Mzee Kilomoni akamatwa na jeshi la Polisi

Mzee Kilomoni akamatwa na jeshi la Polisi

Ndo anachopinga kilomoni hicho. Unadhani Stan Kroonke akitoka pale Arsenal timu itatetereka. Mo ni mdhamini au mwekezaji?! Kikubwa taratibu zifuatwe tu kusiwe na upindishwaji wa mambo.
Unataka kusema kabla ya mo kuwekeza, simba ilikuwa haiteteleki. Husifananishe arsenal na ujinga ulioko huku kwetu
 
Ndo anachopinga kilomoni hicho. Unadhani Stan Kroonke akitoka pale Arsenal timu itatetereka. Mo ni mdhamini au mwekezaji?! Kikubwa taratibu zifuatwe tu kusiwe na upindishwaji wa mambo.
Usilinganishe Arsenal na Simba, timu pekee iliyowahi kuchukua EPL bila kufungwa, Arsenal ni timu ya dunia ya kwanza ina wadhamini na wana hisa wengi kila mtu anaitolea macho.
.
Arsenal ni klabu inayotengeneza faida kila mwaka, tiketi tu za kiingilio cha mechi za Arsenal pale Emirates ukikijua ndipo utajua kuwa unalinganisha umbali wa kutoka mwanza hadi Nairobi na Los Angeles na Mars!
.
Linganisha Simba na Al ahly timu ya mashabiki ambayo mifumo yake ya kiuwekezaji ukiijua utakaa kimya huenda ukamchukia kabisa Mwakyembe!
.
Mafanikio ya Mamelodi Sundowns unajua yamekuja tu kama kimbunga?
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji16][emoji16]
Hahahahahahahahah.....Mpelekeni kunako stahilu mumtoe na Marinda kabisa,Maaamaae zake mpigeni virugu vya kutosha mpaka magoti yageukie magharibi, Ajuza hilo lisilokuwa na haya.
 
tuliza kppa hicho
Makonda kawatuma vijana wake,ila kama Simba wako smart kweli wangemwacha tu Mzee Kilomoni, mbona hawataki aseme?

Ukiona mtu anabana sana freedom of expression,jua kuna mengi yamejificha
 
Kutoka hapa block 41 mzee Kilomoni amekamatwa na Polisi na ameahidi kurejea baada ya dakika 5 lakini amepakiwa kwenye gari la Polisi kwa sababu zilizoelezwa kuwa hakuwa na kibali cha kufanya mkutano huo.
.
Msumari wa moto unataka kumgeukia
Hivi hata nyumbani kwa mtu napo inahitajika kibali?.

Sikubaliani na vurugu za mzee kilomoni, na vile vile Sikubaliani na vurugu za police
 
washenzi sana hawa, wakiona mdhamini nduki kuleta vurugu, yule akilimali hadi leo haonekani akija mdhamini huyo analeta miguu yake kuleta vurugu
Ngoja wakamtatue marinda atie akili. Huyu na yule mwenzake Akilimali ni wa.kupigwa vita lolote.
 
View attachment 1162309

View attachment 1162310

Khamis Kilomoni aliyekuwa Mwenyekiti wa Baraza la Wadhamini wa Klabu ya Simba amekamatwa leo kwa tuhuma za kuitisha kusanyiko nyumbani kwake bila kibali

Leo Julai 25, 2019, Mzee Kilomoni aliitisha mkutano na Waandishi wa Habari, nyumbani kwake maeneo ya Kinondoni Jijini Dar

Hata hivyo Askari wa Jeshi la Polisi walifika na kumchukua kabla ya mkutano huo na Wanahabari kuanza

Hivi karibuni Mzee Kilomoni aliingia kwenye mgogoro na Mwekezaji wa Klabu ya Simba, Mohammed Dewji
Mbona wengine wanafanya press conferences bila kukamatwa? Tena wanafanyia kwenye mahotel ya fahari!
 
1564059882509.png


Milionea mmiliki wa Klabu ya 5IMBA Mzee Hamisi Kilomoni
 
Anayeleta siasa kwenye michezo mi naona ni mwakyembe bora ang'olewe kabisa. Kutuvuruga vichwa wakati tunataka kupeperusha bendera ya Tanzania Africa nzima sio sawa kabisa
Mwakyembe huyu wewe muache tuu.hawa watu ndio wanao mpa kichwa mzee kilomoni.

Leo hii Mwakyembe anajifanya hakuwepo wakati hayo mabadliko ya clab yanafanyika.
 
Ikishuka we utafaidika Na nini acha roho za kichawi
Sijasema hivyo kwa roho mbaya nimeandika hivyo kwa uchungu sana, inawezekanaje timu ianze kupata mafanikio anajitokeza mtu wa kuturudisha nyuma ambaye hana mbele wala nyuma?
.
Na hii sio kwa Simba tu ilikiwepo Yanga mzee Akilimali kamsumbua sana Manji haya kaondoka umewahi kumsikia kalipa mshahara mchezaji hata mmoja au kuisafirisha timu kwa ndege?
Afadhali hata la Yanga, hili la Simba waziri analishupalia kabisa itabidi Mo akae kando tuone kama hata itamtoa De Songo na kulipa wachezaji walioletwa kama haijawa beseni badala ya bakuli.
.
Hatukuchukua ubingwa misimu mitatu mfululizo na hatukuenda kimataifa kama miaka mitano mfululizo MO natamani ajitoe ili mpira wa Tanzania uendelee kuwa upumbavu basi tufanye mambo mengine.
Mwanachama wa Simba sports kadi namba 1123
 
Hivi hata nyumbani kwa mtu napo inahitajika kibali?.
Sikubaliani na vurugu za mzee kilomoni, na vile vile Sikubaliani na vurugu za police
Mzee Kilomoni anaweza kupewa kesi ya uchochezi unafahamu hilo?
.
Anavuruga amani anaweza kuvamiwa kwake na hivi ni rahisi kuingilika wakamuuwa maana analeta hisia za chuki anaudhi sana yule mzee anastahili kupewa kesi ahangaike nayo mpaka anakufa
 
Nashangaa pia, namfahamu mtu mmoja anajiita commando mashimo, yeye huita mikutano ya waandisha atakavyo na sidhani kama huwa anaomba kibali polisi
Athari za mikutano yake na waandishi wa habari ni zipi?
.
Kilomoni athari zake ni kama kuleta chuki na uchochezi na hata kuhatarisha maisha yake
 
Back
Top Bottom