Mzee Makamba: Mchungaji Gwajima anayo laana ya kumtukana Kardinali Pengo

Mzee Makamba: Mchungaji Gwajima anayo laana ya kumtukana Kardinali Pengo

Salman Rushdie na Gwajima Mwenye laana ni yupi? Babu makamba kalee wajukuu!
 


Mzee Makamba anadai kuwa Mchungaji Gwajima anayo laana ya kumtukana Kardinali Pengo. Na kwa tafsiri ya kiafrika mtu mwenye laana siku zote hufanana na mtu aliyechanganyikiwa. Ayafanyayo huwa kituko kwa wanaomzunguka, huwafanya watu waingiwe na huruma.

Lakini naamini lengo la Mzee Makamba kumsema Askofu Gwajima ni kumuongezea uadui miongoni mwa wanajamii kwa kuanzia na watu wanaosali kwake. Lengo jingine ni kumchongea kwa Mwenyekiti Mtarajiwa wa CCM.

Vyovyote iwavyo siuoni mwenendo mzuri katika siku zijazo kwa Askofu huyu. Ni hatari sana pale unapojaribu kujikomba kwa mtu mmoja kwa kumponda mwingine bila ya kuifahamu kwa undani wanapokuwa wamekaa pamoja wawili hao wanaongea vipi na wanaaminiana kwa kiasi gani.

Kiongozi mstaafu siku zote hapungukiwi ushawishi kwa aliyepo pale Magogoni. Askofu alipaswa kupima uzito wa kauli yake ili akwepe kufananishwa na mtu aliyelaaniwa.

Kwani Makamba siyi msataafu anayejikomba kwa Magufuli? Tena amesikika akisema Kikwete alibatiza watu kwa maji lakini Magufuli atabatiza kwa moto? Kwa nini anatumia neno kubatiza na siyo kusilimisha? Aache kabisa kujifanya anajua imani za watu wengine.
 
Salman Rushdie na Gwajima Mwenye laana ni yupi? Babu makamba kalee wajukuu!
Swali lako limejumuisha watu wawili tofauti kabisa, wenye historia zisizofanana, na ambao vyanzo vya kuchukiwa kwao ni tofauti pia.
 
Kwani Makamba siyi msataafu anayejikomba kwa Magufuli? Tena amesikika akisema Kikwete alibatiza watu kwa maji lakini Magufuli atabatiza kwa moto? Kwa nini anatumia neno kubatiza na siyo kusilimisha? Aache kabisa kujifanya anajua imani za watu wengine.
Dini mara nyingi hazina mwenyewe. Ndio maana wapo mapadre ambao wamesomea maandiko ya kiislam pia wapo mashekhe wenye kuijua vizuri Biblia. Unataka kuniambia kuwa wewe unaijua dini sana kiasi cha kukosoa tabia ya mzee Makamba ya kutumia maandiko katika kujenga hoja?.
 
Dini mara nyingi hazina mwenyewe. Ndio maana wapo mapadre ambao wamesomea maandiko ya kiislam pia wapo mashekhe wenye kuijua vizuri Biblia. Unataka kuniambia kuwa wewe unaijua dini sana kiasi cha kukosoa tabia ya mzee Makamba ya kutumia maandiko katika kujenga hoja?.
Hoja gani? Niambie hao waliobatizwa kwa maji ni akina nani? Anajua maana ya kubatiza kwa moto au anaropoka? Bado sijaelewa mantiki ya swali wala hoja yako. What is that you want to ask or tell me? Sijakuelewa? Hao mashehe wenye kujua Biblia sijawasikia wakitamka uongo kama wa Makamba hadharani.
 
Ujumbe wake umeeleweka kwamba Magufuli hataki mazoea ya vimemo,anateua mtu kwa sifa na si kujuana!Hoja yangu hapa ni kuwa mzee kama huyo anakuwaje hazina ya chama huku akipenyeza vimemo?
Siasa za kiafrika hazinaga msafi. Unataka kuniambia gia ya angani ambayo ilimfanya Lowassa asifiwe na wale wale waliomuita fisadi, iliweza kutekelezeka bila ya kutokuwepo kwa mkwanja uliopenyezwa chini ya meza?. Unataka kuniambia ilikuwa ni clean politics kwa EL kupewa nafasi ya kugombea urais?. Siasa zina mambo mengi ambayo hayajulikani hadharani kwa walio wengi.
 
