Mzee atoa machozi kisa mke wake. Watoto acheni ubaguzi badilikeni.

Mzee atoa machozi kisa mke wake. Watoto acheni ubaguzi badilikeni.

Omukisa

JF-Expert Member
Joined
Sep 10, 2024
Posts
642
Reaction score
1,305
Kuna siku nilikuwa nipo sehemu. Watu wakawa wanapiga stori kuhusu wamama kuwafungia vioo waume zao kwa watoto wao ili wasipate msaada. Yaani mama anawaambia watoto wake kuwa baba yenu mkimtumia hela anaimalizia kwa wanawake, pombe etc. ili mradi tu mme wake hasitumiwe hela. Muda mwingine maneno anayosema kwa watoto si ya kweli bali yakutunga au anatia chumvi.

Baada ya hayo maongezi kuna Mzee mmoja alianza kulia maana alikuwa anapitia hiyo hali. Akasema ana maumivu moyoni kwani aliipambania sana familia yake. Watoto wake wamefika hapo walipo kwa nguvu zake hadi wakawa na maisha yao ila inamuumiza kwa kumbagua katika uzee wake. Mke wake kawatia sumu watoto, na watoto wameingia kwenye mfumo. Hela wanamtumia mama yao kwahiyo Mzee akitaka hela inabidi amwombe mke wake. Anaipata kwa masimango.

Ushauri
  • Watoto badilikeni acha kusikiliza maneno ya mama zenu. Baba zenu katika uzee wao wana mahitaji yao binafsi. Kama unatuma tuma kwa wote bila ubaguzi.
  • Waazee watarajiwa weka vitega-uchumi vyako ili husiwe tegemezi kwa watoto. Hii itakusaidia kufurahia uzee wako.
 
Sisi wanaume Kuna mda pia tunazingua, Ukiwa na pesa unatumbua na wanawake na kumuona uliyemuoa sio hadhi Yako na watoto unatelekeza.

Uzeeni ukiishiwa unaanza kulalamika baada ya kuchunwa sana, Sasa umeona watoto wamefanikiwa tena yawezekana bila msaada wako unaanza kulalama
 
Sisi wanaume Kuna mda pia tunazingua, Ukiwa na pesa unatumbua na wanawake na kumuona uliyemuoa sio hadhi Yako na watoto unatelekeza.

Uzeeni ukiishiwa unaanza kulalamika baada ya kuchunwa sana, Sasa umeona watoto wamefanikiwa tena yawezekana bila msaada wako unaanza kulalama
Kuna waliojitoa sana kwa famliia ila uzeeni wakaonekana hawana maana,dawa ni kuwa na wake wengi
 
Hao wakina mama wana nguvu gani hiyo yakuweza kuwafanya watoto wawe wanafuata maelekezo yao tu? Huo mzee kuna mahali alikosea tu hivyo anavuna mavuno yake, yapaswa afurahie mavuno yake sio kulalama tu
 
Hao wakina mama wana nguvu gani hiyo yakuweza kuwafanya watoto wawe wanafuata maelekezo yao tu? Huo mzee kuna mahali alikosea tu hivyo anavuna mavuno yake, yapaswa afurahie mavuno yake sio kulalama tu
Inawezekana alikosea au wenda pia hajakosea kajikuta kwenye hiyo hali.
 
Kikawaida Mtu huvuna anachopanda.

Mama Hana Ñguvu Kwa Mtoto kama hakumlea na kumuonyeshea upendo halikadhalika na Baba.

Hiyo kusema Wanawake wanawapa Sumu Watoto ni uongo. Mtoto hachukui maneno isipokuwa huchukua Kile anachokiona
 
Sisi wanaume Kuna mda pia tunazingua, Ukiwa na pesa unatumbua na wanawake na kumuona uliyemuoa sio hadhi Yako na watoto unatelekeza.

Uzeeni ukiishiwa unaanza kulalamika baada ya kuchunwa sana, Sasa umeona watoto wamefanikiwa tena yawezekana bila msaada wako unaanza kulalama
Mambo yao waachie wenyewe. hela wape kila mmoja kibunda chake.
Apambane na matumizi yake.
 
Back
Top Bottom