Mzee Kikwete aweka rekodi sawa, Uchumi wa Kati waliopanga na Mkapa ni wastani wa dola 3,000 kila Mtanzania

Na magufuli anaingia mikataba gani?mfano kwenye issue ya makinikia Kuna Nini Cha maana,kwenye mikopo ya interest kubwa mpaka sasa yupo juu kuliko mtu yeyote yule
Alafu utasikia tunajenga kwa pesa zetu sijui tunakusanya sana,huyu ukimthaminisha kwenye takwimu alichofanya past 5years unapata F ila kafaulu kutisha watu na kunyamazisha freedom of expression hasa kwa media zinazotumiwa na watu wa kawaida na vyama vya siasa kwa hiyo watu hawajui kitu tofauti na wanachoambiwa na ccm au ambacho kiko controlled
 
Mkuu Ile 2025 national strategy development plan si ya mkapa bali ya nchi,mkapa aliitekeleza,JK kaitekeleza and Magu is doing the same though in very very slow pace
Toka Magu kaingia madarakani sijui kama umewahi msikia akizungumzia dira ya taifa au kuimarisha kipato cha mtu,mimi nachojua yeye anaongeleaga sgr,sijui stiglaz na flyover mengine ni nadra sana
 
Na magufuli anaingia mikataba gani?mfano kwenye issue ya makinikia Kuna Nini Cha maana,kwenye mikopo ya interest kubwa mpaka sasa yupo juu kuliko mtu yeyote yule
Uwezi kufananisha Tanzania inachopata ndani ya Twiga na tulichokuwa tunapata kutoka ACCACIA. Hawezi kufanya kila kitu kwa ufasaha yeye sio financier wala contract lawyer; anachoweza kutaka kuona we get a better deal sasa kama appointed negotiators are unskilled umlaumu yeye for the results. Yeye atabaki na credit he tried.
 
Hao watangulizi wake unawalaumu kwa kuwa walikuwa financier au contract lawyers?au unasukumwa na usukuma?
 
Toka Magu kaingia madarakani sijui kama umewahi msikia akizungumzia dira ya taifa au kuimarisha kipato cha mtu,mimi nachojua yeye anaongeleaga sgr,sijui stiglaz na flyover mengine ni nadra sana
Hayo ni matatizo ya Selemani Jaffo au kitengo chao cha habari wao wakishapita hawa chukui picha za sehemu mbali mbali wakaziweka kwenye website.

Ngoja siku TAMISEMI wakisema waweke picha kwenye website yao za shule zinazo karabatiwa, shule zinazojengwa nchi nzima, miradi ya maji, Zahanati zilizokamilika, hospitali, vituo vya mabasi, Barabara za TARURA; nakuakikishia wengi mtafunga midomo.

Tatizo lenu ivyo vitu mnavisikia majukwaani tu ampati picha yenyewe kuona quality zake, ndugu usifanye mchezo Magufuli kafanya kazi sikia tu.
 
Mkuu naona BAVICHA Wanairuka hii kwa makusudi kabisa, hawatakagi kusikia kabisa.
 
Toka Magu kaingia madarakani sijui kama umewahi msikia akizungumzia dira ya taifa au kuimarisha kipato cha mtu,mimi nachojua yeye anaongeleaga sgr,sijui stiglaz na flyover mengine ni nadra sana
Mkuu sijawahi kumsikia labda hajui anachokifanya
 
Hawezi kufikia ukitaka kujua hilo angalia GNI kuanzia 2005-2015 afu angalia 2015-2020 utakuta inashuka sasa atafikaje Magu? Kiufupi tutamu assess kwa kuangalia dira ya Taifa sio WB wanasemaje maana hawa hawa huwa wakipewa takwimu hasi wananuna
Pili huwezi niambia unawekeza trions of money kwenye mradi usio na maana kama sgr eti utaboresha maisha sahau hili ni mzigo juu kwa juu na deni kubwa kwa nchi
Wenzio kuanzia Moroco,Kenya,Ethiopia nk waliwekeza miradi ya dizaini hiyo kwenye maeneo potentia/shoroba kuu za usafirishaji na uchumi,huku kwetu mtu anawekeza sehemu ambayo hata haina mzigo wa maana sasa itasidia nini?
 
Hao ndio usiwagusie maana mikataba waliyoingia ndio mibovu kweli kweli.
Mkuu sina hakika Kama tunaelewana,nimesema hizo sababu ulizotumia kumtetea Magufuli kwanini pia zisitumike kwa BWM na JK?
 
Mkuu sina hakika Kama tunaelewana,nimesema hizo sababu ulizotumia kumtetea Magufuli kwanini pia zisitumike kwa BWM na JK?
Unaweza fananisha mkataba waliongia serikali ya Mkapa sijui na kampuni gani, ambayo ikanunuliwa na ACCACIA wakati wa JK? Na tulichopata kupitia Twiga.

And what did it take for those changes to take place, jibu lako litakupa tofauti.
 
