Mwl Mwakasege: Niliwahi kutoka nje ya mwili wangu nikaenda Mbinguni na kukutana na Nabii mkubwa, nikamtambua

Mwl Mwakasege: Niliwahi kutoka nje ya mwili wangu nikaenda Mbinguni na kukutana na Nabii mkubwa, nikamtambua

Yesu anakuaje MUNGU sasa?? Hapa ndo wakristo mnaniacha hoi
 
Heri wewe mwenye kuandika haya hakika unyakuo ni wakati wowote endelea kuwa safi maana kufumba na kufumbua unyakuo utatokea na watakaobaki duniani ile miaka 7 ya dhiki kuu itaanza rasmi na wapo watakaokuwa wanarudia kusoma tunayonadika hapa mara kwa mara na wataanza kuuliza Rabbon upo wapi, Salari upo wapi na wengine wengi watatajwa lakini watashangaa mbona IDs hizi zimekuwa kimya ndipo watakumbuka tuliyokuwa tunaandika mara kwa mara kilio na kusaga meno kutakuwa kwingi sana.

Ana heri yeye amuaminiye bwana Yesu sasa na kuishi maisha matakatifu kujianda na unyakuo.
Unyakuo hautakuwa kwa njia ya uficho
 
Yesu anakuaje MUNGU sasa?? Hapa ndo wakristo mnaniacha hoi
Nafsi ya yesu ndiyo mungu ...miili siyo uzima uzima ni nafsi ....kituko ni Muhammad...waislamu wanakuambia Muhammad nafsi yake ilitakasika toka ajafika duniani.. tena wanakuambia kafiri ndiyo anatakiwa kusilimu ...tena wanakuambia mtoto uzaliwa akiwa ni muislamu ...tena wanakuambia mitume wote wa kweli kina musa, issa, nk walikuwa waislamu ...sasa swali je Muhammad alikuwa kafiri maana ana ambiwa na malaika awe wa kwanza kusilimu na mnasema kafiri ndiyo anatakiwa kusilimu ...je Muhammad alikuwa mcha mungu toka udogo wake ? ..kama ndiyo vipi asilimu tena ...kama ndiyo vipi alichanganyikiwa kutokewa na malaika ikiwa alikuwa ni mchamungu tena mkubwa kuliko wachamungu wote ...je muislamu usilimu kuwa muislamu ? Je washia wanaweza kusilimu kuwa wasunni ?
Kama matiki na fafanuzi ya uislamu wenyewe unadhibitisha kuwa Muhammad alikuwa kafiri ndiyo maana alitakiwa kusilimu mapangoni ....pia inathibitisha uislamu ni dini mpya.. FaizaFoxy BWANA UTAMU unisahidie nisipotee kwa kutokuelewa haya....bila ya kumsahau shekh mandazi adriz ... Malaria 2 MduduAli
 
Unyakuo hautakuwa kwa njia ya uficho
Na si wote wataona watu wakinyakuliwa kwa mfano watu wapo wanafanya dhambi kwa mfano ni ndani ya night club chances ni kubwa hapo hata mtu mmoja asinyakuliwe so hawa hawataona hata 1 akinyakuliwa watasikia tu kuwa umetokea.
Au kwa mfano watu wapo kwenye matemple yao let say buddha, na mengine hawa hawataona hata mtu 1 akinyakuliwa.
Au watu wapo kwenye vikao vyao vya kichawi it is obvious hawa hawataona hata mtu mmoja akinyakuliwa kati yao watasikia tu baadae kuwa kuna watu wamenyakuliwa.
 
Swali no 2.

Zamani kabla ya kufufuka Kwa Yesu, WATAKATIFU walikuwa wakifa wanasubiri Mahali paliitwa Paradiso, Mahali pema peponi,

Baada ya Yesu kufufuka, WATAKATIFU huenda mbingu ya kwanza live, na hawahukumiwi tena, maana hayupo wa kuwahukumu.
Wewe hiyo injili yako umeokota wapi 😁😁😁 watakatifu wanahukumiwa pia kwa sababu kuna hukumu 3 ambazo Mungu atawahukumu viumbe wake hukumu ya kwanza ni kuwa tenga watakatifu na wasio watakatifu (wenye dhambi )...hukumu ya pili ni kuwa hukumu watakatifu sawa sawa na thawabu zao yani kuwalipa sawa sawa na uchamungu wao ..mtakatifu wa daraja ya chini hadi wa daraja ya juu ...hukumu ya tatu ni kwa wenye dhambi nao watahukumiwa adhabu kutokana na daraja ya dhambi zao ...hizi ndizo hukumu 3 za siku ya mwisho ....hii ni injili ya kweli siyo hayo matonyaronya ya injili zenu potovu ...HAKI YOYOTE DUNIANI HADI MBINGUNI INA HUKUMU 3 ...Nilazima hukumu 3 Zifuatwe hili hukumu yoyote KUITWA YA HAKI ....Mfano mwizi wa pipi ya sh 200 ukimuhukumu kunyogwa na jambazi sugu ukalihukumu kifungo cha siku 10 je haki imetemdeka hapo ...
KIDUNIA HAKI INATHIBITI KWA HUKUMU 3 NA KIMBINGU NI HIVYO HIVYO HUKUMU 3 ZA MUNGU

