Mzazi mwenzangu hataki mtoto apate Elimu nzuri, nadhani hajui elimu ni kwa faida ya mtoto sio mimi wala yeye

Mzazi mwenzangu hataki mtoto apate Elimu nzuri, nadhani hajui elimu ni kwa faida ya mtoto sio mimi wala yeye

Habarini ndugu

Mimi na mzazi mwenzangu bado hatuna ndoa, ila tumebahatika kupata mtoto mmoja, kwa sasa wamerudi mkoani baada ya kuja na kukaa nyumbani kwetu kwa lengo la kumleta mtoto familia yangu imtambue.

Baada ya mtoto kufikisha miaka mitatu na nusu, nikamwambia mama yake itabidi mtoto aanze shule, na natamani mwanangu arudi Dar asome shule nzuri na ya kisasa.

Mzazi mwenzangu anadai hawezi kuruhusu hilo, ni afadhali mtoto abaki kijijini asome shule za kawaida (serikali). Nikamwambia utamsomesha wewe huko, mimi nilitaka aje Dar asome shule nzuri na tofauti na hapo sitahusika na maswala ya shule endapo atasoma tofauti na nilivyotaka.

Nadhani labda bado anachuki au kinyongo dhidi ya familia yangu, lakini hajui Elimu bora ina faida kwa mtoto na maisha yake ya baadaye, sio mimi wala yeye.

Je ni sahihi nikikataa kutoa huduma za shule endapo atasoma kijijini? Kwani lengo langu lilikuwa aje asome Dar, akae na Bibi yake (Mama yangu) na yupo tayari kwa hilo.
Iyo code mbona rahisi labda tu unajizima Data...Mama mtoto anataka kama ni mtoto kuja Dar aje na yeye mkae wote.
 
Wanawake wengi wanawatumia watoto kama kitega uchumi hivyo ukimchukua atazikosa hata hizo hela ndogo ndogo na hicho ndio kitu wanawake wengi wanawaza.
 
Wanawake wengi wanawatumia watoto kama kitega uchumi hivyo ukimchukua atazikosa hata hizo hela ndogo ndogo na hicho ndio kitu wanawake wengi wanawaza.
Kama ni hivyo basi anajali maslahi yake na si mtoto, ndyomaana hajali kuhusu umuhimu wa Elimu nzuri kwa mtoto
 
Habarini ndugu

Mimi na mzazi mwenzangu bado hatuna ndoa, ila tumebahatika kupata mtoto mmoja, kwa sasa wamerudi mkoani baada ya kuja na kukaa nyumbani kwetu kwa lengo la kumleta mtoto familia yangu imtambue.

Baada ya mtoto kufikisha miaka mitatu na nusu, nikamwambia mama yake itabidi mtoto aanze shule, na natamani mwanangu arudi Dar asome shule nzuri na ya kisasa.

Mzazi mwenzangu anadai hawezi kuruhusu hilo, ni afadhali mtoto abaki kijijini asome shule za kawaida (serikali). Nikamwambia utamsomesha wewe huko, mimi nilitaka aje Dar asome shule nzuri na tofauti na hapo sitahusika na maswala ya shule endapo atasoma tofauti na nilivyotaka.

Nadhani labda bado anachuki au kinyongo dhidi ya familia yangu, lakini hajui Elimu bora ina faida kwa mtoto na maisha yake ya baadaye, sio mimi wala yeye.

Je ni sahihi nikikataa kutoa huduma za shule endapo atasoma kijijini? Kwani lengo langu lilikuwa aje asome Dar, akae na Bibi yake (Mama yangu) na yupo tayari kwa hilo.
Kwani huko mkoani hakuna shule nzuri ya private mtafutie hiyo hiyo kwa sasa huku ukiwaza baadae


Maana hata mikoani zipo shule nzuri tu na zitamjenga, mabishano ya sasa hayatamsaidia

Ila baadae sasa ndio unaweza kumhamishia kwingine
 
Habarini ndugu

Mimi na mzazi mwenzangu bado hatuna ndoa, ila tumebahatika kupata mtoto mmoja, kwa sasa wamerudi mkoani baada ya kuja na kukaa nyumbani kwetu kwa lengo la kumleta mtoto familia yangu imtambue.

Baada ya mtoto kufikisha miaka mitatu na nusu, nikamwambia mama yake itabidi mtoto aanze shule, na natamani mwanangu arudi Dar asome shule nzuri na ya kisasa.

Mzazi mwenzangu anadai hawezi kuruhusu hilo, ni afadhali mtoto abaki kijijini asome shule za kawaida (serikali). Nikamwambia utamsomesha wewe huko, mimi nilitaka aje Dar asome shule nzuri na tofauti na hapo sitahusika na maswala ya shule endapo atasoma tofauti na nilivyotaka.

Nadhani labda bado anachuki au kinyongo dhidi ya familia yangu, lakini hajui Elimu bora ina faida kwa mtoto na maisha yake ya baadaye, sio mimi wala yeye.

Je ni sahihi nikikataa kutoa huduma za shule endapo atasoma kijijini? Kwani lengo langu lilikuwa aje asome Dar, akae na Bibi yake (Mama yangu) na yupo tayari kwa hilo.
Umemzalisha mtoto wa watu then unategemea mama yako ndiyo akulelee huyo mtoto?
Nawe bado ni mtoto acha mama yake aendelee kumlea na kumsomesha huko kijijini.
 
Kuna baadhi ya wanawake ni kama wana LAANA wao wanahisi wanakomoa, lakini kiuhalisia hawamkomoi yeyote.

Mie mzazi mwenzangu alikuja kumchukua mtoto mikononi mwangu akiwa anamalizia darasa la 3, mie mtoto nilianza kukaa nae akiwa na miaka mi4 hivi, nimeishi nae, akaanza la kwanza, la pili, la 3, anaingia la 4 akaja kuleta utata sijui namhitaji mtoto kimeenda kimerudi,sikuona haja ya kumgombea mtoto ukizingatia kisheria mtoto bado ana umri wa kuishi na mama yake, wakati yupo kwangu likizo zoote mwezi wa 6 na wa 12 mtoto alikuwa nampeleka upande wa mama yake kusalimia.
Yeye toka amemchukua mtoto hataki kabisa kunipa mtoto kwenye likizo yoyote, mwaka wa pili huu na mwakani ni wa 3, hakuna likizo kanipa mtoto kila likizo ni visingizio.
Yaani namuona ni kama SHETANI vile, sasa sijui ndio ananikomoa kisa sikumuoa yeyr ama shida nini.. Nahisi kabisa anafanya haya kwa makusudi, na kuna sumu anamjaza mtoto, last time nilifunga safari toka dar mpaka shinyanga kumuona tu mtoto, lakini ule upokeaji, lile vibe la huyu ni baba mwaka wa pili huu sijamuona, halikuwepo, yaani ilikuwa kawaida mnoo, utafikiri tunaishi pamoja na tumetoka kuonana mchana wake

Ila kuna baadhi ya viumbe ni MASHETANI kabisa.
 
Back
Top Bottom