CDM wakitaka kuwakamata maccm kwenye sera kirahisi warejee tu kwenye ilani yao ya 2015
CCM walisema by 2020 kila wilaya itakuwa na hospitali,kila kata kituo cha afya na kila kijiji zahanati sasa je walizojenga ni asilimia ngapi? kumbuka idadi ya watu inaongezeka lakini wakiwaachia wawe wanasema eti tumejenga hospitali 67 na zahanati zaidi ya 400 watashindwa kuonesha kwamba ccm wamefeli,kwa idadi ya kata zaidi ya 3000 na vijiji zaidi ya 12,000 ukitafuta asilimia unakuta hakuna cha maana wamefanya licha ya kujipiga kifua
Pili hata kwenye barabara walisema barabara zote kuu zitakuwa zimeunganishwa na lami yaani mkoa kwa mkoa na nchi kwa nchi,lakini hadi navyoandika hapa kuna mikoa lundo hawajajenga kwa lami na hata huyu ataondoka hajamaimalisha mfano toka 2015 Tabora-kigoma ni vumbi,kigoma-kagera,kigoma-katavi-Rukwa ni vumbi,mbeya-tabora/singida ni vumbi,Arusha-musoma vumbi,Ruvuma-Morogoro,Njombe-Morogoro yote hiyo ni vumbi yaani hii ni baadhi tu
Ukija kwenye shule ni hivyo hivyo walishashindwa kutatua madawati na watoto kulundikana madarsani kama mbuzi ila huwezi ona maana hakuna cha haki elimu wala magazeti kuonesha utachoishia kusikia ni elimu bure sijui tunatoa ngapi kila mwezi ilimradi kuwazingua watu wenye akili ndogo almaarufu wajumbe
 
Unaweza fananisha mkataba waliongia serikali ya Mkapa sijui na kampuni gani, ambayo ikanunuliwa na ACCACIA wakati wa JK? Na tulichopata kupitia Twiga.

And what did it take for those changes to take place, jibu lako litakupa tofauti.
Mkuu hiki inachopata serikali kwenye mkataba na twiga Mimi sikijui na najua serikali hii haioni shida kusema uongo Ila Lissu akifika Ikulu November 2020 tutaujua ukweli
 
Serikali ya awamu ya tano ilipaswa kuwa na kauli mbiu isemayo "hapa Propoganda tu'' badala ya ''hapa kazi tu''
 
Mkuu hiki inachopata serikali kwenye mkataba na twiga Mimi sikijui na najua serikali hii haioni shida kusema uongo Ila Lissu akifika Ikulu November 2020 tutaujua ukweli
Ndio mlivyo mwishowe mnaishiaga kujiridhisha na vitu mnavyofikiria kichwani kwenu badala ya facts. Kama uamini serikali yako tafuta report za Barrick.

Mchana mwema.
 
Ndio mlivyo mwishowe mnaishiaga kujiridhisha na vitu mnavyofikiria kichwani kwenu badala ya facts. Kama uamini serikali yako tafuta report za Barrick.

Mchana mwema.
Niambie kwa nini mkataba umefichwa?
 
Kushuka kwa uchumi kama ulivyosema ni kweli kunawezekana kutokea kwa kuwa uwekezaji wa miundombinu imara ni ghali sana,uchumi utaimalika kwa kasi pindi miundimbinu itakapo kamilika kujengwa.
Sio lazima kila wakati kupanda,kuna wakati unashuka alafu unapanda zaidi (wave) kwa kasi ya kufikia malengo.
Ndio maana yapo malengo ya muda mfupi na mrefu.
Shabaha kubwa ni kufikia malengo hata kama tutakwama katikati/mahala kikubwa ni kusimamia kile tunachoamini kuwa tunaweza kufanya kwa vyovyote vile.
 
Si Mkapa wala Kikwete waliofikia lengo lao.
Yapo kwenye makaratasi tu.Walishindwa kuziba mianya ya rushwa,mikataba michafu,EPA,IPTL,Container Terminal, NBC,Viwanda vya Nyerere vikayeyuka ajira nazo zikapotea.
Ila ni wenzetu lakini uchumi wetu walifulia .
 
Raisi Mstaafu JK kusema hayo, Sisi kama Wananchi wa kawaida, hatuwezi kukosa haya ya kujiuliza

Umiliki wa Uchumi Kwa wananchi, zaidi ya tawala nne zote, wamehangaikia kupata na wakafanikiwa $900, hapo ni zaidi ya miaka 50+

Mpango wa viongozi wetu hao ambapo pia ni Jambo jema, ni kuona kwamba, kufikia 2025 angalau kipato cha mwananchi kifikie $3000

Unajiuliza, Kwa nini miaka zaidi ya 50+, hawakuweza kufikia hata nusu ya mpango wao? Iweje wapange Hilo lifanyike Kwa miaka kumi pekee?

Ukiangalia nchi walivyoiacha, unaona kabisa kwamba mpango wao japo ni mzuri, Ila Bado ulikuwa na mapungufu

Nchi ilivyoachwa, Rushwa ilikuwa ni njenje, Ukusanyaji wa Kodi ulikuwa hovyo, mikataba mibovu, kwenye madini ndio usiseme, bandari nako hakuelezeki, ilikuwa kama wewe ni mtoto wa Fulani unapita bila kuulizwa, wizi wa nyara za serikali, vitalu watu kujimilikisha, gesi kupewa wageni na vitu vingi tu vilivyokuwa ni hovyo

Nchi Kwa mfano ilikuwa na nini cha Maana

Kwa jinsi hiyo, utawekaje sasa mpango wa miaka kumi kwamba uone kipato cha mwananchi kikifikia $3000 ili Hali hawa viongozi wetu hawakuifikia hata Ile robo yake tena zaidi ya miaka 50+?

Je, waliuona Uwezo wa anayekuja kwamba ni mzuri zaidi Kwa maswala ya Uchumi au ndani mwao kulikuwemo unabii?

Kivyovyote vile, Magufuli ni mzuri tena sio kidogo, mbali na Changamoto hizo zote, lakini tunayo macho tunaona

Naamini pia kwamba, kipato hicho ikiwa majanga ya kidunia yataondoka mapema, itakuwa

Mungu Ibariki Tanzania na Watanzania wote
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…