibao ambao wameona hayo mambo ya mbinguni wakiwa duniani .Ufunuo 1:10 hauwezi kuona mambo ya mbinguni kama hauko rohoni ,huko hauendi na mwili wako
 
Kwanini chai? Kama unaamini Biblia, Mbona Yesu akiwa katika Mwili alipiga story na Musa na Eliya pale Mlimani huku akina Petro, Yakobo na Yohana wanashuhudia hadi Petro akasema wajenge vibanda vitatu?

Peleka upumbavu wako huko hata Biblia hujui, Kwa hiyo yote aliyofanya Yesu Mwakasege anafanya?
 
Hakuna aliyeonana na Mungu Baba akabaki salama...



Ila Yesu mbona hujifunua kwa watu Sana... Maana hata kwa Saulul alijitokeza wazi wazi...



Wewe kama kiroho upo chini usitegemee Miujiza hii na bado utaona waliomwona yesu wapigaji



kiroho kila jambo linawezekana



akili za kuambiwa changanya na zako... Zumarid anajiita mungu.. Mwakasege anahubiri habari za Mungu huoni hawa ni watu wawili tofauti kiroho
 
Imekaa kama chai lakini nimeipenda story yako 🤣
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…