Mzee Kinana Umetukataza Kukagua Taa za Magari Mchana, Sawa Tumekuelewa

Mzee Kinana Umetukataza Kukagua Taa za Magari Mchana, Sawa Tumekuelewa

Tena ilitakiwa upelekwe police mess, ukatandike vitanda na kuwahudumia maafande chakula na vinywaji,
 
Mimi trafiki naowajua hawakagui chochote ni kukusanya hela barabarani, Kama huna ndio wanaanza kukagua, huu mfumo unafanya kila dreva LAZIMA awe mtoa rushwa, Hadi watu wanafikiri ni mradi wa serikali, huu mfumo uangaliwe upya.

Yaani kutoka wilaya moja Hadi nyingine uwe na angalau elfu ishirini ya kusafisha barabara hata Kama gari ni jipya. Tusitetee upumbavu
 
Pole sana, unaandika kwa hisia hadi sauti inasikika.

Wako askari waadilifu na wasio waadilofu.

Wasio waadilifu kwenye sekta ya usalama barabarani ndo wamebeba hulka kuwa askari wote wa barabarani ni wasumbufu, wala rushwa etc.
Shukrani sana mkuu
 
Mimi trafiki naowajua hawakagui chochote ni kukusanya hela barabarani, Kama huna ndio wanaanza kukagua, huu mfumo unafanya kila dreva LAZIMA awe mtoa rushwa, Hadi watu wanafikiri ni mradi wa serikali, huu mfumo uangaliwe upya.

Yaani kutoka wilaya moja Hadi nyingine uwe na angalau elfu ishirini ya kusafisha barabara hata Kama gari ni jipya. Tusitetee upumbavu
Umekaririshwa tu ndugu yangu
 
Baada ya agizo lako, tumeitwa na tupo kwenye utekelezaji. Nadhani ajali ya Usiku wa kuamkia leo imesababishwa na Taa.

Tunashukuru, wengine tumebadilishiwa mpaka idara ila sawa tu. Kila la kheri ndugu Kinana endelea kufurahia ku-drive maana hatuta kusumbua.
Nasema Uongo Ndugu Zangu kipindi cha Dkt Magufuli mlifanya kazi vizuri, yaani mlisimamia sheria na mkimkamata mtu kafanya kosa ndiyo mlichukua rushwa ila kwa kosa halisi. Ila kwa sasa mlikuwa mnashindana kuchukua hela hata kama gari halina kosa mnatafuta makosa hasa kwa daladala au basi
 
mnakera. unakaguliwa mara sita ndani ya mkoa mmoja mnauliza vitu vile vile
wekeni utaratibu wa kutokurudia ukaguzi at least on the same day
mfano unatoka kahama unaenda shinyanga, ndani ya mkoa. Unasimamishwa bijampola kwa mbele hapo karibu na daraja, unaombwa leseni, unaomba card ya gari, unaambiwa washa taa
Ukitoka phantom unaombwa vitu hivyo hivyo
kabla ya buwagi hapo vitu hivovivo
kagonwa tena
hali inaendelea hivyo kabla ya isaka na baada tu ya isaka hapo shule ya msingi
itwangi au luhumbo, tinde, baada ya tinde kuna vikosi viwili hadi vitatu kabla ya kuingia shinyanga
Kwa teknolojia tuliyo nayo sasa hapa nchini ni lazima tufanye hivyo ila siku tukiwa na uwezo wa kufunga camera za kufuatilia mienendo ya vyombo wala huta sumbuka.
 
Baada ya agizo lako, tumeitwa na tupo kwenye utekelezaji. Nadhani ajali ya Usiku wa kuamkia leo imesababishwa na Taa.

Tunashukuru, wengine tumebadilishiwa mpaka idara ila sawa tu. Kila la kheri ndugu Kinana endelea kufurahia ku-drive maana hatuta kusumbua.
Trafiki wa tanzania mchango wao mdogo sana kwenye kuzuia ajali..mana hata walipokuwepo ajali zilikuwa zikitokea..wengi ni wazuri na wataalamu wa kupokea rushwa.

Kitengo hichi kifumuliwe na kiendane na modern world...na sio kujaza trafic barabarani.

#MaendeleoHayanaChama
 
Nasema Uongo Ndugu Zangu kipindi cha Dkt Magufuli mlifanya kazi vizuri, yaani mlisimamia sheria na mkimkamata mtu kafanya kosa ndiyo mlichukua rushwa ila kwa kosa halisi. Ila kwa sasa mlikuwa mnashindana kuchukua hela hata kama gari halina kosa mnatafuta makosa hasa kwa daladala au basi
Mudawote mrembo nimemiss sana ile kitu ulinipea... nilikuja Lumumba nikaambiwa haupo tena na simu sikupati. Naomba nitafutie namna tena, Thanks.
 
Nasema Uongo Ndugu Zangu kipindi cha Dkt Magufuli mlifanya kazi vizuri, yaani mlisimamia sheria na mkimkamata mtu kafanya kosa ndiyo mlichukua rushwa ila kwa kosa halisi. Ila kwa sasa mlikuwa mnashindana kuchukua hela hata kama gari halina kosa mnatafuta makosa hasa kwa daladala au basi
Mimi sijawahi kubadilika, nimejifunza kuwa mwadilifu na natambua thamani ya uadilifu, siwezi kusemea wengine ila raia mnatufanyia vibaya mpaka hatufurahii kazi yetu.
 
Walikuwa wanatunyanganya hela hawa trafic.
 
Baada ya agizo lako, tumeitwa na tupo kwenye utekelezaji. Nadhani ajali ya Usiku wa kuamkia leo imesababishwa na Taa.

Tunashukuru, wengine tumebadilishiwa mpaka idara ila sawa tu. Kila la kheri ndugu Kinana endelea kufurahia ku-drive maana hatuta kusumbua.
Mi naonaga trekta zikitembea usiku na zingine mijini utadhani ni magari. Trekta ni mitambo ya kazi mashambani. Serikali itoe elimu na ikataze hii midude kutembea mwisho saa 12 jioni.
 
Pole sana mkuu , mimi binafsi nawapenda sana Trafick wanafanya kazi ngumu wanaochukia ni wale magari yao mabovu , wabongo wengi wanashabikia vitu .
 
Hamjakatazwa kukagua magari Ila mlikuwa Wengi mpaka mnachelewesha safari .Unatoka Bunju kwenda Mbagala hapo hapo Bunju unakaguliwa ,boko Tena Tegeta Tena Mbezi Tena ,Mwenge Tena, Mawasiliano Tena,Buguruni Tena,Uhasibu Tena kwa Aziz Ally Tena ,Mission tena na Zakhem Tena. Yaani 40km unakaguliwa Mara 10
 
Back
Top Bottom