Mzee Kikwete aweka rekodi sawa, Uchumi wa Kati waliopanga na Mkapa ni wastani wa dola 3,000 kila Mtanzania

Tulisema hapa uchumi wa kati FAKE sasa Kikwete kathibitisha. Sasa huyo MKURUPUKAJI hizi details huwa hazijui anakurupuka tu!?
Kapata aibu sana leo..
Maana yeye amekuta pato la Mtanzania lipo USD980 na hiyo ilikuwa 2015..sasa kapandisha kwa miaka mi 5 kwa dola 100 ndio tumefika 1080 basi kelele kila mahali.
 
Na kwa hivyo Lisu atashinda kwa sababu ya hilo?
Sijamtaja Lissu hapa ila nafikiri kwa jinsi watu fulani wanavyo mhofia basi anaweza akawa rais wa sita wa Tanzania endapo kutakuwa na fair play kama ile waliyoonesha uwanja Taifa.
 
Kwanini unakuwa na akili mgando kwamba unaongozwa na vilaza?

Sisi kama mchi hatuongizwi na vilaza! Labda hao vilaza wanakuongoza wewe na familia yako
Mkuu ujenzi wa barabara ya morogoro hasa eneo la mbezi mwisho,Barabara zetu kujaa matuta,sheria za ajabu Kama matokeo ya urais kutopingwa popote nk ni moja ya indicators za ukilaza huo
 
Ishu ya uchumi wa kati sio serikali ya jpm ndio imesema, ni bank ya dunia na vyombo vyake sasa hao ndio muwafungulie uzi wa mapovu na sio jpm...
 
Na kwa hivyo Lisu atashinda kwa sababu ya hilo?
Mtu anayesema uongo kila anapofunguwa mdomo wake anafaa kuwa kiongozi wa wanaccm pekee katika dunia hii ya watu waliostarabika
 
Ishu ya uchumi wa kati sio serikali ya jpm ndio imesema, ni bank ya dunia na vyombo vyake sasa hao ndio muwafungulie uzi wa mapovu na sio jpm...
Pointi yangu Ni kuwa lengo ambalo CCM walijiwekea (dola 3000), halijafikiwa bado
Ndio alichosema Kikwete na ndio Uzi wangu huo,
 
Ngoja nikuache na mtazamo wako wa kichadema!

Basi tufanye Kikwete kamuumbua Magufuli na kwamba tz haijafika uchumi wa kati kama WB walivyosema
Mkuu 2025 development strategy ipo mtandaoni kwa nini usiisome ukajiridhisha?lengo mdogo wangu haikuwa kuingia uchumi wa kati tu bali kipato Cha USD 3000.00 Sasa tupo 1028.00 bado sana,na JK kamwambia bado sana shehe
 
Mara hii wameshaanza kupishana kauli, maara paap Kikwete kahamia ACT wazalendo
 
Lengo la JK ni kututaka watz kuacha porojo na badala yake tuchape kazi ili kufikia uchumi wa kati.
 
Tuliza munkari tuwazodoe vizuri kwa kutudanganya
Ina maana unasikiliza sana propaganda na kuziamini, siku ukiambiwa tofauti unashtuka ulidanganywa

Kweli haukuwahi kusikia kuona kujua, kutambua kuwa 7% ya ukuaji wa uchumi alianza mkapa? Una tatizo gani?


Haya amini leo kuwa mama yako ni mwanaume
 
Ishu ya uchumi wa kati sio serikali ya jpm ndio imesema, ni bank ya dunia na vyombo vyake sasa hao ndio muwafungulie uzi wa mapovu na sio jpm...
Ungeangalia ile hotuba ya Dr. Mpango wakati anatoa hii habari ya kuingia uchumi wa kati ungejua sisi tunasema nini. Sasa kwa kuwa umekaa kusifia kuabudu kusujudu kutamka neno juhudi kama dozi ya TB basi na akili yako umeiweka mfukoni unatembea nayo!
 