Kwani Makamba siyi msataafu anayejikomba kwa Magufuli? Tena amesikika akisema Kikwete alibatiza watu kwa maji lakini Magufuli atabatiza kwa moto? Kwa nini anatumia neno kubatiza na siyo kusilimisha? Aache kabisa kujifanya anajua imani za watu wengine.
Makamba kwa miaka mingi sana amekuwa akikejeli ukristo huku Wana CCM wakicheka. Kuna wakati alimuita YESU kuwa ni Nabii Issa kitu ambacho ni kejeli, dhihaka na matusi kwa ukristo
 
Mtumishi wa Mungu hahitaji kujikomba kwa watawala. Gwajima ana pesa zaidi hata ya Magu
Pesa na busara ya kujua ni wapi niseme kitu gani, ni vitu viwili tofauti sana. Alizivamia kwa pupa siasa, kuropoka kwake hovyo pia kulichangia katika kumuongezea maadui.
 
Makamba kwa miaka mingi sana amekuwa akikejeli ukristo huku Wana CCM wakicheka. Kuna wakati alimuita YESU kuwa ni Nabii Issa kitu ambacho ni kejeli, dhihaka na matusi kwa ukristo
Ndivyo alivyo. Siyo mara moja siyo mara mbili. Mifano yake ya kijinga huwa anatumia Ukristo. Kwani hana dini yeye? Mzee mzima OVYO!
 
Pesa na busara ya kujua ni wapi niseme kitu gani, ni vitu viwili tofauti sana. Alizivamia kwa pupa siasa, kuropoka kwake hovyo pia kulichangia katika kumuongezea maadui.
Nadhani Kuna viongozi wengi sana wa siasa wanaropoka tena saaana (sitaki kutaja jina, wenye akili wanajua). Gwajima yuko sahihi sana kwa matamshi yake. Namuombea kwa YESU amlinde mtumishi wake
 
Ndivyo alivyo. Siyo mara moja siyo mara mbili. Mifano yake ya kijinga huwa anatumia Ukristo. Kwani hana dini yeye? Mzee mzima OVYO!
Anajifanya bingwa wa kuchambua dini ila kosa kubwa anafanya ukristo na uislam kuwa sawa wakati ni tofauti sana. Eti ubatizo wa moto, hapo ni kutukana nguvu ya roho mtakatifu.
 
JK na JPM sivyo kama tunavyowazungumzia mitandaoni. JPM anaweza kuikosoa atakavyo serikali ya awamu ya nne na zile zilizopita lakini mmoja wa washauri wake wa karibu ni JK. Hivyo wanavyokaa pamoja atakayeumia anaweza kuwa ni askofu.
Every person feels important! Labda wanyama wa mwituni inawezekana. Hakuna binadamu anayependa kunangwa mbele za watu! Kucheka au kutabasama hakumaanishi kuwa moyoni unafuraha au unapenda. Katika mazingira fulani binadamu anaweza akacheka hata anapotukanwa ikawa busara zaidi kuliko kukasirika. Mioyo inasiri nzito!
 
Naomba Lowassa aende mahakamani kwa kuitwa fisadi a,siasa za blah blah hatutaki Tena! Akikaa kimya basi amehalalisha jina hilo.
. Gwajima na makamba naona akilizao hazipishani sana...waendelee kupeana maneno
 
Baada ya siku ya leo Jumamosiya sabato kumalizika na mkutano mkuu kumpitisha kikwete,kesho ni siku maalum ya Gwajima kumjibu Makamba,naamini Makamba ameingia choo cha kike na ataomba poo japo kimya kimya na waandishi wa habari msikose Kanisa la UFUFUO na Gwajima kesho,hii ni komedy mpya inayokuja
kama ni mipasho na matusi Gwajima hamuwezi Makamba. Kwanza Gwajima hata kiswahili hakijui sijui ni mtu wa nchi jirani
 
Back
Top Bottom