kisa cha barnaba kuachiwa na yesu kusulibiwa ni kutokufanyika hukumu ya haki katika hukumu ya kwanza ya kutenga haki na ubatili kiusahihi ...muovu ana achiwa mwema ana tiwa hatiani
 
Nafsi ya yesu ndiyo mungu ...miili siyo uzima uzima ni nafsi ....kituko ni Muhammad...waislamu wanakuambia Muhammad nafsi yake ilitakasika toka ajafika duniani.. tena wanakuambia kafiri ndiyo anatakiwa kusilimu ...tena wanakuambia mtoto uzaliwa akiwa ni muislamu ...tena wanakuambiq mitume wote wa kweli kina musa, issa, nk walikuwa waislamu ...sasa swali je Muhammad alikuwa kafiri maana ana ambiwa na malaika awe wa kwanza kusilimu na mnasema kafiri ndiyo anatakiwa kusilimu ...je Muhammad alikuwa mcha mungu toka udogo wake ? ..kama ndiyo vipi asilimu tena ...kama ndiyo vipi alichanganyikiwa kutokewa na malaika ikiwa alikuwa ni mchamungu tena mkubwa kuliko wachamungu wote ...je muislamu usilimu kuwa muislamu ? Je washia anaweza kusilimu kuwa wasunni ?
Kama matiki na fafanuzi ya uislamu wenyewe unadhibitisha kuwa Muhammad alikuwa kafiri ndiyo maana alitakiwa kusilimu mapangoni ....pia inathibitisha uislamu ni dini mpya.. FaizaFoxy BWANA UTAMU unisahidie nisipotee kwa kutokuelewa hab
"kituko ni muhammad"??? respect,respect,respect???
 
mimi simo huko boss, nlitaka 2 nikukumbushe utu kiongozi... ngoja waislamu waje kujibu hilo swali lako, mm ntakuwa pembeni najiuliza kwanini yesu alibatizwa
Mbona swali la kijinga lq ubatizo ...yesu alibatizwa na sababu zimewekwa hapo hapo kwenye tukio la ubatizo kasome vizuri...kumbuka yesu alisema nini kuhusu aliye mkubwa mbinguni ni nani ...ni yeye aliye mdogo kuliko wote na mtumishi chini ya wote yaani kujishusha ...ukisoma utaona yesu alikataliwa kubatizwa na yohana na hoja ya yohana ipo wazi kuwa ni kuwa Yesu ni mkuu kuliko yeye ...hivyo yesu alionyesha na kufundisha kujishusha ...kama alivyo sema 👉kila ajikwezaye atashushwa bali ajishushaye atakwezwa ....kasome pia ...ukialikwa kwenye sherehe keti kiti cha nyuma nk pia ubatizo maana yake ni ujio wa INJILI NA KUITAMBUA KUWA NI KWELI NI KAMA WAISLAMU WANAVYO TAMKA SHAHADA ....kwa waislamu ni SHAHADA kwa wakristo ni UBATIZO
 
Haya tuelezee wewe yesu ni nani na roho mtakatifu ni nini alafu nikuulize maswali unijibu
Kwa hiyo hata pale jangwani "Yesu alipopandishwa na roho nyikani ili ajaribiwe na ibilisi na akafunga siku 40 mchana na usiku" kwa hiyo hapo Ibilisi alikuwa ni sawa na anamjaribu Mungu.

Yaani ibilisi alikuwa anamjaribu Mungu wake aliyemuumba, hivi inawezekana hii kwa akili ya kawaida.

Shetani kuna kauli aliongea pale kuwa "ikiwa wewe ni mwana wa Mungu jitupe chini, maana imeandikwa atakuagizia malaika watakuja kukutumikia usije ukajikwaa kwenye jiwe"

Huyo ambaye shetani anamaanisha "atakuagizia malaika" ni nani ikiwa huyo Yesu alikuwa ndiyo Mungu mwenyewe.

Kwa hiyo shetani anaweza kumpa Mungu amri ambaye ndiye muumbaji wake kwamba "Haya yote (fahari ya ulimwengu) nitakupa ukianguka kunisujuidia"

Yaani Mungu akubali kujaribiwa na shetani mpaka afikie hatua ya kumwambia anguka chini unisujudie, hivi una akili zako zinafikiria timamu wewe jamaaa ?
 