Jina lako lina maana mbili; zote ni kwa lugha(kabila) ya kwetu

Mlimilwa= mmea unaozaa malimilwa (jamii ya maboga)

Mlimilwa= mlimiwa/mlimiwaji-anayelimiwa
 
Hii inaweza kuwa ni kutokana na sifa nyingi za Magu kwa mkapa wameamua kumexpose boss wa sasa
 
Ina maana unasikiliza sana propaganda na kuziamini, siku ukiambiwa tofauti unashtuka ulidanganywa

Kweli haukuwahi kusikia kuona kujua, kutambua kuwa 7% ya ukuaji wa uchumi alianza mkapa? Una tatizo gani?


Haya amini leo kuwa mama yako ni mwanaume
Kwani Mimi nimesema niliziamini?.
 
Nimesikiliza kipande kifupi cha hotuba ya JK ya leo, ama hakika Kikwete anazidi kuthibitisha umwamba wake kwenye fasihi.

Anakuwa shupavu wa muda wote, leo amepiga madongo makali sana kwa maneno mepesi. Nahisi upinzani pia uibe huu ufundi wa JK.

Nimefurahishwa sana pale alivosema target yake yeye na Mkapa ni uchumi wa kati wa per capita ya USD 3,000

Ameweka mzaa kidogo kwamba 'Kama Magufuli akichaguliwa tena, basi ifikapo 2025 basi pato litakuwa limefika USD 3000 kwa kichwa.

Kwa mahesabu yangu ya kiuchumi, ya haraka haraka, ili Tanzania ifikie pato la USD 3000 mwaka 2025 itabidi wastani wa ukuaji wa uchumi na pato la taifa uwe wa zaidi ya asilimia 22 kwa mwaka, na iendelee kuwa hivo kwa miaka minne ijayo.

Hapo ndo naona kwamba Kikwete ameamua kumzabua mtu risasi za moyo kwa kumpa target ambayo kamwe hawezi kuifikia hata robo yake. Kwa tafsiri nyingine ni kwamba leo kuna mtu kavuliwa nguo hadharani. Aisee yule mkwere ni hatari, amedhihirisha kwamba yeye alizaliwa mjini Daslamu na atabaki kuwa hivo

Year
2020​
2021​
2022​
2023​
2024​
2025​
Per capital GDP and projected1,080.001,317.601,607.471,961.122,392.562,918.92
Required GDP growth per capita
22%​
22%​
22%​
22%​
22%​
 
Inaonekana kama mzee Kikwete alijishtukia kwamba amepeleka maneno yenye msumari wa moto mahala. Kiukweli ameongea mengi huku kama kawaida yake akiacha mjadala uki trend huko mitandaoni na hata humu Jf sasa kumekuwa mvurugano baada ya hotuba ya JK. In short hajawahi kuacha upepo tulivu anapohutubia tangia atoke madarakani.

Mwishoni akamwambia Rais Magufuli "Hiyo ndiyo gharama ya kunishtukiza" kisha akamuuliza imetosha au? Kama imetosha naomba uniruhusu nikae! Rais Magufuli kwa moyo mkunjufu akamruhusu akae. Haya maneno haya nayo hatuwezi kuyaacha yapite hivi hivi maana huu ni msimu wa kupiga siasa!
 
Kwakweli mzee Leo uliamua kutiririka kabisa kama mzee mstaafu na asiye na hofu wala kujipendekeza.
Akiwa anatoa salamu katika mazishi ya marehemu Mkapa amesema mengi sana. Na amefanya tumegundua kuwa mipango mingi inayotekelezeka sasa ni ubunifu wake na hata mingine tunayojisifu sasa ni mipango yake japo haijakamilika kama alivyo taka yeye.
Hakika umefunguka, jee ulipania au yamekuja automatic mdomoni?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…