Mzee Bulembo acha kudhalilisha watu kwa kuharibu diplomasia wakati wewe ndio muharibu

Mzee Bulembo acha kudhalilisha watu kwa kuharibu diplomasia wakati wewe ndio muharibu

Bulembo mwizi huyuwa mali za Ccm mwingine.
Bulembo alishindwa biashara akiwa msoma na kujishikisha kwenye chama na ndo walihalibu chama kwa dili za kifisadi mdani ya chama na kufisadi serikali sasa nae anasema nini?

Bulembo hakuwahi kufanya bishara isiyohusiana na tenda za serikali sasa ana ujanja gani wa kukwepa ufisadi?
Hao ndo wahuni sas wnajitokeza wenyewe,
Roho zinawauma wanajitokeza mafichoni.
Ewaaa sasa ili haya yasikike vema mpelekeni kiroboto kwenye huo mdahalo na Bulembo ili kila mmoja atolee ufafafanuzi shutuma zake.
 
Bulembo ameshasema mleteni huyo kiroboto kwenye mdahalo apambane nae kwa hoja na yupo tayari kulipia ukumbi Serena Hotel.

Na muache kelele hilo twangapepeta lina wenyewe.
Kwanza arudishe pesa za shule za jumuia ya wazazi alizowauzia vigogo , Bulembo ni ''zero brain'' kubishana nae ni sawa na kubishana na muokota makopo barabarani.
 
Kwanza arudishe pesa za shule za jumuia ya wazazi alizowauzia vigogo , Bulembo ni ''zero brain'' kubishana nae ni sawa na kubishana na muokota makopo barabarani.
ewaaa haya maelezo mtamuambia kwenye huo mdahalo alioomba kufanya na polepole.
 
1. Polepole ni kijana mwenye akili nyingi sana (intelligent) mwenye shahada ya chuo kikuu. Ni mchambuzi makini (critical analysist) wa masuala mbali mbali ya kijamii, kisiasa na uchumi. Ana a very bright future na ni asset kubwa kwa ccm na taifa kwa ujumla kuwa na vijana wa aina hii. Wengi wanamwona anafanana sana na hayati JK Nyerere kifikira na kimaono. Hata mwandishi nguli, Pascal Mayala kaona hivyo. Vijana kama hawa wanahitaji kuwa supported, encouraged na kuendelezwa for the good future of our nation.

2. Zitto Kabwe naye ni kijana mwenye kiwango kama cha Polepole lakini hamfikii Polepole.

3. Dr Bashiru na Prof Kabudi: hawa ni magwiji wabobezi wenye elimu za PhD.

4. Bulembo elimu yake ni ya darasa la saba lakini ni mbumbumbu. Huwezi kumlinganisha na akina King Msukuma na Kishimba ambao ni werevu. Eti huyu Bulembo anaomba afanye mdaharo na akina Polepole, Bashiru na Kabudi? Si itakuwa ni kichekesho (commedy) ya karne? Si akafanye mdaharo na Masanja Mkandamizaji, hapo ndipo itakuwa poa. Alichokiongea Polepole huyu mzee Bulembo hakuelewa cho chote. Kakurupuka kama yule brother K wa Futuhi anavyokurupukaga.

Lakini Huyo mzee havuti bangi Chato
 
Kutokana na uchu na tamaa ya madaraka mzee wangu Abdalah Bulembo na wengine wanakuita alhaji ulitoa kauli ambayo iliishtua dunia na pengine dunia kuamini Tanzania ni nchi ambayo serikali inaua watu wanaohoji pesa za miradi

Kufuatia mkopo wa benki ya dunia(WB) kwenye mambo mbalimbali ambayo yangechochea maendeleo hususani suala la watoto wa like waliopata ujauzito kurudi shule ambalo ni suala ambalo uongozi uliopita haukuliona lipo sawa, zitto kabwe aliitoa maoni yake juu ya sharti hilo kutofanyika kwa kilichokusudiwa kwa mkopo huo na kuomba usitishwe.

Kufuatia maoni hayo ya zitto tarehe 03/02/2020 mzee bulembo ulitoa kauli hii, nanukuu: "Kuna mtu mmoja aliyechukua maswala yetu ya ndani na kuyapeleka nje ya taifa , hafai kuruhusiwa kurudi na anafaa kuuawa pale alipo .Uhaini! kile ambacho bwana Zitto Kabwe amekuwa akilifanyia taifa hili ni uhaini''.

Kauli yako hii ingeweza kuwa ni chanzo cha kuvunjika kwa mahusiano yote ya kimataifa lakini haikuwa hivyo hivo kwa uongozi unaosema ulivunja mahusiano hayo ulijitahidi kwa gharama yoyote kuyalinda. Hakuna mahali popote Rais Magufuli au waziri Kabudi aliwahi kutotoa kauli yenye kuhatarisha na kuchochea kuvunjika kwa mahusiano hayo ila ni wewe ulifanya hivyo kwa sababu ya uchu ulionao wa madaraka.

Napenda kukumbusha tu mzee bulembo katika uongozi wa hayati Magufuli mahusiano yetu na nchi nyingine yalikuwa ni imara sana hivyo tunajisikia aibu mzee kama wewe unapojaribu kupotosha umma kwa maslahi ya tumbo lako.

Tunaomba ukae kimya na uache kumuongelea vibaya hayati Magufuli kwa sababu utaishia kudhalilika na kuabika hata kwa wajukuu zako ambao wanaona mazuri yake kwa nchi hii.

Amelifanyia nini hili taifa huyu Bulembo.
Polepole anapigania haki za Watanzania kujieleza, kujitambua na kutambua haki zao.

Anatoa Elimu juu ya , haki, misingi, chanzo, maana ya demokrasia.

Watu wamebaki kumpinga kwa mipasho,KY jelly walioiweka wao, ili kuwatoa watu kwenye hoja.

Mmevamia nyumba yake, mmeiba TV, mmeweka KY mezani muipige picha, mmetupa vitu vyake vyote kama toilet papers, towel, kila kitu ili kumdhalilisha , kuondoa crecibility yake.

Hoja hata moja hamjawahi kuijibu. Kimsingi anasema hakuna awamu ya sita, ni kwamba anakwambia kiongozi aliondoka ni Mmoja JPM. Wote walikuwa wasaidizi wake, walipigania timu moja, sera moja. kitu kimoja. Awamu hii haikuchanguliwa upya na sera mpya, bali wanatekeleza sera za awamu ya tano.

Sasa hivi wanasema kila kibaya ni cha awamu ya Tano, Wakati walikuwa wasaidizi wakuu. Kila kizuri ni awamu ya sita.

Hata mkimuua Polepole, itakuwa ni sawa tu, yeye alishaamua kujitoa kutetea Watanzania mkisema ni gay ni sawa, wana propaganda za kitoto sana. Sababu kubwa hawana uwezo wa kujenga hoja.
 
Back
Top Bottom