Mzee atoa machozi baada ya kumuona Lissu aliyepigwa risasi 16 akiwa hai

Mzee atoa machozi baada ya kumuona Lissu aliyepigwa risasi 16 akiwa hai

Mimi ile September 7, 2017 niliona hapa JF kwanza kwamba Lissu kapigwa risasi na hali yake ni mbaya sana. Nilijua ni uongo wa buku 7 hivyo sikuamini ila nikawa busy kwenye simu kutafuta ukweli. Nilipofahamu kama ni kweli nililia kama mtoto hata sijui machozi yalitokea wapi. Mwenyezi Mungu ni mkubwa.
Wa aina yako tuko wengi, ni mtu pekee aliye hai niliyewahi kumlilia
 
Mke wangu kila siku akimwangalia Lissu katika picha huwa analia. Nimejaribu kumpa counselling ila ni ngumu kwake. Anasema kwa kuwa ana watoto wa kiume na wa kike walitoka kwenye kitovu chake na anajua uchungu wa labour basi ni lazima alie. Akifika hapo huwa nakaa kimya.

Kupona kwa Lissu ni Muujiza wa Mungu. Ujasiri wake hata baada ya jaribio kubwa la kumuua kufeli na kumuacha na Kilema basi huyu ni Simba. Hata kama si Rais 2020 lakini watanzania wafikiri sana heshima ya huyu kijana.

Kwanza ni mwadilifu mno hana skendo yoyote Ile. Hakika ingekuwepo skendo ungekuta zimeshawekwa hadharani. Ni pure heart person. Pamoja na kuumizwa kule na kumbadilishia mfano wa maisha kuwa mkimbizi wa huduma za afya lakini bado anacheka na kufurahi na wala haonyeshi kinyongo akiongea. Ni wachache mno wanaweza hii na aliweza Marehemu Nelson Mandela tu.

Mimi kama Mtanzania niliyezaliwa na kukua kipindi cha hayati baba wa Taiifa hili nimesema kuwa malezi yale yalinifanya niwe mtu wa tofauti sana ninayejali utu kuliko siasa za chuki na kubwa watu kwa ukabila na ukanda wao. Tunasherehekea miaka 21 ya kufa kwako nikiwa na kidonda moyoni kwangu.

Basi tukiwa wakweli hivi tunaambiwa eti tunakisaliti chama na ni wapinzani. Sijawahi kuwa chama chochote cha upinzani nchini na sitegemei kuwepo huko bali nitakuwa mkweli mwenye utu na sitabadilika.
 
Back
Top Bottom