Salaam, Shalom!!

Akifundisha katika semina jijini Mbeya Jana tarehe 26 January,Mwalimu Christopher Mwakasege amerudia kauli aliyowahi kuitoa kabla.

Amesema, asubuhi, walipokuwa katika bible study ya familia asubuhi ya jumapili hiyo, Mkewe alimuuliza swali kuwa ikitokea ametokewa na YESU atamtambuaje?

Mwalimu Christopher Mwakasege akamjibu Kwa kumkumbusha juu ya siku aliyotoka ndani ya MWILI wake na kwenda Mbinguni, alipofika Mbinguni, alikutana na Nabii Musa yule Nabii wa kale, na alimtambua, akaongeza kusema, Ukiwa katika mwili wa kiroho, huhitaji kutambulishwa sababu Roho inajua yote na kutambua yote yajayo na yaliyokwisha pita.

..... Mwisho wa kunukuu....

Naungana na Mwalimu Christopher Mwakasege juu ya UKWELI wa jambo hili, mbingu IPO na ni halisi, Mimi pia nimewahi kwenda Nchi nzuri sana, mfano wa uzuri wa Nchi Ile hauelezeki, mji huo hakuna jua Wala mwezi, IPO Nuru nzuri sana ambayo macho hayachoki kuitazama,

Nimewahi kuandika pia juu kupewa taarifa juu ya ujio wa Yesu kulinyakua Kanisa Kwa kumwona Yesu akiwa na jeshi la Malaika, amepanda farasi mweupe wakienda Kwa Kasi mawinguni.

Ndipo tujue yafuatayo.

1. Mbingu ni halisi Si hadithi.

2. WATAKATIFU wote wapo Mbinguni, wakifa hawakai kaburini.

3. Mungu yupo na ni MMOJA, na Jina la Mungu huyo mmoja tulilopewa WANADAMU liwezalo kuokoa ni Yesu Kristo/YESHUA HAMASHIACH.

Wasio amini wasubiri sikuitapofika ambayo kutakuwako na kusaga meno na kila aina ya vilio ndipo watataka kutubu na kuamini ila watakuwa wamechelewa sana
 
Kwa hiyo hata pale jangwani "Yesu alipopandishwa na roho nyikani ili ajaribiwe na ibilisi na akafunga siku 40 mchana na usiku" kwa hiyo hapo Ibilisi alikuwa ni sawa na anamjaribu Mungu.

Yaani ibilisi alikuwa anamjaribu Mungu wake aliyemuumba, hivi inawezekana hii kwa akili ya kawaida.

Shetani kuna kauli aliongea pale kuwa "ikiwa wewe ni mwana wa Mungu jitupe chini, maana imeandikwa atakuagizia malaika watakuja kukutumikia usije ukajikwaa kwenye jiwe"

Huyo ambaye shetani anamaanisha "atakuagizia malaika" ni nani ikiwa huyo Yesu alikuwa ndiyo Mungu mwenyewe.

Kwa hiyo shetani anaweza kumpa Mungu amri ambaye ndiye muumbaji wake kwamba "Haya yote (fahari ya ulimwengu) nitakupa ukianguka kunisujuidia"

Yaani Mungu akubali kujaribiwa na shetani mpaka afikie hatua ya kumwambia anguka chini unisujudie, hivi una akili zako zinafikiria timamu wewe jamaaa ?
Nilitaka kukuambia hiyo point ya siku 40 ...tena ni point kubwa sana
 
Salaam, Shalom!!

Akifundisha katika semina jijini Mbeya Jana tarehe 26 January,Mwalimu Christopher Mwakasege amerudia kauli aliyowahi kuitoa kabla.

Amesema, asubuhi, walipokuwa katika bible study ya familia asubuhi ya jumapili hiyo, Mkewe alimuuliza swali kuwa ikitokea ametokewa na YESU atamtambuaje?

Mwalimu Christopher Mwakasege akamjibu Kwa kumkumbusha juu ya siku aliyotoka ndani ya MWILI wake na kwenda Mbinguni, alipofika Mbinguni, alikutana na Nabii Musa yule Nabii wa kale, na alimtambua, akaongeza kusema, Ukiwa katika mwili wa kiroho, huhitaji kutambulishwa sababu Roho inajua yote na kutambua yote yajayo na yaliyokwisha pita.

..... Mwisho wa kunukuu....

Naungana na Mwalimu Christopher Mwakasege juu ya UKWELI wa jambo hili, mbingu IPO na ni halisi, Mimi pia nimewahi kwenda Nchi nzuri sana, mfano wa uzuri wa Nchi Ile hauelezeki, mji huo hakuna jua Wala mwezi, IPO Nuru nzuri sana ambayo macho hayachoki kuitazama,

Nimewahi kuandika pia juu kupewa taarifa juu ya ujio wa Yesu kulinyakua Kanisa Kwa kumwona Yesu akiwa na jeshi la Malaika, amepanda farasi mweupe wakienda Kwa Kasi mawinguni.

