Mzazi wangu hajaridhika na mchumba wangu, hajasema lakini nimeona ishara

Mzazi wangu hajaridhika na mchumba wangu, hajasema lakini nimeona ishara

Yani wewe ni tatizo kubwa wewe huwezi kujenga mji wako kamwe na hakuna mwanamke wa kuvumilia ujinga wako uo inaonekana kila jambo lako lazima lipitishwe na Mama yako nakupa pole sana
Mama yangu ni Nguzo yangu, Angekuweopo baba huenda ningekuwa na mshauri mzuri zaidi lakini nimebaki na Mama na siwezi kumpinga
 
Madhara gani? Mimi nafurahi kuwa na mtoto na sioni kama napaswa kujuta au kulaumu, hakuna kitu mtoto amekosa, kama ni malezi yapo tena mazuri tu
Mtoto amepata baba mjinga asiyejielewa, laiti huyo mtoto angefahamu kuwa Una mpango wa kumtelekeza mama yake
 
Habarini ndugu

Baada ya kupata mtoto, ilibidi mzazi mwenzangu aje nyumbani kwetu kumleta mtoto Bibi yake amuone kwani alikuwa na shauku ya kumuona mjukuu wake.

Walikaa kwa kipindi cha miezi kadhaa, na walikaa kwa furaha na amani. Mama yangu alifurahi kwani mwanzo aliona na kusifia tabia nzuri na kujituma kwa binti yule.

Kadri siku zilivyokuwa zinasonga, nikahisi kuna jambo halipo sawa, kila nikiongea na Mama kuhusu mipango ya baadae alikuwa haonyeshi dalili za kubashiri ndoa yangu na binti yule. Nikajua tu hajaridhika nae.

Lakini naamini Mzazi wangu ananijua vizuri na anajua ni kipi kitanifaa na kuendana na mimi, nahisi kuna vitu amegundua kwa binti yule kwa muda aliokaa nae.

Mimi sina tatizo na mawazo na ushauri wa Mzazi wangu, lakini najiuliza je ni sahihi kuendelea kumuaminisha binti huyu kwamba nitamuoa ilihali najua Mzazi wangu hajaridhika nae?

Najiuliza nimwambie mapema kwamba haitowezekana kufunga ndoa hapo badae? Naogopa kumpa maumivu na kumfanya akose amani.......

Ni uamuzi gani wa busara napaswa kufanya wadau? Naombeni ushauri wenu bila kebehi na masihara..

Asanteni.....
1.Mzazi wako ni mama tu?
2.baba yako anasemaje?
3.Viashiria vipi umeviona?
4.kwa nini umezaa ndio unataka uoe?
5.kwa hio,huyo atayaridhika naye mama yako naye utazaa naye kisha ndio utamuoa?
Ukiweza kujibu hayo maswali kutoka moyoni,una 97% za kutatua kinachokusumbua
 
Unahitaji msaada wa kisaikolojia tunza comment yangu ipo siku utajutia kwa kuharibu familia yako ili kufurahisha familia ya Mama yako
Kuharibu familia yangu kivipi? Hata mama yangu ni familia yangu
 
Mama yangu ni Nguzo yangu, Angekuweopo baba huenda ningekuwa na mshauri mzuri zaidi lakini nimebaki na Mama na siwezi kumpinga
Ndio shida ya kulelewa na Single Mother yani ni kama umeharibika kisaikolojia nakuonea huruma sana upo controlled na Mama yako ukihitaji msaada wa kujitambua utasema nikusaidie maana akili zako zimeshikwa na Mama yako
 
Kuharibu familia yangu kivipi? Hata mama yangu ni familia yangu
Mama yako ni mzazi wako na ana familia yake lakini uyo binti ulie zaa nae uyo na mtoto ao ndio familia yako kwasasa inatakiwa uijenge vizuri na kama unataka kuendelea kua familia ya mama yako basi usinge mpa mimba uyo binti ungekaa kwenu na Mama yako mfurahie maisha yenu
 
1.Mzazi wako ni mama tu?
2.baba yako anasemaje?
3.Viashiria vipi umeviona?
4.kwa nini umezaa ndio unataka uoe?
5.kwa hio,huyo atayaridhika naye mama yako naye utazaa naye kisha ndio utamuoa?
Ukiweza kujibu hayo maswali kutoka moyoni,una 97% za kutatua kinachokusumbua
1. Mzazi ni mama tu
2. Baba hayupo
3. Bado hajanipa viashiria na nitamuuliza aniambie
4. Tayari nimezaa na siku hazirudi nyuma
5.sina mpango wa kuoa kwa sasa mpaka nimalize masomo
 
Ndio shida ya kulelewa na Single Mother yani ni kama umeharibika kisaikolojia nakuonea huruma sana upo controlled na Mama yako ukihitaji msaada wa kujitambua utasema nikusaidie maana akili zako zimeshikwa na Mama yako
Mama yangu ni nguzo yangu
 
Mama akiniambia sababu na mimi nitazichunguza, nikiona ni sahihi nitafanya maamuzi
🤣🤣🤣🤣 Nishaona tuna hangaika kushauri mbuzi kuacha kula manyasi aya kila la kheri kwenye maisha yako ya hovyo ayo
 
Sasa kiherehere gani kilikupeleka kuharibu maisha ya uyo binti si ungekaa na uyo nguzo yako kivyenu yani wewe akili huna kabisa
Nimeharibu maisha yake kivipi? Mbona bado anaishi vizuri tu na hana tatizo
 
Kwanza hujaeleza baba yako yupo wapi, kama amekufa baba mdogo/mkubwa wanasemaje? Baraka hazitoki kwa mzazi mmoja tu wa kike peke yake. Baraka ni pande 2 na za baba ni final n conclusive.
 
Back
Top Bottom