Ndipo tujue yafuatayo.

1. Mbingu ni halisi Si hadithi.

2. WATAKATIFU wote wapo Mbinguni, wakifa hawakai kaburini.

3. Mungu yupo na ni MMOJA, na Jina la Mungu huyo mmoja tulilopewa WANADAMU liwezalo kuokoa ni Yesu Kristo/YESHUA HAMASHIACH.

Mungu awabariki.
Namba 2 NI UONGO.
MENGINE NAWEZA KUMUELEWA.
NGOJA NIKUPE MFANO,ELISHA NABII ALIKUWA MTAKATIFU,ILA MIFUPA YAKE ILIKUWA KABURINI NA HADI LEO YUPO ARDHINI AKISUBIRI UFUFUO.
 
Huyu mzee huwa naumuelewa sana mafundishobyake lakini akishaanza hayo mambo ya kufanya conversations na Mungu huwa napoteana ...sjui ni mm pekee huwa naimani haba kwamba huyu Mungu tunaemuomba huwa anawatokea wengine na wanaganya mahojiano wanaulizana maswali na kujibiwa papo hapo.
 
Nilitaka kukuambia hiyo point ya siku 40 ...tena ni point kubwa sana
Majibu yako ni "nilitaka kukwambia" haya bwana mwanatheolojia na huyo Mungu wako ambae anaweza kujaribiwa na kiumbe ambacho amekiumbe mwenyewe alafu eti kimwambie "Mali zote za ulimwengu nitakupa ukiinamana kunisujudu" ni aina flanu mtazamo wa kiazimu hivi.

But to me, God is a living entity greater than Jesus.

And the idea that "GOD BECAME A MAN IN JESU" is a very late idea.

Mungu ni Mungu na wala hajawahi kugeuka kuwa Yesu.

Kitu pekee kipya ambacho nimekuja kukigundua hivi karibuni kutokana na kusoma biblia ni kwamba, Yesu ni kana kwamba maisha yake hayakuanzia duniani.

Ni kiumbe ambacho kilishakuwepo mbinguni mda tu na kilikuwa kikiishi huko kabla kuja duniani kuzaliwa na kuishi kama mtu.

Hii haina maana kuwa kuwa kuishi kwake mbinguni ndiyo alikuwa Mungu, hapana

Bali alikuwa tu na uhusiano wa karibu na Mungu kuliko hata malaika.

Ndiyo maana baadhi ya wanatheolojia wameenda mbali zaidi na kusema kuwa, Mungu kabla kuumba kitu chochote kile, alimuumba mwanae wa pekee Yesu kristo kwanza kabla ya kuumba chochote kile.

Then baada ya hapo ndipo akawaumba malaika na vitu vingine vilivyofata.

Ngoja tu niishie kwanza hapa, kwa sababu at the end of the day siku ya kiama tutahukumiwa kwa DHAMBI na wala si kwa sababu uliamini Yesu ni Mungu au Siyo Mungu, wala si kwa sababu uliamini ukristo au uislam.

Tutaenda kuhukumiwa kwa dhambi zetu wala si kwa dini zetu.

Na Uzuri dini zote tatu za Ibrahim (Ukristo,uislamu na uyahudi/Judaism) zinakataza maovu ambayo kwa kiasi yanafanana kwa imani zote tatu.

Ndiyo maana mimi naonaga anae ona ukristo ni dini isiyo ya haki au Islam ni dini isiyo ya haki ni anajihemkisha kidini tu.

Ila Mungu hajawahi kuwa fala kama sisi wanadamu, anajua vizuri tu mgawanyiko wa hizi dini hadi na madhehebu yake, na huenda ni mango wake wa maksudi kabisa ili tu muitafte kweli vizuri, tofauti na mngekuwa dini moja tu dunia nzima huenda mngekuwa mafala zaidi.

Ni kama tu mnara wa babeli Mungu alipo uangusha alafu kesho yake kila mtu akaamka anaongea lugha yake,hakuna anamwelewa mwenzie na umoja wao ukaishia hapo.

Probably hata huku kwenye mgawanyo wa dini na madhehebu huenda ni strategy ya Mungu kukufanya wewe ujaribu kumtafta kwa biidi zaidi na kueneza habari zake.

Angalia wale wanafunzi 12 wa Yesu walivyo tawanyika baada ya Yesu kupaa.

Wengine wakaenda ulaya huko kama kina petro na Paulo sijui, wengine wakaja Africa (Ethiopia) lengo kueneza habari za Mungu.

Unadhani wangebaki pale pale middle Eastern countries huko kwingine duniani watu wangemjuaje Mungu.
 
Back
Top Bottom